Showing posts with label Peramiho. Show all posts
Showing posts with label Peramiho. Show all posts

December 30, 2017

PUGU HADI PERAMIHO; Kijiji cha Dar, Utemi wa Wangoni na kumbukizi maridhawa.

Katika kitabu cha "PUGU HADI PERAMIHO" kuna masimulizi ya kutoka mwaka 1888-1988 na ujio wa Wamisionari wa kijerumani kupitia Shirika lao la Benedictine Fathers lenye makao yale mjini Peramiho kwa sasa.  
Kitabu hiki ni mkusanyiko wa barua na kumbukizi binafsi (Diaries) zilizoandikwa na Mapadre, Mabruda, Masista wakielezea masuala ya ukoloni wa Kijerumani, Injili, Umisionari, Wapagazi, Wangoni na kupenda vita na starehe pamoja na mahusiano ya kibadamu kati ya wazungu na waafrika.

PADRE ANDREAS AMRHREIN
Kitabu hiki kinaanza kwa maandiko ya Abate Lambert Doerr, OSB. Kwanza "Abate" ni wadhifa waliopewa wakuu wa mashirika ya Benedictine Fathers. Lambert anafungua pazia la masimulizi ya Wamisionari Wabenediktine kusini mwa Tanzania.