February 03, 2018

MUHUKURU: MGODI WA PILI WA MAKAA YA MAWE MKOANI RUVUMA

NA MWANDISHI WETU
 
KAMPUNI ya KAMBAS GROUP yenye makao yake Makuu jijini Mwanza imeanza kazi ya uchimbaji makaa ya mawe katika Mgodi Mpya wa Muhukuru wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Kwa mujibu wa Afisa Mahusiano wa Kampuni hiyo, Issa Litunu amesema tayari kampuni hiyo imefungua tawi mjini Songea ambapo hatua za awali za uchimbaji na usafirishaji zimeanza.

Litunu amesema katika kipindi cha wiki moja Kampuni hiyo imechimba zaidi ya tani 1000 za makaa ya mawe ambayo yanasafirishwa kutoka mgodini umbali wa zaidi ya kilometa 100 toka mjini Songea, yanawekwa eneo la Likuyufusi lililopo Kata ya Lilambo Manispaa ya Songea kabla ya kusafirishwa kwa wateja jijini Dares Salaam.

Hata hivyo Afisa huyo amesema kazi rasmi ya uchimbaji inatarajia kufanyika baada ya kupungua mvua za masika ambazo hivi sasa zinaleta Changamoto ya barabara.Amesema taratibu zote zimefuatwa kabla ya kuanza kazi ya uchimbaji.Huu ni mgodi wa pili wa makaa ya mawe katika mkoa wa Ruvuma. Mgodi wa kwanza wa makaa ya mawe ni wa Ngaka uliopo wilayani Mbinga.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako