June 12, 2008
Mnyasa,Mwanakijiji na Markus X
Kuna tofauti kubwa kati ya wivu na usongo,vivyo hivyo wivu humuua mtu mjinga,na huwezi kumchukia mtu unayemuona halafu ukampenda mungu usiyemuona yani itachekesha sana.Unajua kwanini?Kuna jamaa anapenda sana kupongezwa basi jana nikamwambia haniwezi mimi mtoto wa kijijini,mnyasa na mwana wa Malcom X.kilichofuata ni kicheko,halafu akagundua kuwa nimekasirika kisa kabeza majina yangu,nikasema hana jipya mimi ni mwanakijiji,myasa mpaka kufa halafu nikaongeza Markus X.Ndiyo mimi ni mnyasa wala hilo halina ubishi,kwani hiyo ni fahari yangu wala haina maneno.Pili Mwanakijiji,ni kweli kwani mimi nimezaliwa kijijini Lundu hivyo napenda kuitwa Mwanakijiji yaani toka huko nyasa kwenyewe.Sasa unajua kisa cha kujiita Markus X?Nimeamua kujita hivyo labda nitaridhika maana kila ninapoona sura yake Malcom X na kusoma hoja zake basi nahisi navaa ushujaa na ukombozi wa watu wa nyasa lakini sina maana kwamba wanamatatizo bali napenda nikimaliza ujuzi wangu ninaoutafuta sasa nataka nikawe mwenyekiti wa kijiji chetu cha Lundu.Napenda falsafa za Malcom X mpaka napata wazimu{natania usije ukadhani kichaa kweli}.Ni kweli nimeamua kujiita Markus X ili mjue kwamba nina utajiri wa akili lakini nimekuwa fukara wa kipato lakini ni mimi Markus X,Mwanakijiji na Mnyasa asilia.
Madhumuni
Hisia za moyo,
kwambe,
soga
June 10, 2008
TANGAZO; Nafasi Ya Kazi Nyasa

Madhumuni
amani na upendo,
ughaibuni
June 09, 2008
Hapa Kazi tu Hakuna Kuremba

June 08, 2008
Hatujashindwa Tunasonga Mbele kama Hivi...
Madhumuni
kumbukumbu,
Liwazo,
soka
Janeti na Hamu ya Njika kusoma Blogu
Kuna jamaa hapa ananitazmasana sijui anashangaa nini.Labda tokana na kasi yangu ya kundika hapa bloguni.Lakini namfahamu sana huyu jamaa unajua jina lake nani?nimemkumbuka umeona jina la mtu mwenye hamu ya kublogu hapo juu?Ndiye huyo anaitwa Njika Clara ni ndugu yangu,basi leo nimemnogesha kublogu nakwambia amebaki kutola mate tu jinsi anavyonogea mmm halafu ananiudhi amshika shavu sijui anamanaa gani.Najua hapa akitoka hapa nyasa anahamu ya kwenda kumtembelea shangazi yake mtaa fulani najua anafuata samaki tu si unajua wanyasa kitoweo chao.uache hilo,kuna mwingine tazama jina lake mwanzo "Janeti" basi jana kasoma blogu ya nyasa hii mpaka akakasirika kisa wivu eti wanyasa wanajidai na blogu yao.Haa nikammwambia mbona nawe mnyasa?akaniambia haijalishi ila wanyasa tunaringia kublogu.Lakini akamaliza kwamba hata yeye Blogu hii inamhusu shauri ye mnyasa.Basi huyu Njika anasoma blogu hii naona mpaka njaa inamuuma sijui hajala..ebu mtazama huyo hapo pembeni anakunja ndita sababu gani?.Mmmmm timu yetu ya taifaimefungwa na CapeVerde bao moja jana mmmm inauma sana
June 06, 2008
Wanyasa Tumuombe mungu Tushinde
Timu Ya Taifa Imeondoka Leo
Madhumuni
kumbukumbu,
soka
Subscribe to:
Posts (Atom)