January 21, 2018

ERATOSTHENES WA KIRENE: MWANAHISABATI ALIYEISHI AFRIKA NA KUKADIRIA MZINGO WA DUNIA KWA KIVULI CHA MWANZI.

Na Kizito Mpangala

Eratosthenes alizaliwa mwaka 276 KK (Kabla ya kuazaliwa Yesu Kristo) mjini Kirene, Libya ya sasa. Kirene ni mji mashuhuri ulioundwa na Wagiriki wa kale walioishi Afrika ya Kaskazini hasa Libya ambako ndiko ulikokuwa mji wa Kirene maeneo ya Tripolitania ( sasa ni Tripoli), na Misri maeneo ya Alexandria ilikokuwa maktaba mashuhuri iliyotumiwa na wataalamu wengi wa Ugiriki ya kale. 

Alikuwa akifanya mazoezi mbalimbali ya viungo kila siku asubuhi na jioni. Alijifunza kusoma, kuandika, na kuhesabu. Ni kama vile falsafa ya elimu ya msingi inayotumiwa nchini Tanzania yaani KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu). Pia, alijifunza uandishi wa mashairi na vilevile masuala ya muziki.

January 20, 2018

NDANI YA KISIWA CHA FALKLAND

NA ALBANO MIDELO, LITUHI
HIKI ni kisiwa kidogo cha Falkland ambacho kipo kwenye maingilio ya Mto Ruhuhu katika Ziwa Nyasa.Kisiwa hiki kinamilikiwa na wavuvi toka Ludewa mkoani Njombe na Nyasa mkoani Ruvuma.
Asili ya kisiwa hiki kuitwa Falkland ni mgogoro wa kugombania kisiwa hicho uliotokea mwaka 1982 kati ya wavuvi wa Ngelenge wilayani Ludewa wakati huo mkoa wa Iringa hivi sasa Mkoa wa Njombe na wavuvi wa Lituhi wakati huo wilaya ya Mbinga ambapo sasa ni wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

January 19, 2018

MTO MAKATA WASABABISHA USUMBUFU KWA VYOMBO VYA USAFIRI MBAMBA BAY

Tukiwa tunasubiri Ujenzi wa Barabara ya Mbinga-Mbambabay mwezi February 2018, hali ya barabara MTO Makata mjini Mbambabay leo si nzuri kwani imesababisha masuala ya usafiri kusimama kwa muda. 
Basi la Abiria likiwa limeshindwa kuendelea na safari kutokana na eneo la mto Makata kuwa bovu.
Picha kwa Hisani ya Egbert Jemeny(pichani).

HAPO NI ENEO LA LWIKA KATIKA KIJIJI CHA LUNDO

Leo hii hakuna Mawasiliano ya Barabara toka Mbamba Bay to Kilosa....Bus zilizotoka   Mbinga na Songea Zimeishia shell pale Tambachi Kuna Calvart Limekwenda na maji watu wanahangaika hawajui cha kufanya.Hali ya mawasiliano kwa njia barabara ilikuwa mbaya sana siku ya tarehe 18/1/2017.

TAITU BETUL: MALKIA JASIRI ALIYEASISI MJI MKUU WA ETHIOPIA, ADDIS ABABA.

Na Kizito Mpangala

Taitu Betul alizaliwa mwaka 1851 nchini Ethiopia ambayo wakati huo ilikuwa ni Milki ya Ethiopia kabla ya kuwa Jamhuri. Neno Taitu kwao lilimaanisha “mng’ao wa jua au jua”, hilo ndilo lilikuwa jina lake la asili.
Baada ya kubatizwa katika kanisa la dhehebu la Orthodox aliitwa Walatta Mikael, lakini baadae alilirudia jina lake la asili yaani Taitu Betul. Baba yake alikuwa aliitwa Betul Haile Maryam ambaye alikuwa na uhusiano na ukoo wa Mfalme Sulemani. Lakini baba yake huyo hakufahamika sana kama alivyofahamika mjomba wake  aliyeitwa Dejazmach Wube Haile Maryam, ambaye alikuwa mtawala wa Ethiopia Kaskazini miaka ya 1840.
Familia ya baba yake Taitu ilikuwa imeweka makazi yake katika mkoa wa Semien ambao ulikuwa ukitawaliwa na Mfalme Susenyos I. Baba yake alikuwa ni mjukuu wa Ras Gugsa ambaye alikuwa mshirika wa familia iliyotawala eneo la Yejju iliyokuwa na asili ya kabila la Oromo. Baba yake huyo alikuwa Muislamu na baadae akabadili dhehebu akajiunga na Ukristo.

