November 25, 2017
JINA LA WILAYA YA NYASA LINAPOPATIKANA NDANI YA JIJINI DAR ES SALAAM
Madhumuni
Nyasa
UCHU WA MADARAKA DHIDI YA UZALENDO
KITABU: ZIMBABWE: STRUGGLES-WITHIN-THE-STRUGGLE (1957-1980)”
MWANDISHI: PROFESA
MASIPULA SITHOLE
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA
JESHI la Zimbabwe limetangaza wiki iliyopita kuchukua madaraka nchini humo na kumwondoa Rais Robert Mugabe ambaye ametawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 38 hadi sasa. Kutokana na hali hiyo tunalaizmika kukumbuka namna mwanazuoni Profesa Masipula Sithole alivyobainisha matatizo ya Zimbabwe kupitia kitabu chake cha “Zimbabwe: Struggles-within-the-struggle (1957-1980)”
JESHI la Zimbabwe limetangaza wiki iliyopita kuchukua madaraka nchini humo na kumwondoa Rais Robert Mugabe ambaye ametawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 38 hadi sasa. Kutokana na hali hiyo tunalaizmika kukumbuka namna mwanazuoni Profesa Masipula Sithole alivyobainisha matatizo ya Zimbabwe kupitia kitabu chake cha “Zimbabwe: Struggles-within-the-struggle (1957-1980)”
November 24, 2017
JIWE LA POMONDA NA FORODHANI PANAWEZA KUTUPATIA WATU WA 'DIVING' KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.
NA HONORIUS MPANGALA
LICHA
ya kuwa mazingira mazuri na yenye kila aina ya vivutio lakini wafrika
tunashindwa kuwa wabunifu wa katika kuyafanya kama fursa.Mungu aliiumba Afrika
hivi ilivyo na kuweka jiografia ambayo nyakati zote watu Wa mataifa ya ulaya
wamekuwa wakivutiwa nayo.
![]() |
Mmmoja wa Warukaji katika Jiwe la Pomonda, Ziwa Nyasa |
Iko
michezo mingi inayochezwa Ulaya na Amerika inatokana na jinsi wenzetu walivyo
makini katika kutumia mazingira yao katika kujipatia fursa ya maisha yao.
Nyakati zote mataifa ya wazungu yamekuwa na michezo mingi ambayo ina mashabiki
na wanafanya vyema,hakuna michezo ambao unakosa mashabiki Amerika na Ulaya.
Madhumuni
afya,
amani na upendo,
Nyasa,
utalii,
uzuri
TANZIA: MBUNGE WA SONGEA MJINI AFARIKI DUNIA
November 23, 2017
ABDI BANDA AMETUONYESHA MAANA YA “SOKA LA KULIPWA”
![]() |
Abdi Banda |
KATIKA pambano la kirafiki kati ya Tanzania na Benin pale mjini Porto Novo nilimshangaa Abdi Banda. Kama tumjuavyo Banda ni kiraka katika kucheza soka anauwezo wa kucheza nafasi za ulinzi kama mlinzi wa kushoto, beki ya kati na kiungo wa ulinzi kwa usahihi mkubwa.
Sasa
alichokuwa akikifanya pale Benin alikuwa anatuonyesha utulivu wa akili yake katika
maeneo hayo mawili yaani kumudu hulka yake na kuwa mzuri katika kucheza soka
lenyewe. Banda
alikuwa mtu aliyewatuliza wachezaji wenzake waliokuwa wamepatwa na hasira kwa
maamuzi ya mwamuzi wa mchezo ule. Kwa penati iliyotolewa na mwamuzi ambayo
mpira ulionekana wazi kuguswa na mchezaji wa Benin lakini pigo likawa kuelekea
katika goli la Tanzania.
Madhumuni
Michezo
FREDDY MACHA ALIVYOLIZUNGUMZIA JUKWAA LA KISWAHILI SOCIETY
NA
MARKUS MPANGALA
SWALI: Naam, shikamoo Mzee Macha?
SWALI: Naam, shikamoo Mzee Macha?
FREDDY
MACHA; Marahaba. Habari zako bwana! uko wapi wewe siku hizi? Maana tangu
tuliposalimiana pale Soma Café,Mikocheni na baadaye Nyumba ya Sanaa, Dar es
Salaam wakati wa warsha nilizoendesha huko.
SWALI;
Nipo hapa Bongo naendelea vema tu. Ni kweli, kitambo hatujawasiliana, pia
nilifaidika sana na warsha zako hata hivyo si neno, tutaongea kidogo leo.
![]() |
Freddy Macha |
FREDDY
MACHA; Asante. Nadhani leo unalo la kuongea zaidi. Karibu.
SWALI;
Ni kweli, nahitaji mengi kutoka kwako mzee wangu. Kiu yangu ni huu mradi wa
Kiswahili Society, kwani umeeleza mahala fulani nikasoma nami nimevutiwa ili
niwaarifu wasomaji. Je mradi huu ulianza lini na wapi?
FREDDY
MACHA; Umeanzishwa na wanafunzi na Wahadhiri wa Kiswahili pale chuo cha lugha
cha SOAS (School of Oriental and African Studies) hapa London,Uingereza.
SWALI:
Nini dhumuni la kuanzishwa kwa Kiswahili Society?
FREDDY
MACHA; Kuunganisha Wazungumzaji wa Kiswahili duniani lakini hasa hapa
Uingereza.
SWALI:
Nashukuru sana. Ndugu Macha, wewe ni Mwanamuziki,Mwanafasihi,na Mwandishi
mkongwe. Katika fani hizi kuna mambo mengi umejifunza kutoka bara letu la
Afrika,Latin Amerika,Marekani na sasa Ulaya. Unadhani jamii za watu wa Ulaya
hususani Uingereza zinaweza kuhamasika kukiendeleza Kiswahili?
Subscribe to:
Posts (Atom)