March 17, 2008

Nyasa na Mambo ya nyakati hizi

Kipindi hiki ni cha masika kwa wanyasa wengi kwani hutumia kwa shughuli za kilimo na uvuvi pia.Ni kipindi cha wavuvi kufanya kazi mbili yaani uvuvi na kilimo kwani hii husadia kujipatia kitoweo na mlo wa uhakika katika maisha yao.Kwa kawaida hapa nyasa tunalima mihogo,mpunga na mazao mwengine pia hata viazi hupatikana.Sasa wakati huu kuna aina ya samaki ambao kupatikana kipindi kingine ni adimu hivyo watu wako makini na hilo kwani ndilo linalowafanya wawepo hapa nyasa.Juzi hapa nilikuwa kijiji cha Mbaha nikakutana na watu wanatoka mashambani na kujimwaga ziwani huku wakiwa na majembe yao.Nikwauliza vipi jamani majembe mpaka ziwani wakaniambia ni bora kuunganisha tu pale unapotoka shambani kwani ukienda nyumbani mwili huchoka hivyo kazi inendelea.Hawa jamaa walinishangaza kwani kazi waliyofanya ni ngumu lakini wanakwenda kutoa nyavu zao walizotega ili kupata mlo,yaani kwa mnyasa bila samaki hawezi kukamilisha siku.Kuna jamaa mmoja hapa alinidokeza kwamba imani juu ya samaki ni kubwa ndiyo maana wanyasa hawana tatizo la kuongezewa damu kwani wanakula mboga za majani za asili na aina ya mapishi yao ni ya asili hivyo hayana hata kemikali zozote.Mwingine leo kaniambia hata kama wengine watabeza lakini hawaondoki nyasa hata kidogo.Halafu kuna jamaa ananiuliza hapa pembeni hiki ninachoandika,wakati anayo kompyuta yake wala haoni haya kuchungulia maandiko haya ya wanyasa,nimemkasirikia halafu namtazama kama samaki wanaojificha kwenye makoro makubwa,unawajua,ni mandongo.Yani haachi eeeh wewe jamaani vipi.Kumbe mmatengo

1 comment:

  1. mabo ya nykati ni mhumi sana kwani hueleza mambo yajayo kwa watu wengi

    ReplyDelete

Maoni yako