Showing posts with label Liwazo. Show all posts
Showing posts with label Liwazo. Show all posts

November 08, 2017

WAAMUZI WETU NA MITIHANI YA SIMBA NA YANGA



NA HONORIUS MPANGALA

TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazotajwa kuwa na amani na hii ni kutokana na muingiliano wa mambo manne.  Yako makundi yaliyojikita katika masuala ya dini, siasa, ushabiki wa soka na mwisho hali ya kuoleana.

Kupitia makundi hayo manne kunapelekea jamii ya watanzania kuishi pamoja. Makundi hayo hukutanisha watu tofauti kutokana na ufuasi wake. Haitakuwa ajabu unapomuona Waziri wa Mambo ya Ndani na kada wa CCM Mwigulu Nchemba akikaa jukwaa moja na kiongozi wa upinzani Freeman Mbowe na kuipa hamasa klabu wanayoipenda ya Yanga. Pia haitashangaza kwa kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe kukaa pamoja na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa na kuipa hamasa klabu yao pendwa ya Simba. Hayo yote hufanyika bila kujali itikadi za kisiasa walizonazo.

November 14, 2012

SHULE ZA AWALI NYASA ZINAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI


Na Albano Midelo, Nyasa
SERIKALI kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi iliamua kuanzisha mfumo wa elimu ya awali katika shule za msingi kwa lengo la kuwaandaa watoto wenye umri kuanzia miaka mitano.
Wizara ya elimu imedhamiria kuhakikisha kuwa watoto wenye umri wa miaka mitano hadi sita wanasoma darasa la awali kabla ya kuanza kuingia shule ya msingi wanapokuwa na umri wa miaka saba.
Uchunguzi uliofanywa katika kata za Kihagara na Liuli umebaini kuwa madarasa ya awali katika shule hizo yanakabiliwa na changamoto mbalimbali hali ambayo inaathiri utoaji wa elimu hiyo muhimu kabla ya kuanzia shule za msingi.

Wanafunzi wa Darasa la Awali wapatao 90 katika Shule ya Msingi PUULU, Kata ya LIULI, wilayani Nyasa wakiwa katika darasa ambalo halina dawati hata moja.

Mwalimu wa taaluma katika shule ya msingi Ndonga kata ya Kihagara Amos Kilongo anasema shule hiyo ina darasa la awali lenye wanafunzi 37 ambao wanasomea kwenye mti kutokana na kukosekana kwa chumba cha darasa na kwamba mwalimu anayefundisha katika darasa hilo ni aliyemaliza kidato cha nne.
“Wanafunzi wa darasa la awali hawana darasa wanasomea chini ya mti,pia darasa halina madawati wa awali wanakaa  wakati wa mvua wanafunzi hao wanasome katika kanisa katoliki ambalo tumewaomba wamiliki wa kanisa hilo wamekubali kutusaidia’’,alisisitiza.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kihagara Anet Ngindo anasema shule hiyo ina darasa la awali lenye wanafunzi 52 ambao wanasomea chumba cha shule ya msingi wakifundishwa na mwalimu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu na sio mwajiriwa analipwa posho kupitia michango inayochangwa na wazazi.
Mwalimu mkuu katika shule ya msingi Tumbi  Evaristo Ndiwu anasema katika shule yake kuna darasa la awali lenye watoto 45 ambalo halina chumba cha kusomea ambapo mwalimu wake hana taaluma ya ualimu ni mhitimu wa kidato cha nne analipwa posho kutokana na michango ya wazazi na walezi.
Katika shule ya msingi Mango,mkuu wa shule hiyo anasema katika shule yake kuna darasa ka awali lenye wanafunzi 60 ambao hawana chumba cha kusomea na  wanafundishwa na mwalimu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu sio mwajiriwa badala yake analipwa posho na wazazi kati ya shilingi 30,000 hadi 50,000 kwa mwezi.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ngehe Silivanus Mbeya anasema katika shule yake kuna darasa la awali lenye watoto 36 ambalo halina chumba cha kusomea na linafundishwa na mwalimu ambaye amehitimu kidato cha nne hana mafunzo ya ualimu analipwa posho na wazazi ambayo haikidhi mahitaji ya mwalimu huyo.

Uvuvi ni shughuli inayoongeza kipato na ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa wilaya ya nyasa. hapa wavuvi wakiwa kazini.

Katika shule ya msingi Puulu  mwalimu mkuu wa shule hiyo Cathibert Maluka anasema katika shule yake kuna darasa la awali lenye wanafunzi 90 na kwamba wanafunzi hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo na ukosefu wa madawati ambapo wanafunzi wote wanasoma kwa kukaa chini.
“Darasa la awali katika shule yetu limebahatika kuwa na walimu wawili ambao wamepata mafunzo rasmi ya kufundisha wanafunzi wa darasa la awali hali ambayo inawawezesha kutoa elimu ya awali kulingana na malengo ya wizara ya elimu licha ya wanafunzi kusomea chini’’,alisema .
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nkali Erasmus Haule  anasema shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi 210 ina darasa la awali lenye wanafunzi 45 ambao hawana darasa badala yake wanasomea kwenye banda ambalo jioni linatumika kama klabu cha pombe na kwamba mwalimu anayefundisha hajasomea.
Katika shule ya msingi Hongi  kwa mujibu wa mwalimu mkuu Simon Ndunguru shule hiyo ina darasa la awali lenye wanafunzi 52 changamoto kubwa hakuna chumba maalum cha kusomea na kwamba mwalimu anayefundisha sio mwajiriwa na wala hajasomea kufundisha darasa la awali.
Katika shule ya msingi Mwongozo yenye wanafunzi 654 inakabiliwa na changamoto ya ubovu wa darasa la awali lenye watoto 81 halina sakafu lina mwalimu mmoja ambaye hana mafunzo ya ualimu ,hajaajiriwa analipwa posho na wazazi wenye watoto hao
Baadhi ya wadau wa elimu katika kata za Kihagara na Liuli ambao ni Neema Msumba,John Ndunguru,Joel Makelele,Melikion Mapunda na Victor Komba wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa kila shule ya msingi inajenga darasa rasmi kwa ajili ya elimu ya awali badala ya shule nyingi kutumia vyumba vya shule ya msingi.
Wameitaka wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi kuhakikisha kuwa kila darasa la awali inapeleka walimu waliopata mafunzo rasmi ya namna ya kufundisha watoto wa awali badala ya tabia ambayo inafanywa na shule nyingi kuwatumia vijana ambao wamehitimu kidato cha nne huku wakiwa hawajapata elimu ya ualimu.
Mratibu elimu kata ya Liuli Abrahamu Challe amesema kata yake imejipanga kuhakikisha kuwa changamoto zote zinazoikabili elimu ya awali katika kata yake yenye shule saba zinatafutiwa ufumbuzi haraka ikiwemo kuwa na chumba rasmi kwa ajili ya awali,walimu na madawati.
Challe ametoa wito kwa serikali kutumia mfumo wa uboreshaji wa elimu ya awali kama ilivyokuwa kwa uboreshaji wa elimu ya msingi na sekondari kwa kujenga  vyumba viwili vya madarasa kwa kila shule na kusisitiza kuwa vifaa vyote vya ujenzi vitolewe na serikali na wananchi waachie ujenzi.
Afisa elimu msingi katika Halmashauri ya wilaya ya Mbinga David Mkali ambaye anahusika na wilaya ya Nyasa anasema elimu ya awali ni sera ya wizara ya elimu kuhakikisha kila shule ya msingi inakuwa na darasa la awali kwa lengo la kuinua elimu hapa nchini.
Ameahidi kushirikiana na viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani,watendaji wa vitongoji,vijiji,kata,tarafa pamoja na wenyeviti wa vijiji kuhakikisha wanahamasisha wananchi katika maeneo yao kusimamia ujenzi wa madarasa ya awali na kutengeneza madawati ili watoto hao waweze kusoma katika mazingira bora.
“Ni ukweli madarasa ya awali yaliyo mengi yanafundishwa na walimu wasiopata elimu ni kutokana na uhaba mkubwa wa walimu uliopo katika shule nyingi nchini,lengo ni kuhakikisha tunapata walimu wa kutosha ikibidi hata kuwatumia walimu wanaostaafu kufundisha katika madarasa ya awali’’.alisisitiza.

Unaweza kuwasiliana na mwnadishi kwa anuani ifuatayo: albano.midelo@gmail.com,simu 0766463129

May 27, 2010

HAPO VIPI?

April 17, 2010

SIRI

HIVI KUNA SIRI YA WATU WAWILI? KWANINI?

April 05, 2010

NATUMIA HUDUMA HII

Baada ya kipindi fulani kutumia huduma za Zantel ambazo kidogo zilikuwa zikikasirisha kwa mambo kadhaa ikiwemo usumbufu fulani. Nilivumilia lakini yakanishinda.

Nakubali hudma ya Zantel katika mtandao wa Tarakilishi ni nzuri na rahisi unaweza kusafiri nayo kwenda popote huku tukuwa na Tarakilishi ndogo.

Lakini sasa natumia huduma hiyo hapo juu, huduma hii unaweza kupata mtandao wa Tarakilishi kwa njia ya simu ya mezani,simu na Flash diski, haya ni mapinduzi katika teknolojia.

Ni huduma poa, ikinusumbua tu nawafuata katika ofisi zao na kufaytuka kwa huduma mbovu sitaki utani tena. Lakini niseme tu ukweli ni huduma ambayo imeniridhisha sana, nimeikubali naiona poaaaaa kabisa. Je wewe unangoja nini? Usipitweeeeeeeeeeeeee

March 26, 2010

NAMJADILI KOERO JAPHET MKUNDI...


NILIAMUA KUIPITIA BLOGU YA RAFIKI YANGU KOERO MKUNDI KWA UMAKINI KABISA. NIMEFANYA HIVYO MAKUSUDI NA NATAKA YEYE MWENYEWE AYASOME MAONI HAYA YALIYOPO KATIKA BLOGU YAKE AKIJADILI SUALA LA UKANDAMIZWAJI WA WANAWAKE.

ZIPO SABABBU ZILIZONIFANYA NIKAMUA KUFANYA HIVI, NA NAAMINI ENDAPO ATASOMA KWA UMAKINI HALAFU AKARUDI KATIKA HOJA ZA MAKALA ZAKE, KUNA JAMBO ANAWEZA KULIONA KWA JICHO LA TATU.

SIWEZI KUSEMA NI NINI, LAKINI INAHITAJI AKILI NDOGO TU KUBAINI. SASA NIMEAMUA KUYAVULIA NGUO MAJI NA KUYAOGA,

 ANGALIA KWA UMAKINI MAONI HAYA AMBAYO NIMETAOA KATIKA BLOGU YAKE WALA SIJAONGEZA AU KUPUNGUZA, NINA HAKIKA UTAFAHAMU KWANINI NASEMA ......NAMJADILI KOERO JAPHET MKUNDI......

PENGINE BAADA YA MAONI YA WASOAMJI NAMI NITAWEKA HOJA YANGU KATIKA UKURASA.........someni wenyewe, na yeye mwenyewe apitie maana katoweka kijiweni kwangu na sababu anazijua mwenyewe...........

wavuti-nukta77 said...


Dada Mdogo Koero,
- uhuru wa kuandika haujaondoshwa.

- hujakiuka sheria wala kanuni.

- hujamzuia yeyote kusema ama kuandika kwa uhuru wake na kwa mujibu wa sheria.

- ukiandika kuhusu wanawake kwa kuwa ndiyo imekugusa na mwingine akataka kuandika kuhusu wanaume kwa kuwa ndiyo imemgusa, ni uchaguzi na uamuzi huru.
Sasa basi,

Makala uliyoandika kipindi kilichopita niliisoma na niliuelewa mtizamo wako na nilisoma baadhi ya maoni ya wachangiaji kwa wakati ule, nao walichukulia kwa mtizamo wako japo ni kweli kuwa wapo waliotoka katika mada kuu na kushambulia mwandishi, nani asiyejua kuwa binadamu ndivyo tulivyo? hasa pale unapokuwa unataka kutoa dukuduku kwa kisa kingine na kufananisha kisa cha sasa na kile kilichopita, ni rahisi sana kubwatuka yote yaliyoujaza moyo wako. Ila hiyo uichukulie kama changamoto kwani hakuna vita rahisi, hasa vita ya kudai haki yako. Unapozungumzia kuhusu wanawake si lazima matatizo yao yawe yamesababishwa na wanaume ingawaje ni vigumu kwa wengine kuliona hilo, vile vile unapozungumzia matatizo ya wanawake hutaacha kugusa wanaume kwa upande mwingine kutokana na jamii ilivyowalea na kuwakuza. Ndiyo maana jamii na jamii hutofautiana, hasa zile jamii ambazo kufanya kazi na kulea familia ni jukumu la wote kwa kuwa si rahisi kumpata 'yaya' wa kuwatunza watoto.

Usichoke kuandika, na mara zote uwe tayari kupokea mitizamo tafauti, inayolenga mada, na inayokulenga wewe binafsi kisha kama ulivyosema, 'ujumbe umefika' nami naongezea, 'that which will not kill you, will make you strong'.

Iko kazi pevu katika kuwaelimisha wanawake juu ya 'misingi na haki ya binadamu' humo ndani kumejaa kila aina ya mazagazaga ya imani, mila, desturi, taratibu, nk nk, tukivuka kigingi hicho tutakuwa tumepiga hatua moja nzuri sana.

PS: Si wewe peke yako unayedhaniwa kuwa kwa kuzungumzia habari za 'wanawake' basi ni 'feminist' ni wengi, mimi pia ni mmojawapo wa kuambiwa hivyo, inagwaje sijawahi kuisoma wala kutaka kuifahamu dhamira ya feminism. Ikiwa kinachoniudhi kimefanyika dhidi ya mwanamke, mwanaume, mnyama nk na inaonekana ni feminism, basi na iwe hivyo, ila kuandika ikiwa kipo cha kuandika ama kusema ikiwa kipo cha kusemea tutaendelea (hata tusipoandika ama kusema sisi, wapo watakaofanya hivyo).

Over and Out!

March 24, 2010 8:24 AM

Fadhy Mtanga said...

Da Koero, mimi sioni tatizo lako. Labda kama mtu ataniambia ukweli ni tatizo. Kama ukweli ni tatizo, basi wewe na da Subi mna matatizo na mnapaswa kuogopwa kama nini sijui!

Tutaishi hivi hadi lini? Kama tunayakubali mabadiliko mengine katika maisha, kama maendeleo ya teknolojia na sayansi, kwa nini hatuyakubali mabadiliko kijamii? Wanawake wataendelea kuwekwa second class hadi lini? Lazima usemwe ukweli. Na ukweli mzuri ni ule unaosemwa na mwathirika wa moja kwa moja wa kadhia fulani. Mambo ya wanawake lazima yasemwe na wanawake wenyewe. Kwani wao ndio waathirika wa moja kwa moja na manyanyaso na kutengwa.

Pana tatizo la wanaoitafsiri dhana ya feminism. Feminism maana yake ni tapo la kupigania ukombozi, haki na usawa wa wanawake. Kiufupi tunasema ni nadharia ya usawa wa wanawake. Ni mtu wa ajabu atakayeona hilo ni tatizo. Kama kuna hitilafu ya mbinu labda zinazotumika katika feminism, hilo ndilo linapaswa kusemwa.

Kuna watu na akili zetu timamu, tunapokusudia kumnyanyasa mwanamke, tunafungua hata Biblia, tunasimamia Mwanzo 3:16 "Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala."

Nimesoma kifungu hicho kwa sababu nikiwa mdogo nilipata kusikia mahubiri mahali kuhusiana na kifungu hicho.

Nimesema mengi. Nifupishe kwa kusema, ni wajibu wenu na haki yenu wanawake kupigania haki zenu.

Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

March 24, 2010 8:49 AM

Yasinta Ngonyani said...

Koero kwanza ahsante sana kwa mada hii nzuri na ambayo imerudiwa mara kwa mara na ambayo mada inarukia upande mwingine.

Saw:- Nimekuwa mara nyingi nikijiuliza hivi kwa nini mwanaume unajifanya kuweza kila kitu lakini lijapo suala la jamii linamshinda tuanze na shughuli za nytumbani utakuta mume anamwambia mke nimekuoa na kukulipia mahari kwa hiyo utazaa watoto, utawalea, utapika, utaleta maji, kuni na shughuli zote za nyumbani. Yaani anamfanya ni mtumwa kabisha Je huu kweli ni upendo wa mke na mume? Na hii inaendelea kizazi hadi kizazi Hivi hayupo au haiwezekana kuwe na MWENYEKITI WA DUNIA WA WANAWAKE. Maana hili swali sio nyumbani Afrika tu wanawake kupata mateso.

Hakika nawaambieni tukijaribu kuwaacha wanaume nyumbani yaani kubadili kazi itakuwa kasheshe. Kwa sababu mwanaume bila mwanamke bado hajakamilika lakini hata hivi anamfanya mwanamke ni mtumwa.Kweli hii ni haki je ule usawa upo wapi?

Tukija kwenye swala la elimu nimeshuhudia mwenyewe na pia kusoma katika vitabu mbalimbali kuwa kuna jamii nyingi wanaamini kuwa hakuna faida kumshomesha mmtoto wa kike, ni kupoteza pesa bure tu. Ndio lakini wanasahau kuwa ni watoto wakiume ndio wawapao mimba watoto wa kike na mwisho kuacha masomo. Kama alivyosema D Subi hii yote inatokana na bado tupo kwenye zile imani za zamani, pia mila na desturi.Kwa hiyo hii ndio inatufanya tuamini kuwa wanawake hawawezi kitu hakuna haja ya kumsomesha kwani akishaolewa basi anakuwa ukoo mwingine. Basi kama wendawazimu na tutakuwa tu kwani ni lazima hili swala la haki za wanawake lipiganiwe na muda wenyewe ndio sasa.Upendo Daima!!

March 24, 2010 2:38 PM

Anonymous said...

Ningependa sana kusikia wanawake mnaongelea nini cha kufanya sasa kuweza kujenga uhusiano na hisia mpya ambayo itampa mwanamke haki sawa na mwanaume bila kuathiri jinsia ya mtu.

Pia, kama wanawake wataacha kupoteza muda mwingi kuzungumzia historia, badala ya kupanga mikakati ya kuondokana na tatizo hili, basi itakuwa ni kupoteza muda bure.

Ukitanguliza chuki kwa kutafuta haki, hata yule ambaye anashutumiwa kwa kukalia haki hataweza kukaa na wewe kusikiliza mlolongo wa pointi za maana ulizo nazo.

Koero, mada zako unazileta vizuri sana, lakini unaingia kwa gia ya hasira na chuki kwa wanaume kiasi kwamba unaonekana kama ....... kwa wanaume, matokeo yake unaishia kusemewa hovyo tu.

Mimi nafikiri mabadiliko yamesha anza kujitokeza, usitegemee kwa usiku mmoja utageuza dhana hii iliyopo.Mambo ni polepole

Bado mimi binafsi sijakuona kama kweli wewe ni mtetezi au mtu wa kukashifu jinsia fulani ndani ya ukweli unaoutoa.

March 24, 2010 4:29 PM

Mzee wa Changamoto said...

"The Way You See The Problem Is The Problem"

Ameeeen

March 24, 2010 11:38 PM

Masangu Matondo Nzuzullima said...

I second the motion..."The Way you see the problem is the problem"

Safari bado ni ndefu!

March 25, 2010 2:55 AM

Markus Mpangala said...

KOEROOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! andika kwa uhuru, andika kwa



mtazamo wako sidhani kama kuna haja ya kuangalia nani anasema nini. Hujui watu tunatofautiana? nakumbuka ulinishtua shutuma hizo, lakini niliandika inawezekana kila mtu anaona aonavyo, hivyo wewe andika unachoamini.

Ingawaje mimi huwa napingana na mambo kadhaa ikiwemo la kulazimisha vita dhidi ya wanaume au kumtazama mwanaume kama tatizom lakini naheshimu sana mchango wako na wengine, nawasikiliza sana kama nilivyosema kwa

Dk Benadetha Kilian kwamba siyo haki kudai usawa wa uwiano wa maamuzi kati ya wanaume na wanawake kwamba lazima tuunde mfumo wa kulenga jinsia, nsema katiba inasema wazi wote ni sawa na hakuna mwanaume aliyepewa haki zaidi.


si kweli kwamba wanawake wananyima haki, usawa hauombwi jamani, utafuteni, sidhani kama wanaume walipewa haki au usawa, na nani aliwapa?

kwa ypte haya lakini nakubali tunahitajika kuzingatia katibu na siyo kusema tuwape upendeleo wanawake na swali linakuja nai alimpa mwanaume?


KWAHIYO, KWA MAONI YANGU KOERO unastahili kuandika kwa haki na kwa ujnzi wa hoja, mwangalie Rais Arroyo hakufika pale kwa kupendelewa bali ana sifa.

kama wanawake kupata fursa au kukandamizwa mimi nalia na hawa wanaharakati wanaotumila 'mihela' kufanya makongamano huku wahitaji wanaumia.

inakera, lakini nani alipewa dhamana zaidi wakati katiba inatamka wote sawa/

ANDIKA, NDIYO UANDISHI WA RAIA HUU, WATU TUNATUKANWA SANA KATIKA MAKALA ZETU, MIMI NI MPINZANI WA MASUALA KADHAA YA MAREKANI

nimeshaitwa gaidi mara kadhaa na nimeongea sana na wakurugenzi wa ubalozi wa marekani mwaka 2008 nikiandikia Rai, nilisema nitaacha kuipinga endapo itaacha ufidhuli.

ninatukanwa hadi kesho na hata na rafiki zangu, lakini nasema mimi siyo RUNNING DOGS vile vijibwa vinavyobweka lakini having'ati na havina msimamo wa masuala wnayotetea.

kwahivyo SIMAMA andika bila WEWE WANAWAKE

WATASAIDIWAJE?????????????????????????????? ANDIKA ANDIKA ANDIKA tena uwe unaandika ukiwa na HASIRA KALI ndiyo hoja inapanda vema kichwani.

March 25, 2010 8:12 AM

John Mwaipopo said...

Leo sichangii.

March 25, 2010 12:31 PM

Anonymous said...

Mwaipopo una busara. Kama mambo menyewe ndio haya. Haina haja bro! Even me, sitacomment again on this childish blog. Koero is an emotional wreck and I swear she will never have a stable marriage huyu. Frustrated and emotionally unstable women like these are dangerous even if they have kids.

Blogs zingine ni miyeyusho tu. Kwa nini ufungue blogu if you can handle the heat? Unataka kila mtu akubali tu mawazo yako finyu? Jesus was criticized sembuse weye uliyekimbia shule? Please? Kama ligwaride limekuwa too much, funga blogu ukauze....bullshit!

March 26, 2010 3:19 AM

Anonymous said...

Mdau wa March 26,2010 3:19, Taratibu ndugu yangu wewe ni mtu mzima na watu tunakueshimu. Kuna haja gani ya wewe kutumia lugha chavu za mitaaani kwenye blog hii?

"Kaero is an emotional wreck" sasa umeishageuka psychologist, wakati unashindwa kujitibu mwenyewe.

Blog za watanzania zimejaa, haukulazimishwa kuingia humu au kucomment chochote, Please grew up!!!

Bloggers, msiwanyamanzie watu kama hawa pindi wanapoingia kwenye viwanja vyenu, kwani njemba kama hizi lengo lao ni kulimit the freedom of speech.

HAHAHAAAAAAAA! HE CAN'T STAND WOMEN IN PANTS.

March 26, 2010 2:50 PM

Anonymous said...

Mdau wa March 26,2010 3:19, Taratibu ndugu yangu wewe ni mtu mzima na watu tunakueshimu. Kuna haja gani ya wewe kutumia lugha chavu za mitaaani kwenye blog hii?

"Kaero is an emotional wreck" sasa umeishageuka psychologist, wakati unashindwa kujitibu mwenyewe.

**************

YOU DON'T HAVE TO BE A PYSCHOLOGIST TO IDENTIFY SOMEONE WHO IS SICK AND NEEDS EMOTIONAL HELP

*************************

Blog za watanzania zimejaa, haukulazimishwa kuingia humu au kucomment chochote, Please grew up!!!

************************

I AM FREE TO VISIT ANY BLOG AND LEAVE MY COMMENTS. PLEASE GREW UP - NO COMMENT HERE. HUNIJUI!!!

*************************

Bloggers, msiwanyamanzie watu kama hawa pindi wanapoingia kwenye viwanja vyenu, kwani njemba kama hizi lengo lao ni kulimit the freedom of speech.

***********************

IT IS PEOPLE LIKE YOU WHO WANT TO LIMIT THE FREEDOM OF SPEECH. SIMPLE, KAMA HAMTAKI KUWA CRITICIZED, THEN DISABLE YOUR COMMENTS PAGE. YOU ARE STILL KIDS WHO CANNOT BE CHALLENGED. MKIGUSWA KIDOGO TU MNAPIGA MAKELELE. THIS BLOG HAS A LOT OF PROBLEMS AND YOU KNOW IT!!!

**************************

HAHAHAAAAAAAA! HE CAN'T STAND WOMEN IN PANTS.

*************************

NAKANYAGA WANAWAKE KWA UZURI NA I AM NOT SCARED OF NO ONE, EVEN YOUR MOM. UKIMLETA MI NABWENGA TU...

KOERO, CLOSE THE BLOGU IF YOU CAN'T HANDLE THE HEAT..........

chib said...

Mengine yanarekebishika, suala la kuzaa ni la mama pekee, lakini pale wanapolazwa zaidi ya mmoja kitandani, ni uelekeo mbovu wa uongozi. Lakini hata ukienda wodi za watoto hospitali za watu wote, utakuta hadithi ni ile ile, sasa sijui hapo tena kuna akina mama basi ndio inakuwa hivyo.....

Kuna mtu alisema... suala la ukombozi kwa wanawake, litaanzia kwa wanawake wenyewe.....

Mambo ya kusutana kwa tarumbeta yaishe nk

Je wanawake mko tayari? Au kimebaki ni kilio cha walio wanyonge tu!! Na wale wenye uwezo wamekaa kimya tuuuu

March 4, 2010 2:14 AM

Albert Paul said...

Kuna kina mama waendao umbali mrefu kuteka maji lakini kwa kutumia magani, wapo pia wanawake waendao umbali mrefu kuchukua kuni na mkaa kwa magari,kwa kuwa tu anaendesha gari au huduma hizi zipo karibu(lkn swala ni lile lile la utekaji wa maji au uletaji wa mkaa) hapa haionekani kama ni unyanyasaji,na hakuna aulizaye waume zao wako wapi.

Wapo wanawake wafuao lundo la nguo za waume zao. Kwa sababu tu umechukuliwa kama utaratibu,basi hata wanawake wenyewe hawaoni kwamba ni unyanyasaji bali ni wajibu wao. Kijana amekuwa akifua nguo zake hadi alipooa lakini baada ya kuoa,swala la kufua linakuwa si wajibu wake tena,kwani tayari yupo mtu mahsusi.Kuna makabila fulani ambayo mwanamke ili amsalimie mwanaume ni lazima apige magoti,au akimkaribisha mwanaume chakula lazima apige magoti,makabila mengine chakula kikitengwa,wanaume wanakula kwanza,wakishiba,kinachobaki ndio wanawake huanza kula. Ajabu kabisa,wanawake wa jamii hizi wanaridhika kabisa na yote haya. Nataka tu kusisitiza pointi ya Ndugu Chacha Wambura kuwa kuna some social and cultural factors lazima zibadilishwe. Kingine ni kuwa tunajaribu kulinganisha mazingira tuliyokulia sisi na mazingira waliokulia watu wengine na kisha tuna conclude kuwa upande ambao unaishi chini ya standard yangu basi unanyanyasika na bila kujua kuwa pamoja na mgawanyo wa majukumu,wanawake wanalazika kukabiliana na hali halisi ya mazingira yao. Kama nilivyotangulia kusema,wakati mwamke wa kijijini anatembea umbali mrefu kuteka maji na kuchanja kuni,mwanamke wa mjini anaendesha gari umbali mrefu kuchukua maji au mkaa au kuni au kwa sababu huduma ya maji ipo karibu basi haoni tabu wala kuhisi ananyanyaswa bali anaona ni wajibu wake.

Ninachoshauri hapa ni kuwa,mbali na kuelezea madhila yawakutayo wanawake ktk mazingira waliyopo,pia fursa nyingi zitumike kutoa elimu juu ya namna rahisi ya kukabiliana na hali halisi za mazingira yao,kutoa elimu kwa jamii juu ya usawa wa kijinsia,uhamasishaji kwa jamii mbalimbali juu ya kuachana na tamaduni na kanuni ambazo zinamlazimisha mwanamke kukubali na kuona mambo fulani (ambayo kimsingi hayakuwa haki yake) kuwa sehemu ya maisha yake na mwisho kuihamasisha jamii na serikali juu ya uboreshaji wa mazingira waishio ili kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu za jamii na zilizo ktk ubora unaotakiwa.

March 4, 2010 11:50 AM

John Mwaipopo said...

Koero asante kwa hii makala. nadhani mimi ni mmoja wa walengwa wa makala hii.

tofauti na chapisho lililopita, hili linaongelea zaidi sera na sio kuonewa ama mfumo dume kama ambavyo matatizo ya wanawake yamekuwa yakitafutiwa mchawi.
tunaposema matatizo ya wanawake tusisahau kuna matatizo ya wanaume hata kama hawayasemi. post iliyopita ilikuwa inamfanya mwanaume aonekane chanzo cha matatizo ya wanawake, kitu ambacho nilitoa angalizo kuwa umetuonyesha wanawake wakitaabika lakini hukuonyesha wanaume zao wako wapi na wanafanya nini. kujifungua ni wajibu wao na nilisema tutamuuliza mungu kwa nini wajifungue wanawake tu. nikauliza hao waume zao wako wapi ili tubaini unyanyasaji huu. sijapata jibu bado.

matatizo ya wanawake mara nyingi yanahusishwa na wanaume. ni kama vile matatizo ya afrika yanapohusishwa na ukoloni kila uchao pasi na kujiangalia kwanza sisi wenyewe. matatizo aliyokuwa nayo mama yangu katu hayakusababishwa na baba yangu.

kwa mfano unaongelea wakinamama kurundikana mawaodini wakati na baada ya kujifungua. sidhani kama hili linasababishwa na wanaume wao. wanaume wao wanakuwa wamehusika na kuwapa mimba tu. hili ni la kisera na kiuongozi kama alivyosema chib. katika hili wote wanawake na wanaume wanahusika. sio wanaume peke yao. tanzania tuna uchaguzi wa kuiweka serikari madarakani kila baada ya miaka mitano. wanaojitokeza kupiga kura wengi ni wanawake. sasa kwa nini wasichague serikari ambayo itajenga mahospitali ambayo hawatalala wawili-waili. watawachagua walewale ambao hawanunui vitanda na hawajengi hospotali.

suala la maji nalo ni kama hilo hapo juu. ni la uongozi ambao sote, wanawake na wanaume, tunauweka madarakani.

Umeongelea kulea kwa shida kuwa wanawake wanahangaika mfano feri kuchuuza samaki kwa ajili ya malezi ya watoto wao. kwanza sidhani kuwa suala la kuzaa ni bahati mbaya. ni makubaliano ya mwanamke na mwanaume kuzaa isipokuwa kama mama alibakwa. Pili kibaolojia tu mtoto akiwa mdogo atakuwa karibu na mama yake ili ahudumiwe ipasavyo. hii haimaanishi baba zao hawajishughulishi na malezi ya watoto. unapotoa mfano wa wakinamama pekee kurundikana feri kuchuuza samaki, pia usisahau ni akina baba wangapi wanasukuma mikokoteni (ukilinganisha na wanawake),wanapiga debe na kadhalika ili kupata kipato cha kusaidia kulea watoto wao. kati ya wafungwa wa wakina mama na akinababa wapi ni wengi ambao walidiriki kujihusisha na uhalifu ili kusaidia familia zao. jibu unalo.

bado hujabainisha unaongelea jamii ipi. kwenye post iliyopita nilikuuliza vipi jamii za kipemba na baadhi kule tanga na hata dar es salaam ambako mwanamke ni marufuku hata kwenda sokoni kununua dagaa kwa pesa alizotafuta mumewe. kaziye ni kupaka hina mwili mzima. haruhusiwi kujishughulisha kwa lolote.

ili tuimbe wimbo mmoja naomba mnisaidie haya mambo.sidhani kuwa matatizo ya wanawake yanaletwa na wanaume. huwa najiuliza hivi kwa nini wanawake wengi ma-activists huwa ama wameachika kwa wame zao ama ndoa zao ziko alijojo. hili sijapata jibu kokote kule.

March 4, 2010 12:02 PM

Anonymous said...

Naona unataka watu wote wakubaliane na wewe kwa kila unachosema. This is not your first time to complain. Ukipingwa au kuhojiwa kiduch tu "Oh, you people hamnielewi"....

You are missing the big picture. One goal ya kuanzisha blogu ni pamoja na kuwa ready to be criticized, querried etc. Not everytime watu wakikuquestion unaanza kulalamika. Anakuwa questioned professor Mbele sembuse wewe!

Your argument here is flawed because you are trying to look at women problems in ISOLATION. May be you need to look at comparative data across Africa; then you will be able to make informed claims. Women problems are deep rooted and will not be dealt with properly by superficial attraction of sympathy.

Next time you see women going to fetch water, ask yourself and then ask them why?

Bear this in mind!

March 4, 2010 10:51 PM

Msomaji Wako said...

Nimependa sana waliochangia wote hasa waliokusahihisha, hasa Albert na John. Hakika hao ni wachambuzi makini, na nimefurahia ya kwamba hata hawachoki kukukosoa kila mara.

Una nia nzuri ya kuwatetea wanawake wenzako lakini kwa njia mbovu, maana wewe unaenendeshwa na hisia na hasira kali badala ya kutumia busara na hekima. Hujiulizi chanzo na hulka za watu, unaiga malezi ambayo si ya kiafrika na wakati huo unawatetea waafrika. Ni sawa na wale wanaotetea ushoga uwepo Afrika bila kuzingatia maadili ya kiafrika.

Hoja zako ni za chuki kwa wanaume, unawaona kama mashetani, kama ukiondoa dhana hiyo utagundua wewe una hisia tu, na kulazimisha wasomaji wako waamini kwamba wanawake wanafanyiwa ukatili na wanaume na ndio maana umezungumzia kuzaa kwa shida, sasa ulitaka wanaume na wao wazae!!! Huu usawa ukitumiwa vibaya ndio utaona watu wanalazimisha kuoana wakiwa wa jinsia moja. Hoja yako ni kupandikiza chuki na wala sio kutetea wanawake.

Kuna baadhi ya wanawake ni makatili kuliko hata wanaume, zingatia yule mama wa Mbagala aliyekuwa anamtesa mtoto wa kike wa kambo mpaka kumsokomeza vitu kwenye njia ya kizazi, je huyo mama ni mwanaume!Mbona hujamzungumzia!!

Wanaharakati wa kike ambao wanakuja kwa hasira sana kama zako huishia kuachana na wanaume wao. Utawakuta wote wenye midomo fyongo hawana wanaume, maana wako kwenye kilele cha chuki na hawaambiliki.

Nakuhakikishia wanawake wengi wakimwona mwenzao anamwachia mume wake kufagia nyumba, kumtawaza mtoto, kupika, kupepeta mahindi, kudeki, kubeba kuni,nk watashamshangaa mwanamke mwenzao huyo hata kama huyo mwanamke atakuwa anapasua mawe, kupiga debe, kubeba watu kuvuka mto wakati wa mafuriko, kuzibua au kuchimba choo na makaburi nk

Unapaswa kuelewa kuna tofauti ya mwanamke na mwanaume, usilazimishe usawa wakati hata kimaumbile kuna tofauti.

Rudi kwenye biblia usome, maana hata Mungu alisema mwanadamu atazaa kwa uchungu, kama unapingana na Mungu, nakutakia kila la heri, na nitashauri uende pale Muhimbili kitengo cha magonjwa ya akili. Kama una sikio la kufa, basi hapa tunampigia mbuzi zumari.

Mwisho ukiona kila mtu hakuelewi, basi ujiulize kwa nini, maana wewe ndio unaweza kuwa tatizo, nyani haoni..........

March 5, 2010 12:15 AM

Anonymous said...

Naona watu wanazungumza kwa hisia kali sana, karibu wamevuka mipaka karibu ya kumkashifu hata na Koero!

Ni kweli Koero unaandika makala na kuhitimisha bila hisia ya kisayansi. Unatakiwa ufanye utafiti uwaulize hao wakina mama kama kweli wanaona wanafanya kazi wasizostahili. Usikurupuke na kumwaga hasira kwenye blogu yako.

Mie nina mke mfanyakazi na kipato chake ni zaidi ya cha kwangu, na kila mtu nyumbani anafurahia majukumu yake hata kama mimi nimechelewa kurudi nyumbani, natekeleza yale yanayonihusu.

Huo usawa unaoupigania ni wanaume kuchukua majukumu ya kina mama, lakini mbona haupiganii wakina mama kwenda kugonga kokoto, kuchimba madini kama akina wana apolo, kwenda kuvua samaki usiku wa manane na wanaume wawahi feri asubuhi kuja kununua samaki. Mbona pale kunapotokea vita ni wanaume wengi ndio wanaenda huko kuuwawa na wanawake wanabaki kutunza familia. Huoni ni mgawanyo wa kazi, au hujui?!.

Kwa ujumla kazi za wanaume ni hatarishi kuliko za wanawake, lakini wanaume wameumbwa na mioyo migumu na kijasiri, badala ya kulalamika tu.

Mija alisema wanawake mnapenda sana upendeleo, ni kweli kabisa, na hiyo inawadhalilisha, inabidi mjitutumue lakini sio kwa kuchukulia mambo kijuujuu na hasira ya mfumo dume.

Mara ngapi kwenye misururu akiwepo mwanamke pekee wanaume wanampa fursa ahudumiwe kwanza, ni sawa na bomba la maji hapo Kigogo.

Mnasahau ya kwamba wanawake ndio wana maamuzi yote nyumbani ya kitu gani kitapikwa nyumbani, nini anunue nk. Ukiwapa wanaume utalia

Wanaume tupo tayari kwa usawa lakini iwe pote, piganieni na nyie kuwa matopazi, ingieni vitani, bebeni mizigo hapo kariakoo, geuzeni wanaume wazae na kunyonyesha. Ukipata mtoto wa kiume anayetaka kuolewa na kidume mwingine mpe haki yake nk.

Pole Koero, acha jazba, andika kama mwanaharakati na wala sio kama mbeijing!

Wanaume watakuwa tayari kubadilika wakiletewa hoja zenye maana na sio za kufikirika

March 5, 2010 10:42 AM

Upepo Mwanana said...

Hii mada imenichanganya kidogo hasa baada ya kusoma hisia za watu!

Mimi namshukuru Mungu kwa kunipa baba aliyenipa muongozo wa kuishi na watu wote, nawashukuru na kaka zangu kwa kunipa heshima kubwa kama mtoto wa kike. Imenipa fursa ya kufanya kazi na wanaume huku nikiwa naheshimika kama ninavyowaheshimu na wao, na nimekuwa planner wakati wao wamekuwa watekelezaji bila kupunguza heshima.

Kwa mtazamo wangu siulaumu kwa hisia kali mfumo dume, nahisi tatizo lipo kwetu wanawake pale tunaposhindwa kujitambua ya kuwa tunatakiwa kuwa ngangari kwenye kila kitu tukija na nguvu ya hoja na sio hoja ya nguvu.

Matatizo mengi ya akina mama yanahusiana na mfumo mbaya wa kiungozi au kisiasa, kukosekana kwa hospitali za kujifungua sio sababu ya mfumo dume, kwani wanaokufa ni wengi wakiwemo watoto na wanaume pia.

Sababu za akina mama kuzaa majumbani ni tatizo la akina mama wenyewe, kwani kuna ushahidi kuna sehemu wakunga wa jadi huwalazimisha mabinti wawapo hospitali kuondoka wakati wa kujifungua ukikaribia, pia wauguzi wakunga wengine (tena wanawake), wana matusi mabaya sana wakati wa uchungu, pia kukosekana wa zana za kujifungua watu hunyang'anywa walizokuja nazo kuwasaidia wasio nazo, hivyo akina mama wajawazito huchelewa makusudi ili zana zao zisichukuliwe, na pia kuepuka kulala wengi kitanda kimoja. Mfumo dume hauna chochote hapa.

Hulka ya waafrika pia ni chanzo cha baadhi ya MATATIZO YA AKINA MAMA.

Kwa mtazamo wangu nafikiri hatuwezi kuubadili kwa ghafla mfumo huu, tunahitaji kuwaelimisha akina mama wenzetu kwanza na ndipo hapo shughuli ya kuweka huo usawa wa kweli utakuja, lakini siamini ya kuwa total reversal is fair, yaani leo baba aanze kulea mtoto nyumbani, afue nk, je akina mama usawa utakuwa wapi, kwenda kufanya kazi ngumu? La hasha, tunapaswa kuheshimiana na kupendana, we need badly each other. Hakuna mambo ya visasi au kukomoana. Mimi naona wanawake tuache kufikiria kupendelewa au kuonewa huruma kwanza, tuingie kwenye ushindani wa kikweli na wanaume kama tunataka usawa. Angalau huo ndio mtazamo wangu binafsi

Yasinta Ngonyani said...

Kwa kweli inaumiza sana jinsi wanaweke tunavyoteseka. Sijui hii ni laana. Nashindwa hata la kusema maana ni kweli watu tunalia na tunalia lakini......basi ngoja niache kwani chozi lanidondoka hapa sioni kitu..

March 1, 2010 11:18 AM

Mija Shija Sayi said...

Yasinta si laana wala nini, ni kwa sababu wanawake tumezidi kulialia sana na kupenda upendeleo. Kwa ufupi sisi wenyewe tunayataka, hebu angalia uwezo tulio nao wa kuyakabili maisha, kuanzia zoezi zima la mimba hadi kuzaa, kuitunza familia peke yetu huku waume zetu wakiwa vilabuni, kudunduliza vijihela vidogo tulivyo navyo hadi kusomesha wanetu na mengi mengine.

Kama yote haya tunayaweza tujue hata machozi tunaweza tukajifuta wenyewe tusisubiri kufutwa, ni suala la kuamua na KUJIAMINI tu.

Tusikubali na tusikubali kwa vile:-Nia tunayo na Nguvu tunazo za kuweza kumuangamiza huyu adui UWOGA.

Subirini niingie madarakani.

March 1, 2010 3:40 PM
Kissima said...

Dada Koero, yawezekana kabisa wanawake hao walikuwa wanakabiliana na hali halisi ya mazingira yao,ninamaanisha kwamba hali hiyo wasingeweza kuikwepa kulingana na mazingira yao. Je, unafahamu waume zao walikuwa wapi kwa wakati huo? Yawezekana kabisa kuwa kuna mgawanyo wa majukumu kiasi kwamba waume wao nao walikuwa ktk mazingira fulani wakipigika vilevile na pengine kwa kazi wazifanyazo ungeweza tena kuwahurumia mara mia zaidi. Kwa hiyo kabla ya kusema wanawake hao wananyanyasika ni vema pia tukajua upande mwingine nao unafanya nini na kama hakuna mgawanyo sahihi wa majukumu pia ijulikane.

March 1, 2010 4:49 PM

John Mwaipopo said...
au inawezekana koero uliwaona wanawake wajane tu. huko ulikopita hakukuwa na wanaume? na kama wakikuwako wakikuwa wanacheza karata ama wanakunywa pombe? kama walikuwa wakistarehe, basi tuna haja ya kuwalilia wanawake watesekao. nasema watesekao maana wengine wanatesa kutegemea jamaii na jamii. kule tanga na pemba mwanamke haruhusiwi kufanya kazi ama hata kwenda sokoni kufanya manunuzi. kazi yake ni kupaka hina kila mtindo na kujifukiza udi na kula kungumanga. mchangiaji mmoja ameongelea pengine ni mazingira yao ndio yanawalazimu kufanya hivyo. hebu tujuze waume zao walikuwa wapi na wakifanya nini.

hilo la kubeba mimba na kuzaa tutamuuliza mungu siku ikifika.

March 1, 2010 6:11 PM

Mzee wa Changamoto said...

Ouch!!!!

Heaven Help Us All

March 2, 2010 6:04 AM

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Mnalitazama hili suala kwa mtazamo na mantiki gani? Mmejaribu kuongea na akina mama hawa wakawaambia kwamba wana shida? Kuweni makini na jambo hili ili msije mkaingia katika mkumbo ule ule wa 'wataalamu" wa Anthropolojia na Historia kutoka Ulaya waliofikia majumuisho (generalizations0 ya kushangaza walipotia guu lao Afrika kwa mara ya kwanza!
Nendeni mkaongee na wanawake hawa kwanza. Mtakayojifunza huko yatawashangaza na pengine yatabadili maoni yenu kabisa. Nina mifano mingi ya ninachokisema hapa!

March 2, 2010 11:20 PM

Mija Shija Sayi said...

Hii ndiyo raha ya kublogu jamani, tunajifunza mengi. Mwl Masangu umeongea jambo la msingi sana.

March 3, 2010 3:03 PM

Anonymous said...

You ran away from UDSM claiming that the education there is NO good. It is beginning to show now; and you will live to regret that decision of yours regardless of whether you are rich or not.

Probably people don't understand you because your articles are superficial, emotional and half cooked. If you had stayed at Mlimani ant took classes on Philosophy, Psychology and Fundamental Statistics/Logic, it would have helped you a lot - not to become rich but kupanua akili yako and your thinking capacity.

Punguza kupiga makelele. There is a reason people don't understand you. Your mother was right; and she will always be right. You need to go back to school girl!!!

MWISHO WA KUNUKUU. LEO SITASEMA, KWANI HAPO NDIPO PENYE AKILI NA HEKIMA.
NAWASILISHA!

Markus H. Mpangala

June 18, 2009

Nani anapenda KISWAHILI chenu kichafu???

Kila nikipitia mitandao au kusoma magazeti nakutana na matumizi mabaya ya kiswahili, wengi tunatumia kiswahili vibaya, mtamshi mabaya, silabi mbovu, kanuni za lugha zimetupwa yaani kila kitu ovyoovyo tu.
Sina hakika kwanini jamo hili linasingiziwa kwa njia ya teknolojia lakini nidhahiri utandawazi ni nguvu ya utamaduni mwingine kwahiyoiwapo nchi inakuwa kama kundi la magabachori wale wasiojali hali za wengine na kukumbatia hali zao hata kama mbovu basi mambo ni juu ya mambo kuwa mabaya.

Yaani neno AAMINI= wanamaanisha HAAMINI
AMNA= wanamaanisha HAMNA
KUWA NA KUA= linatumika vibaya kwa kudhani ni maana moja
LISAA NA MASAA= wanamaanisha SAA
UJUI wanamaanisha HUJUI
UO wanamaanisha HUO.
ALAFU wanaamisha HALAFU

Nani kasema huo ndiyo ukweli wa lugha yetu adhimu? Kiswahili gani kibovu namna hii halafu mnasingizia zama mpya? Natamani kumezwa na ardhi yeoteee inifunike ili nikose kuyaona lakini natamani kuendelea kuishi. Badilikeni lugha iwe katika mhimili wake

November 01, 2008

mto ruvuma unaotenganisha TZ na Msumbiji

hapo sawa tu. KARIBUNI RUVUMA, WEKEZA UFAIDIKE SASA.

October 14, 2008

kama ninge...... kama ningekuwa Nabii Mwalimu Nyerere

wale wanaoabudu dini zao wana manabii wao. Nami sioni soni kukuita Nabii wa kweli kwa imani ya kiafrika wala iyo wale waliozaliwa mashariki ya kati. Mungu wetu yu pamoja nawe. kama ningekuwa wewe .........

October 09, 2008

habari ndiyo hiyo

hapa hakuna la mnadi swala wala sauti za kanisa, mchezo ni kujiburudisha, mchezo kufurahi yanini kujibana wakati muda wenyewe robo eti tutakwenda peponi mmmm

October 04, 2008

karibuni nyasa

njooni nyote marafiki na waio marafiki nyote mwakaribishwa

September 26, 2008

nchuwa/bao.........................jaza jina unalolijua

September 21, 2008

haaa haaa haaaa sicheki nafurahia ngoma

angalia uone utamu wa kupenda utamaduni wako, si unaona ilivyo na raha? kazi kweu msiopenda utamaduni mtamu kama wa kiafrika.

July 15, 2008

ujumbe wa leo

'Utii bila uhuru ni utumwa'

July 05, 2008

Kimya Kimya Leo Mawazo Sana

June 14, 2008

Tulimwomba Mungu Atulinde kama Hivi

Hivi wachezaji wetu walivyomwomba mungu awalinde shauri ya kuwakilisha taifa dhidi ya kameruni leo jumamosi

June 08, 2008

Hatujashindwa Tunasonga Mbele kama Hivi...

Ni kweli Timu yetu ya Taifa imefungwa jana na Timu ya Cape Verde bao moja, lakini haimaanishi kwamba tumeshindwa,tutashangilia na kujionea fahari ya timu yetu yaTaifa 'TAIFASTARS' kama hivi,tena kwa moyo mmoja,upendo mmoja,amani moja na juhudi Moja wala siyo The Philosophy Of loser.Tunaimanai na Maximo Wetu tuna imani na kila mchezaji kwani hao ndiyo mtaji wetu wa kuelekea kuwa na kina Zidane wetu,saa zaja,wakati waja twende pamoja jumamosi tukawashangilie kaka zetu vijana wenzetu dhidi ya kina Eto'o wa Kameruni.....Twende pamojaaaa iwe kwa upendooooo .....marafiki zaidiiiiiii..

Janeti na Hamu ya Njika kusoma Blogu

Kuna jamaa hapa ananitazmasana sijui anashangaa nini.Labda tokana na kasi yangu ya kundika hapa bloguni.Lakini namfahamu sana huyu jamaa unajua jina lake nani?nimemkumbuka umeona jina la mtu mwenye hamu ya kublogu hapo juu?Ndiye huyo anaitwa Njika Clara ni ndugu yangu,basi leo nimemnogesha kublogu nakwambia amebaki kutola mate tu jinsi anavyonogea mmm halafu ananiudhi amshika shavu sijui anamanaa gani.Najua hapa akitoka hapa nyasa anahamu ya kwenda kumtembelea shangazi yake mtaa fulani najua anafuata samaki tu si unajua wanyasa kitoweo chao.uache hilo,kuna mwingine tazama jina lake mwanzo "Janeti" basi jana kasoma blogu ya nyasa hii mpaka akakasirika kisa wivu eti wanyasa wanajidai na blogu yao.Haa nikammwambia mbona nawe mnyasa?akaniambia haijalishi ila wanyasa tunaringia kublogu.Lakini akamaliza kwamba hata yeye Blogu hii inamhusu shauri ye mnyasa.Basi huyu Njika anasoma blogu hii naona mpaka njaa inamuuma sijui hajala..ebu mtazama huyo hapo pembeni anakunja ndita sababu gani?.Mmmmm timu yetu ya taifaimefungwa na CapeVerde bao moja jana mmmm inauma sana

June 03, 2008

Washashi Nao Wamegota Nyasa

Naona nisiandike mengi,kwani nianchofanya ni kutoa ushuhuda wa "Karibuni Nyasa' ona Washashi nao wamegota.Washashi ni wazungu si unajua lugha za maeneo ya kizungu kwa vijana.Hatushangai tunajiunga nao tu...

June 02, 2008

Nyasa .....Hiyo usiulize Maswali picha itakasirika ..

Usiul;ize mnyasa vipi mbona kuna mtu hapo humtaji au hao huwataji?Mimi nakupa madoido ya Nyasa wala sitaki kelele.Mimi mtoto wa kinyasa utanimbia nini wakati najua utamu wa kuishi nyasa.Ngoja kwanza...jana kulikuwa na kichekesho eti jamaa alitaka kunitwanga ngumi wakati naadaa hizi picha,kisa eti wanyasa wanajiona matawi ya juu wakati hawana lolote.Mimi nikamwambia ingelikuwa hawana lolote basi wangelikuwa vichaa kwani mungu katuwekea kitu na tunacho nacho ni ubongo hivyo huwezi kumwambia mtu hana lolote kimaisha.Labda akifanya ujinga au kuleta ujivuni wakati hana ujuzi wa kile anachokisema au kukifanya.Yaani wapo watu ambao hawapendi kuheshimu wanachofanya wenzao hata kama ni jambo dogo....Nakwambia nilikasirika nikapiga ngumi kali ukutani lakini niliumia mpaka sasa nimefungwa bandeji nauugulia sana kisa kutetea wanyasa...njooni mnipe pole hata kuandika hapa natumia mkono mmoja tu wa kushoto......mbona hamnipi pole nanyi mna kisirani na wanyasa.....nitalianzisha varangati....ooooo ngoja nipone kwanza.