June 24, 2013

RASIMU YA KATIBA MPYA, KUNA MASWALI YANATAKIWA KIJIBIWA


TANZANIA: 
Tumeelekeza nguvu na akili zetu kwenye uchaguzi mkuu 2015. 
Mpaka sasa hatuna mwafaka wa uchaguzi huo kwamba tutumie Katiba ipi, ya zamani ama hii iliyoko kwenye hatua ya Rasimu itakapokamilika. 

Tukumbuke wanachama wa shirikisho la Muungano; Zanzibar na Tanganyika watahitaji kutunga Katiba zao. Zanzibar wanayo Katiba yao, je watakubali kutunga katiba mpya? 

Je, mwanachama mwingine Tanganyika atakubali kuwa yeye ni Tanzania Bara halafu kwa wakati huo huo akiwa mwanachama wa shirikisho akatumia Katiba ya Tanganyika? 

Ni Tanganyika ama Tanzania Bara? Kama wewe unasoma RASIMU YA KATIBA, hakika kuna mengi unapaswa kuyatafakari kwa maslahi ya nchi. 

Nadhani tuitishe uchaguzi mkuu mwaka 2017, tujipange kwa kuwekeza kwenye MUDA kukamilisha zoezi hili, sio jepesi hili, halihitaji 'fasta fasta'.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako