Showing posts with label Mazingira. Show all posts
Showing posts with label Mazingira. Show all posts

March 05, 2018

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU BUSTANI YA MUNGU- HIFADHI YA KITULO.

1.Hifadhi ya Taifa Kitulo ndiyo eneo pekee Tanzania lenye ndege aina ya tandawala machaka (Denhams Bustard) wenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.
2.Hifadhi hiyo inayopita katika mikoa ya Mbeya na Njombe ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005 ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo, msitu wa Livingstone na bonde la Numbi.
3.Kitulo ina ukubwa wa kilometa za mraba 442. Awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick Elton kupita eneo hilo mwaka 1870. Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) lilichukua eneo hilo kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
4. Ndege aina ya tandawili machaka hawapatikani sehemu nyingine yoyote hapa Tanzania zaidi ya Kitulo.
5.hifadhi hiyo ndiyo eneo pekee ambalo ndege hao hutaga mayai na kuzaliana kwa wingi kabla ya kusafiri kwenda mabara mengine.

December 27, 2017

NYASA; DISEMBA 20 ILIPONIREJESHA MIAKA 13 ILIYOPITA

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
TULIANZA safari yetu na dadangu kijijini kwetu Lundu na kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mbamba Bay. Changamoto za barabarani hazikukosa kwasababu ya mvua zinazonyesha. Tukifika na kukamilisha yaliyotupeleka huko. 

Saa kumi jioni nilipofika kituo cha mabasi cha Mbamba Bay sikukuta gari ya kugeuza kwenda kwetu Lundu. Ikatulazimu tupande ya kuishi njiani, gari iliyotoka Mbinga kwenda Kihagara. Nikiwa nawaza namna ya kutoka Kihagara hadi Lundu lakini nikapanga jambo kuwa bodaboda ziko kila eneo sikuhizi,na sikutoa nauli ya yangu na Dada nikamwambia waambie natoa Mimi. Nikamwambia konda natoa Kihagara kuna mtu anatusubiri,nilifanya Kwa maksudi.

November 22, 2017

MAONI YA MHARIRI: ‘Nani atalinda samaki wa Ziwa Nyasa?


Naanza katika maliasili zetu. Sisi kama Tanzania tuna maliasili nyingi sana na watu wengi hawajui kabisa hilo na pia tuna wataalamu wangeweza kuwafumbua watu macho. Tukianza kwa kusafirisha nje ya nchi, Samaki hai wa maji baridi yaani Tanzania ndio ina samaki wa bei kubwa kuliko wote duniani. 

October 17, 2017

TAKWIMU MUHIMU ZA WILAYA YA NYASA HADI OKTOBA 2017


1. Total Number of Hamlets in the District = 425

2. Total Number of Households for Nyasa dc = 31,146

3. Total Female Population for Nyasa dc = 74,768.


4.Total Male Population for Nyasa dc = 71,392.

5. Total Population for Nyasa dc = 146,160.

6. Total Number of Secondary school = 14

7. Total Number of Primary School = 106
Total Number of Villages = 84


8. Total Number of Ward = 20

9. Total Number of Division = 3

CHANZO: Nyasa dc statistics

October 16, 2017

“RAIS ANA MIAKA 31”


Sebastian Kurz
JUMAMOSI nilikuwa nasoma makala ya James Masters kwenye tovuti ya CNN. Sentesi yake ya kwanza ilinivutia sana, “Ulikuwa unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Ingawa aliendelea na mengine lakini staili pekee haikuwa kivutio bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi.
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye amewahi kuwa waziri wa  Ushirikiano wa Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.  Sebastian  Kurz ambaye amekuwa Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu. 

Ni mwenyekiti wa chama cha  OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama chake kushinda viti vingi vya bunge. 

October 14, 2017

WATU WASIOJULIKANA WATAIKIMBIZA AFCON U-17 2019

NA HONORIUS MPANGALA 
 
MWANDISHI maafuru wa fasihi kutoka Nigeria,marehemu Chinua Achebe katika kitabu cha 'Things Fall Apart' alisema kukimbia matatizo sio njia sahihi ya kutatua hayo matatizo. Wakati msomaji wa fasihi hiyo akiona kama burudani kusoma vibweka vya Okonkwo lakini kuna mafundisho katika kitabu kile. Nyakati zote huwezi kuona ugumu wa jambo kama halijakutokea.
Chinua ananifanya nihusianishe matukio ya watu wasiojulikana na hatima ya Nchi katika nafasi ya kuandaa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa chini ya miaka 17.
Serengeti Boys wakifurahia katika moja ya mabao waliyofunga katika mechi za kimataifa
Ukimya wetu katika kuchukulia kila jambo ni kitu kinachofanyika na tukashindwa kutambua tatizo au kuwabaini wahusika linaweza kutuondolea mwonekano wetu nje ya mipaka ya nchi.

Matatizo yanatakiwa kutatuliwa kwa kufahamu chanzo na kuchukua hatua ya kuyamaliza. Sisi kama Taifa tuna hamu kubwa na kuona tukifanikisha Michezo inafanyika vyema hapa nchini kwa kuhusisha sekta zote kushiriki vyema.
Labda nikumbushe jambo moja baada ya Afrika kusini kutangazwa kama waandaaji wa fainali za kombe la dunia mwaka 2010. 

October 11, 2017

SOMO LA LEO

“Mheshimiwa Kakunda (Joseph –Naibu Waziri Tamisemi) nakuagiza kuanzia leo maana wewe ndiyo nimekukabidhi jukumu la elimu, nataka mtihani wa 2019 shule za vipaji zote 22 ziongoze mtihani wa Taifa na shule binafsi ziwe nyuma, lakini tuongoze kwa halali si ubabaishaji hapo ndipo shule binafsi za makanjanja zitajifuta zenyewe,”

-Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo.

January 21, 2013

UHARIBIFU WA MAZINGIRA MDUNDUALO-MBINGA


Egbart Jeremy
Na Egbart Jeremy, Mbinga

Utunzaji wa mazingira umekuwa jambo muhimu sana. Kwa muda mrefu ripoti mbalimbali zimekuwa zikielezea juu ya umuhimu wa kutunza mazingira. Kuna wataalamu wa mazingira wamekuwa wakishughulikia ukaguzi wa mazingira katika maeneo mbalimbali kwenye wilaya ya Mbinga. Miongoni mwao ni hapa pichani wataalamu wa mazingira wakikagua uharibu wa mazingira uliojitokeza kwenye maeneo mbalimbali.
Mathalani ni kijiji cha Mtundualo, kilichopo kwenye wilaya ya Mbinga ambako kunaendeshwa uchimbaji wa makaa ya mawe (TANCOAL). mtundualo ni miongi mwa maeneo yanayokaguliwa mara kwa mara kutokana na hali iliyowahi kujitokeza pia katika kijiji cha Ndumbi, kilichopo wilaya ya Nyasa.

Mtaalamu wa mazingira kutoka ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa wilaya, Egbart Jeremy akijadiliana jambo na ofisa usalama na mazingira kutoka mgodi wa makaa ya mawe(TANCOAL) kuhusu uchafuzi uliofanywa na 




Timu ya wataalamu wa mazingira wakikagua uharibu wa mazingira kijiji cha Mdundualo
                            
Mtaalamu Egbart Jeremy akikagua maji yanayodaiwa kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira kutokana na uchimbaji wa makaa ya mawe(TANCOAL)