
September 09, 2008
hakuna kulala
September 06, 2008
umewaona hawa jamaa vema?

Madhumuni
amani na upendo,
ughaibuni,
urafiki
Olimpiki 2012 nyie chekeni tu...kazi ipo
Haya tena dadangu Yasinta kacheka sana niliposema maandalizi ya olimpiki nayaanza. unajua kwanini anacheka? ngoja nikumegee siri...aaah nimeghairi usije ukamwambia lakini sikiliza najua anawivu hawezi kukimbia mita 10000,pia 100 inamsumbua si umemuona alivyo? labda enzi zile akiwa kama Madonna mwaka 1992 angeliweza lakini sasa thubutu yake atajiju leo. Nakwambia sasa ni shughuli kwelikweli sitaki blah blah hapa wala mzaha. Najua hata Erick hawezi kuufikia moto huu yaani ni zaidi ya Usain Bolt yule jamaa anayetokea kule walikuwa wanahusudu sana BLACK BAMBOO eti sasa wanatingisha dunia kwa kukimbiza upepo. Asikwambie mtu yaani mpango wa kwanza kwenda kutambika mizimu kule BUTIAMA kwa Mwalimu JK Nyerere hakua kwere hapa. baada ya kutafuta pumzi sasa inatafutwa kasi. Ngoja nitakwambi nilitumi muda gani mita 10000 lakini mpaka nikaague kwanza kwa mganga ili nijue nitakimbia muda gani.....
Subscribe to:
Posts (Atom)