November 15, 2017

KIFAHAMU KISIWA CHA LUNDO KILICHOPO ZIWA NYASA


HISTORIA ya kivutio cha utalii, kisiwa cha Lundo kilichopo Ziwa Nyasa, inaonesha kuwa kisiwa hicho kina ukubwa za hekta 20 kimepewa jina la Lundo kwa sababu watu wa kwanza waliovuka kisiwa hicho kwenda ng’ambo ya pili walifikia kijiji cha Lundo.

Kisiwa hicho tangu zamani kilikuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa vijiji vya Lundo,Ngindo na Chinula kwa sababu wakati wa vita ya Majimaji vilivyotokea kati ya mwaka 1905 hadi 1907 watu walikuwa wanakimbilia katika kisiwa hicho ambacho kina maeneo ya maficho.

Baada ya vita ya Majimaji kuanzia mwaka 1908 kisiwa hiki kilitumika na wakoloni wa kijerumani kuwahifadhi watu waliopata ulemavu kutokana na ugonjwa wa ukoma ambao baada ya uhuru walihamishiwa katika makazi ya Ngehe wilayani Nyasa. Serikali imependekeza visiwa vya Lundo na Mbamba Bay kuwa hifadhi za wanyamapori.

Visiwa hivyo vitakuwa ni hifadhi ya pekee ya wanyamapori pamoja na samaki wa mapambo wanaozaliana katika visiwa hivyo ndani ya ziwa Nyasa hivyo kuvutia watalii kufika kusini na kutekeleza Sera ya nchi ya kufungua biashara ya utalii Kusini.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako