1.Hifadhi ya Taifa Kitulo ndiyo
eneo pekee Tanzania lenye ndege aina ya tandawala machaka (Denhams Bustard)
wenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.
2.Hifadhi hiyo inayopita katika
mikoa ya Mbeya na Njombe ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005
ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo, msitu wa Livingstone na bonde
la Numbi.
3.Kitulo ina ukubwa wa kilometa
za mraba 442. Awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick
Elton kupita eneo hilo mwaka 1870. Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo
(FAO) lilichukua eneo hilo kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
4. Ndege aina ya tandawili
machaka hawapatikani sehemu nyingine yoyote hapa Tanzania zaidi ya Kitulo.
5.hifadhi hiyo ndiyo eneo pekee
ambalo ndege hao hutaga mayai na kuzaliana kwa wingi kabla ya kusafiri kwenda
mabara mengine.









