December 30, 2017

DALILI ZA UWEPO WA MAFUTA BONDE LA RUHUHU

NA MWANDISHI WETU, SONGEA
SASA tunahesabu saa kadhaa zimebaki kuelekea Tamasha kubwa la aina yake la utalii na uwekezaji katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma .Kulingana na taarifa za uongozi wa wilaya ya Nyasa tamasha hilo linatarajia kuanza Januari Mosi 2018 na kilele chake ni Januari 6,2018 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa.
Tamasha hilo ambalo sasa litakuwa linafanyika kila mwaka limelenga kuvitangaza vivutio vya utalii na uwekezaji vilivyopo katika wilaya ya Nyasa ili vitambulike na kuvutia wawekezaji wa ndani na nje.
Tukiendelea kuviibua vivutio hivyo ni taarifa za uwepo wa dalili za mafuta katika bonde la Ruhuhu.Bonde la Ruhuhu mwambao mwa ziwa Nyasa Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa maeneo ambayo Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) imetaja kuwa yana miamba tabaka ambayo inaweza kutoa mafuta ya petroli na kwamba utafiti wa kukusanya data katika bonde hilo bado unaendelea.
 
Dalili za Kupatikana kwa mafuta Tanzania ni ishara ya kukua kwa uchumi kimataifa.Kutokana na dalili hizo zinazotia moyo, ni lazima nchi tajiri zenye Kampuni za kimataifa za utafiti na uchimbaji wa mafuta zifike katika maeneo yenye dalili za uwepo wa mafuta kama Bonde la Ruhuhu ili kuhakikisha mafuta hayo yanapatikana.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako