October 21, 2007

Nyasa,habari,mseto na karibu njema

Naam leo nizungumzie jambo lamseto tu au kama habaro fulani tu ili tuendele na mambo ya ukanda huu.Ni maeneo ya ajabu sana kwani kuna baadhio ya maeneo yana kumbukumbu za vita baina ya wanyasa,wamatengo dhidi ya wangoni wavamizi hawa waliotoka nchi za kusini mwa afrika.kuna mapango yenye kusimuliwa na wazee wetu namna vita hivyo ilivyokuwa huku wanyasa wakipoana tokana na uwezo wao wa kuogelea hivyo walipozidiwa walikimbilia ndani ya maji.Tukumbuke wakati huo sialaha kubwa ilikuwa mishale,majambia,mapanga n.k lakini maadui waliweza kuopeshwa na silaha hizo.Maeneo haya yana mambo ambayo wakati mwingine hayajionyeshi kwa uwazi bali mpaka unapofanya uchunguzi na kuwahoji waliokula chumvi nyingi ndipo unaweza kupata habari motomoto za nyasa.Mfanao wenye asili ya wanyasa ni kundi kubwa ambalo limesambaa Malawi kwa kiasi kikubwa na lugha zao hushabiahiana hata asili ya majina yao.Nilibahatika kukutana na "mkoloni" mmoja hivi{mzungu} yeye ameweka maisha yake katika mji wa Mbamba Bay ambao ni kama kitovu kikuu ca maeneo haya achilia mbali Liuli na Lituhi au Lundu.Yeye anauwezo wa kuongea kiswahili fasaha kuzidi mzaliwa wa nchi yetu.anavutiwa na historia inayofungamana ya wanyasa,wangoni,wamatengo na wenyeji wengi wa malawi.Nyasa ina mambo mengi ya kumbukumbu ya taifa ambayo hayaandikwa.Mfano uwepo wa kituo cha Jando na unyago katika kijiji cha KILOSA ambapo majengo au eneo lake limehifadhiwa kwa ajili ya kumbukumbu za vizazi vijavyo.Tutaendelea polepole na mengine mengi,huu ni mwanzo tu na mengi ya mkoa wa Ruvuma hususani wilaya ya Mbinga tutajadili na kuyaweka pazuri.KARIBUNI NYASA.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako