Showing posts with label wageni. Show all posts
Showing posts with label wageni. Show all posts

October 21, 2017

TABASAMU NA KITABU


Ragin Mmbanga (kushoto) na Markus Mpangala (Kulia)
Huyu ni rafiki yangu. Anaitwa Ragin Mbaga, ila tuwapo farashani hupendelea kumwita "Mzee wa bustani ya usomaji". 

October 17, 2017

MANDHARI YA KIGOMA

Kigoma Tanzania, Barabara ya kuelekea Makumbusho ya Dr. David Livingstone Ujiji.

December 02, 2012

TAARIFA KWA WAWEKEZAJI WAPYA KATIKA KILIMO CHA MITI YA MBAO, KARATASI NA NGUZO.

Fresh Farms & Tours (T), biashara tanzu ya Anesa Co.,Ltd (Nyaluke Business Empire); inayojishughulisha na upandaji, utunzaji na uendelezaji wa mashamba ya miti ya mbao, karatasi na nguzo-mkoani Iringa. Pia inahusika na uvunaji na usambazaji wa mazao ya miti, (mbao na nguzo za umeme) sambamba na ufugaji.
Fresh Farms ilianzisha programu maalumu, mapema mwaka jana; inayolenga kuwawezesha watanzania wengine kuwekeza katika kilimo cha miti kwa urahisi. Tayari makumi wa watanzania wamechangamkia fursa hii. Fresh Farms & Tours (T) tunapenda kuwaarifu wale wote wenye nia ya kuwekeza nasi; KWAMBA kuanzia tar 1, Feb, 2013 kutakuwa na mabadiliko ya bei na gharama za uendeshaji kwa mashamba ya miti. Mashamba tunayoyauza laki sita kwa sasa; bei mpya itakuwa milioni moja; na yale tunayouza laki nane gharama yake itakuwa milioni moja na nusu.
Bei hizi hazitawaathiri wateja wa awali na wale ambao wamekwisha wasilisha oda zao. Fresh Farms & Tours (T) tunaendelea kuboresha huduma, taarifa na usaidizi kwa wote wanaowekeza nasi. Kabla ya mwisho wa mwaka huu; tutazindua tovuti maalaumu itakayobeba taarifa za uwekezaji katika kilimo na ufugaji; pia kila anaewekeza nasi atapata nafasi ya kufungua akaunti yake katika tovuti hiyo; na akaunti hiyo itamwezesha kufuatilia mwenendo wa mashamba yake popote alipo duniani. Fresh Farms & Tours (T)-GREENING THE WORLD AND FEEDING PEOPLE. (C) Anesa Co., Ltd

October 17, 2012

HARAKATI ZA MAENDELEO WILAYA YA NYASA, KARIBU KUWEKEZA


Wilaya ya Nyasa ni miongoni mwa Wilaya mpya zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya nne. Habari za kuundwa wilaya ya Nyasa nilianza kuzisikia mwaka 1993 nikiwa shule ya msingi. Lakini mwaka huu Wilaya ya Nyasa imezinduliwa rasmi na shughuli za maendeleo zinaendelea ili kukidhi mahitaji ya wananchi. Katika harakati hizo ni pamoja na huduma ya Maji ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Hapa ni picha mbalimbali ambazo zinaonyesha suala la upatikanaji wa maji katika vijiji mbalimbali wilayani humu.  Bila shaka wageni na wenyeji watavutiwa kuwekeza katika wilaya mpya ambayo fursa mbalimbali zinajitokeza. karibuni. Picha zote na Hoops Kamanga
 Chanzo cha Mradi wa maji kikifanyiwa ukaguzi.
 Tenki la Maji katika mradi wa maji katika kijiji cha Ng'ombo wilaya ya Nyasa
 Mradi wa Maji katika kijiji cha Kindimba Juu ambao umekamilika na wananchi wanategemea kutumia siku chache zijazo. Hapo fundi anamalizia marekebisho katika tenki.

May 26, 2010

WASOMI WETU, WANALILIA UPONYAJI!

Na: Albert Sanga, Tumaini University, Iringa

Nimeamua kuandika makala hii baada ya kutafakari kwa kina swali ambalo liliulizwa na kijana wa kitanzania kupitia katika mtandao wa internet. Kijana huyu anayefahamika kwa jina la Raymond Magambo, ni mwanafunzi wa shahada ya sayansi ya kompyuta Chuo Kikuu Cha Dodoma; anamiliki blogu inayofahamika kwa jina la {raymagambo.blogspot.com}. katika moja ya kurasa za blogu yake ameuliza swali lifuatalo “are the university students in Tanzania well prepared to bring changes in the country? Why?” tafsiri ya Kiswahili ya swali hili ni “Je wanafunzi wa vyuo vikuu katika Tanzania wanaandaliwa vema kuleta mabadiliko nchini? Kwa nini?”.

Kwa bahati nzuri sana ninamfahamu vema huyu kijana Raymond Magambo kwa sababu nilisoma naye kidato cha tano na sita pale Ilboru Sekondari. Ni moja ya vijana ambao wamekuwa na ndoto za kuona wanafanya vitu vya tofauti na vyenye historia za pekee katika dunia hii.

Vijana wa jamii kama ya Raymond Magambo hakika ndio wanaohitajika sana katika kuleta mabadiliko kwa jamii hasa ya kitanzania. Ukiona kijana kama huyu angalau anahoji uthamani na uwezo wa elimu anayoipata basi uwe na uhakika kuwa kuna mambo anatamani yafanyike katika namna fulani ambayo ni nzuri zaidi. Hawa ni watu ambao mimi nawaita “wanamapinduzi wa kutuokoa katika utumwa tuliouridhia”

March 09, 2010

NIAZIME KONDOMU, NIPO BAGAMOYO

Hakika nakuomba msomaji wangu, watu wangu NIAZIMENI KONDOMU usifanye mchezo nimezidiwa kiasi ambacho inanilazimu kuomba msaada wa kondomu. Haya ni maisha ya huku sasa, maana kila mmoja anafanya kile anavyojisikia, ingawaje ni kawaida sana.

Sasa mimi nasema naomba msaada wa kondomu maana usiku nilivyoupitisha, nimeletewa MAKAHABA wawili, halafu kahaba wa pili akaomba kondomu ili amsadie kahaba mwenzie kwakuwa dume lake halikuwa na kondomu.

Siku zote naamini utafiti wakati mwingine inabidi uingie mwenyewe ushuhudie, na mchakato wangu wa kitabu kile ni lazima niingie maeneo magumu yenye vishawishi adhimu. BASI jana usiku nilikuwa na rafiki zangu, na kwakuwa hawa jamaa wamekuja na Wapennzi wao, wakaanza kunishambulia eti nitajiuuuuu(ulikuwa utani) wakati tukiendelea na porojo akaja mzee wa mapokezi akaniambia 'mjukuu usipate taabu wewe sema tu sasa hivi utapata, huu ni mji wa kimataifa bwana'.

Ikabidi nitulie kisha nikamjibu hebu niletee binti mmoja nimchungulie kidogo. Wakati nipo sehemu ya chakula, chumba changu nimekifunga, kumbe yule mzee akampigia simu kahaba mmoja hivi, nadhani anafahamiana nao. Akajiingiza hapa kwenye nyumba tuliyopo, lakini mlango wangu ukawa umefungwa(sikuwepo).

Punde niliporejea, nikaona mzee ananilaumu mbona binti alikuja, ila ameahidi kuwa atakuja tena. Kweli zilipita dakika 15 hivi, nikiwa chumbani naongea na rafiki zangu, mara mlango ukagongwa na yule mzee, nikawaambia jamani waungwana nendeni chumbani kwenu. Mzee akanikabidhi binti tuelewane......
Akakaa kitini na kuniambia anisikiliza, ikabidi niulize inakuwaje mbona unanijia? Akaniambia kuwa alielezwa na mzee kuwa nahitaji kupunguza ngare.

Nikauliza bei gani bila kondomu na bei gani kwa kondomu. Duh! jamani niazimeni kondomu .......tafadhali sina huku Bagamoyo. Yule binti bila kusita akaniambia kuwa hawezi kulala hapo kwangu kwani mtoto wake yuko nyumbani, kwahiyo bila kondomu 10.000 na tukitumia kondomu 5000.

Upo hapo? nikauliza swali inakuwaje mtoto aachwe nyumbani halafu yeye yuko hapo? Nikajibiwa hayanihusu, bali tufanye kazi(ku*******) kisha atimue zake. Nikatoa amri moja 'nenda kwenu kapumzike na mwanao, siwezi kulala na wewe wakati mwanao yuko mpweke hana mapenzi ya mama. Jamani akaniambia labda sina haja, nataka kumchezea tu kwa muda wake, nikafungua mlango nikamwabia hamna noma wewe nenda tu................

Kumbe yule mzee anakuwa na kigawo chake baada ya shughuli maana alinilalamikia vipi mjukuu unanikosesha kipato? Nikamwambia tafuta mwingine, huyo amezaa kwahiyo mimi na huyo ni mwiko.
Nikaletewa mwingine, huyu ndiye aliniacha hoi kwamba atalala hadi asubuhi hii ninavyoandika hapa, ila suala la kondomu au bila kondomu ni chaguo langu ila bei 10000. Dakika hiyo amekaa kitandani, na mzee ananiambia bei ndiyo hiyo kwahiyo kazi kwako.

Nikasema asante, waweza kwenda binti. Kitu nilichojifunza ni kwamba, niliuliza swali kwa binti huyo na mzee wa mapokezi ni kwanini anadhani kumekuwa na wimbi la ukahaba katika miji mbalimbali duniani? Nilijibiwa ni MAISHA TU. Sijui wewe unayesoma unaelewa nini maana watu wamegeuza miili yao kuwa biashara. Nimejiuliza sana kwanini binti aseme kuwa suala la kondomu ni uamuzi wangu ila anachohitaji ni malipo yake.
Mwenzangu yakanishinda, nikaomba niachwe kama nilivyo... nikawafuata rafiki zangu nikawaambia ipo kazi hapo ni 'cleverness without wisdom'.

KITUKO KIKALI
Mzee wa mapokezi anaye mkewe, lakini siku ya jana amefumaniwa baada ya kuchukua mwanamke mmoja hivi akataka amfi**** unaona yaani nyu***. Sasa alikuwa anataka kumlipa huyo mwanamke 20000 ili afanikiwe kuachiwa nyu****. Lakini ugomvi ukazuka, nyumba nzima zogo, watu wakashituka kuna nini, kumbe jamaa analazimisha ataufune uvungu wa nyuma. Ili kumnusuru ilibidi baadhi wapangaji wamshambulie yule mzee ili kumwachia yule mwanamke, lakini haikuwa hivyo kwani baada ya kuitafuna ile ya kawaida jamaa akawa anataka atafune na nyingine ndogo***.

Mungu wangu makahaba wanaushirikiano, na wanamfahamu mke wa yule mzee ilibidi wachukue hatua za kwenda kumchukua....wakakodi pikipiki(hapa ndiyo usafiri wa haraka sana usiku)..... ili amfumanie mumewe.... halafu kumbe nyumba ndogo naye alikuwa akicheza karibu na sehemu ya tukio ili kujionea...... jamani nipeni kondomu hakika hali hiiiiiiii we acha tu.
Baada ya fumanizi yule mzee kwakuwa alitaka kumfi**** yule kahaba kwani haikuwa siri tena yule mwanamke alikuwa akipayuka na kuwaeleza watu anataka kinyumenyume.....akasimulia yaani jana nimelala saa sita usiku hivi duh!
Sijui nisemeje kwani hii hali inaonekana wazi kuwa inashamiri na sisi wanadamu tunaonekana utashi wetu unadidimia kila kukicha.

Lakini mimi naomba kondomu ili nami nijinufaishe hapa, na rafiki zangu wananicheka sana na kituko changu cha kumkataa kahaba aliyezaa, kisha kumkataa mwingine ambaye baadaye aliomba msaada wa kondomu. Ni mambo juu ya mambo yamenikuna sana, najikuna na kujifunza.......lakini naomba sana mnitumie kondomu maana hapa nilipo sina kwahiyo nahitaji sana msaada wenu waungwana. Karibu Bagamoyo tutalii kwa raha lakini msisahau kuniazima kondomu....

February 16, 2009

Kitendawili kimewashinda? Karibuni tule basi!

Nilikuwa nangojea waungwana mjitahidi kufunua bongo zenu, nilidhani kwa wanazuoni kama ninyi lazima jawabu lipatikane ..... lakini wapi bwana, maji yamezidi unga..... yaani tatu bila, tatu bila. Haya basi nimekuja na chakula hiki sijui tutashiba maana samaki mmoja, kwahiyo kula ni kula mbaya kukoimba mboga jamani. Karibuni mkekani, mlozowea mezani msahau kwa leo.

February 06, 2009

ndiyo maana nakupenda sana

Daima nawaza, nakumbuka enzi za uvuvi bwana,kabla sijajua kubonyeza niandikacho. Mmmmhh Koero aliagiza samaki, akadai anahitaji Kamongo, DUH! Pengine sijui hawa samaki wapo wapi lakini sijui kama ziwa letu lina Kamongo. Mmmhh labda nimesahau mambo yetu. Haya weeeeee tayarisha ugali mimi naandaa mboga, wala usilete kitu tofauti na ugali tena wa muhogo.

January 26, 2009

Baridi sana, Nipo Mbeya

Duh! Hii hali bwana we acha tu! Nipo Mbeya jamani, mapumziko ya siku saba hivi lakini naamini kila kitu kinakwenda kama ninavyopanga na ninavyotaka bila kujali ni namna gani nakarahishwa na hii hali. Baridi inanikamata halafu hakuna hata chembe ya faraja, duh! labda kama alivyonipatia wimbo Keoro kuwa niskilize wimbo wa Ziggy Marley.
Jana nilikuwa njiani kuja hapa, mvua, kumbukumbu za maisha yangu ya shule, mitikasi na vioja vya hapa na pale. Mji umekuwa na mabadiliko ambayo naamini kama jiji limepiga hatua kiasi fulani tofauti na mwenendo wa maeneno ya Dar kwenu.
Vipi wanablogu mnaonaje kadiri siku ziendavyo mnafikiria nini kuhusu blogu. Najua wapo wajuaji wa blogu na wale wajuao mchanganuo wa hoja, huku wakipendacho kiwepo ndicho wafanyacho kwakuwa wanajua wafumbacho ni huishia ubongoni mwao! Aiseh!
Tafadhali usiwaaambie uhamiaji kama kesho naingia zangu Malawi kwanza kwa rafiki yangu. Duh! Hii inakuwa ngumu sijui lakini uhamiaji usiwaambie kwani nina kitambulisho cha maktaba tu sina kitu kingine.
Haya, lakini bado nawaza mambo ya mlimani akili imekufa ganzi. Kwaheri kwa leo jamani ila usiwaambie uhamiaji kama kesho navizia kuingia Kalonga kisha ndani ya nchi kabisa.
Pamoja daima! Baridi sana, mapumziko safi-nasonga kwa wajomba unyanjani.

January 24, 2009

ndiyo kazi zetu, ndiyo utamduni wetu

Hii nayo ni kama vile ujuavyo kula na kulala au kupenda na kupendwa. Pengine unajua kuwa tunajua haya mambo. Jamani sijui unawaza nini, au mimi ndiyo nawaza nini. Sijui labda UA alangu, thubutu mmhh pengine. Lakini Koero aliuliza kuhusu picha fulani kuhusu mimi. Eti hii nayo vipi, kweli mimi nipo au? Sijui, lakini haya ndiyo maisha yetu tunatafuta shibe, furaha na pumziko. karibu sana.

January 08, 2009

Maisha! maisha! maisha

Duhh! jamani wakati fulani pale mji wa Mzuzu-Malawi, nilijiuliza mambo kadhaa kuhusu maisha yetu. Samahani usiwaambie uhamiaji kama situmii pasipoti wala mayai visa, maana wale ni ndugu zetu bwana tunalonga kinyanja na kuingia kwa mitumbwi poa. Haya maisha ya Bongo na kule naweza kusema aheri kwetu japo kwa sumuni. Jamani nakumbuka baadhi ya vijiji au mitaani tu wapo wanaoamini Wabongo maisha tunapeta, lakini sote tunajua kinachoendelea. Sasa kwa kawaida huwa najiuliza sana maisha yetu hapa kijijini Lundu na haya ya ndugu zangu wa damu kule Mzuzu na maeneo mengine! Jamani maisha! maisha! maisha! maisha! maisha! maisha!

January 05, 2009

Gumzo letu na dada Yasinta

Jamani natumaini hamjambo woteeeeeee wa kijiwe cha maswali magumu. Nipo kamili tena nazidi kuwakilisha kama kawaida.
Nadhani wengine mlikuwa mnangoja kujua labda tulipiga gumzo gani na dada Yasinta. Bila shaka mambo ya wanablogu yanafurahisha sana na utamu wa mashairi kama kaka Fadhy poa sana.
Katika kupiga gumzo na dada Yasinta, kuna jambo amenifanya nitafakari sana na wakati mwingine huwa najiuliza nianze vipi.

Gumzo la kawaida kuhusu mambo ya teknolojia, blogu na maisha kama ilivyoblogu yake. Jambo lenyewe linahusu VITABU. Nilimkuta kashika kalamu ya wino anaandika, nikauliza kulikoni mwenzetu huchoki? Akatabasamu na kusema 'kutafakari jambo muhimu lazima uandike ukizingatia kuandika ni jambo muhimu pia". Hapo gumzo likazama kuhusu vitabu maana kama ajuavyo napenda kuandika vitabu kuhusu jamii yetu.
Lakini alikuja na swali hili: "Kwanini huandiki vitabu kama unaweza? Si ni jambo la kukaa na kutafakari tu kisha unaandika kwa uamkini?akaongeza, Au hakuna soko la Vitabu? Basi andika vitabu vya wototo, haiwezekani?"
sijui kama mnanielewa ninachotaka kukisema? Ni jambo la kujiuliza sna katika jamii zetu kwani waandishi wa vitabu wanapotea, wengi waliopo wanaandike vile ambavyo vinadumu kwa muda mfupi.
Ni vigumu kupata vitabu kama RAI YA JENERALI, MAKUADI WA SOKO HURIA achilia mbali vile vya Issa Shivji{mwaka jana katoa Pan africanism or Pragmatism?} kizuri. Kwa kweli dada Yasinta kanipandisha moli kama wamasai.
Ndiyo maana nilisema katika maoni yangu fulani kama Simon Kitururu anapaswa kuandika vitabu vya falsafa, Fadhy naye awe Shaban Robert wetu, mzee wa changamoto nye awepo, dada Koero kama vile kitabu cha THINK BIG{umekisoma?}, Bwaya, Kaluse, Kalama tuleteeni UTAMBUZI wenu jamani. Ni hayo tu

December 27, 2008

Dada KOERO karibu ndani !!

Jamani eeeeeeeeeeh, sina neno ila karibu sana tena sana dada KOERO, hakika tutajenga mnara katika miamba. hakuna jambo rahisi kama kuifanya nafsi ifurahia kile unachokiona kinafaa daima. Ni jambo ambalo kila mtu anaweza kulitenda ikiwa tu anaongozwa na dhamira imara lakini ni uwezo wa kuyabadili mazingira yetu kwa wakati wetun ndiyo huu ni WAKATI WETU, TUNAWEZA HAYA TWENDA NA DADA KOERO. KARIBU NDANI katika SHAJARA wengine mnasema BLOGU poa tu.

Ni mimi Markus Honorius Mpangala mvuvi wa nyasa na mnyasa wa nyasa.

December 17, 2008

maneno ya Al-rawahy hilal

"Hi, Brother, Nimefurahi zaidi kwa ushindi wa Taifa Stars. Hongera kubwa kwa Taifa Stars na JK na WADAU WOTE WA BLOG YAKO, Hongera Bongo na watanzania wote popote walipo mimi ni mdau mkubwa wa blog zote za Bongo, napenda kufuatilia na kujua habari zote, nakuomba kama ndugu upost furaha yangu hii na hongera zangu hizi kwa wadau wote kwa ushindi mkubwa wa kuingia fainali za kombe la afrika, Tunaombea zaidi Stars wafanye vizuri katika michuano hiyo kila la kheri amin"
http;//www.borntosuffer1.blogspot.com
hilal24356@yahoo.vom

NB; ujumbe huu ulitumwa nyasa desemba 14.2008 kwahiyo waungwana wote Raha na shangwe kwa ushindi wa Stars

December 16, 2008

yote maisha+ipo siku yatakwisha.....

karibu sana wala usiogope ndugu, karibu nyumbani maskani wala usitie shaka. hapa ndiyo nyumbani karibu sana

December 10, 2008

wanablogu karibuni ndani

jamani wana-shajara za mtandaoni karibuni ndani. atakayepuuzia shauri yake. karibuni sana, mambo ndiyo hayo

kwa kweli nakupenda sana

nina HAMU ndiyo maana nakambia nakupenda sana NYASA. Gego na Fizi zinakupenda sababu ya utamu. angalia picha hiyo kwa umakini halafu niambie kama hutamani kweli!!! mmm nakupenda saaaaaana nyasaaaaaaa. karibuni

December 09, 2008

Najua unanogea+mate yanatoka=urudi nyumbani

najua kabisa unanogea, najua nakupatia HAMU. maana najua bila hamu huwezi kukumbuka kitu. Hawa siyo sawa na dagaa kigoma wanaochacha kama wa enzi zile za KIGONSERA a.k.a CAIGO BOYS, umenisoma kaka Mtanga ha ha ha ha Nina HAMU ndiyo ndiyo maana nakwambia haya. Watazame walivyoanikwa mchangani vizuri halafu unapata NG'ONDA upo hapo. RUDI NYUMBANI ha ha ha ha ha

December 08, 2008

kazi+juhudi+ubunifu+mapenzi=MAISHA

maisha tu haya kama utapenda nunua tu utakuwa umenisaidia sana maana mwanangu namsomesha kwa kutegemea hii kazi yangu. Nahiheshimu sana. Ni kama anasema hivyo

December 06, 2008

maandalizi ya Noeli, karibu

kambale bwana, unakumbuka utamu wake? kwa wale wasiomla poleni huyo ndiyo kambale toka BABU hadi Mjukuu wanakula. ERIK UMEWAHI KULA KAMBALE WEWE? mwambie mama asiwe na roho mbaya hivyo akutafitie huko Uswidi , mkikosa njoeni nyasa