Showing posts with label Teknolojia. Show all posts
Showing posts with label Teknolojia. Show all posts

October 21, 2017

TABASAMU NA KITABU


Ragin Mmbanga (kushoto) na Markus Mpangala (Kulia)
Huyu ni rafiki yangu. Anaitwa Ragin Mbaga, ila tuwapo farashani hupendelea kumwita "Mzee wa bustani ya usomaji". 

October 16, 2017

CHUO CHAANZISHA SHAHADA YA WADUDU

NAIROBI, KENYA

KITUO cha Elimu na Utafiti kinachofadhiliwa na Benki ya Dunia kimeasisiwa katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogo Oginga Odinga na kinasubiri ruhusa ya kuanzishwa kwa programu za Uzamifu na Uzamili kuhusu wadudu wanaoweza kuliwa.

Taasisi hiyo inapania kubuni njia za kuzalisha wadudu hao kwa wingi bila ya kuharibu mazingira ili kukidhi utashi mara baada ya wazo hilo likifanywa kuwa biashara.Wadudu wanaoliwa sana maeneo ya Magharibi mwa Kenya, ambao wana wingi wa madini ya protini na Zinki watafanywa kuwa biashara ili kuimarisha uwepo wa chakula cha kutosha, na kuondoa dhana mbaya katika kula wadudu. 

October 11, 2017

SOMO LA LEO

“Mheshimiwa Kakunda (Joseph –Naibu Waziri Tamisemi) nakuagiza kuanzia leo maana wewe ndiyo nimekukabidhi jukumu la elimu, nataka mtihani wa 2019 shule za vipaji zote 22 ziongoze mtihani wa Taifa na shule binafsi ziwe nyuma, lakini tuongoze kwa halali si ubabaishaji hapo ndipo shule binafsi za makanjanja zitajifuta zenyewe,”

-Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo.

September 30, 2017

UTUNZI WA VITABU NA KISWAHILI CHA PROFESA SHAOPING

NA KIZITO MPANGALA

KESI YA ALMASI ni kitabu kilichoandikwa na Profesa Rao Shaoping wa China. Kitaaluma yeye ni mhandisi. Alijifunza Kiswahili nchini Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja na ushee, mwalimu aliyemfundisha aliitwa Ali Omari Mzee.
Profesa Shaoping ndiye msimamizi wa kazi za TAZARA wakati inajengwa. Alikuwa akimtafsiria Mwalimu Nyerere mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na wenzake. Pia alikuwa mkaliamani kwa Mh. Salim Ahmed Salim, Mh. Rashid Kawawa, Spika Adam Sapi kwa mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na Wachina wenzake. Na mwaka 2013 Profesa Shaoping alikuja tena nchini Tanzania kumtembela Mzee Ali Hassan Mwinyi.

Profesa Shaoping anasema hivi "ninaipenda Tanzania. Ninawapenda watu wa Tanzania". Profesa Shaoping anayafahamu maeneo mengi nchini Tanzania ambayo amewahi kutembelea, maeneo hayo ni kama vile Kisuwa cha Saa Nane, Arusha, Ifakara, Iringa, Kimbwe, Kidatu, Mikumi, Makambako, Mbarali, Tunduma, Zanzibar, Moshi, Dodoma na kadhalika.

Profesa Shaoping ameandika kitabu hiki kwa bidii mno. Anasema tangu tuwe Koloni la Mjerumani na baadae Mwingereza, wageni hao hawakuwa na morali ya kutunga riwaya za Kiswahili lakini yeye kama mgeni alipenda sana kuacha kitabu kwa Kiswahili, naam, ndicho hiki hapa pichani.

June 16, 2013

MADE IN TANZANIA: HATIMAYE, HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUWA



Mwanafunzi wa Chuo kikuuu cha Dodoma, ndugu Justice Donatus amefanikiwa kutengeneza mtandao wake wa kijamii JUST LIKE FACEBOOK IS,uitwao MAYOCOO ambao utasaidia kuiunganisha jamii ya kitanzania na kimataifa....Mtandao huu umezinduliwa Jumamosi iliyopita tu....Watanzania tunaweza jamani,haya mambo sio tu Mark Zuckerberg aliweza,hata sisi tumeweza...Nampongeza sana dogo,ndo yuko mwaka wa 3 pale UDOM...Namuombea asiache chuo kama alivyofanya Mark,Warren Buffet na Bill Gates...WATANZANIA WENZANGU TUSAPOTI KILICHO CHETU....Mimi Nimeshajiunga na MAYOCOO, Follow me kwa jina la GIOVANNI

Habari hii kwa hisani ya SETH DE JESUS GIOVANNI



January 02, 2013

TOKA ANALOJIA HADI DIGITALI: NINI MAONI YETU?


John Mnyika, MB

Na John Mnyika, Dar es salaam
Naomba majibu yenu kwa kuzingatia kuwa kazi ya wabunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali: baada ya kutekelezwa kwa uamuzi wa kuhama kutoka analojia kwenda digiti kwa mkoa wa Dar es salaam; kwa watumiaji, nini faida na athari mlioanza kuzipata kwa wenye ving’amuzi? Na nini kikwazo kwa wengine ambao hamjahamia mpaka sasa? Na nini mnataka watoa huduma na mamlaka zingine kuzingatia? Katika hatua ya sasa, ni muhimu Tanzania Consumer Advocacy Society (TCAS) ifanye tathmini ya kina kwa niaba ya watumiaji kwa ajili ya hatua zake.  
Ikumbukwe kwamba Consumer Federation of Kenya ilikwenda mahakamani na kuzuia mitambo kuzimwa watumiaji tarehe 31 Disemba 2012, na mahakama imesitisha mpaka itakapofanya uamuzi wake wa msingi.
Kwa upande mwingine, Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Tanzania (TCRA-CCC) litumie mamlaka yake kwa mujibu wa kifungu cha 37 cha Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano namba 12 ya mwaka 2003 na vifungu vingine vinavyohusika kushughulikia malalamiko yaliyotolewa kwa nyakati mbalimbali kwa kuzingatia tahadhari tuliyotoa kwa serikali bungeni miezi mingi iliyopita kuhusu athari zitazojitokeza kwa kutozingatiwa kwa maandalizi muhimu.

NB: John Mnyika ni mbunge wa jimbo la Ubungo