June 08, 2008

Janeti na Hamu ya Njika kusoma Blogu

Kuna jamaa hapa ananitazmasana sijui anashangaa nini.Labda tokana na kasi yangu ya kundika hapa bloguni.Lakini namfahamu sana huyu jamaa unajua jina lake nani?nimemkumbuka umeona jina la mtu mwenye hamu ya kublogu hapo juu?Ndiye huyo anaitwa Njika Clara ni ndugu yangu,basi leo nimemnogesha kublogu nakwambia amebaki kutola mate tu jinsi anavyonogea mmm halafu ananiudhi amshika shavu sijui anamanaa gani.Najua hapa akitoka hapa nyasa anahamu ya kwenda kumtembelea shangazi yake mtaa fulani najua anafuata samaki tu si unajua wanyasa kitoweo chao.uache hilo,kuna mwingine tazama jina lake mwanzo "Janeti" basi jana kasoma blogu ya nyasa hii mpaka akakasirika kisa wivu eti wanyasa wanajidai na blogu yao.Haa nikammwambia mbona nawe mnyasa?akaniambia haijalishi ila wanyasa tunaringia kublogu.Lakini akamaliza kwamba hata yeye Blogu hii inamhusu shauri ye mnyasa.Basi huyu Njika anasoma blogu hii naona mpaka njaa inamuuma sijui hajala..ebu mtazama huyo hapo pembeni anakunja ndita sababu gani?.Mmmmm timu yetu ya taifaimefungwa na CapeVerde bao moja jana mmmm inauma sana

No comments:

Post a Comment

Maoni yako