October 20, 2007

CHIWANDA;wanyasa na eneo lake

Hiki kijiji cenye sifa zinazokaribaiana na vijiji vingine,kinapaka na chimate kwa upande wa kusini.Nacho kipo mwambao huohuo wa nyasa na shughuli kubwa hapa ni kilimo,ufugaji,uvuvi, na biashara.Eneo kubwa la kijiji hiki ni tambarare sana hivyo hutofautiana na jirani zake wa chimate.ardhi yake ni ya udongo wa kichanga ambao upo katika maeneo mengi ta barabarani na pia kuna maeneo makubwa sana ya kilimo hususani katika maeneo yenye ardhi inayokubali kilimo cha mpunga.Maendeleo si makubwa kiasi cha kufananisha na miji ambaypo angalau ina miundo mbinu fulani lakini jitihada zipo kwani wananchi wake wamekuwa wakajituma katika shughuli za kujiletea maendeleo kuliko kusubiri serikali,Pia raia wake katika kijiji hiki wanasaka elimu kwani walikuwa katika muungano wa kata yao katika ujenzi wa shule ya sekondari iliyopo katika kijiji cha chimate.Kubwa zaidi hapa ndipo Meli zinazofanya usafiri katika ziwa nyasa upande wa Tanzania ziliweka kuwa kituo cha mwisho na kurejea tena Itungi,lakini tokana na asbabu mbalimbali ikiwemo kina cha maji kituo hicho kikaondolewa na kuwekwa mbamba bay.hata hivyo mabaki ya majengo yake yanatumika kama sehemu ya mafunzo ya uvuvi kwa wakaazi wa eneo hilo na kuwa makao makuu ya vijiji vingine kwa shughuli za ukaguzi wa zana imara za uvuvi ambazo hazihatarishi maisha yao.Naam tuonane katika kijiji kingine na habari zaidi za vijiji nilivyoandika tutarejea ili kuona mambo yaliyopo maeneo ya NYASA na WATU wake.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako