October 14, 2017

KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE



Pichani ni Nyumba ya Mwalimu Nyerere iliyopo eneo la Magomeni ambayo kwa sasa ni makumbusho ya Taifa. 

Mwaka 1957 Mwalimu akiwa anafundisha shule ya Sekondari Pugu alikusanya mafao yake ya ualimu na akamwomba rafiki yake Mustafa Songambele amtafutie kiwanja katika maeneo hayo, naye akamtafutia kiwanja hicho kilichopo Magomeni, Mtaa wa Ifunda.

Enzi hizo Magomeni ndiyo ilikuwa kama Masaki ya sasa na Mwalimu alitaka kukaa mahali penye mazingira salama na ulinzi ili kuendelea na harakati za kulikomboa Taifa kutoka kwa Mkoloni wa Kiingereza. 

Lakini baadae Mwalimu kwa Moyo wa ajabu akaitoa nyumba yake mwenyewe aliyoijenga kwa jasho lake na mafao yake na kuikabidhi kwa Serikali ya Tanzania ili iwe Makumbusho ya Taifa kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo vikumbuke ni wapi tulipotoka na wapi tunaelekea.


Mwalimu wakati wa Uhai wake katika Ngazi ya Familia alikuwa Baba na Babu pia, angeweza kujilimbikizia yeye na familia yake Mali zote za Taifa lakini kwake Tanzania na Afrika nzima ilikuwa Zaidi ya Maisha yake binafsi na Familia.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako