Showing posts with label Mafanikio. Show all posts
Showing posts with label Mafanikio. Show all posts

October 26, 2017

MWALIKO; WOTE MNAKARIBISHWA KWENYE MJADALA HUU


October 21, 2017

UCHAMBUZI WA KITABU CHA UHAMASISHAJI

KITABU: ISHINDE TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO
MWANDISHI: JOEL NANAUKA
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA


JOEL NANAUKA ni miongoni mwa waandishi wazuri katika vitabu vya uhamasishaji na utambuzi. Kitabu chake cha “Ishinde Tabia ya Kughairisha Mambo” kimechapishwa na kampuni ya Benison Communication &Printing iliyopo Dar es salaam na kupewa nambari za usajili ISBN 978-9987-761-99-9.

October 16, 2017

CHUO CHAANZISHA SHAHADA YA WADUDU

NAIROBI, KENYA

KITUO cha Elimu na Utafiti kinachofadhiliwa na Benki ya Dunia kimeasisiwa katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogo Oginga Odinga na kinasubiri ruhusa ya kuanzishwa kwa programu za Uzamifu na Uzamili kuhusu wadudu wanaoweza kuliwa.

Taasisi hiyo inapania kubuni njia za kuzalisha wadudu hao kwa wingi bila ya kuharibu mazingira ili kukidhi utashi mara baada ya wazo hilo likifanywa kuwa biashara.Wadudu wanaoliwa sana maeneo ya Magharibi mwa Kenya, ambao wana wingi wa madini ya protini na Zinki watafanywa kuwa biashara ili kuimarisha uwepo wa chakula cha kutosha, na kuondoa dhana mbaya katika kula wadudu. 

“RAIS ANA MIAKA 31”


Sebastian Kurz
JUMAMOSI nilikuwa nasoma makala ya James Masters kwenye tovuti ya CNN. Sentesi yake ya kwanza ilinivutia sana, “Ulikuwa unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Ingawa aliendelea na mengine lakini staili pekee haikuwa kivutio bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi.
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye amewahi kuwa waziri wa  Ushirikiano wa Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.  Sebastian  Kurz ambaye amekuwa Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu. 

Ni mwenyekiti wa chama cha  OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama chake kushinda viti vingi vya bunge. 

September 29, 2017

UTAFITI: UHANDISI NI FANI INAYOLIPA ZAIDI

WANAFUNZI wa elimu ya juu ambao husomea taaluma ya uhandishi au biashara katika wana nafasi kubwa kuwa mabilionea kuliko wanafunzi wanaosomea taaluma nyingine.

Aidha, wanafunzi wale ambao tayari wameingia katika soko la ajira katika kazi ya mauzo au biashara ya hisa ni miongoni mwa wenye fursa kubwa  kuwa katika sehemu watu matajiri duniani.

Kwa mujibu wa utafiti uliyofanywa hivi karibuni na shirika la ajira la Aaron Wallis, ambalo utafiti wake umeangalia watu matajiri duniani zaidi 100 ili kuona kama kuna uwiano au uhusiano wowote kati ya taaluma yao ya kwanza na jinsi walivyokuwa matajiri au kutengeneza utajiri.

Ripoti hiyo ilibaini  kwamba kazi yao ya kwanza, kati ya mabilionea wakubwa wa juu waliajiriwa kwa mara ya kwanza katika mashirika ambalo sio yao. Pia  kuna wajasiriamali ambao walianza kampuni zao wenyewe na wengine wale walioajiriwa katika biashara za kifamilia  katika nafasi masoko na mauzo.
Mabilionea 10 wa mwanzo kati ya 53 ambao waliajiriwa  katika shirika ambalo sio yao wakati mabilionea tisa tu walianza kazi yao kama mfanyabiashara wa hisa au mauzo.

Utafiti huo pia uligundua kuwa matajiri wakubwa duniani 75 kati ya watu 100 akiwemo Bill Gates, Warren Buffet, George Soros na Jeff Bezos wana elimu ya ngazi ya shahada tu.

Kati ya hao 75,  matajiri 22 walisomea shahada katika taaluma ya uhandisi (ikiwa ni pamoja na mwanzilishi wa mtandao wa Amazon, Jeff Bezos na  mwanzilishi wa Google Larry Page, aidha matajiri 16 walisomea masuala ya biashara ambapo 11 wamesoma taaluma ya fedha na uchumi.

Mabilionea 30 kati ya 100 wanautajiri wa kurithi au wanafanya kazi katika biashara ya kifamilia, wakati 17 walianza kampuni zao wenyewe. Mwezi Julai mwaka huu, muda mfupi tajiri Jeff Bezos alichukua nafasi ya Bill Gates kuwa mtu tajiri zaidi duniani baada ya kuongezeka kwa hisa katika mauzo ya mtandao kabla ya ripoti yake ya mapato, lakini hisa zilishuka tena na Gates alirejea katika nafasi ya kwanza.

Bill Gates ambaye ana utajiri wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 87, na amekuwa mtu tajiri  zaidi duniani tangu mwaka 2013. Billionea huyu mwenye moyo wa kusiadia ametoa dola bilioni 31.1 ya utajiri wake katika kusaidia jamii kupitia taasisi mbalimbali, wakati Jeff Bezos ametoa dola milioni 100 kwa mujibu wa jarida la Forbes  la nchini Marekani.

Hata hivyo, ripoti imebaini kuwa matajiri wengi katika 100 wamesomea shahada ya kwanza ya uhandisi kama orodha ilivyoeleza. Matajiri wakubwa 22 duniani wanataaluma ya uhandisi, ambapo matajiri 16 wamesomea masuala ya biashara, katika fedha na uchumi (11) sheria (6) sayansi ya kompyuta (4) historia (3) Falsafa (2), Siasa (2), lugha ya Kiingereza (2), Historia (2), Hisabati (2) na masuala ya madawa (1).

©MTANZANIA


January 29, 2013

WATOTO/VIJANA WASOMAO NJE YA NCHI



Haika Lawere
Na Haika Lawere, via Facebook

Huwa nawatazama wazazi wengi hapa Tz wanavyojinyima usiku na mchana ili kupata ada kuwalipia watoto wao school fees uko nje eg USA/UK,India,Malysia,SA nk nk,wengine huiba ktk ofisi zao ili tu mtoto asome,wengine watauza properties ili mtoto ailimike,wengine hukopa,wengine hata maendeleo binafis yana simama ili vijana wasome!!! 
ila sasa...huko waliko hawa watoto,baadhi yao hawasomi,wengine huishia kuzaa na foreigners ili kupata papers,wengine hu-cohabitate na strangers ili kupata unafuu wa kodi,wengine ni mwaka wa 10 na zaidi hata Certificat/Diploma hawana hata darasa hawajawahi kuingia!!wingine wameshajilipua hata wazazi wakiumwa/kufa hawaji kuwaona!!
Wengine huaribikiwa kabissaaa kitabia/ kiakili/ki-mtazamo na wanakuwa hawa-fit mazingira ya uku!!mi niwasihi tu wadogo zetu ambao wazazi wenu wana-sacrifice kuwasomesheni nje muwe apprecitive,waoneeni wazazi wenu huruma wanavyoteseka,bongo pagumu jamani!! someni na muelimike na mkimaliza shule, ni vizuri mkarudi kutumikia nchi yenu,jamii yenu na kuwatunza wazazi wenu hapo watakapozeeka!!!msizamie nchi za watu wakati kwenu kuna-oppoturnities chungu-mzima!!!simhukumu mtu,ni mtazamo tu anyone can challenge!!

January 08, 2013

WATANZANIIA TUNAWEZAJE KUISHI KWA GHARAMA KUBWA KILA MWEZI?


Na Yasinta Ngonyani, Sweden
Fikiri, matumizi nyumbani:- chakula, umeme, gesi, maji, soda au juisi za wageni. Ada za watoto zinazolingana na za vyuo vikuu. Na hapa nazungumzia ada za shule za binafsi sio zile za serikali  kwani tunajua unafuu wake. Matumizi mengine matibabu hospitalini, pesa ya walinzi kwa kila mwezi, sherehe za kuaga na kukaribisha mwaka mpya.
Zaka ya Kanisani na Misikitini, kupanda Mbegu/ Sadaka, Shukurani ya neno, ahadi na makusanyo, shukrani ya chakula cha Bwana kanisani, marekebisho ya Kitasa cha mlango kabla mwenye nyumba hajashtuka, gharama za marejesho ya mkopo wa Saccos kazini.
Tozo za Flying (wazoa takataka wa mikokoteni ambao huzitupa hapo hapo), Madalali wa nyumba, viwanja, pango la nyumba, fremu ya biashara na ofisi.
Mitandao ya simu (airtime vouchers), mafuta ya gari, walindaji na waoshaji magari. Daima kauli zao “oyaah sista/blaza, mdogo wako nipo apaaa.”
Tozo za kuegesha magari, makato ya mikopo, tozo za internet cafe ili uweze ku-surf. Rambirambi ya mfiwa mtaani kwetu, harusi ya ndugu yako wa ukoo na zawadi.
Bado sijamaliza kutaja, kuna Sendoff ya mtoto wa mdogo wake rafiki yako na zawadi, kumuaga mfanyakazi mwenzetu na zawadi, michango ya komunio ya 1 & 2 na kipaimara.
Michango ya birthday party na zawadi; Ndugu wa kule kijijini, mshahara wa hausigeli na hausiboi; matumizi ya Bodaboda, teksi na bajaji. Duka la dawa kwa mchaga, tuisheni ya mtoto, kuchangia wahanga wa mabomu na mafuriko. Mengine ni kwenda kumuona mtoto aliyezaliwa, kununua CD/DVD ya uzinduzi wa Kwaya yetu.
Chakula cha mbwa, mchango wa ujenzi wa kupanua Kanisa, kuchangia Uinjilisti Masasi, outing ya kitimoto, ujenzi wa Nyumba Mabwepande, Kuendeleza shamba Mkuranga (linalotaka kutaifishwa kwa kutoendelezwa). Na matumizi mengine kwa wale wenzetu wanaokwenda umbali wa Viti Virefu, moja moto, moja baridi. Maji ya Trafiki, Chai ya Nesi na Daktari, Kahawa ya Hakimu, Karani na PP.
Matumizi ya Vishoka waunganisha maji na umeme; Kidogo dogo cha mjumbe na mtendaji wa mtaa, makaribisho ya get together na dinner kwa rafiki wa kikazi ambaye hamjuani ila kweye simu tu.
Mchango wa matibabu ya mtoto nyumba ndogo kule Ngusero, mchango kidogo kwa rafiki aliyevamiwa na vibaka na kuumizwa vibaya. Gharama za malipo ya Mkulima Bar Moshi, manunuzi ya maji ya Kilimanjaro uwanjani Sheikh Amri Abeid, Ukiangalia mechi ya Yanga na JKT Oljoro, malipo kwa ajili ya Uji wa Shangazi, baada ya kazi Njiro jioni ya Alhamisi. Vipi manunuzi ya kandambili kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Hivi hali inakuwaje?
Mia mbili ya watoto wa mtaani au ombaomba, kitu kidogo cha wale wanaolazimisha kuosha kioo cha gari kwenye foleni barabarani. Umeme uliopanda bei, gesi iliyopanda bei, maji yaliyoadimika, bado contingency maana huu usafiri unaotembelea ball joint, bush, feni belt havijafa, hapo bado hujafanya service. Bado msosi wa mchana kazini hasa kama maofisi yetu akina Mama Ntilie na vyakula vyao vinapokaribiana bei za restaurants, bado mchango wa kitchen party na sare, kuna hii baby shower.
Na hapo bado hujatoa watoto outing jumapili, Upo wapi uwezekano wa kununua laptop mpya ambayo ni muhimu katika mfumo wa maisha ya kisasa. Desktop nyingine kwa ajili ya watoto nyumbani, rim mpya za gari ambazo zimeingia kwaajili ya ku-modernize gari lako kuu kuu. Vipi kuhusu gharama za kujipendekeza kwa kimwana wa kazini kwako ambaye amekubali kwenda nawe out leo.
Gharama za matibabu katika hospitali binafsi kwa kuwa madaktari wa serikali wapo katika mgomo. Dogo naye “Bro ninunulie basi japo kasimu ka promosheni, ile yangu imedondoka chooni” Mara “Bro/Sister Next week on Saturday shuleni tuna-visit snake Park na sina shilingi 3000 za mahudhurio”.
Mke naye nyumbani anaongeza yake, “Daddy leo Mwakasege yupo relini, vipi tutapitia? Hapo unatakiwa kujua kichwani mwako kuwa gharama ya taxi baada ya semina.
Vipi tozo za Toyo kwa kuwa nimeachwa na gari la ofisi (Staff Bus). Mwingine kama kawaida anakusubiri uwajibike kwa gharama zako hana muda wa kudhani unahitaji msaada. Mama yangu!
Ukigeuka huku na huko unajikuta nafuu yenyewe ni pale mwajiri anapokuongezea mshahara kwa 7% tu wakati inflation ni juu ya 19%. Ukifikiri kwa makini, unajiuliza Watanzania wanaishi vipi kwa mtindo huu?
Ndipo unapoimba "Mwokozi nitoe roho niepuke, hili balaaa." Napenda msomaji utafakari mwenendo wako wa matumizi kulingana na hali hali ya uchumi wan chi na jamii yetu.
Kama ukiyumba kwenye suala la kuweka akiba, basi maisha yako yatakuwa yanakabiliwa na ukosefu wa msingi wa muongozo au utakuwa unatumia gharama kubwa kwa mambo yasiyoweza kusaidia familia yako.

December 20, 2012

MAKAA YA NGAKA KUIMARISHA UZALISHAJI VIWANDANI


Mitaa ya mbinga mjini.
picha kwa hisani ya Prof Joseph Mbele

Uzalishaji wa makaa ya mawe unatarajiwa kuongezeka baada ya mradi wa uchambiaji wa makaa ya mawe mjini NGAKA wilayani MBINGA katika mkoa wa Ruvuma kufanza kufanyiwa kazi na kampuni ya uchimbaji makaa hayo wilanai humo.
KWA TAARIFA ZAIDI BONYEZA HAPA KUSOMA HABARI NZIMA

SERIKALI YATENGA SH. BILIONI MOJA KUJENGA DARAJA LA KAVUU

mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi.

SERIKALI imetenga kiasi cha sh. bilioni moja kwa ajili ya kazi za awali za ujenzi wa daraja la mto Kavuu linalounganisha kata za Mamba, Kasansa, Majimoto, na kijiji cha Inyonga yalipo makao makuu ya wilaya mpya ya Mlele. 

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana jioni (Jumatano, Desemba 19, 2012) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mamba kwenye uwanja wa mpira akiwa katika siku ya saba ya ziara yake jimboni kwake Katavi wilayani Mlele, mkoani Katavi. 
Waziri Mkuu alisema Serikali ina nia ya kufungua mawasiliano kati ya bonde la Rukwa na mikoa ya kaskazini ambako kuna uhaba wa chakula. “Bonde hili linasifika kwa uzalishaji mkubwa wa nafaka kwa hiyo kujengwa kwa daraja hilo ni ukombozi mkubwa wa kufungua soko kwa mazao mnayozalisha huku,” alisema. 
Alisema katika mwaka huu wa fedha, barabara ya kutoka Sitalike kupitia Kibaoni, Majimoto, Mamba hadi Kasansa yenye urefu wa kilomita 33.5 imetengewa sh. milioni 837/- na kwamba wakandarasi wawili wamekwishapatikana ili kuifanyia ukarabati barabara hiyo.
Kuhusu barabara ya Majimoto hadi Inyonga yenye urefu wa kilometa 135, Waziri Mkuu alisema zimetengwa sh. milioni 943/- kwa ajili ya ujenzi wa madaraja katika barabara hiyo. 
Alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa fedha hizo, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Katavi, Mhandisi Isaack Kamwelwe alimthibitishia Waziri Mkuu kuwepo kwa fedha hizo. 
“Fedha zimeshatengwa na leo nimepokea kibali cha kutangaza zabuni za ujenzi wa daraja hilo. Zabuni zitatangazwa kuanzia Januari 2013,” alisema. 
Kutokuwepo kwa daraja la Kavuu kunawafanya wakazi waishia bonde la Rukwa (maeneo ya Majimoto na Mamba) kila wanapotaka kwenda Inyonga, walazimike kupitia Mpanda yaliko makao makuu ya wilaya yao ambako ni zaidi ya kilometa 350. 
Kesho (Ijumaa, Desemba 21, 2012) Waziri Mkuu atakwenda kata ya Usevya ambako atazindua mradi wa umemejua kwenye sekondari ya kata ya Usevya na kuhutubia wananchi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, DESEMBA 20, 2012.

December 19, 2012

WAKAZI WA WILAYA YA NYASA WATAMUDU KULIPIA GHARAMA ZA KUUNGANISHWA UMEME?


Na John Chitanya, Nyasa

Wilaya ya Nyasa ni miongoni mwa wilaya mpya zilizoanzishwa mwaka huu kwa mujibu wa sheria za TAMISEMI chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Juhudi za kuanzishwa kwa wilaya mpya, sote tunajua linalenga kusogeza huduma kwa wananchi ili kukabiliana na matatizo mbalimbali na kuweza kujiletea maendeleo.. Wakala wa Nishati Vijijini kwa mujibu wa sheria Na.8 ya Bunge ya mwaka 2005 inaeleza kuhamisha, kusimamia na kuruzuku miradi ya Nishati vijijini ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa nishati bora vijijini kwa ajili ya shughuli za uzalishaji,  mali na kijamii.
Wakala wa Umeme vijijini umeandaa mpango wa kusambaza umeme uitwao Underline Transformers na unatarajiwa kuunganisha vijiji zaidi ya 726 katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Kwahiyo jukumu la wakala wa umeme katika maeneo ya vijiji kwa maana ya kujenga ‘Backbone Transmission Line’ inatakiwa wananchi kulipigia gharama za kuunganishwa kwenye ofisi za TANESCO zilizopo karibu na eneo la kijiji chao.


Wanafunzi wakienda shuleni katika shule ya Kata wilayani Nyasa.
Picha kwa hisani ya jaizmelaleo blog.


Miongoni mwa vijiji vitakavyopitishwa nyaya za umeme ni vijiji vya wilaya Nyasa. Kutokana na hali hiyo, nikiangalia hali ya uchumi ya watu wa vijiji vya Nyasa hakika najikuta nabaki na swali, ni namna gani wataweza kumudu gharama za kuunganishiwa umeme katikati yamiundombinu mibovu iliyopo wilaya hiyo? 
Kwa sasa harakati za kutengeneza miundombinu inafanyika. Ujenzi wa Barabara kutoka Mbamba Bay hadi Liuli, kisha kutoka Liuli hadi Lituhi, ikiwa na lengo la kurahisisha usafiri kwa wakazi wake. Mpango wa serikali ni mzuri, lakini ni vema tukaangalia namna ya kuhakikisha gharama za kuunganishiwa umeme zinatozwa kulingana na eneo husika.
Kusema hivi sina maana kwamba wakazi wa wilaya ya Nyasa wapate upendeleo, la hasha ila kwa hali ya uchumi wa wilaya hiyo naelewa ugumu wao kuweza kulipigia gharama za kuunganishiwa umeme. Wilaya Nyasa ni changa, na wakazi wake wanategemea shughuli za kilimo na uvuvi.
Kilimo cha mpunga, kahawa, mahindi, mtama, uwele, ulezi, zinaweza kuwakwamua ikiwa watajengewa miundombinu mizuri. Lakini suala la nishati ya umeme licha ya kuwa muhimu katika maisha yao, bado naona taswira ngumu kwa wakazi wa wilaya hiyo.
Miji muhimu kama Lituhi, Lundu, Kihagara/Njambe, Liuli, Mkali, Lundo, Mbamba Bay,na Kilosa inaweza kujipatia huduma za umeme kwa baadhi ya wananchi. 855 ya wakazi wa wilaya Nyasa hawatakuwa na uwezo wa kulipigia gharama za kuunganishiwa umeme.
Hiki ndicho kitendawili ninachoona hapa. Wakala wa umeme kwa kushirikiana na TANESCO wanatakiwa kufanya tathmini juu ya mazingira ya wakazi wa vijijini kuunganishiwa umeme.
Ni rahisi kuunganisha umeme katika mji wa Mbinga ambapo shughuli za kiuchumi ni kubwa na zimekuwa zikifanyika kwa muda mrefu. Lakini kwa wakazi wa wilaya mpya kama Nyasa, hakika ni mtihani mkubwa kwa wakazi wake.
Nadhani tunao wajibu sio wa kuwaelimisha juu ya matumizi ya nishati ya umeme, bali umuhimu wa kuwawekea mazingira mazuri ya kufanikisha upatikanaji nwa umeme. Ni vyema kabisa wahusika wakaelewa hili kuwa suala la wakazi wa wilaya ya Nyasa kulipia kuunganishiwa umeme ni kitendawili.

November 20, 2012

KARIBUNI SANA NYASA, MLO WENYE VIRUTUBISHO VYA ASILI

                                                            KARIBUNI NYASA
Hilo tunaloweza kusema kuhusu wilaya ya Nyasa. Ni wakati wa kuburudika zaidi na kupata vyakula vyenye virubisho vya asili kama vinavyoonekana pichani.


November 01, 2012

JAMES ZOTTO ALIPOZUNGUMZIA MGOGORO WA ZIWA NYASA, KABLA YA KUWASILISHA UTAFITI WAKE KWENYE UMOJA WA AFRIKA NCHINI ETHIOPIA

Mgogoro wa mpaka Malawi na Tanzania: siasa na ukweli

Na James Zotto, University of Dar es Salaam
Ndugu zangu watanzania, naamini mnafuatilia vizuri tatizo la mpaka wetu wa ziwa Nyasa na Malawi! Na pia mmefanikiwa kusikia au kusoma hotuba ya Waziri wa Mambo ya nje, Benard Membe. Nilishtushwa kidogo na hotuba hiyo. Niharakishe kusema, mimi napenda utaifa wangu na uzalendo wangu. Lakini napenda sana kutetea mambo yangu kwa kukubali ukweli, kujua hali halisi, kukubali hata zile zinazonipinga, ili nami nijipange kujenga joja. Niongeze tu kuwa, eneo hili nafanyia study yangu ya PhD. Sidhani kama nipo sahihi zaidi na lengo langu si kusema nani anamiliki nini!  
James Zotto akiwa pembezoni mwa ziwa Nyasa.
Ukweli ninaofahamu, tatizo si kubwa sana kama tunavyolifikiri, na pengine tutachukua muda kupitia nyaraka zote muhimu. 
Kwanza, tunahitaji kwenda Idara ya Kumbukumbu ya Uingereza(Public Records Office). Pili tunapaswa kufuatilia Colonial Archives Potsdam, Ujerumani. 
Aidha, tufuatilie pia Malawi National Archives, Tanzania National Archives, Maktaba Chuo Kikuu cha Dar es salaam(UDSM) na Chancellor College Malawi. Ninaamini ubishi utaisha kwa kuwa nyaraka zote zipo.
Naomba nianze kujadili kwa kuweka angalizo katika suala hili ili ikilazimika, Malawi wasalimu amri kwa njia yoyote tutakayoamua, nitasema hapo baadaye. 
Angalizo lenyewe: ziwa Nyasa liligawanywa na mabeberu wa Kiingereza, Kijerumani na Kireno. mkataba wa mwaka 1890 uitwao Anglo-German Agreement, unasema mpaka wa uliokuwa miliki ya Ujerumani au kwa kiingereza German East Africa (Tanzania Bara ya leo) na Nyasaland (Malawi ya leo) unapita kando kando ya ziwa Nyasa kutoka mto Ruvuma(mkoani Ruvuma) mpaka mto Songwe(mkoani Mbeya).
Mkataba huo upo katika nyaraka nyingi sana. Mathalani katika Sheria za Kimataifa (International Law) wanafahamu jambo hilo na sina shaka ndugu zetu wanasheria wa kimataifa (International Lawyers) wanaelewa nini nazungumza! 
Sehemu nyingine ilikuwa ya mkataba ilikuwa mwaka 1891 kati ya Ujerumani na Ureno. Kulingana na mkataba huo, walikubaliana kuwa mipaka ilianzia mto Ruvuma kuelekea Portuguese East Africa (Msumbiji ya leo).
Mkataba mwingine ulikuwa ni kati ya Ureno ambayo ikawekeana mipaka na British Nyasaland (Malawi), kwahiyo, kipindi cha Ujerumani, mipaka inasomeka 'it passes along the shore of the lake (Nyasa).”
Hata hivyo kuliwahi kutokea mabadiliko ya mipaka hiyo. Mabadiliko ya mipaka yalianza kipindi cha ukoloni, kabla ya Ujerumani kuondoka.
                    
                             Kikwete na Banda
Marekebisho ya mipaka yalifanyika kati ya Ujerumani na Ureno kwa kusogeza mipaka mbele na kutamka, “0.5 KM from the original tripartite point” na vijisiwa vya mto Ruvuma vikagawanywa. Mipaka hiyo ipo hivyo hadi leo. 
Na eneo lingine ni kati ya Uingereza na Ureno, ambapo, kisiwa kilichopo eneo la Malawi kinamilikiwa na Msumbiji mpaka leo na eneo la ardhi lililopo Msumbiji linakaliwa na Malawi. 
Huo ulikuwa mkataba wa marekebisho na ipo hivyo mpaka leo. Kwahiyo, tulivyorithi mipaka, tumerithi na mabadiliko haya na hivyo hatuwezi kugombana na Msumbiji wala Msumbiji hawawezi kugombana na Malawi. 
Mpaka wetu na Malawi haukurekebishwa popote pale mpaka Ujerumani ilipoondoka nchini. Nafikiri viongozi wajiandae pia kwa hili ili tuweze kuwashinda ndugu zetu wa Malawi.
Marekebisho ya mipaka kipindi cha Uingereza:- sote tunajua German East Africa, ni sisi(Tanzania) pamoja na Rwanda na Burundi tuligawanywa katika sehemu kuu mbili.
Mosi, tulipokuwa chini ya League of Nations tukiangaliwa na Uingereza. Kuna mambo nahitaji tuweke sawa ili kuongeza hoja kwa mheshimiwa waziri wa mambo ya nje, Bernad Membe. 
Tulipokuwa chini ya League of Nations, tukaitwa ‘Mandated Territory’, na Uingereza ikawa ni ‘Mandatory Power’. Turudi katika Kamusi tutofautishe “a an annexed colony and a mandate.” 
Mpaka ukawekwa kati ya Ubelgiji na Uingereza, uliitwa The Milner-Orts Agreement of 1922! Naam, katika mkataba huu, mto Kagera ulikatwa katikati , hivyo  hadi naandika makala hii mipaka hiyo tumerithi hivyo. 
Hapakuna mahali popote pale ambapo eneo la ziwa Nyasa kama palirekebishwa kwa njia ya mkataba baina ya Nyasaland State na Tanganyika State.
Isipokuwa tofauti na Mandates zote, Tanganyika pekee, ilikuwa na tofauti ndogo, ambapo mpaka wake wa ziwa Nyasa ukapewa wanachoita 'Wording'. Na hivyo, ramani ya Tanganyika na Official Records zikaonyesha kuwa mpaka umepita katikati ya ziwa Nyasa! 
Hapa ndipo tatizo linapoanza na sisi tumeshindwa kusogea mbele kidogo. Ninachokisema hapa kipo pale National Archives Secretariat Files, Accession Numbere AB 8 na AB 30!

                 
James Zotto akiwasilisha utafiti wake kuhusu mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa.
Nafikiri hotuba yote ya mhehimiwa Waziri Membe imetokana na Files hizo, ndizo walizopelekewa. Ndugu zangu watanzania, ni muhimu kujadili zaidi ya hapo.
Twende mbele kidogo, ni kweli kama mheshimiwa alivyosema katika hotuba yake, ramani nyingi kuanzia mwaka 1922 hadi mwaka 1939 zinaonyesha mpaka upo katikati ya ziwa Nyasa! 
Je, ukweli huu utatutosha pekee mbeleni tukifikishana mbali? Hapana, tuendelee kusaidiana kwa hili, nafikiri ujumbe utawafikia tu.
Waziri Membe hakusema kuwa ramani zingine, japo chache muda huu na Official Reports hazionyeshi mpaka au zinaonyesha mpaka upo chini. Lakini ni chache! Kwanini hili?
Bado natafuta majibu, lakini kwa haraka, tunaweza kusema kuwa Uingereza ilitamani Tanganyika iwe koloni lake na si Mandate! Na pia ilishinikizwa na wawekezaji na hata jeshi ilisema afadhari waiteke ili liwe koloni na waachane na Mandate
Nahitaji tuelewe maana ya mandate. Hii yote ilitokea baada ya gavana Donald Cameroon, wa Tanganyika kusema kuwa “Tanganyika is a part of the British empire and it will remain so”.
Hii ni siasa na si ukweli kama unaelewa maana ya kuwa wao hawakuwa wamepewa koloni kama mali yao, bali kuliangalia hadi wananchi wapate 'akili' ili wapewe uhuru! 
Kwa hiyo na kimsingi, kwa maana ya sheria ya kimataifa, Tanganyika haikuwa Part ya British Empire kama yalivyo makoloni yaliyotekwa moja kwa moja na Uingereza yenyewe! 
Hapa pakatokea mvutano mkubwa sana katika House of Lords na House of Commons! Na hivyo basi, mtafaruku huu wa mipaka ulianzia hapo, hivyo hata waingereza wenyewe walivutana kuhusu mipaka. 
Kwa mfano, mwaka 1926, wajumbe wa mabaraza waliibana serikali iseme mipaka ya Tanganyika na ule wa ziwa Nyasa! Mabishano, kama haya yetu leo yalikuwa makubwa, ila si kwa kutishiana kwa kuwa walikuwa wenyewe na walitaka kuwekana sawa!     
                              
