Showing posts with label utulivu. Show all posts
Showing posts with label utulivu. Show all posts
March 07, 2018
KITABU KIPYA KUTOKA KWA MWANDISHI BEKA MFAUME
March 05, 2018
MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU BUSTANI YA MUNGU- HIFADHI YA KITULO.
1.Hifadhi ya Taifa Kitulo ndiyo
eneo pekee Tanzania lenye ndege aina ya tandawala machaka (Denhams Bustard)
wenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.
2.Hifadhi hiyo inayopita katika
mikoa ya Mbeya na Njombe ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005
ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo, msitu wa Livingstone na bonde
la Numbi.
3.Kitulo ina ukubwa wa kilometa
za mraba 442. Awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick
Elton kupita eneo hilo mwaka 1870. Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo
(FAO) lilichukua eneo hilo kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
4. Ndege aina ya tandawili
machaka hawapatikani sehemu nyingine yoyote hapa Tanzania zaidi ya Kitulo.
5.hifadhi hiyo ndiyo eneo pekee
ambalo ndege hao hutaga mayai na kuzaliana kwa wingi kabla ya kusafiri kwenda
mabara mengine.
January 06, 2018
JIMBO LA NYASA: KWANINI WANANCHI WAISHI BILA HUDUMA ZA POLISI?
NA MARKUS MPANGALA, August 24,
2017
JESHI la Polisi limepata
Kiongozi mpya, Kamanda Simon Sirro. Kiubindamu Kamanda Sirro si mtu mpya
kwakuwa anafahamika tangu makuzi yake. Kiuongozi Sirro anafahamika tangu akiwa
askari wa cheo cha chini, Mkuu wa Operesheni na Mafunzo na baadaye Kamishna wa
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam.
| Nikiwa nazungumza na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa. |
Hii ni sehemu ndogo tu kumhusu
Sirro ndani ya Jeshi la Polisi. Kwa maana hiyo kiongozi huyo mpya aliyechukua
nafasi ya Ernest Jumbe Mangu anao wajibu wa kuendeleza na kuleta ufanisi wa
utendaji wa Jeshi la polisi nchini.
Pamoja na hayo ninalo jambo
linaloniogopesha mno kwenye jamii zetu. Nimechunguza kwa muda mrefu na baadaye
kuchora picha ya miaka ijayo, kwamba ni kwa namna gani tutaendelea kuishi
katika jamii ambayo haina vituo vya Polisi?
Ni kwa vipi wananchi wawe mbali
na walinda usalama na mali zao? Ni kwanini wananchi washindwe kupata huduma za
Jeshi la polisi nchini kwenye baadhi ya maeneo? Chukulia mfano maeneo yaliyoko
mipakani, lakini hayana vituo vya jeshi la Polisi.
Takwimu za Jeshi la Polisi
zilizoko kwenye tovuti yao (www.policeforce.go.tz) zinaonyesha kuwa matukio ya
uhalifu na ajali zilizoripotiwa kati ya Januari hadi Desemba 2015 ni 1,909,685.
November 09, 2017
WILAYA YA NYASA INAO UTAJIRI WA VIVUTIO VYA UTALII
Madhumuni
mbamba bay,
Nyasa,
utalii,
utulivu
MAMBO 50 YA KISAIKOLOJIA YATAKAYOKUACHA KINYWA WAZI
NA VITUS MATEMBO, MBAMBA BAY
![]() |
| Mwonekano wa ufukwe wa Mkwakwa katika Ziwa Nyasa. |
Hii ni kweli hata kama ulikua hujui kubali tu, maana ndio
ukweli uliopo.
1. Mtu hufanya ishara nyingi za mikono akiwa anazungumza
ukweli. Azungumzae uongo mikono yake huwa imetulia zaidi.
2. Sikiliza kwa makini namna mtu anavyozungumzia watu
wengine akiwa na wewe, na ndivyo atakavyokuzungumzia wewe akiwa na watu
wengine.
3. Ndoto zako zinabeba ujumbe mhimu sana. Asilimia 70 ya
ndoto zako zina ujumbe wa siri.
