April 23, 2008

Kutoka Nyasa + Marekani =Kurudi Teja

Ndiyo kuna jamaa mmoja hapa amenishangaza kama siyo kuniacha hoi,ni kisa hiki lazima nikiweke hapa ili tuelimishane wanyasa.Huyu jina lake maarufa la Kessi.Kipindi cha nyuma alifanikiwa kuwepo nchini Marekani kwa Joji Kichaka,akiwa huko aliishi na dada yake.Lakini pamoja nia nzuri {sina hakika kama ni nzuri} ya dada yake kuishi naye huko jamaa kawa ovyoovyo hata haeleweki.Akaanza kubwia madawa ya kulevya,akapiga kete hizo kwa kipindi kadhaa mpaka akawa mwendawazimu sasa.Basi jamaa karudi nyasa hapa kawa kituko heshima yake imetoweka siyo kama awali,akili yake haina tofauti na kichaa shauri ya madawa hayo,hajiwezi kwani maisha ameyachezea sana.Alipokuwa hapa nyasa kipindi cha nyuma na baadaye kupata nafasi ya kwenda kwa akina Joji Kichaka hakuwa hivyo,ila sasa hali ni mbaya,usicheke tafadhali.Siyo siri hali ya Kessi ni mbaya ,akili yake ovyoovyo wala hajielewi shauri madawa ya kulevya yamemwathiri .kwasasa anaweza kuongea na kucheka pekee yake kwa siku nzima huku akikumbuka namna alivyokuwa akibwia kete za madawa ya kulevya na rafiki zake.Hivi wewe unayesoma hapa hiki kisa kinakukuna sana?unajifunza nini?unatumia madawa ya kulevya?na hii hata hiyo bangi mnayotumia vijana wa kisasa eti ni fasheni au kuongezea mzuka,midadi n.k kumbukeni ukichaa unawanyemelea karibuni.Madawa ya kulevya ni hatari jihadharini sana,ndiyo maana nasema kutoka nyasa+marelani=kurudi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako