February 21, 2008

LUNDU na LUNDO ni vijiji tofauti

Lundu ni kijiji kilichopo ukanda wa nyasa katika kata ya Mbaha,na kwa urahisi unaweza kufika kijiji hiki kwa kupitia Lituhi ama toka Mbinga kwa kupitia Ngumbo na maeneo yanayoweza kukurahisishia usafiri hususani wa meli kwa kupitia Mbamba bay au Itungi-kyela na kushuka bandari ya LUNDU.Ni kijiji ambacho Mimi nimetokea na kuishia mpaka sasa.LUNDO ni kijiji kilichopo kilometa chache sana toka mji wa Mbamba bay au kutoka mji wa Liuli.Ni kijiji ambacho kina sekondari na kumbukumbu ya kutunza wakimbizi wa Msumbiji kabla ya kurejeshwa mwaka 1995 baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kwisha ambavyo RENAMO walipigana na wenzao wa FRELIMO.Ingawa vijiji hivi wilaya ya Mbinga lakini vinatofautiana na kwa herufi za mwisho tu,na Lundu ni kijiji kilichopo na uhusiano na vijiji vya mbali kidogo vya Manda.Sifa na tofauti yake ni kwamba Lundu ni bandari ndogo katika shughuli za usafiri katika ziwa nyasa na Lundo ni kumbukumbu ya wakimbizi,sekondari na mashamba makubwa ya kilomo cha mpunga na hata Rais Jakaya analijua hilo.

1 comment:

  1. jamani shibe mwana malevya kulala na njaa nyasa kupenda au uwongo wenzangu

    ReplyDelete

Maoni yako