September 09, 2008

hakuna kulala

September 06, 2008

umewaona hawa jamaa vema?

kwahiyo hawa jamaa yaani mama na mwana wanataka kushindana na mimi. hiyo olimpiki nawaambi kasi mlete daktari wa kuwatibu au natania? ndiyo nao wanajiandaa kwa olimpiki ijayo huko London kwa Toni BULEYA na mwenzie Godoro la KAHAWIA pamoja na MALIKIA ELIZETI. nakwambia hamnipiti mnajua dawa za Lupocho,Ntambitambi,Ngelengana,Matungulusi,na N'kwanchu? nakwambia. haya njooni huku nyasa muone jasho na damu... lakini nawapenda sana eti eeeh. Sitaki naona mnataka kuniharibia maandalizi{natania}. oooo nipo bize marafiki tuonane labda London kwa siku moja tu tutaongea najua hiyo hali hampendi lakini nina mambo mengi....nina mzizi ya kila kitu nawaambia mtavua jezi hizo sawa?{natania}

Olimpiki 2012 nyie chekeni tu...kazi ipo

Haya tena dadangu Yasinta kacheka sana niliposema maandalizi ya olimpiki nayaanza. unajua kwanini anacheka? ngoja nikumegee siri...aaah nimeghairi usije ukamwambia lakini sikiliza najua anawivu hawezi kukimbia mita 10000,pia 100 inamsumbua si umemuona alivyo? labda enzi zile akiwa kama Madonna mwaka 1992 angeliweza lakini sasa thubutu yake atajiju leo. Nakwambia sasa ni shughuli kwelikweli sitaki blah blah hapa wala mzaha. Najua hata Erick hawezi kuufikia moto huu yaani ni zaidi ya Usain Bolt yule jamaa anayetokea kule walikuwa wanahusudu sana BLACK BAMBOO eti sasa wanatingisha dunia kwa kukimbiza upepo. Asikwambie mtu yaani mpango wa kwanza kwenda kutambika mizimu kule BUTIAMA kwa Mwalimu JK Nyerere hakua kwere hapa. baada ya kutafuta pumzi sasa inatafutwa kasi. Ngoja nitakwambi nilitumi muda gani mita 10000 lakini mpaka nikaague kwanza kwa mganga ili nijue nitakimbia muda gani.....