October 28, 2008

unanipenda?? unanitega?? Je hivi utaweza??

ukinipenda haya utaweza? au unanitega kwamba unanipenda? aaa karibuni sana yaani bado tupo tupo sana nyasa, bado tupo tupo kwanza.

usafiri upo usihofu

tafadhali ukiwa na njaa kali toa taarifa

October 25, 2008

raha+utamu+upendo= nyasa

karibuni lakini wale walevi hatuwataki dada Yasinta na mwenzake kaka Simoni. sharti mje mnywe komono na pombe zote za huku lakini hizo za mujini hatuzitaki

karibuni Chinula jamani

yaani raha sana karibuni. WEKEZA SASA MKOA WA RUVUMA USINGOJE

vijana wapya Jamani wapeni moyo.

Inaonekana kama nimekuwa mvivu kuhusu blogu siku hizi, lakini amini nawaambia siyo ila mambo ya hapa na pale kuvua samaki kuogelea sana mpaka machp yawe mekundu kama wale mabibi wa shinyanga halafu mseme uchawi.
Kuna vijana wapya nawasaka wamekuja katika blogu jamani. Kazi yangu nyingine sasa ni kuhamasisha kuanza blogu kwahiyo msione kimya. He waangalieni hawa vijana ambao nimefanikiwa kuendeleza kazi za Ndesanjo Macha

www.kambilisports.blogspot.com
www.shamakala.blogspot.com

wapeni moyo, nafanya juhudi kubwa kuhamasisha kuhusu blogu

October 22, 2008

mabusu + mabusu mpaka jela !!!!!!!!!!!

ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha jamani mambo juu ya mambo, kilichonifanya niblogu leo ni hiki ninachoandika achana na picha hizo hapo chini. hizo ni changamoto tu.nilikuwa mapumzikoni kwa juma moja lakini utamu wa kublogu bwana!!!!! wanaoacha na kupuuza shauri yao. basi nitawapatia ile santuri ya ETAT MAJOR ya wale vijana wa EXTRA MUSICA, nawapenda mno, au Kwaito ya MANDOZA ya zamani ile ya M DO or DIE. ha ha ha aha ha kazi kwenu mnaoacha kublogu.

DUBAI
Ingawa DUBAI imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika biashara yake ya utalii, ikiwa ni pamoja na kujenga hoteli za kadhaa za kitalii, imetuma ujumbe kote duniani kwamba pamoja na hamu yake ya kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea lakini haiko tayari kutelekeza utamaduni wake na sheria zake.
Ujumbe huo umetumwa kupitia kwa raia wawili wa Uingereza kwa kuhukumu kwenda jela miaka mitatu kwa kosa la kufanya mapenzi ufukweni. Michelle Palmer(36) na kidume chake Vince Acors(34) ambao siyo wanandoa. wali-BANJUKA huko ufukweni DUBAI, lakini kwa mujibu wa sheria za nchi hilo ni kosa. Jamaa walikuwa wakipigana MABUSU na inasemekana wali-BANJUKA ingawa wamekanusha KUBANJUANA huko wanatakiwa kwenda jela kosa lao kupigana mabusu.

CHANZO: gazeti makini la Raiamwema

hawa nao,wanatukatishia utamu au?

ONE LOVE yaleyale UKIMWI, eeeh mimisijui kama ukimwi nini, lakini unajua utamu ukikolea unaliza sana .......... la asali. eeeh jamani kama huji kufa tazam makaburi... lakini utamu nao...........

tamu+tamu= lakini chungu

harakati za kupiga vita ukimwi ndiyo hizo, sasa msifikirie hapa nyasa hatufanyi hivyo. Lakini swali kweny tuta utamu nao una ukakasi? mmm utamu utaliwa kwa maganda? ebo mnyasa vipi miye? oooh najiuliza tu