December 26, 2007

NYASA;krisimasi,furaha,burudani na uhai wa wanyasa

Naam nilikuwa katika kijiji lundu kujionea burudani na furaha ya kusherehekea krisimasi ambayo bila shaka ni ni wakati wa wazazi,watoto,ndugu,jamaa na marafiki kujumuika katika simu hii ambayo hupatika mara moja kwa mwaka pale wakristo wanapokumbuka siku ya kuzaliwa Yesu krsito.Ni kawaida yangu kutulia katika siku za aina hii lakini nilishindwa kutulia ilibidi nijiulize nitaandika nini nikifika Mbinga asubuhi hii maana wenzenu mambo ya mtandao haya mapaka tusafiri kidogo ndipo tuandika katika blogu namna hii.Naam nimekuwa katika mzunguko mkali wa siku hiyo ya krisimasi ili kujionea burudani,furaha na uhai wa wanyasa katika maisha yao lakini nikaona sisi bina damu tuna kawaida ya kusahau matatizo siku kama hizi maana nikaona hata wale maadui wanakumbatiana kwa wema kuikumbuka siku ya mwokozi wao.Asubuhi hii ikawa balaa maana kuna jamaa alikwenda kuvua samaki hivyo nimemwahidi kwenda kupata japo kitoweo kumbe mwenzie naondoka zangu kusafisha macho mjini Mbinga angalu nione wamjini wanaburudika vipi hata siku kama ya leo.Nimekuta watu wamelewa,wanatapika hovyo,mara mafumanizi na uchafu kibao na nikaambiwa na mwenyeji wangu kuwa kuna mwanamke mmoja kafumaniwa na kijana wa kinyasa mtaa wa Flastoo.Hapo nikaguna huyu mnyasa yuko hai kweli? nikambiwa wanyasa wana mbio katika hatari maana jamaa kachia mbio kuokoa uhai wake....si unajua fumanizi za wenyemali.Sasa badala ya furaha,burudani na uhai wa wanyasa jamaa kasafiri hadi hapa mjini halafu anajiona wa leoleo na vihela mbuzi vyake akakoswakoswa na wenye uchu wa kutanya uhai wa wenzie na bahati yake kwa wanyasa kuwa mbio kali ni sifa moja ya uhai wako nyakati za hatari.Ndiyo wanyasa wa mbio za ajabu mithiri ya swali mbugani.Lakini baada ya kuandika hapa mjini katika blogu hii natarajia niende zangu kijiji maana jamaa akija nadhani ataghadhibika kwani nimeahidi kununua samaki wake ili apate pesa za kuburudika na furaha ya familia maana jana kalewa mipombe halafu kasahau familia lakini kaahidi leo ni burudani ya familia yote sasa watoto wako juu kwelikweli maana wanataka kuonyesha uwezo wao wa kuburudika. mapumziko mema,watu wote wa ughaibuni maana najiuliza hivi Ndesanjo anasoma habari za wanyasa kweli?vipi kaka Jeff,DaMija,Michuzi na kitoto pale London?sijui lakini polepole,KARIBUNI NYASA!

No comments:

Post a Comment

Maoni yako