August 31, 2007

Da' Maria karibu

Kupiga gumzo mtandaoni ni raha sana,basi jana nikaanza kuandika ujumbe kwa dada Maria Mtawali..sijui yuko wapi siku hizi hasemi mahali alipo labda ananiogopa.Nikawa naandika ujumbe kadhaa kwa ajili yake...mara nikakuta ujumbe unaoniuliza 'nyasa' ni nini? halafu...'wewe ni mnyasa?' duuh! kufikia hapo nikaona sasa dadangu amenikuana sana anaponiuliza kuhusu nyasa.

Ndiyo..tunavua samaki aina tofauti,kwanza hata wengine hawajui hata nikisema samaki ndio nin..si hiyo misangara yenu ila mandongo,kambale,ngorokoro n.k au waulize wale wazungu kule Liuli wanafanya nini,kisha njoo makao makuu yangu hapa LUNDU niambie unataka samaki wa aina gani au unataka mihogo ya kutafuna ambayo huko ughaibuni wengine wanasikia tu hewani.

Lakini dada maria miye ni toto la kinyasa yaani usijaribu yaani nakupenda nyasa kwangu hapa,kwani nguvu za kukaa katika kompyuta wananipa wao.Jana nilikula sana samaki kutoka mtera halafu nikabeza hawana hata harara kwa mwenye njaa.
Da' maria mi ndio mwenyewe nipo nimetulia nakukaribisha.....njooooo...katika darasa la Ndesanjo hili tujidai mpaka basii