Showing posts with label Muziki. Show all posts
Showing posts with label Muziki. Show all posts

February 19, 2018

FEROUZ, BABA YAKO YUPO KIJIJI CHA MATIMBWA, BAGAMOYO

Na. HONORIUS MPANGALA
MAISHA kama yalivyo na tafsiri pana kwa binadamu tunaoishi katika hii dunia,inatufanya tusiwe na maana halisi.Ujana kwa jinsi zote mbili yaani ya kike na ile ya kiume una changamoto nyingi.  

Waswahili husema ujinga wa ujanani ndio umaskini wa uzeeni. Katika umri huo yatupasa kujiandalia kila aina ya mazingira ili tuweze kuwa na uwepesi katika kutimiza majukumu yetu uzeeni. Unamjua msanii wa bongo fleva aliyesifika kwa kutoa wimbo ambao ulikuwa na ujumbe mzito wa Starehe. Anaitwa Ferouz Mrisho kama watanzania wanavyomfahamu. Kabla ya hapo alikuwa kundi la Daz Nundaz pamoja na Daz Baba.

February 14, 2018

HARUFU YA PILAU LA MAMA BONI ILIWAVUTA ASLAY NA NANDY.

NA HONORIUS MPANGALA
Ni mwendo wa Kilometa 30 kutoka Mlandizi ili ufike Kijiji cha Matimbwa. Pia ni kilometa 8 ukitokea Bagamoyo Mjini ili ufike hapo kijijini. Ilinichukua masaa yasiyo zidi manne kutoka Morogoro hadi nafika kijijini hapo. Yawezekana ikawa ni jina la kijiji ambacho wengi wao wasiweze kukifahamu kama ilivyo Msata katika wilaya hiyo ya Bagamoyo. Ni eneo la jimbo la mheshimiwa Shukuru Kawambwa. Wakazi wake wengi wakiwa Wazaramo,huku Wakwere nao wakiwepo kwa kiasi.
Nyumba mojawapo iliyoko katika video ambapo Nandy kaonekana kaegemea kwenye ukuta huku akiimba
Wakati napanda gari Mlandizi wenyeji wangu Mathayo Venance na Saidi Zimbwe wakanipa maelezo shukia kituo cha Matimbwa Magengeni. Nilikuwa na shauku ya kuijua Matimbwa na Bagamoyo kwa kweli na nilifika salama na kufanya kazi yangu vyema. Jambo kubwa ninalotaka kuwajuza sio mimi nilisafiri vipi kufika huko. Bali nataka nikupe umaarufu wa Matimbwa ambao hata mtayarishaji wa picha mnato Hans Cana autambue vyema.

Ni katika picha mnato ya wimbo wa ‘Subakheri mpenzi’ ulioimbwa na Aslay na Nandy ulimfanya mtayarishaji Hans Cana awapeleke Kijiji cha Matimbwa na kufanya video huko. Kama umjuavyo msanii Aslay huwa mtu wa kupenda picha mnato ambazo hupendwa na watu wa viwango vyote vya Maisha. Hupenda kufanya video akiwa kijijini na huvaa uhusika haswa uhalisia Wa mazingira. 
Pikipiki iliyotumika katika wimbo wa Subakheri Mpenzi

February 10, 2018

‘LOCATION’ YA WANAMUZIKI WA BONGOFLEVA ASLAY NA NANDY


Unaupata wimbo unaobamba sana katika vituo vya redio, kwenye magari ya abiria, bodaboda na Bajaj wa “SUBAKHERI MPENZI” ulioimbwa na wanamuziki wawili; ASLAY na NANDY?

Sasa hii pikipiki niliyokaa ambayo inamuundo wa aina yake imetumika katika video ya huo wimbo, maana ina usukani kama gari na makorombwezo ya mfumo Wa gari. Cratch inakanyagwa kama ya gari. Subiri kile ambacho wenye maeno yao wanavyosema pale inapotokea msanii anafanya video ya wimbo au kazi nyingine ya Sanaa kama filamu wao wanavyojisikia na namna gani wananufaika kupitia Location za hizo video zinazochukuliwa.

 Honorius Mpangala,

Matimbwa, Bagamoyo

January 04, 2018

NURU THE LIGHT AMERUDI TENA ULINGONI


MWANAMUZIKI Nuru Magram au maarufu kwa jina la Nuru The Light amerejea tena kwenye ulingo wa muziki baada ya kukamilisha wimbo wake mpya uitwao "UMENIACHA" kama unavyoonekana pichani. Mwanamuziki huyo mwenye makazi yake nchini Sweden anatarajia kuachia wimbo huu kwenye vituo mbalimbali vya redio hapa nchini ili kuwapa burudani wapenzi wa muziki wake.
Baadhi ya nyimbo zake zilizotia fora  ni "CHAPA LAPA", "NISUBURI USILALE", "L" (Love,Life&Light)?, "WALIMWENGU"?....
Hebu fanya kujikumbusha hapo YouTube, bonyeza NURU THE LIGHT.

