Showing posts with label Huzuni. Show all posts
Showing posts with label Huzuni. Show all posts

February 19, 2018

MAMBA AKATISHA UHAI WA MJASIRIAMALI NGINDO

NA THOMAS CHIHONGAKI
Majonzi na Simanzi Vimetawala katika Kijiji cha Lundo na Ngindo Kata ya Lipingo kutokana na tukio la dada yetu Neema Kalanje(25) kupoteza maisha kwa kushikwa na kuuliwa katika Mto Lwika uliopo Kijiji cha Lundo. 

Dada yetu amekutwa na umauti huo jana Saa 5 Asubuhi akiwa katika shughuli zake za ujasiriamali wa kuuza Dagaa Nyasa aliowanunua Ziwani Asubuhi na kwenda kuwauza katika Kitongoji cha Zambia katika Kijiji cha Ngindo.

Marehemu alipofika katika Kivuko cha Mto Lwika kuna dalaja dogo la Mbao akaamua kunawa Maji ghafla mamba akatokea na Kumkamata. Baadae Taarifa zilisambaa kijijini  kwa mayowe na hatimaye Wananchi wakakusanyika na kuanza kutafuta na kufanikiwa kuuona mwili wa Marehemu.

Eneo hilo ni hatari kwani mwaka 2015 palitokea ajali na kujeruhiwa kwa kijana Ignas Magic Kalenyula na kumuua Thomas Nkoma. Rai yangu kwa Halmashauri kupitia Idara ya Maliasili kuangalia uwezekano wa kuwasaka wanyama hao na kuwatokomeza kabisa.

Pia Idara ya Ujenzi Nyasa kutusaidia kujenga daraja la kudumu katika eneo hilo. Picha za tukio nii kwa hisani ya C.Ngwata Diwani wa Kata ya Lipingo (Chadema). Natoa pole zangu kwa Familia ya akina Kalanje na Mdogo wangu Elisha Magunga kwa kumpoteza Mke wake Mpendwa...
RIP Neema

February 17, 2018

R.I.P AKWILINA, ETI MKOA WA DAR ES SALAAM UNA BARABARA ZA HEWANI ZA KUPITA DALADALA!!


 MIAKA mitano iliyopita nilipata kuandika kuwa, ‘utamaduni wa wananchi kupigwa risasi, kushambuliwa kwa riasi za moto, kushuhudia wapendwa wao wakifariki dunia mbele ya macho yao, kuna matokeo hasi yenye athari kubwa nchi yetu. 
 
Nilisema wananchi wanazoeshwa kupigwa risasi za moto. Wanazoeshwa kuuana. Watatamani kuuana. Watatamani kujiua. Wanazoeshwa kuchukia kwa vitendo vinavyoumiza mioyo yao.  

Mwishowe nilisema kuwa wananchi hawa wanapotenda jinai wakitumia mapanga, marungu au visu, jawabu ni kwamba wanatumia vitu hivyo kwasababu ‘hawana bastola wala bunduki’. 

December 07, 2017

TUNAUNGA MKONO ARUDISHWE MWANDISHI MWENZETU.


December 04, 2017

MFADHILI WA DHIKI

Nikiwa katika ufukwe wa forodha ya Lundu, Nyasa.
Nilitamani nguo kupiga pasi,
Hakika hilo tena siwezi,
Kwetu umeme wa manati,
TANESCO hisani nifanyieni,

Umeme wahakika nipatieni.

Mimi ni muuza Juisi
Kama yule fundi Kinyozi,
Jenereta kwetu hatuwezi,
mitaji yetu kama mkwezi,
Umeme wahakika nipatieni.


May 31, 2013

MWENYEZI MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA ALBERT MANGWEA

Mwanamuziki mashuhuri wa Bongofleva, marehemu ALBERT MANGWEA. Amefariki huko Afrika Kusini mapema wiki hii

March 29, 2013

BREAKING NEWS: JENGO LA GHOROFA 16 LAPOROMOKA JIJI DAR ES SALAAM

Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, na marafiki wote walio kumbwa na kuanguka kwa jengo lenye gorofa 14 (Mtaa wa Morogoro, Dar-es-salaam) kwa namna moja au nyingine. Inasikitisha sana kwani vifo vingi vimetokea.    


Mtaa wa Mosque katikati ya jiji la Dar es salaam


BADO WATU WAPO ENEO LA TUKIO WAKIWEMO VIONGOZI WAKUBWA WA MKOA;ASILIMIA KUBWA YA WATU WAMEOKOLEWA HUKU VIFAA DUNI VYA UOKOAJI VIKIKWAMISHA KAZO HIYO;WATU KADHAA WANAHOFIWA KUFA JAPOKUWA SINA IDADI KAMILI


MAONI YA MHANDISI EGBART JEREMY KATIKA UKURASA WANGU WA FACEBOOK
anasema, matatizo kama haya yanachangiwa na ....

COLUM ZIMEFELI TATIZO LA WAKANDARASI ,NA WAMILIKI UNAWEZA KUKUTA KUNA KIBAO CHA KUTAMBULISHA KAMPUNI INAYOJENGA LAKINI KAMPUNI HAIPO WALA WATAALAM NI KIBAO TU KIPO LAKINI UJENZI UNAFANYWA NA MMILIKI WA JENGO. NI TANZANIA ZAIDI UIJUAVYO...... anaendelea kusema ....


NILIKUWA NAANGALIA KWENYE TV YA CHANEL TEN JINSI LILIVYO POROMOKA LIMESHUKA LOTE NIKAGUNDUA KUWA COLUMN ZIMEFELI KUBEBA MZIGO MZITO