4. Kwa kawaida watu huwa waaminifu na wakweli mwili ukiwa
umechoka, na ndio sababu hutubu na kutoa siri zao kwenye mazungumzo yatekeayo
usiku wa manane,
Madhumuni
Nyasa,
Sayansi na Teknolojia,
utulivu
October 17, 2017
MANDHARI YA KIGOMA
Madhumuni
Maendeleo,
mila na desturi,
utulivu,
wageni
October 16, 2017
CHUO CHAANZISHA SHAHADA YA WADUDU
NAIROBI, KENYA
KITUO cha Elimu na Utafiti kinachofadhiliwa na Benki ya Dunia kimeasisiwa katika Chuo Kikuu cha
Sayansi na Teknolojia cha Jaramogo Oginga Odinga na kinasubiri ruhusa ya
kuanzishwa kwa programu za Uzamifu na Uzamili kuhusu wadudu wanaoweza kuliwa.
Taasisi hiyo inapania kubuni njia za kuzalisha wadudu hao
kwa wingi bila ya kuharibu mazingira ili kukidhi utashi mara baada ya wazo hilo
likifanywa kuwa biashara.Wadudu wanaoliwa sana maeneo ya Magharibi mwa Kenya, ambao
wana wingi wa madini ya protini na Zinki watafanywa kuwa biashara ili
kuimarisha uwepo wa chakula cha kutosha, na kuondoa dhana mbaya katika kula
wadudu.
Madhumuni
habari,
Mafanikio,
maisha,
Sayansi na Teknolojia,
Teknolojia,
uhai,
Utafiti,
utulivu,
Vitabu
October 14, 2017
WATU WASIOJULIKANA WATAIKIMBIZA AFCON U-17 2019
NA HONORIUS MPANGALA
MWANDISHI maafuru wa fasihi kutoka Nigeria,marehemu Chinua Achebe katika kitabu cha 'Things Fall Apart' alisema kukimbia matatizo sio njia sahihi ya kutatua hayo matatizo. Wakati msomaji wa fasihi hiyo akiona kama burudani kusoma vibweka vya Okonkwo lakini kuna mafundisho katika kitabu kile. Nyakati zote huwezi kuona ugumu wa jambo kama halijakutokea.
Chinua ananifanya nihusianishe matukio ya watu wasiojulikana na hatima ya Nchi katika nafasi ya kuandaa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa chini ya miaka 17.
Ukimya wetu
katika kuchukulia kila jambo ni kitu kinachofanyika na tukashindwa kutambua
tatizo au kuwabaini wahusika linaweza kutuondolea mwonekano wetu nje ya mipaka
ya nchi.
Matatizo yanatakiwa kutatuliwa kwa kufahamu chanzo na kuchukua hatua ya kuyamaliza. Sisi kama Taifa tuna hamu kubwa na kuona tukifanikisha Michezo inafanyika vyema hapa nchini kwa kuhusisha sekta zote kushiriki vyema.
Labda nikumbushe jambo moja baada ya Afrika kusini kutangazwa kama waandaaji wa fainali za kombe la dunia mwaka 2010.
MWANDISHI maafuru wa fasihi kutoka Nigeria,marehemu Chinua Achebe katika kitabu cha 'Things Fall Apart' alisema kukimbia matatizo sio njia sahihi ya kutatua hayo matatizo. Wakati msomaji wa fasihi hiyo akiona kama burudani kusoma vibweka vya Okonkwo lakini kuna mafundisho katika kitabu kile. Nyakati zote huwezi kuona ugumu wa jambo kama halijakutokea.
Chinua ananifanya nihusianishe matukio ya watu wasiojulikana na hatima ya Nchi katika nafasi ya kuandaa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa chini ya miaka 17.
![]() |
| Serengeti Boys wakifurahia katika moja ya mabao waliyofunga katika mechi za kimataifa |
Matatizo yanatakiwa kutatuliwa kwa kufahamu chanzo na kuchukua hatua ya kuyamaliza. Sisi kama Taifa tuna hamu kubwa na kuona tukifanikisha Michezo inafanyika vyema hapa nchini kwa kuhusisha sekta zote kushiriki vyema.
Labda nikumbushe jambo moja baada ya Afrika kusini kutangazwa kama waandaaji wa fainali za kombe la dunia mwaka 2010.
September 30, 2017
UTUNZI WA VITABU NA KISWAHILI CHA PROFESA SHAOPING
NA KIZITO MPANGALA
KESI YA ALMASI
ni kitabu kilichoandikwa na Profesa Rao Shaoping wa China. Kitaaluma yeye ni
mhandisi. Alijifunza Kiswahili nchini Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja na
ushee, mwalimu aliyemfundisha aliitwa Ali Omari Mzee.
Profesa
Shaoping ndiye msimamizi wa kazi za TAZARA wakati inajengwa. Alikuwa
akimtafsiria Mwalimu Nyerere mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na wenzake. Pia
alikuwa mkaliamani kwa Mh. Salim Ahmed Salim, Mh. Rashid Kawawa, Spika Adam
Sapi kwa mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na Wachina wenzake. Na mwaka 2013
Profesa Shaoping alikuja tena nchini Tanzania kumtembela Mzee Ali Hassan
Mwinyi.
Profesa
Shaoping anasema hivi "ninaipenda Tanzania. Ninawapenda watu wa
Tanzania". Profesa
Shaoping anayafahamu maeneo mengi nchini Tanzania ambayo amewahi kutembelea,
maeneo hayo ni kama vile Kisuwa cha Saa Nane, Arusha, Ifakara, Iringa, Kimbwe,
Kidatu, Mikumi, Makambako, Mbarali, Tunduma, Zanzibar, Moshi, Dodoma na
kadhalika.
Profesa
Shaoping ameandika kitabu hiki kwa bidii mno. Anasema tangu tuwe Koloni la
Mjerumani na baadae Mwingereza, wageni hao hawakuwa na morali ya kutunga riwaya
za Kiswahili lakini yeye kama mgeni alipenda sana kuacha kitabu kwa Kiswahili,
naam, ndicho hiki hapa pichani.
Madhumuni
diplomasia,
elimu,
falsafa,
Teknolojia,
utulivu
September 29, 2017
UFUKWE WA BANDARI YA MBAMBA BAY
September 27, 2017
UHONDO WA KITABU
Wahenga wanasema kitabu ni sila. Mwanamke huyu alikutwa akisoma kitabu ndani ya Basi la Mwendokasi kati ya Mbezi-Posta kupitia barabara ya Morogoro jijini Dar es salaam.
Usomaji wa vitabu huongeza maarifa.
Mwanamke huyu alikutwa akichagua kitabu cha kujisomea katika eneo la Mbezi jijini Dar es salaam.
Huyu alitafuta eneo zuri kwake linalomwezesha kusoma kitabu kwa utuvuli.
PICHA ZOTE NA KIZITO MPANGALA
September 21, 2017
UJENZI WA UKUTA MKOANI MANYARA
PICHANI: Meja
Jenerali Michael Isamuyo atua Mererani, Mkoani Manyara kukagua maeneo ambayo
ukuta utajengwa kwa ajili ya ulinzi wa madini.
May 30, 2013
MANDHARI YA FUKWE ZA ZIWA NYASA KATIKA WILAYA YA NYASA
| |
| Ardhi yenye rutuba wilaya ya Nyasa |
![]() |
| Beach ya BioCamp-kijiji cha Ndengere wilaya ya Nyasa |
![]() |
| Kilimo cha Maksai katika kijiji cha Lundo wilaya ya Nyasa |
![]() |
| Ufukwe wa Mbamba Bay upand wa kaskazini kuanzia bandarini |
![]() |
| Ufukwe wa Mbamba Bay upande wa kaskazini kuanzia bandarini. |
![]() | |||
| Zabibu Nyasa |
October 27, 2012
NYUMBANI LUNDU
Picha hii inaonyesha maeneo ya kijiji cha Lundu. Maeneo hayo ni mtaa wa Maliwa au Missionari, na wka upande wa magharibi kushoto unaonekana mlima ambao unaitwa Chipyaghela. Kisha maji ya ziwa Nyasa yanaonekana. Huu ndio mji ulionikuza na kunilea, katika mitaa yangu ya Maliwa, au missionari.
Picha hii imepigwa na kaka Egbert Jeremy aliyeko wilaya ya Nyasa katika shughuli za ujenzi wa miundo mbinu. Lundu ni miongoni mwa vijiji ambavyo anaendelea kujenga miundombinu ya wilaya hiyo. Karibuni kuwekeza wilaya ya Nyasa ambayo imeanza kutoa fursa mbalimbali. KARIBUNI NYASA
Picha hii imepigwa na kaka Egbert Jeremy aliyeko wilaya ya Nyasa katika shughuli za ujenzi wa miundo mbinu. Lundu ni miongoni mwa vijiji ambavyo anaendelea kujenga miundombinu ya wilaya hiyo. Karibuni kuwekeza wilaya ya Nyasa ambayo imeanza kutoa fursa mbalimbali. KARIBUNI NYASA
Madhumuni
amani na upendo,
falsafa,
familia,
habari,
Hisia za moyo,
kumbukumbu,
mila na desturi,
Nyasa,
siasa,
soka,
uchambuzi,
Uchumi,
urafiki,
utamaduni,
utulivu,
uzuri
October 17, 2012
HARAKATI ZA MAENDELEO WILAYA YA NYASA, KARIBU KUWEKEZA
Wilaya ya Nyasa ni miongoni mwa Wilaya mpya zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya nne. Habari za kuundwa wilaya ya Nyasa nilianza kuzisikia mwaka 1993 nikiwa shule ya msingi. Lakini mwaka huu Wilaya ya Nyasa imezinduliwa rasmi na shughuli za maendeleo zinaendelea ili kukidhi mahitaji ya wananchi. Katika harakati hizo ni pamoja na huduma ya Maji ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Hapa ni picha mbalimbali ambazo zinaonyesha suala la upatikanaji wa maji katika vijiji mbalimbali wilayani humu. Bila shaka wageni na wenyeji watavutiwa kuwekeza katika wilaya mpya ambayo fursa mbalimbali zinajitokeza. karibuni. Picha zote na Hoops Kamanga
Chanzo cha Mradi wa maji kikifanyiwa ukaguzi.Tenki la Maji katika mradi wa maji katika kijiji cha Ng'ombo wilaya ya Nyasa
Mradi wa Maji katika kijiji cha Kindimba Juu ambao umekamilika na wananchi wanategemea kutumia siku chache zijazo. Hapo fundi anamalizia marekebisho katika tenki.
June 03, 2010
NIKUPE NINI??
Moja ya wasanii wa Mukirikiri, ila samahani nimeshindwa kutamka kwa ufasaha jina lao. Jamani ugonjwa wangu wa utamaduni ulinifanya nitulize 'boli' hapa kwa kujinufaisha na kujipendelea kutazama tu aina ya mvao wa kitamaduni.
Angalia na hapa chini kidogo iko vipi kadiri utazamazpo?
Mimi naona vizuri a.k.a African Bantu hadi nimemkumbuka Bambuu, yule mwanamuziki wa Kenya. Mwenye namba yake ya simu au anuani pepe naomba tafadhali..............Lol
April 09, 2010
HERI WAZAZI WANAOKULEA CAMILLA T.K!
CAMILLA T.K
Umekaa umetuliya,
kazi zako jifanyiya,
mafunzo shikiliya,
Camilla nakushangliya,
mwana kujifuniya
baba na mama fikiriya,
malezi kushikiliya,
mema kujivuniya,
makuzi yasikurabiya.
Heri baba alinaekulea na heri mama anayekulea
Camilla, bado kazi moja ya kulima maana sijui (?) kama umeshaanza. Ila usilalamike sana, ungekuwa kipindi hiki Bongo kuna kiubaridi ambacho kingekufanya uache kushinda ndani ya maji kama samaki...Lol..
Heri wazazi wanaokulea, heri kwao kukupatia malezi bora,kazi kujifunzia na mengineyo mema. Love you Baby Gal
Umekaa umetuliya,
kazi zako jifanyiya,
mafunzo shikiliya,
Camilla nakushangliya,
mwana kujifuniya
baba na mama fikiriya,
malezi kushikiliya,
mema kujivuniya,
makuzi yasikurabiya.
Heri baba alinaekulea na heri mama anayekulea
Camilla, bado kazi moja ya kulima maana sijui (?) kama umeshaanza. Ila usilalamike sana, ungekuwa kipindi hiki Bongo kuna kiubaridi ambacho kingekufanya uache kushinda ndani ya maji kama samaki...Lol..
Heri wazazi wanaokulea, heri kwao kukupatia malezi bora,kazi kujifunzia na mengineyo mema. Love you Baby Gal
Madhumuni
kumbukumbu,
ughaibuni,
utulivu,
uzuri
May 15, 2009
"HAPPY BIRTHDAY MARKUS"

Hongera MARKUS HONORIUS MPANGALA, mwana wa nyasa umpendaye MALCOM X kila leo au JENERALI ULIMWENGU na JULIUS NYERERE, amani kwao watu hawa!
UPENDO UWE NANYI
Nashukuru baba na mama
Kwa kunileta hapa duniani
Nami najivunia kuishi ndani
Nashukuru sana wangu maanani
Kwani yupo nami kwa shida na raha
Kama machozi na majonzi naamini yanapita
Nashukuru ndugu waliopo hai
Na wale wasiohai, nawapenda kikweli
Upendo wangu, zaidi ya mshumaa
Nitawaangzia kwa uwezo wangu daima
Ningali nawajali, upendo usiopimika
Kwani ni tunu yake maulana
nawashukuru marafiki zangu nyote
Bila ninyi nikiri siyo mwenyewe
Najua imani yangu nimejaza kibaba
Naamini mola yupo nasi daima
Anajali,kutulinda na kutuhusudu
Ndiyo maana avumilia wetu utundu
Nawashukuru enyi wapenzi mlokuwa nami
Nawapenda kama amri ya mola
Kwani ni agizo la thamani daima
Nipo nanyi kwa mapenzi ya maulana
Nawashukuru maadui wote
Kwani mnanifanya niwe kama nilivyo
Bila ninyi sitokamilika, nawapa upendo
Mungu mkubwa.
Ni siku yangu ya kufurahia kuzaliwa kwangu, nashukuru wanablogu wote mliopo karibu nami. kwa pamoja tuseme waweke upanga au shoka au kufa ama kupona-mtaani tutabanana kwa pamoja tutafanikiwa kile kinachotakiwa kufanikiwa.
Na kwa yule mke/mchumba/mpenzi/demu n.k, ingawa nanua hujui kama wewqe ndiwe ninayekuhitaji. Labda hujui kama wewe ndiwe ninayependa uwqe demu/mchumba/mke wangu, lakini leo ujue ni siku yangu ya kuzaliwa.
Ingawa leo malaria yamenibana lakini nashukuru manesi ingawa wameshika matako yangu na kunidunga sindano. Najua kwa nia njema nitapona ndiyo maana ukichomwa sindano takoni unaambiwa poleeeeeee, ingawa nilisahau kumjambia ili nimwambia nami poleeeeee.
Najua kila mmoja anayozawadi yake lakini Koero Mkundi sijaona zawadi yako, unabifu na mimi au? Nashukuru Yasinta Ngonyani, zawadi yako nimeipenda sana1 daima tupo pamoja! OOOOhhh kwa wazee wangu nawaambia mjue mtoto wenu ni mwingi wa utani, mnivumilie ninaposema nesi amechezea TAKO langu. nadhani mnajua mambo ya kutaka uzima
LAKINI
atakayeweza anitunuku kitabu cha THE WORLD IS FLAT cha Thomas Friedman, nimtafuta hadi najamba. Mwenyewe ninacho mknoni JULIUS KAIZARI na CRYSTAL RAPTURE pia nakwenda duku la vitabu sasa kujinunulia zawadi. Bwaya, Kaluse,Kamala, na wengine naweka ..................................... ili ujaze jina lako kama nimesahau.
upendo daima, salama kwa mchumbangu usiyejijua kama ni wewe, naweka ........ andika jina lako
November 26, 2008
ndizi ndizi KAPOLOTA karibu sana
Madhumuni
mengineyo,
mila na desturi,
ughaibuni,
utulivu
October 31, 2008
tunaweza kutunza mazingira yetu siyo samaki tu
Madhumuni
amani na upendo,
maisha,
mapenzi,
utulivu,
uzuri
Subscribe to:
Posts (Atom)





















