Showing posts with label Usalama. Show all posts
Showing posts with label Usalama. Show all posts
February 14, 2018
UTEUZI WA MNADHIMU MKUU JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA
Madhumuni
Usalama
January 19, 2018
MTO MAKATA WASABABISHA USUMBUFU KWA VYOMBO VYA USAFIRI MBAMBA BAY
Tukiwa tunasubiri Ujenzi wa Barabara ya Mbinga-Mbambabay
mwezi February 2018, hali ya barabara MTO Makata mjini Mbambabay leo si nzuri
kwani imesababisha masuala ya usafiri kusimama kwa muda.
Basi la Abiria likiwa limeshindwa kuendelea na safari kutokana na eneo la mto Makata kuwa bovu.
Picha kwa Hisani ya Egbert Jemeny(pichani).
January 12, 2018
JIMBO LA NYASA: KWANINI WANANCHI WA TARAFA YA RUHUHU WAMEACHWA UKIWA?
NA MARKUS MPANGALA
Kwa
mujibu wa sensa ya mwaka wa 2012, Kata ya Mbaha ilikuwa na wakazi wapatao 6,972.
Ni Kata ambayo ndiyo mwenyeji wa Shule ya Sekondari ya Monica Mbega iliyoanzishwa
rasmi mwaka 2006. Jina la shule hiyo lilitokana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa
Ruvuma, Monica Mbega kabla ya kuondoka.
![]() |
| Ubovu wa Barabara katika kijiji cha Ndumbi. |
RUHUHU
ni miongoni mwa Tarafa zinazounda Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa. Wilaya hii ni
miongoni mwa zingine kama Songea Vijijini, Songea Mjini, Mbinga, Namtumbo, Tunduru
zilizopo mkoani Ruvuma. Wilaya ya Nyasa ilianzishwa rasmi mnamo Machi 2012 baada
ya kugawanywa wilaya ya Mbinga. Eneo la wilaya ya Nyasa liko kando la Ziwa
Nyasa.
Tarafa
ya Ruhuhu ipo kwenye mwambao huo, ikiwa ni miongoni mwa maeneo yaliyoachwa nyuma
kimaendeleo na kiuchumi. Tarafa hiyo inazo Kata za; Mbaha, Lituhi, Ngumbo na
Liwundi.
Kwa
mujibu wa sensa ya mwaka wa 2012, Kata ya Mbaha ilikuwa na wakazi wapatao 6,972.
Ni Kata ambayo ndiyo mwenyeji wa Shule ya Sekondari ya Monica Mbega iliyoanzishwa
rasmi mwaka 2006. Jina la shule hiyo lilitokana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa
Ruvuma, Monica Mbega kabla ya kuondoka.
Wananchi
wa Tarafa hii wanakabiliwa na changamoto nyingi mno hali ambayo inadhoofisha
ukuaji wa uchumi. Changamoto hizo zinatokea katika nyakati tofauti na kuziba
mianya ya kujipatia pato kutokana na huduma kadhaa wa kadhaa kuwa dhaifu.
October 16, 2017
“RAIS ANA MIAKA 31”
![]() |
| Sebastian Kurz |
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye
amewahi kuwa waziri wa Ushirikiano wa
Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.
Sebastian Kurz ambaye amekuwa
Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu.
Ni mwenyekiti wa chama cha OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili
aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama
chake kushinda viti vingi vya bunge.
Madhumuni
Digitali,
diplomasia,
falsafa,
habari,
Historia,
Maendeleo,
Mafanikio,
Mazingira,
mila na desturi,
Politics,
Sheria,
siasa.,
uchambuzi,
Uchumi,
Usalama
September 27, 2017
ADHABU KWA MWENDESHA BAISKELI
Jana
mchana mwendesha Baiskeli alipita kwa kasi katika makutano ya barabara ya Bibi
Mohammed na Morogoro bila kuruhusiwa na taa za kuongoza magari. Wakati anapiga
taa zilionyesha magari yapite, na yalikuwa yakipita kwa mwendo kasi mno, kiasi
kwamba ingetokea gari linalopita basi angegongwa na kusababisha matatizo
makubwa.
Madhumuni
Usalama
December 17, 2013
JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YAANZISHA BARAZA LA AMANI NA USALAMA
KAMPALA, Uganda
VIONGOZI wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki wametia saini kuanzishwa rasmi Baraza la Usalama la
Jumuiya(East African Peace and Security Council) ambalo litashughulikia mambo
mbalimbali ya ulinzi na usalama kwa nchi wanachama wa Afrika Mashariki.
Viongozi hao kutoka
Uganda, Tanzania, Kenya, Rwanda na Burundi wamefikia uamuzi huo juzi jumamosi
wakati wa mkutano wao uliofanyika mjini hapa. Uamuzi wa kuanzisha Baraza la
Usalama la Afrika Mashariki ni kutokana na kitisho cha kusambaa kwa ugaidi kama
ambavyo yalivyotokea Dar es salaam(1998), Nairobi(1998 na 2013), na
Kampala(2010).
Akizungumza mbele ya
viongozi waliohudhuria katika mkutano
Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Richard Sezibera, alisema “Nathibitisha uamuzi
uliofikiwa katika mkutano huu kuanzisha Baraza la amani na Usalama kwa nchi
wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwa na lengo la kuhakikisha ulinzi
na usalama wa eneo hili dhidi ya tishio lolote litakalotokea,”
Wanachama wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki wanakabiliwa na tishio la ugaidi unaofanywa na kundi la Al
Shabab ambalo lina uhusiano na Al Qaeda. Kwenye mkutano huo,
nchi wanachama wamekubaliana kukabiliana na tishio la ugaidi kwa pamoja ili
kuepusha matukio kama yaliyokea mjini Nairobi katika maduka ya Westgate ambapo
zaidi ya watu 60 wasio na hatia walifariki dunia na wengine 175 wakiwa
majaerhu.
Mwaka 2010 kundi la Al
shabab lilidaiwa kufanya mashambulizi katika jiji la Kampala na kusababisha
vifo vya watu 70 baada ya mabomu mawili ya kutegwa ardhi kulipuka.
Madhumuni
Hisia za moyo,
ughaibuni,
Usalama
August 15, 2013
JESHI LA POLISI LAANZA OPERESHENI MAALUMU
Na Mwandishi Wetu, Dar es
salaam
Jeshi la Polisi nchini
limewaomba wananchi kuimarisha na kulinda amani na usalama kwa kuwafichua
wahalifu wa aina yeyote wakiwemo wahamiaji haramu ambao wamekuwa wakilisumbua
jeshi hilo.
Kwa mujibu wa Msemaji
wa jeshi la Polisi, Advera Senso, alisema kuwa uamuzi wa Jeshi la Polisi
kuwaomba wananchi washiriki katika zoezi hilo ni kutimiza amri ya Rais Kikwete
ambaye alitoa siku 14 kwa vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinawakamata
wahalifu na wahamiaji haramu pamoja na wanaomiliki silaha kinyume cha sheria
hususani maeneo ya mipakani.
“Jeshi la Polisi
linasisitiza wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama nchini wawe tayari kuwafichua
wahalifu wa aina yeyote ile wakiwemo wahamiaji haramu kwa vyombo vya dola au mamlaka
yoyote ya serikali, wananchi wasikubali kuwahifadhi wahamiaji haramu na watoe taarifa wawaonapo wakiingia kwenye maficho
maarufu kama njia za panya,” alisema Senso.
Aidha, msemaji huyo
aliongeza kuwa ni lazima jamii ihamasike kulinda amani na usalama, pia Jeshi
hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola limepanga kuendesha operesheni
maalumu ya kuwabaini na kuwamata watu wote wanaokiuka sheria au kuhatarisha
ulinzi na usalama hapa nchini
“Tunawaomba wananchi
washirikiane na vyombo vya dola, hii itsaidia nchi yetu kuendelea kuwa salama, hususani
wananchi waishio mipakani. Baada ya siku kumi na nne alizotoa Mhe. Rais
kumalizika, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na
usalama vitaendesha operesheni kali ya kuwabaini ikiwemo wanaomiliki silaha
kinyume cha sheria,”
June 13, 2013
ULINZI NA USALAMA WETU:
Na Edgar Mwandemani
Leo naomba nijitumbukize katika mjadala mgumu kidogo. Ni hili suala la ulinzi na usalama wa watanzania na mali zao. Natambua kuwa hapa nchini tunavyo vyombo vilivyokasimiwa majukumu ya kuhakikisha ulinzi na usalama wa maisha ya watu na mali zao upo, unadumishwa na kuondoa aina yoyote ya tishio dhidi ya raia.
Tunalo Jeshi la Polisi, JWTZ, JKT, Magereza, Uhamiaji, Usalama wa Taifa kwa kutaja vichache. Vyombo hivi pamoja na mambo mengine vinahudumiwa na kodi za raia ili vitulinde lakini vyote pia vinaundwa na raia wa nchi hii. Kwahiyo, usalama wa raia ndio usalama wa vyombo hivi.
Nijielekeze kwenye lile nililotaka tujihoji. Siku za hivi karibuni kumeibuka mlolongo wa matukio ambayo yanatuingiza shakani kama nchi, japo inaonekana ni matukio yanayolenga kundi fulani tusipongalia yatasambaa na kumhusu kila raia.
Ukiondoa matukio ya vifo na majeraha yanayotokana na vurugu za raia, mapigano baina ya makundi kama wakulima na wafugaji, vifo vilivyotokana maandamano na migomo. Ni dhahiri kwamba katika maeneo fulani majeraha na vifo ni matokeo ya mikakati madhubuti inayopangwa ama na watu binafsi, vikundi au taasisi zetu rasmi ambazo kwa upande mwingine zilipaswa kuhakisha hayo hayatokei.
Matukio ya kuumizwa na kuuwawa
kwa raia wasio na hatia wakiwa katika himaya za vyombo vyetu vya ulinzi na
usalama yameongezeka nitakumbusha machache tu. Wale wafanyabiashara wa vito
"kesi ya Zombe", yuko dereva teksi pale Kimara, kijana mwingine
aliwawa kule Chunya akiwa kituo cha polisi.
Unyama dhidi ya waandishi Saed
Kubenea na Ndimara Tigambwage, Dr. Stephen Ulimboka, Daudi Mwangosi kule
Iringa, na hivi karibuni mwandishi Absolom Kibanda. Huyu wa mwisho ameweza
kutoka hadhani na kutuambia "haya yote ni matukio ya kupanga kutokana na
namna yanavyojitokeza" na akahoji kuwa pamoja na ahadi nyingi kwamba
"tutahakikisha wahusika wanakamatwa mara moja na kufikishwa mbele ya
vyombo vya sheria" hakuna lililokwisha kufanyika akichukulia mfano wa
tukio lililomkumba yeye binafsi.
Inawezekana tukaona matukio haya yote hayatuhusu, lakini nina hakika kuwa iko siku sisi sote tutahusika kwa sababu tumekubali utaratibu huu ndio uongoze maisha yetu. Hatuwezi kudumu katika vurugu hizi harafu siku moja zisiiangamize jamii nzima!
Inawezekana tukaona matukio haya yote hayatuhusu, lakini nina hakika kuwa iko siku sisi sote tutahusika kwa sababu tumekubali utaratibu huu ndio uongoze maisha yetu. Hatuwezi kudumu katika vurugu hizi harafu siku moja zisiiangamize jamii nzima!
Kwanini vyombo vyetu vya ulinzi
na usalama vinashindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kushindwa
kushughulikia wahalifu hawa wanaoumiza, kutesa na kuua wasio na hatia. Je,
vinataka tuamini kuwa navyo vinahusika na uchafu huu unaondoa hali ya amani na
utulivu. Hali inayokaribisha ile dhana ya "survival for the fittest".
Tujiulize itakuwaje pindi kila raia atakapochukua jukumu la kujilinda mwenyewe?
Mbaya ya jambo hili ni kuwa hivi sasa limefanywa ni silaha ya kisiasa. Hivi sasa pande zinazohusika katika siasa za nchi hii zimekuwa haziishi kutuhumiana kwa mauaji na utesaji. Kila upande umekuwa ukieleza kuwa una ushahidi na unawajua watekelezaji wa unyama huu. Na wengine wamekuwa wakiwatumia wahanga wa matukio haya ili kuendeleza agenda za kisiasa ikiwemo kuonyesha ubaya wa upande wa pili.
Mbaya ya jambo hili ni kuwa hivi sasa limefanywa ni silaha ya kisiasa. Hivi sasa pande zinazohusika katika siasa za nchi hii zimekuwa haziishi kutuhumiana kwa mauaji na utesaji. Kila upande umekuwa ukieleza kuwa una ushahidi na unawajua watekelezaji wa unyama huu. Na wengine wamekuwa wakiwatumia wahanga wa matukio haya ili kuendeleza agenda za kisiasa ikiwemo kuonyesha ubaya wa upande wa pili.
Muda wote huo sisi kama raia
tumekuwa tukichekelea na wengine kushabikia upuuzi huu, huku upande wa vyombo
vyetu vya ulinzi na usalama ukiwa hauonekani kushtushwa na hali ya mambo. Ni
kutokana na hali hii wahanga wa matukio haya wameanza kujilinda kwa makundi
yao: waandishi wanalia kivyao, viongozi wa dini nao wanabaki kulalama; raia
kule mtaani nao hivi sasa wameanza hata kuvamia na kuchoma vituo vyetu vya
polisi kwa hisia kwamba vimepoteza maana. Wakati wa matukio ya kule Mtwara
inaelezwa kuwa gari la Afisa usalama lilitekezwa kwa moto.
Naomba tushirikiane katika tafakuri hii juu ya hali ya ulinzi na usalama wetu, huku tukiendelea kudadisi yaliyomo katika rasimu ya Katiba iliyotoka hivi karibuni
Naomba tushirikiane katika tafakuri hii juu ya hali ya ulinzi na usalama wetu, huku tukiendelea kudadisi yaliyomo katika rasimu ya Katiba iliyotoka hivi karibuni
Madhumuni
Usalama
March 11, 2013
KUFUKUZA MAKURUTA 95 WA JESHI LA POLISI HAITOSHI
![]() |
| Markus Mpangala |
Na Markus Mpangala, Dar es Salaam
Tukio la waziri wa Mambo ya Ndani
Emmanuel Nchimbi kuwafukuza Makuruta 95 wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi kwa kile
alichooita kugundulika kutumia rushwa kujipatia ajira, bado linaelea katika
vichwa vya watu juu ya msingi wa maadili yetu.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,
Renatus Chalamila amehusishwa na rushwa katika kuajiri. Waziri Nchimbi
amechukua hatua zaidi baada ya kumsimamisha kazi Kamishna huyo. Alisema pia taarifa za uchunguzi za
Kamishna huyo, ambaye anashughulikia masuala ya ajira zimewasilishwa kwa Rais
wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete ambaye ana mamlaka ya kumfukuza kazi au
uamuzi mwingine wowote.
Japokuwa waziri Nchimbi ametaja pia
maofisa kadhaa wa Jeshi la Polisi ambao wamehusishwa na makosa mbalimbali
lakini binafsi nimeguswa na huku chini kabisa (Makuruta). Kwa maana nyingine harakati za vijana 95
ambao wamefukuzwa na waziri Nchimbi waliokuwa wakitarajiwa kuingia kwenye ajira
ya ndani ya Jeshi la Polisi, linatuletea swali la msingi juu ya maadili na
namna tunavyojenga usalama wetu nchini. Hii ina maana katika Makuruta hao 95
tulikuwa na watu wenye tabia tofauti, lakini baya zaidi wamekutana katika
msingi wa kutoa rushwa ili wapate ajira.
Namna nyingine tunajiuliza mfumo wetu wa
jira katika sekta za ulinzi na usalama ukoje na nani anawajibika kuutengeneza
pale unapokwenda kombo. Makuruta 95 ni wengi au hata wangelikuwa
watano tu, lakini ukweli tunabakia katika mwenendo mbovu wa jamii iliyochoka
kufuata kanuni hivyo kila kitu kinatakiwa kwenda ‘fasta fasta’. Ni tabia hii ya ‘fast tracking’
inatufikisha mahali pabaya kabisa na kushuhudia vijana wadogo wakijihusisha na
rushwa.
Naam kufukuzwa kwao ni ushahidi wa wazi
kabisa jamii yetu imeoza na hata wale viongozi kule juu akiwemo Kamishna Renatus
Chalamila, ni taswira iliyoko huku kondeni. Kama CCP leo hii imegubigwa na vikwazo
vya ajira mpaka vijana wetu watoe rushwa ina maana mfumo wetu wa kutumia
rasilimali watu umegubikwa na maadili duni. Wengi wanatoa ajira kwa misingi ya
jinsia, wajihi, rushwa, na kadhalika.
Kwa namna nyingine sio sifa nzuri kwa
Jeshi letu adhimu la Polisi. Mwanazuoni wa masuala ya kijeshi Sun Tzu kwenye
kitabu chake cha ‘The Art of War” anasema kama jeshi likiingia vitani kisha
likapoteza mwelekeo basi wakulaumiwa ni Jenerali wa jeshi husikal Sun Tzu
anasema iwapo jeshi likiwa kwenye gwaride linatii maagizo yote; kushoto geuka,
kulia geuka, au mbelee tembeaaaa!
![]() |
| Waziri Nchimbi |
Iweje jeshi hilo likapoteza umahiri huo
ndani ya uwanja wa vita. Bahati mbaya Sun Tzu alisahau kuwa katika uwanja wa
vita kuna matukio ambayo yanaweza kubadilisha mwelekeo au tabia za jeshi. Kama mwanajeshi hakuwa thabiti licha ya
mafunzo yake, basi haitashangaza kuona siku moja akishindwa kuingia uwanja vita
sababu tu ya kukosa misingi binafsi ya kulitumikia jeshi.
KWANINI JESHI LA POLISI LIWE NYENZO?
Moja makosa makubwa yanayofanyika katika
jamii yetu ni kushindwa kuelewa watoto wetu wanatakiwa kufanya kazi gani katika
maisha yao. Wapo wazazi ambao hawajui na watoto nao
hawajui wafanye kazi gani hata wanapofika kidato cha nne. Wengi wao wakishapata
matokeo ya mitihani yao ndipo huanza kujiuliza wafanye kazi gani.
Kwa Makuruta 95 waliokubali kutoa rushwa
ina maana kuwa walikuwa wanataka kulitumia Jeshi la Polisi kama nyenzo ya
kufanya kazi nyingine hapo baadaye. Mtu makini akichambua hili na kuangalia
mwenendo wetu kwa Jeshi la Polisi, wapo wanaojiunga sio sababu ya mapenzi yao
bali kwakuwa wanataka ‘kutoka’ kimaisha hivyo mwelekeo uliopo ni CCP Moshi. Sina shaka kabisa, Jeshi la Polisi
linaweza kufanya uchunguzi wa mambo mbalimbali ikiwemo hili. Ni rahisi
kukukotoa idadi ya wahitimu wa Jeshi la Polisi kila mwaka na wanakopelekwa na
muda wao kazini.
Kisha Jeshi la Polisi linaweza kuanza
kufuatilia wahitimu hao kama wameendelea na kazi ya Upolisi kwa muda gani na
wanafanya nini baada ya kujiondoa katika jeshi la Polisi. Ninasema hivi kwakuwa katika nyakazi zetu
Jeshi la Polisi kwa baadhi ya watu wanatafsiri kama sehemu ambayo wanakwenda
vijana walioshindwa maisha hivyo kwa muda fulani wanajua wataweza kupata nyenzo
ya kufanya kazi nyingine.
Ni wazi wengi waliowahi kujiunga Jeshi la
Polisi kwa uadilifu wamedumu na wanaendelea kuheshimu taalumu yao. Lakini wapo
wengine wanalitumia Jeshi la Polisi kama nyenzo ya kufanikisha mipango ya
maisha. Ni kweli wana haki, lakini hawa vijana
wetu baadhi yao wanaweza kabisa kuwa ndani ya jeshi la Polisi kisha baadaye
wakipata njia za kufanya shughuli nyingine (baada ya kuelimishwa na au
kulifanya jeshi kuwa mtaji).
Endapo Jeshi la Polisi limeweza kugundua
Makuruta 95 wameingia kwa rushwa safari hii ni vema likafanya uchuguzi mwingine
juu ya wahitimu wake na vituo vyao vya kazi.
HASARA
Hakuna hasara kubwa kama watu kutumia
idara za usalama kama nyenzo ya kufanikisha mipango yao. Tunahitaji askari
waadilifu na wenye kuipenda kazi yao. Tunahitaji watu ambao sio tu watakuwa
wakilalamikia mishahara midogo bali kutumia kidogo hicho kwa uadilifu na
kulinda maslahi ya nchi yetu.
Lakini hakuna hasara kubwa inayotokea
kama kitendo cha Makuruta 95 hao au wale waliowahi kupitia CCP Moshi na
kadhalika wanaoingia maisha ya kawaida ya mtaani. Katika mazingira haya, “hisia” za
ongezeko la Uhalifu haliwezi kukosekana kabisa. Na ili kukabiliana nalo ni vema
kutafuta njia mwafaka za mkunusuru Jeshi letu la Polisi ili lisiwe na
linakusanya tu kama kokoro na kujikuta limejaza askari wasiowaadilifu.
Ni mbaya, na hatutakuwa tumeokoa jamii
inayoamua kufikiria RUSHWA kwanza ndipo ipate ajira. Ni vyema katika tukio la
Makuruta waliofukuzwa wafuatiliwe na kuhojiwa zaidi, na iwapo wazazi wao
walihusika kuchochea (kama) basi nao wanatakiwa kupitiwa na mkono wa sheria.
Kuwafukuza Makuruta pekee hakutoshi mheshimiwa Waziri Nchimbi. Nimemaliza.
Madhumuni
elimu,
kumbukumbu,
Polisi,
Usalama
Subscribe to:
Posts (Atom)







