
Mi naihusudu bwana, si unaona ilivyojipangia mikakati? Halafu siku ile pale ulinizome ilipofungwa na MTL Wanderers, we haya tu bwana...... eti akacheka kwa mikogo ati. Ngoja na Mbinga magharibi sasa kuna mchakato wa kuifanya Mbinga magharibi kuwa wilaya rasmi.
Najua watagombania kati ya LIULI, MBAMB BAY na LITUHI wapi waweke makao makuu. Maana hata wiki jana nilikuwa na rafiki yangu kipenzi Raymond Ndomba..... kijana mcheza soka ninayemshangaa.... anaweza kucheza namba yoyote utakayo mpanga uwanjani tangu golikipa hadi winga wa kushoto....lakini shule imemfanya awekeze huko.......na sasa anawania kupata nini kile kinaitwa MASTERS. Huyu alinidokeza kuwa wazo la makao makuu la Wilaya Mbinga magharibi litakuwa shubiri maana kila mji unapenda iwe hivyo...nadhani LIULI wanaweza kupendelewa eti ni katikati ya wilaya yenyewe.
Tuache hayo, twende katika samaki wetu hawa watamu sana na adhimu duniani. Ni nyasa bwana wapi kwingineko utakako pata samaki hawa, ha ha ha ha raha sana. KARIBUNI NYASA, KARIBUNI SANA lakini neno langu siyo sheria au vipi waungwana? Pendaneni kwa mpango!
Somba, somba, mwenge na ugali wa mayao kunoga kweli mpaka utajiuma vidole. Umenikumbusha sana chakula changu. Nakumbuka mwaka juzi nilipokuwa nyumbani nilitembelea kijiji nilichozaliwa sio kingine tena ni LUNDO mjombwa wangu wa vile anajua jinsi nilivyo mroho wa samaki akaenda ziwani na akaja na samaki MAGEGE. Basi naishia hapa....
ReplyDelete