October 13, 2017

TUACHANE NA DUNIA YA MICHONGO NA MADILI.


NA KIZITO MPANGALA
 
PICHANI ni duka la dawa za binadamu. Unaona limefungwa. Limefungwa kwa sababu maalumu kisheria. Tazama jinsi lilivyo, kwa nje hata utambulisho ya kwamba hili ndilo duka mojawapo miongoni mwa maduka ya dawa za binadamu lifahamikalo katika mtaa husika.

 Hatupo kwa ajili ya kuharibiana wasifu. Hatupo kwa ajili ya kubaniana michongo na madili. Hatupo kwa ajili ya kukatishana tamaa. Wakati ule nilipokuwa Mseminari tulikuwa tukifimdishwa kitu kinachoitwa "DHAMIRA". Tuwe na dhamira zenye kujali uwepo wa wengine.

Duka hili lililofungwa liwe funzo kwa wengine ambao bado hamkuguswa kwa maana unyoya bado unapepea na utakuja kukuguseni popote mlipo. Ninaheshimu wasifu wenu nyote, ila uwe wasifu wenye nia nkema na kuachana na dunia ya michongo na madili.

Aliyekuwa anasimamia duka hili na ambaye ndiye mhusika mkuu wa umiliki wa bidhaa zilizokuwemo dukani humu HANA UJUZI WOWOTE UNAOHUSU FAMASIA. Hivyo, alikuwa akiuza dawa na kuandika maelekezo ya matumizi ya dawa kwa mgonjwa kwa kutumia UJANJA. Alikuwa ANABASHIRI tu. Ukihitaji Magnesium (Mg) anakutazama kwa makini na kukuambia POLE SANA, UNA MINYOO. Huu ni mchongo wa kibedui kabisa! Duka limefungwa.

Ifahamike kuwa dawa ya minyoo nfani yake lazima ihusishe chembe za dutu Silver (Ag), hivyo ni niambata vya "pergertives" Duka limefungwa.
Wale wenye maduka ya dawa za binadamu hata mifugo kuweni makini. Kuuza dawa iliyokwisha muda wake ni kosa na ni uharamia dhini ya uhai wa binadamu na mifugo. Faida ya fedha haikatazwi lakini tazama yule anayekuletea faida mjengee uwezo ili akufae kwa faida wakati mwingine tena. Duka limefungwa!

Siyo maduka ya dawa tu, yako maduka ua namna mbalimbali. Hata wauzaji wa simu wapo wanaouza simu zilizotumika mida mrefu lakini huvikwa vifaa vipya ili zionekane murua. Duka limefungwa!

Leo tumakinike na masuala ya dawa kwanza. Maana inawezekana mtu akakuambia anauza "Morphine" tena kwa bei kubwa lakini huenda ikawa imekwusha muda. Kama anadai kuitengeneza yeye mwenyewe huenda akawa amezidisha viambatanisho au ameweka pungufu. Ni biashara safi, lakini CHEZA KARATA YAKO VIZURI. Duka limefungwa!
© Kizito Mpangala

No comments:

Post a Comment

Maoni yako