August 15, 2013

KOCHA ARSENAL ATUA SONGEA



Na Amon Mtega, Songea

JOPO la makocha kutoka timu ya Arsenal  ya  Uingereza wamewasili Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ukocha ya siku tano ya mpira wa miguu kwa walimu wa shule 40.

Akizungumza jana na waandishi wa habari, Mratibu wa mafunzo hayo  Selwin Ngonyani  alisema makocha hao kutoka timu ya Arsenal  Uingereza wamefika mkoani hapa kutoa mafunzo kwa lengo la kuibua vipaji kwenye shule hizo.

Alisema mafunzo hayo yanafanyika kutokana na ushirikiano uliyopo kati ya Shule ya Sekondari ya wasichana ya Peramiho na Mtakatifu Arouse  ya Uingereza ambayo ina urafiki na timu ya Arsenal.
  
“Mafunzo hayo yatatusaidia kuwafundisha vijana wetu  shuleni  kwa kuibua vipaji vyao ili na sisi kwa siku za baadae tuwe na wachezaji wazuri wenye viwango vya hali ya juu,” alisema.

Kwa upande wake mmoja wa makocha hao, Tony David   alisema Tanzania ni nchi yenye vijana wenye vipaji vya michezo hasa mpira wa miguu kwa kuwa wanafundishika na kuelewa haraka.


No comments:

Post a Comment

Maoni yako