1 Kijana mimi
rijali, ninaishi Afrika,
Nipo hapa kwa
asili, siwezi kubadilika,
Jambo hili
nakubali, kichwani halitatoka,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Juzi nilipata
shida, tatizo langu kusema,
Nilimueleza
dada, akamueleza mama,
Nilingoja kwa
muda, na kichwa kikiniuma,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Dada na mama
wakaja, ili kuijua homa,
Mahoma
nikayataja, yakamshangaza mama,
Madakitari
kataja, basi homa itakoma,
Madakitari ni
wengi, waniweka niiapanda.
Kwa mchungaji
tukaja, yasemwa ni dakitari,
Mahoma
nikayataja, asema nina kiburi,
Zikanijaa na
hoja, nikawa natafakari,
Mdakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Mahoma ninayo
mengi, kwanza ni maisha bora,
Ninataka pesa
nyingi, ninaitaka ajira,
Niinunue na
rangi, nikajifunze kuchora,
Madakitari ni
wengi, waniacha niapanda.
Homa za vijana
wengi, Afrika nako Asia,
Matarajio
nimengi, hayajapata tulia,
Ndoto zimekuwa
nyingi, ndani ya hii dunia,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Msikie mchungaji,
na dawa yake jamani,
Anautaka ulaji,
homa hizi maishani,
Anautaka na
uji, nipeleke kanisani,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Anasema
niokoke, homa zote zitaisha,
Kisha hela
nimtoe, ndio malipo ya dawa,
Kesho yake
nikamwone, vidonge kuniongeza,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Homa zilezile
tena, kwa dakitari mwingine,
Tena bado
sijaoa, anipatia mawenge,
Asema jini
mahaba, hataki mie nioe,
Madakitari ni
wengi, waniweka niapanda.
Kukosa kwangu
ajira, kijana mie Afrika,
Asema jini Makata, anazuia ajira,
Nimesikiliza
sana, nimeishia kununa,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Mpiga tunguri
nae, anasema nimerogwa,
Tena homa
zilezile, kweli amelikoroga,
Na kwenye ungo
tupae, nionyeshwe aloroga,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Homa sijapata dawa,
kwa madakitari wote,
Homa ya
kuajiriwa, dawaye hakuna mwote,
Homa ya
kutajirika, hainayo dawa kote,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Kwa dakitari
mwingine, asema nina mapepo,
Ninataka
niwaone, mapepo hawa walipo,
Hahitaji
niwaone, eti ni kama upepo,
Madakitari ni
wengi, waniacha njiapanda.
Mwote
nilimopitia, sumuni nimelipia,
Dawa
wameshaikosa, wamebaki kujificha,
Nimewajaribu
sana, na hawajafurukuta.
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Siwadharau kabisa,
madakitari murua,
Imanini wajitosa,
dawa hawajaijua,
Kwa nini
wameikosa, dawa kuigundua,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Afrika funguka
sasa, tuchape kazi jamani,
Kujifunza nako
ruksa, tujinasue tunduni,
Imani zetu
kabisa, zisituchoshe jamani,
Madakitari ni
wengi, waniweka njiapanda.
Mungu
hatatushushia, tusipofanya bidii,
Shughuli
kukazania, na bidii haiozi,
Mwanatunguri
tulia, si kila kitu uchawi,
Madakitari ni wengi,
waniweka njiapanda.
Na Kizito Mpangala
Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
ReplyDeleteMwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ndiyo tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com