August 31, 2007

Upweke mmhh

Jamani wakati mwingine huwa najichekea peke yangu au nikimwona mtu ninaye mfahamu huu napenda sana utani matokeo yake naambiwa nina tatizo la kisaikolojia.Hivi unajua kwanini?. Mara nyingi nakuwa mpweke sana yaani napenda kuwa sehemu tulivu mno.

Huwa naongea peke yangu mara nyingi tu huku nikitoa nafasi kwa ubongo wangu kufanya kazi sawa sawa si unajua tena mambo ya kuvua samaki nyavu inapaswa kuwa salama muda wote..
Acha bwana yaani najiona bonge la mjanja nikiwa pekee halafu nikikutana na washkaji naambiwa oooo nina ugonjwa sijui nini huko...

Hivi unavyonitazma kweli unaweza kuamini eti nina unini sijui.. ...sawa lakini napanga mikakati ya kuikamata nchi yaani kuwa rais halafu Ndesanjo anakuwa waziri mkuu,kisha Fred Macha naye anakamata wizara ya utamaduni..ili acharaze vyema gitaa lake...aaa sijashau bwana Michuzi anakama wizara ya sheria ili asiibiwe tena wahuni toka Nigeria maana wataiba hata *****za ndani jamani si fujo hizo hebu lete fimbo jamaa kaandika neno la minyotanyota kibao hapa nani huyu alaa.