November 15, 2017

MAYANGA,UMEKUBALI YAISHE KWA MOLLEL?


Na Honorius Mpangala
ORGENESS Mollel ni moja ya vijana wa kitanzania wanaocheza soka Ulaya. Ni katika klabu ya Famalecao ya Ureno ndiko anakocheza kijana huyu Wa kitanzania. Kwa kipindi amacho kocha Mkuu Wa taifa Stars Salum Mayanga amekuwa muumini Wa kuwapa nafasi wachezaji wanaocheza soka nje ya Tanzania. Jambo afanyalo Kocha huyu unaweza kusema kama ni chachu ya kuthamini uwezo Wa wachezaji hao wanaowakilisha taifa letu nje ya mipaka ya Tanzania. 


Kwa Mara ya kwanza kocha wa Taifa stars anamjumuisha Mollel nilijikuta natamani kufahamu mengi toka kwake. Hamu hiyo ilikuja baada ya kufahamika hatoweza kujiunga na timu kutokana na kibali chake anachotumia kuto mruhusu kutoka na kuingia kwa kutumia kibali hicho. Niliifuatilia hati ya kuzaliwa ya Mollel na kugundua anatumia hati ya Tanzania na kumwonyesha ana umri Wa miaka kumi na tisa. Nilikuja kushangazwa zaidi alipoitwa kwa Mara nyingine na kushindwa kuungana na wenzake kwa Mara ya pili. 

Waweza kusema kila mmoja na anabahati yake kama ilivyo kwa Mollel. Bahati ya Mollel yawzekana wako watu kama Emily Mgeta kule Ujerumani wanaitazama kwa jicho la matamanio sana. Sio kama kila mmoja ataweza kuushawishi uongozi Wa benchi la ufundi liweze kukujumuisha katika timu ya taifa. Kinachofanyika ni kufuatiliwa kwa mchezaji ndiko kunakoweza kutoa majibu kuwa maendeleo yake yakoje ili aweze kuitwa.


Iliwahi kutokea kwa Adam Nditi ambaye mwaka 2013 alikuwa katika timu ya vijana ya Chelsea akikumbana vikumbo na Paul Pogba,Nathan Ake,Gael kakuta,Adnan Januzaj na vijana wengine Wa vilabu vya ligi kuu nchini Uingereza. Wakati matamanio ya wapenzi wengi walitamani kumwona katika jezi ya timu ya taifa Nditi aliyeyuka kama barafu katika maji ya uvuguvugu. Hadi leo hakuna kocha anayetamani hata kufahamu Nditi yuko wapi kwa sasa. Miongoni mwa mambo yaliyopelekea kuachana na kijana huyo ilikuwa baada ya kubainika hati ya kusafiria anayotumia inamtambulisha kama Mwingereza na sio Manzania tena kama ilivyotarajiwa na wengi.

Nafasi aliyoitoa Mayanga kwa Mollel inaweza kuwatazama wengine. kwasababu hadi sasa ni kama Klabu yake ya famalecao haitoi ushirikiano na Tanzania pale wanapomhitaji kijana huyo anapoitwa timu ya taifa.

Nchini Austria kuna kijana Wa kitanzania ambaye ana matamanio sana ya kuja kuitumikia nchi yake. Ni Thomas Lema ambaye ana umri Wa miaka 17 tu. Amekuwa na wakati mzuri sana katika klabu Yale kwani licha ya kuwa na hati ya kusafiria ya Austria lakini kwa umri wake hazuiliwi kuchagua timu anayotaka kuichezea.Iliwahi kutokea kwa Fredrick Kanoute,Karim Zian na wengine ambao waliwahi kuichezea timu ya taifa ya Ufaransa lakini baadaye wakaamua kuchagua kuichezea timu ambayo ni ya Asili yao.Haikushangaza kumwona Kanoute akikipiga katika nchi ya Mali na Karim Ziani akikipiga Algeria.

Ni wakati Wa kuwafuatilia vijana wote wenye hati za kusafiria za kitanzania. Katika nchi ya Afrika kusini kuna vijana kama Jaffary Kapolo Wa Real Kings daraja la kwanza. Ni moja ya vijana ambao naamini kama watapewa nafasi ya kujumuishwa tu katika kikosi itakuwa ni 'credit' kwa timu yake na yeye mwenyewe nankuaminika katika klabu.

Ujerumani licha ya kuwepo kwa Emily Mgeta ambaye hucheza nafasi ya ulinzi daraja la tano katika klabu Freund Spiel Lauffen pia kuna Mtanzania mwingine aitwaye Charles Mishetto aliyeko katika klabu ya daraja la nne inayoitwa S.P.B.G 1914 Selbitz. Yawezekana kama tumeegemea katika kuwafahamu Simon msuva na wenzake ambao kiuchezaji wameanzia nyumbani Tanzania. Lakini tujaribu kuwafuatilia vijana wetu yawezekama huko waliko vilabu yao vikatamani kuona wakiitwa timu zao za taifa.

Hamis Mroki ni mmoja ya vijana ambao Kocha Jamhuri kihwelo aliwahi kuwajumuisha katika kikosi cha taifa kwa vijana Wa umri Wa chini ya miaka 23. Mroki ni mchezaji Wa ligi daraja la pili nchini Thailand akiichezea klabu ya Kabin United. Huyu tayari alikuwa na mwanzo mzuri ambao kwani tayari alishavaa jezi ya taifa katika u23 kwenye mechi dhidi ya Kameruni. 

