June 27, 2014

NGUZO ZA UMEME ZAPELEKWA NYASA



Na Egbart Jeremy,Mbamba Bay
 
Hatimaye shehena ya kwanza ya Nguzo za Umeme iliwasilishwa Juni 20 mjini Mbambabay ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kusambaza umeme vijijini pamoja na wilaya Nyasa ambayo ni mpya.

Kwa mujibu wa msimamizi wa mradi huo, Bwana Hugo alisema kuwa licha ya ubovu wa barabara lakini walifanikwia kuwasilisha shehena hiyo.

Alisema kuwa gari lilikuwa linakwama mara kwa mara ana kutokana na vifusi vilivyowekwa ikiwa ni jitihada kubwa zilizofanywa na Mbunge, John Komba kuwasiliana na maofisa wa TANROD mkoa wa Ruvuma wamwamuru mkandarasi kusambaza vifusi.

Kwa mujibu wa msimamizi wa mradi huo, alisema juhudi za kupeleka umeme wilaya ya Nyasa zimetokana na na  mbunge huyo. Mradi huo ulitakiwa kuanzia wilaya ya Tunduru lakini Mbunge Komba amejenga hoja hadi mpango ukabadilishwa kuanzia wilaya ya Nyasa

No comments:

Post a Comment

Maoni yako