Rais Kikwete na Joyce Banda walipokutana katika kikao cha SADC mjini Maputo, Msumbiji.
Naam, ndipo Secretary of state for colonies alibanwa na mjadala ulikuwa wa kisheria zaidi ukihoji Status of the Mandate, British Empire n.k, na kama waingereza wana mamlaka ya kujipangia kuhusu koloni walilokabidhiwa kuliangalia(nieleweke na sio kulimiliki koloni).
Mwishowe wenye dhamana(Waingereza) walisema kwamba, hata wao wanashindwa kuelewa, 'What exactly is the sovereignty of  Tanganyika lying', jamani mnamwelewa huyu mtu wa kiingereza? 
Kwamaana hiyo, haelewi vizuri mipaka yetu, ambayo wenyewe ndo wameirekebisha au kuipa 'Wording'! hivyo, tatizo linaanzia hapa na si muda mwingine wowote!
Jambo kubwa ambalo Waziri Membe hakusema ni hili: kuanzia mwaka 1939, mambo yalibadilika na hawa hawa watu(Wakoloni) tunaochukua ushahidi kutoka kwao, wakafanya madudu! 
Na ilipoisha vita ya pili ya dunia, jamani oneni haya, hawa waingereza katika ramani zao, tena nyingi mno, tuangalie East Africana Section ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, katika sehemu ya Thesis, kuna Cabins 3 zimejaa ramani na bado ni mpya sana kutokana na kutunzwa na pia kutotumika sana.
Zinaonyesha, bila shaka yoyote, kuwa mpaka wa Tanganyika na Nyasaland unapita pembeni mwa ziwa na sio katikati! Nieleweke naonyesha tu mambo yalivyo ili tuweze kuchukua hatua zaidi. 
Hotuba ya Waziri Membe, iliishia nyaraka za mwaka 1939! Kumbe hawa jamaa walichora tena ramani zote zikionyesha mpaka upo pembeni mwa ziwa! Kwanini hili? Natafuta majibu.
Lakini kwa haraka naweza nikakisia mambo mawili. Mosi, karibu na vita vya pili vya dunia, ilisikika tetesi kule duniani(ughaibuni) kuwa, Ujerumani inarudi na inakuja kuchukua makoloni yake. 
Tukitaka kuhakikisha jambo hili, tusome National Archives of Tanzania, Secretariat Files zote zenye kichwa cha habari, 'The future of Tanganyika in British Empire'
Kwa hiyo, waingereza walihofia kutimuliwa na kurudi kwa wajerumani, na hivyo, wakarudisha ule mpaka wa awali wa mwaka 1890 unaotumiwa tena na Malawi kwa sasa! 
Na pia, katika kipindi hicho, baada ya kumalizika vita hivyo, Tanganyika ikawa chini ya Umoja wa Mataifa(United Nation Organisation), ambapo ilipewa Trusteeship Status!
                            
                                      RAMANI YA ZIWA NYASA.
Maana ya hii ni rahisi kuliko Mandate! Kwanini? Hii ilimaanisha ‘to be granted immediate independence’! maana ya neno ‘immediate’ hapa ni kwamba, kwa tafsiri yangu, waingereza walifahamu wanatimka mapema mno kwani mkataba unasema hivyo.
Nafikiri, wakarudisha ramani zikionyesha mpaka upo pembeni mwa ziwa na kitabu cha ‘Nyasaland’ cha mwaka 1958, kinaonyesha mipaka ya Nyasaland na ziwa lote likiwa kwao! 
SASA TUFANYE NINI WATANZANIA?
Tukitaka kuwashinda watu wa serikali ya Malawi, lazima tukisome vizuri kipindi hiki na tuelewe ukweli, hoja zipi zinawapa kiburi. Na hoja zipi sisi tuzitumie kupambana nao, tunaweza! 
Kwahiyo hatima ya nchi yetu haikujulikani itakuwaje. Kipindi hiki, pamoja na mipaka yake pia, tujiulize, kwa maana ya Mandate, waingereza walikuwa na ‘Legal Authority  'kurekebisha' mpaka wa ziwa nyasa? 
Na je makosa waliyofanya waingereza, ndio Legal backing yetu sisi Watanzania?  Hebu tuzame tena tutafute ukweli zaidi ili tuwashinde hawa jamaa wa Malawi!
Tulishindwana na Uingereza kurekebisha mipaka. Mwalimu Nyerere, alisubiri hadi Malawi ipate uhuru, ndipo akatoa miaka mitatu tu na asingetambua mipaka ya kikoloni(Soma Hansard, 1962). 
Malawi walipopata uhuru, kukawa na matatizo ambayo Waziri Membe aliweza kuyaeleza. Nampongeza kwa hilo, ni dhahiri mwaka 1964 wakati wa mgogoro wa baraza la mawaziri la Malawi, na baadhi ya mawaziri kutorokea nchini kwetu kupitia ziwa Nyasa, Rais Kamuzu Banda akaona ziwa ni infiltration route
                                
                             WAZIRI MEMBE akinawa maji ya ziwa Nyasa mjini Mbamba Bay.
Sera zetu za mambo ya nje za Tanzania zilikuwa tofauti na Malawi. Tanzania ilikuwa nchi iliyoongoza ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika, wakati wenzetu Malawi wakaunga mkono Makaburu na Wareno na wakawa na balozi sehemu hizo
Rais Banda akagombana na Mwalimu Nyerere, na matukio ya kutishiana kijeshi yalijitokeza kati ya miaka ya 1967-8; matusi na kejeli zikatawala kati yetu na wao.
Tunakumbuka tuliimba, .....kipara cha Kamuzu Banda kina magamba”, tuliimba tukiwa jeshini hayo. Mwalimu Nyerere  akasema suala mipaka ni hadi Malawi itakapota Sensible Leader akitokea Malawi ndipo tutajadili tena, sio utawala ule wa Kamuzu Banda! 
Kipindi chote hicho tulikuwa kimya, na kuanzia mwaka 1975, hatukuwa na tatizo, lakini sio kusema kuwa tulitatua tatizo la mipaka yetu na Malawi! 
Tulikaa kimya! Mipaka haina tatizo isipokuwa ni time bomb ambapo ikitokea rais mwendawazi akamwaga petroli tu, basi ni vurugu kubwa! 
Tuliirithi kupitia Article III ya Azimio la Umoja wa Afrika la mwaka 1964(OAU Charter, 1964), baadaya ya majadiliano makubwa na wengi wakaridhia “uti possidetis, ita possidetis principle” (so as you exist, so may you exist).
Kama kawaida yetu tulinakili kanuni za mipaka za kibeberu za Westphalia(Westphalia border inviolability)! Hatukupata muda mwingi wa kutafakari na kuangalia kila mpaka na matatizo yake....tulirithi na matatizo na yanatutatiza leo!!!
UTATUZI WA MGOGORO: Tusonge mbele! Nakiri tuna namna tatu ya kulimaliza;- moja ni kwa majadiliano ya kawaida(Diplomacy) kama Waziri Membe alivyosema katika hotuba yake. 
Pili ni kupigana vita (war is another means of diplomacy). Ndugu zangu watanzania nadhani mnataka kuniona kichaa kutamka hilo! Huo ndo ukweli, atakayeshindwa atasalimu kama ilivyokuwa kwa Uganda na sisi watanzania. 
                        
                     WAZIRI WA MAMBO YA NJE, BERNARD MEMBE.
Tatu; ni Mahakama ya Kimataifa(International Court of Justice) hapa nina wasiwasi. Kama nyaraka zenyewe ni zile za Waziri Membe tu, sijui kama tutafanikiwa kushinda kesi.
Tutulie, tuite wataalamu wetu wajikite ndani sana. Ni kweli kama alivyosema Waziri Membe kwenye hotuba yake kwa kunukuu kesi nyingi na zilizoshinda, na kwa kusema kuwa, tukienda mahakama ile sisi ndo tutashinda. 
Nina shaka, tumejipa favour  ya verdict, kabla ya kesi. Sijui, ila nina shaka kubwa, kuna kushinda, kushindwa au suluhu! Ninashaka tena na tena!
Mimi ni mzalendo, nataka ukweli kwa njia ya mahojiano na kuumiza kichwa, tutetee mali zetu tukijua tunawashinda kwa hoja.
WASIWASI: Inasemekana kuna mafuta ziwani,  kwahiyo tujue Marekani na washirika wake hawako mbali! Kampuni ya Surestream ya Uingereza ndio ilipewa leseni ya kutafiti mafuta na utawalawa Bingu wa Mutharika.
Lakini, tujue operesheni ya majeshi ya kibeberu na huyu mama Joyce Banda, ambaye ni mpwa wa Kamuzu Banda, anapata wapi hiki kiburi? Nyuma yake kuna nini na nani? Tuangalie haya pia. 
HITIMISHO: Tusiwe na hoja moja tu mkononi kama ndio water-tight evidence yetu kwa serikali na wananchi kwa ujumla. Tujaribu kuzibishanisha hoja zetu. Na hoja nzuri ni zile zinazopingana nasi na tusizozipenda, tukizielewa na kuzikubali ndipo tutajipanga namna ya kuzigalagaza. Tumwelewe vizuri adui yetu. Mungu ibaraki Tanzania, ziwa Nyasa, wanyasa, na watanzania! Tusing'ang'anie tu Reparian Law.
James Zotto ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam(UDSM).