Yawezekana kila mmoja huandikiwa njia za kufanikiwa lakini ufuatiaji kwa vijana wa kitanzania ni jambo muhimu kwetu. Haiwezi kuwa na faida yoyote kama tutaishia kujisifu kwa kumwona Saidi Mhando akija kucheza ligi kuu Italia toka daraja alilokuwa sasa seria B na klabu yake ya Brescia Calcio. 

Maana yawezekana hata wao huweza kufikia maamuzi kama yakiyokwisha fanyika kwa baadhi ya wachezaji kuzikacha nchi zao na kuchezea mataifa mengine ambayo yamewainua kimpira. Ilitokea hivyo  kwa Edson De Souza 'Deco' na mlinzi matata Pepe ambao waliichezea Ureno badala ya Brazil. 

Labda nikujuze jambo moja kuna kijana mmoja wa kitanzania ambaye hufahamika kwaji moja LA Faheem alifanikiwa kusainishwa na klabu ya Sporting Lisbon ya vijana akiwa na miaka 19. Ni kijana wa kitanzana lakini inasemekana tayari wareno wamempa uraia huku wazazi wa kiana huyo wakiwa Watanzania. Tuna kila sababu ya kuwalinda vijana wetu Kwa kuwajumuisha katika kikosi cha timu ya taifa.Ni vyema mwalimu Wa timu ya taifa akajaribu kufuatilia hata TFF kutazama ni wachezaji gani ambo wako nje na wamepewa vibali vya kucheza huko na shirikisho ili kuweza kuleta urahisi Wa kuwafuatilia.

Kila mpenzi Wa soka nchini Tanzania atakuwa na kumbukumbu ya mchezo Wa Yanga dhidi ya Zanaco. Kijana Wa kitanzania Ayoub Lyanga ambaye ni mdogo Wa Danny Lyanga aliingia akitokea benchi na kushirikia katika mchezo huo Wa ligi ya mabingwa. Lyanga ni kijana aliyecheza katika klabu ya African sports kabla hajaenda kufanya majaribio katika klabu hiyo na kufanikiwa kusajiliwa na Zanaco. Moja ya mambo yaliyo nishangaza ni pale nilipotembelea tivuti ya klabu ya Zanaco na kuona katika orodha ya Wachezaji wao Lyanga kawekewa Bendera ya Zambia ikimtambulisha kama ni raia wa Zambia.Suala la kufuatilia maendeleo ya mchezaji lazima liwe kwa mgawanyo Wa majukumu ili kuleta ufanisi wa uteuzi Wa timu taifa.

Tujaribu kutoa nafasi kwa watu wengine zaidi na zaidi ili kuonyesha tunahazina kubwa ya wachezaji walioko nje. Itafurahisha na kuwafanya wapenzi Wa soka wajivunie uwepo Wa vijana kama George Mtemahanji anayekipiga daraja la pili katika klabu ya Modena fc pale Italia,Golikipa Abasi Pira,Hassan Sembi ambao kwa namna moja au nyingine wanaweza kutoa changamoto kwa wachezaji wanaocheza ligi ya ndani.

Wakiwa wananolewa na Milutin Sredojovic Micho,timu ya taifa ya Uganda waliamua kumwachia fungu la pesa kama nauli ili kuweza kusaka wachezaji wenye asili ya uganda na kuwatambua na hatimaye kujumuishwa timu ya taifa. Michu alifika hadi katika nchi kama Lebanon akawakuta wachezaji Wa Uganda na hata katika taifa la Vietnam na wachezaji wake walikuja kuwa msaada Wa timu ya Uganda hadi akafuzu kucheza Afcon pale Gabon. 

Hata Siku moja daraja la nne katika nchi ya Ujerumani haiwezi kufanana kiuendeshaji Wa klabu Sawa na ile klabu ya ligi kuu Tanzania. Miundombinu hadi utawala lazima vitakuwa tofauti kwasababu wenzetu wanatambua umuhimu Wa madaraja hayo kwani ni chachu ya kuwapata wachezaji wazuri.

Kama famalecao hawakutoa ushirikiano kwa Tanzania ili kumtumia Orgeness Mollel katika timu ya taifa. Ni nafasi sasa kwa vijana wengine kutoka nje kuna kuitumikia nchi yao. Nimefurahishwa na Kujumuishwa kwa Yohana Nkomola pamoja na Dickson Job vijana hawa Wa timu ya vijana wamenifanya nikumbuke nyakati ambazo Kocha Mbrazil Marcio Maximo alipokuwa akiwajumuisha Jerry Tegete na Kiggy Makasi. Akaja pia kuwa na utaratibu Wa kuwajumuisha Himid Mao ,Omega Seme na Thomas Ulimwengu. Kuwajumuisha vijana hao huleta faida baada kwa taifa kwani tumeona kwa Tegete,ulimwengu na Himid walivyokuja kulisaidia Taifa hili kwa vipindi tofauti.

Watanzania waonapo vijana kama Abdul Mohammed toka Tusker na Hamis Abdallaha wakijiunga taifa stars kwa kuwasili uwanja Wa ndege wa Mwalimu Julius K Nuerere inatia hamasa. Hata wachezaji wenyewe wanaona sasa ile thamani yetu ya kucheza nje ya mipaka ya nchi yetu inaonekana. Kila la kheri Mayanga katika maandalizi yako dhidi ya Benin. Watanzani wote wako pamoja nanyi katika kuwaombea na kuwatakiwa mambo mazuri.

0628994409

No comments:

Post a Comment

Maoni yako