November 22, 2017

WEMA SEPETU NA KISA CHA J.LO

NA MARKUS MPANGALA
NIMEPATA tabu kuandika makala haya tangu kumalizika mahojiano ya mwigizaji wa filamu na mshindi wa taji la Miss Tanzania, Wema Isack Sepetu aliyofanyiwa wiki iliyopita (Mei 24/2016) na kampuni yetu ya New Habari (2006) Ltd inayochapisha magazeti ya Rai, Mtanzania, Dimba, Bingwa na The African.
Mwandishi wa makala haya akiwa na mwanamitindo Wema Sepetu.
Tabu hii niliyopata ni kutokana na kuujua ukweli wa pili kuhusu maisha ya mlimbwende huyo. Ni mhariri wa Michezo wa gazeti dada na hili la Mtanzania, Mwani Nyangassa ndiye hasa aliyefanikiwa kumbana vilivyo Wema Sepetu na kujikuta akifunguka zaidi kuhusu maisha yake na mambo mengine yanayomzunguka kama msanii wa filamu, mjasiriamali na mwanasiasa na kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM). 

Mambo yaliyonishtua ni uamuzi wa Wema kueleza kiundani kabisa nini kinachoyasibu maisha yake kwa ujumla kwenye filamu na maisha binafsi. Makala haya naelezea mambo ya kujifunza kwa Wema Sepetu pamoja na kisa cha Jennifer Lopez. 

October 27, 2017

FELA ANIKULAPO KUTI: MWANAMUZIKI ALIYEASISI MTINDO WA PIJINI KATIKA MUZIKI NCHINI NIGERIA NA KUOA WANAWAKE 27.

NA KIZITO MPANGALA

TUNASIKILIZA muziki wa Nigeria mara kwa mara na pengine huenda uliwahi kujihoji aina lugha wanayotumia kuimba na hata katika mazungumzo ya kwaida ya wananchi wa Nigeria. Mtindo huo umejaa pijini kwa kiasi kikubwa hali iliyopelekea kuitwa NIGERIAN ENGLISH.

Fela Anikulapo Kuti alizaliwa  mjini Abeokuta nchini Nigeria mwaka 1938. Alipewa majina OLUFELA OLUSEGUN OLUDOTUM RANSOME ANIKULAPO KUTI lakini alifupisha na kuwa FELA ANIKULAPO KUTI. Mama yake alikuwa ni mwanaharakati wa haki za wanawake katika utawala wa kikoloni wakati huo, na baba yake alikuwa ni mwalimu na vilevile alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza mweusi wa chama cha walimu nchini Nigeria. Fela ni binamu ya Akimwande Oluwole Babatubde Soyinka maarufu kama Wole Soyinka.

Fela alisoma nchini Nigeria na baadae mwaka 1958 alikwenda nchini Uingereza kwa ajili ya kusoma Udakitari wa Dawa lakini alipofika huko alivutiwa na masomo ya muziki hivyo akasoma masomo hayo ya muziki katika chuo cha Trinity. Fela alikuwa mjuzi wa kupiga tarumbeta na Saxophone.

Alianzisha bendi yake iliyoitwa Koola Labitos ambayo ilipiga muziki aina ya jazz.  Huko alimuoa mwanamke aliyeitwa Remilekun Taylor na wakawa na watoto watatu. Mwaka 1963 alirudi nchini Nigeria na kuendelea na bendi yake aliyoianzisha na pia utangazaji katika shirika la utangazaji redioni la Nigeria.
Mwaka 1967 alihamia nchini Ghana na kuanzisha mtindo mpya wa muziki ambao uliitwa Afrobeat. Mwaka 1979 alisafiri kwenda Marekani na alikaa kwa muda wa miezi 10 jijini Los Angels, huko alibadili jina la bendi yake na kuitwa NIGERIA 70. Baadae alitimuliwa nchini humo pamoja na waimbaji wenzake kwa kutokuwa na kibali cha kufanya kazi nchini humo.

July 06, 2013

KUNDI LA MUZIKI LA NDEGE WATATU LIMEINGIA KATIKA SANAA


Kutoka kushoto ni Paulyne Zongo, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Joan Matovolwa.

Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo litakalojulikana kwa jina la NDEGE 3

Kundi la Ndege 3 linaloundwa na wanamuziki wakongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi na kizazi kipya Joan matovolwa, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Paulyne Zongo, hivi karibuni limeshatoa kibao chake kinachokwenda kwa jina la 'MISUKOSUKO YA MAPENZI' ambacho redio kadhaa nchini zimeanza kukirusha.

MISUKOSUKO YA MAPENZI ni nyimbo ambayo imetungwa kwa umahiri wa hali ya juu, na kuonyesha viwango vya juu katika uimbaji na utunzi.

Kwa sasa Joan Matovolwa na Paulyne Zongo ni wanamuziki huru wakati Khadija Mnoga (Kimobitel) ni mwanamuziki anayeimba katika bendi ya Extra Bongo inayoongozwa na Camarade Ally Choki.