September 05, 2007

Tufunge na Kuomba Mungu...

Ndiyo tunalazimika kusali sala za imani yoyote ili kuwawezesha waqvuja jasho wetu wa Taifa Stars kushinda mechi yao a mwisho dhidhi ya Wamachina toka Msumbiji.Yaani tunahitajika kuwa na moyo wa chuma kwelikweli ili tushinde.

Sala zetu ziwe na haja ya kupata magoli 3 kwa nunge kwani wale jamaa kule Senegali lazima watakataa kuadhibiwa idadi kubwa ya mabao lakini tunahitaji sala za maombezi kwa wote Rastafarian,wakristo,wabudda,waislamu n.l ili mradi tuwe na lengo moja tu la kushinda mchezo huo.

Tulia kwa dakika 5 tu omba kadiri uwezavyo angalau uwe na moyo wa huruma kwa vjana hawa wanaoteseka kwa kuweka rehani mioyo yao ili wapate ridhiki ya maisha.

Hapa nilipofika leo Mbinga kuna watu tokana na baridi+Taifa Stars=kihoro na homa matumbo zimejaa tele kumbe watu wanaugulia mechi hiyo,wanajiuliza itakuwaje yaani hata maofisini mambo ni hayo hayo.
uhuru daima

1 comment:

  1. haya kama mungu yko nasi basi tutashinda kwa pamoja tutafurahia tu

    ReplyDelete

Maoni yako