Taitu Betul alikuwa na nafasi kubwa ya kuwepo katika ngazi za juu katika maeneo hayo kutokana na ndugu zake wengi kuwa katika nafasi za milki mbalimbali hasa katika ngazi za mikoa. 

Taitu Betul aliolewa mara nne na kuachwa kabla ya kukutana na Mfalme Menelik wa Shewa kama mke wa tatu. Muda mfupi baadae, baada ya kuolewa na Mfalme Menelik wa Shewa, Mfalme huyo akatawazwa kuwa Mfalme wa Milki ya Ethiopia (Ethiopian Empire). Taitu Betul akiwa kama Malkia pamoja na mumewe Mfalme Menelik II walikuwa wanamiliki watumwa elfu sabini (70,000).

January 18, 2018

HAPA NI UFUKWE WA CHIWINDI MPAKANI MWA TANZANIA NA MOZAMBIQUE.

Picha kwa hisani ya Egbert Jemeny

HAKUNA CHAMA KINACHOENDESHA MAISHA YA MPIGA KURA.

NA HONORIUS MPANGALA, BAHI
NILIPOKUWA mdogo niliamini maisha ni jambo ambalo liko tofauti na la kuogofya sana katika jamii. Sababu kubwa ni pale nilipokuwa nayasikia maneno kama “Usicheze na maisha”. Fikra zangu zilinipeleka kuwa maisha ni jitu linalotisha sana katika jamii.

Baada ya makuzi nikapata misemo kama “Maisha yenyewe ndiyo haya haya” nikaanza kutambua kumbe mwenendo wa kuanzia asubuhi unaamka hadi usiku unaingia kulala hizi harakati zote ufanyazo ndiyo maisha yenyewe.

Katika vipindi ambavyo wapiga kura na wananchi wa kawaida toka vyama vya siasa wanajiona kama na wao ni wenyechama basi ni katika kampeni za uchaguzi. Kipindi hiki kila mwanachama anajiita ni mwenyechama. Ni kipindi ambacho watu hao hudiriki kunukuu maneno ya wagombea wao na kuiaminisha hadhira aliyonayo kuwa chama chetu kitatekeleza mambo kadha wa kadha.

KABWILI ASINGEKUBALI KUFUNGWA PENATI TANO ZA URA.

Na. HONORIUS MPANGALA
MIONGONI mwa utofauti ambao binadamu tunao ni jinsi ya kuzitumia akili zetu. Utofauti huo huweza kumtofautisha yule mwenye uwezo mkubwa katika kubaini jambo na kutafuta ufumbuzi na mwingine kubaini jambo kunachukua muda na kulifanyia ufumbuzi. Licha kuaminika kuwa tuko sawa lakini katika baadhinya nyanja hatuwezi kuwa sawa ndo maana wako warefu na wemgine wafupi ukiwalinganisha hao unapata utofauti. 

Yanga moja ya akili kubwa waliyoitumia kufanikisha saini ya Ramadhani Awam Kabwili Kwa mkataba Wa miaka mitano. Sijajua nani alisimamia kusaini Kwa Yohana Nkomola maana nilifikiri nae wangemalizana nae Kwa mtindo kama Wa Kabwili. Hata hivyo Kwa vile yuko katika milki yao wataweza kutenda jambo nae siku za usoni.


Licha ya mashaka makubwa wanayokuwa nayo mashabiki dhidi ya wachezaji vijana katika vikosi mbalimbali vya timu,ila hao ndio watu makini sana katika kitenda licha ya kwamba kuamua jambo kwao kunaweza kuwa na wasiwasi Wa hofu ya kuogoa kukosea. Wapo ambao wanakuzwa katika misingi ya kuamua Kwa kutenda Kwa wakati na kuamua Kwa ufasaha licha ya umri wao kuwa mdogo.

January 17, 2018

KUPIGA MARUFUKU MAVAZI YA NUSU UCHI

NA PROFESA ANNA TIBAIJUKA (MB)
Profesa Tibaijuka.

 UKIONA watu wanahangaika na suala la mavazi hasa kukazania yale yanayoficha mwili wa mwanamke ujue wana matatizo yao wamelishwa kasumba ya wageni. Dhana ya kuficha mwili ni kweli haina Uafrika wowote ndani yake. Mwafrika katika asili yake haangaiki kuficha mwili wa mwanamke. Hauoni kama chombo cha kumfurahisha mwanaume bali kiungo muhimu kumruhusu mwanamke kutimiza wajibu wake.

Kwa mfano wakati mwanamke wa kizungu anahangaika kujificha kunyonyesha mtoto Mwafrika asili anatoa ziwa mtoto ananyonya hadharani. Hapa titi ni mali ya mtoto siyo ya mume.

Kwa hiyo kabla ya wakoloni kufika na wamisionari walioandamana nao wakiwa wamevaa nguo ndefu watoto walikuwa uchi wasichana walipewa ngozi kujisitiri sehemu za siri wakivunja ungo na wanawake nao yalikuwa hayo hayo. Kulikuwa hakuna ubakaji kwa sababu hiyo. 

Ni kweli utasema jamii ilikuwa haijaendelea na maskini. Unaweza pia kusema hali ya maendeleo ilikuwa duni.Nguo hakuna. Lakini hoja hapa ninayolenga kupangua ni ile kwamba wanawake wakijifunua kwa kuonyesha uso au mikono au matiti au miguu yao au mapaja wanawakwaza wanaume. Sio kweli. Mbona mababu zetu hawakukwazika hizo enzi nilizoelezea? Mbona hawakubaka watoto na wasichana kama ilivyo sasa?

WASHINDI WA TUZO ZA USHAIRI NA FASIHI

HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA INAO WAJIBU WA KUHUDUMIA BARABARA ZAKE

NYASA inahitaji matibabu kamili (kama dawa ya Mseto) sio kutuliza maumivu (Panadol). Matengenezo haya nimeyakuta mwezi Disemba 2017. Niliwaacha watengenezaji wakiwa kijiji cha Ndumbi, lakini yanaonekana yameanzia kijiji cha Amanimakolo (nako kunajazwa vifusi na kukarabati).
UJUMBE WANGU: Halmashauri ya Nyasa inao wajibu wa kuhudumia barabara zake wakati wote si kujaza vifusi kwakuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu anapotembelea au kiongozi yeyote, au shughuli yoyote ya muda inapofanyika. Barabara ni nyenzo muhimu sana ya kukuza uchumi wa eneo lolote. Kila la heri wahusika. Tutaendelea kukumbushana.

HONGI NYASA: KISIWA KILICHOWEKWA RADA YA RAIS WA MALAWI

NA ALBANO MIDELO, LIULI

MBUNGE wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stella Manyanya hivi karibuni kwenye tamasha la utalii wa Nyasa alitamka wazi kwamba wilaya ya Nyasa ni Benki ya vivutio lukuki vya utalii hali ambayo inaifanya wilaya hiyo kuwa kitovu cha utalii katika ukanda wa kusini.
 
Afisa Maliasili na Utalii wa wilaya ya Nyasa Bugingo Bugingo anakitaja Kivutio kingine ambacho hakifahamiki lakini ni maarufu katika wilaya ya Nyasa kuwa ni kisiwa cha Hongi kama ambavyo unakiona kwa mbali kilichopo Kata ya Liuli ambacho ni kidogo lakini chenye kilele ambacho kabla ya uhuru wa Tanganyika, Nchi ya Malawi wakati huo ikiongozwa na Dk. Ngwazi Kamuzu Banda “Wamuyaya” iliweka Rada ambayo ilijulikana kwa jina la “Taa ya Banda”.

January 15, 2018

ELIMU BURE INAVYOTESA WATOTO WA WANANCHI WA HALI YA CHINI

NA HONORIUS MPANGALA
KITAALUMA na hisia zangu zimenifanya niwe mtu tofauti kabisa kuhusiana na matumizi ya baadhi ya maneno hapa nchini. Mengi hutumiwa na viongozi wa ngazi za juu kuwaona wale waliopo chini au wasio na vyeo kama wao kuwa  wenye kiwango fulani cha dhiki kinachostahili kuitwa cha chini. Ni hapo ndipo nakuwa na hisia tofauti sana juu ya kutumia maneno fulani dhidi ya kundi jingine hasa lile ninaloongoza au viongozi wanaloliongoza. 
Japokuwa nimekuwa mtu nisiyependezwa na na hili neno “Wananchi wa hali ya chini”' lakini najiuliza hao wa hali ya juu ni akina nani, wanafanya nini kutokuwa na hali ya chini na njia zao zikoje ili tuwaambie wa hali ya chini wajifunze kwenda huko juu? 

KARIBUNI RUVUMA. KARIBUNI KUTALII TUNDURU

Hili ni Jiwe kubwa sana ambalo linavutia watalii. Hili ni mojawapo tu, maana yapo zaidi ya haya. Mawe haya yanapatikana kilometa chache tu kutoka Tunduru Mjini mkoani Ruvuma.