January 29, 2014

WILAYA YA NYASA YABEBA MAJUKUMU YAKE


Mwandishi Wetu, Mamba Bay
BAADA ya kutegemea shughuli zake kufanyika wilayani Mbinga, hatimaye sasa wilaya ya Nyasa imeanza kushughulikia majukumu yake.
Miongoni mwa majukumu hayo ni utumishi, ardhi, na mengine yanayohusu maendeleo. Hapa ni sehemu ya majukumu yaliyoanza kufanyiwa kazi;-
Tambua kuwa Wilaya yako mpya inatoa huduma karibu 99%. Idara zote zipo sasa Nyasa.
Vyeti vya kuzaliwa vinapatikana kwa bei nafuu. Wakubwa - Tsh.10000, na watoto wadogo Tsh.5000.
Leseni za biashara zipo. Uhamisho wa wanafunzi na wafanyakazi unashughulikiwa hapa hapa Wilayani Nyasa. Vibali navyo vipo vya kila aina.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa, mwanzoni alikuwa wa Halmashauri ya Mbinga.

1 comment:

  1. Ni wakati bora kabisa huu kwani wilaya ilitakiwa kitambo sana

    ReplyDelete

Maoni yako