January 07, 2013

MUNGU ALIANZA UJASIRIAMALI TANGU KITAMBO NA WANAOTAKA KUFANIKIWA 2013


Na Albert Nyaluke Sanga, Iringa
Tangu siku Mungu anamuumba Adam, alimuumba kijasiriamali na alimwagiza akawe mjasiriamali. Unashangaa? Soma Biblia yako kitabu cha Mwanzo. Twende polepole utaelewa tu. Unajua neno Ujasiriamali/biashara linamaanisha nini? Ngoja nikujulishe. Biashara/Ujasiriamali inamaanisha, ubunifu wa uzalishaji (production), uongezaji wa ulichobuni ama kuzalisha (multiplication), usambazaji (distribution) na kutawala soko (dominion over market and ideas/innovation). Umeelewa enhee? Sasa turudi kwa Adamu. 
Mungu alipowaumba Adamu & Eva aliwambia hivi, "Enendeni mkazaliane, mkaongezeke, mkaijaze nchi na kutawala vitu vyote". Wengi wanaposoma Biblia huwa wanadhani kuzaana ni "kupata watoto pekee"; lakini ukisoma English Bible (KJV) ina-highlight vizuri neno hili kuzaana; "Fruitful". Kuwa "Fruitful" inamaana "kutumia materials/rasilimali/akili ulizonazo ili kupata ama kutengeneza kitu chenye thamani zaidi", kwa lugha nyepesi ni 'uzalishaji (production). Tunaenda pamoja? 
Hebu turudi kwenye yale maagizo ya kijasiriamali ambayo Mungu aliwapa akina Adam na mkewe, "Enendeni mkawe wazalishaji (fruitful/production), mnachozalisha kikaongezeke (multiplication), mnachokiongeza mhakikishe kinajaa dunia yote (distribution), hivyo mnavyovijaza dunia yote hakikisheni mnaweza kuvitawala (dominion over market and ideas)" 
Haaa! haaa! Nimekupoteza? Usijali! Rudia kusoma pole pole, afu ujitahidi kuwa unasoma Biblia kwa tafakari; utaelewa! Sasa yoooote haya namaanisha nini? Ni hivi: Mungu alimuumba kila mwanadamu kufikiria na kuishi kijasiriamali. Si lazima kufanya ujasiriamali wa kupata fedha, lakini mtazamo wa kiujasiriamali utakupa ushindi wa maisha ya Kimungu wakati wote. ~SmartMind~

KWA WALE TU! WANAOTAKA KUFANIKIWA 2013!
Nimekuwa nikieleza mara nyingi kuwa; mafanikio katika maisha hayaji kwa lelemama! Iwe unataka uchumi mzuri, ajira nzuri, mke ama mume mzuri; ni lazima jasho likutoke. Hata hivyo sote tunatambua kuwa mafanikio yanaanza katika ufahamu wako. Namna unavyowaza inaamua namna unavyotenda, namna unavyotenda inadhihirika katika maisha uliyonayo hata sasa. Huwezi kudanganya! Tukiyatazama maisha yako, "automatically" tunajua mfumo wa mawazo na fikra zako. 
JE WAJUA? Kuwa mfumo wa mawazo yako ni matokeo ya mambo unayoyaingiza katika ubongo wako kupitia kusikia, kutazama na kusoma? Kama umenasa kwenye uhaba wa kifedha basi utambue kuwa ubongo wako umejaza "matango mwitu" kuhusu fedha, kama mapenzi yanakutesa, uwe na uhakika kuwa fikra zako zimejaa "upupu" kuhusu unavyotakiwa kubehave kwenye mapenzi. 
Soko kuu la Songea mjini
Kama upo kwenye ajira "isiyolipa" ama hujapata "japo pa kujishikiza"; basi ujue mtazamo wako kuhusu ajira na maisha "umejaa matope"!
UNAJIKWAMUAJE KUTOKA HAPO? Jibu ni rahisi! BADILISHA MTAZAMO NA NAMNA UNAVYOFIKIRI! Utabadilishaje? Jifunze kutoka kwa waliofanikiwa kufika unapotaka kwenda, Soma vitabu vinavyojenga fikra na mitazamo chanya, ama fanya yote mawili. Mimi ngoja nikusaidie moja: NITAKUPA VITABU VYA AINA HIYO! Kwa mwaka mzima nitakuwa nikituma vitabu viwili (2) kila mwezi kupitia baruabebe(email) vilivyopo katika mfumo wa pdf; kwenda kwa marafiki wote waliopanga kufanikiwa 2013. Kwa kuanza na mwezi huu Januari nitatuma vitabu vifuatavyo: 1) THE SCIENCE OF GETTING RICHER 2) COACH YOURSELF TO MAXIMUM EMOTIONAL INTELLIGENCE. Kwa rafiki unayehitaji ninapenda unijulishe email yako hapa (ama inbox) kisha utapokea vitabu hivi. KAMA UNATAKA KUFANIKIWA, KUJIFUNZA HAKUKWEPEKI. ~SmartMind~

1 comment:

Maoni yako