November 14, 2012

UHARIBIFU WA MAZINGIRA KIJIJI CHA NDUMBI??

 Zipo taarifa kwamba kampuni ya uchimbaji ya makaa ya mawe, TANCOOL katika kijiji cha NDUMBI kilichopo wilaya ya Nyasa imesababisha uharibu wa mazingira ndani ya kijiji hicho. Taarifa hizi zimeifikia mtandao huu wa KARIBUNI NYASA kupitia kwa mdau wetu Egbert Jeremy, ambaye yupo kwenye wilaya hiyo katika shughuli za utengenezaji wa Barabara na mradi mkubwa wa mami safi na salama wilayani humo. 
Kutokana na suala hili, mtandao huu unafuatilia kwa karibu taarifa za kampuni ya TANCOOL ili kubaini ukweli, na ikiwezekana kuishauri njia na umuhimu wa kulinda mazingira mbali ya mradi wao wa uwekezaji. Tuna imani wataelewa na watasaidia ulindwaji wa mazingira ya kijiji cha NDUMBI ambacho kama kitaharibiwa bila shaka yoyote kinaweza kuwa Jangwa kutokana na hali yake ya hewa kukosa uoto wa asili.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako