Showing posts with label Maarifa. Show all posts
Showing posts with label Maarifa. Show all posts

March 07, 2018

KITABU KIPYA KUTOKA KWA MWANDISHI BEKA MFAUME

March 01, 2018

USHAURI KWA RAIS: NAKUOMBA KUBALI TUENDELEE KUCHANGISHANA

NA.HONORIUS MPANGALA
KWANZA kabisa nianze na kukusalimia shikamoo mheshimiwa Rais wangu, Dk. John Pombe Magufuli. Najua hii kazi ni ngumu kama usemavyo wewe mwenyewe lakini sina budi kukuombea uione nyepesi ili uweze kupata nguvu ya kututumikia vyema kama yalivyokuwa malengo yako siku unaenda kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Mheshimiwa nikiwa safarini kuelekea makao makuu ya nchi yetu Dodoma, katika gari nilipata tafakuri  ambayo ilinifanya nitoe kitabu changu cha kuandika kumbukumbu na kuhifadhi mawazo yangu ambayo nimeona nikuandikie. 

Hoja yangu kubwa ambayo ilikuwa ikizunguka katika kichwa changu ni ile niliyokumbuka kauli yako ya kupiga marufuku wananchi kuchangishwa mchango wowote katika shule za serikali.

February 26, 2018

ZAWADI YA VITABU KWA MARA NYINGINE

JUMAMOSI Februari 24 mwaka huu nilipatiwa zawadi ya vita viwili kutoka kwa Bwana Ragin Mmbaga, kama vinavyoonekana pichani. Vitabu hivyo vimeandikwa na Bwana Johne Wisse. Kuna kitabu cha TONE LA DAMU cha lugha ya kiswahili na THE BROKEN CAMPUS RULE cha lugha ya Kiingereza. 
Ninawashukuru kwa kujali kuwa visima vya maarifa. Hakika mwaka huu nimeanza kwa furaha kubwa kwani huyu anakuwa mtu wa tatu kuniletea vitabu kibaruani kwangu. 

Usomaji wa vitabu ndicho kitu ninachokipenda zaidi. Ndicho kilevi au kitu ambacho kinachukua muda wangu wote kuhakikisha nafurahi. Zaidi ya hapo navutiwa na mchezo wa soka. Vitabu ni kitu muhimu sana. Namshukuru Ragin Mmbaga kwa niaba ya John Wisse. ASANTENI SANA

-MARKUS MPANGALA

January 22, 2018

UCHAMBUZI WA VITABU KILA IJUAMAA


Kwa mwezi safu hii inachambua vitabu vinne (4). Kwa mwaka inachambua vitabu 48. Ni safu maalumu kwa uchambuzi wa vitabu pekee. Ni safu iliyodumu kwa miaka minne sasa ndani ya gazeti hili. Ni safu inayopendwa na kampuni za uchapishaji wa vitabu, waandishi na wasomaji pia. Ni safu inayotanua masimulizi au maarifa yaliyomo. 
Una kitabu chako wataka kichambuliwe? Wenzako wanakuja, kwanini wewe usubiri u! Ongea nasi, uwafikie wadau wengi…..

January 04, 2018

ZAWADI YA MWAKA MPYA 2018! KITABU

Adella
ADELLA ABELL ni mtani wangu. Jirani yangu nyumbani. Sahibu wangu. Dada yangu. Ni msomaji mzuri wa vitabu. Katika kuanza mwaka mpya amenipatia zawadi ya kitabu hiki chenye masimulizi ya visa, mikasa, kesi,upelelezi na hukumu mbalimbali zilizowahi kutolewa na mahakama ndani na nje.
Mojawapo ya mkasa uliomo kitabu ni ule wa familia ya George Liundi, mkewe Doris Liundi na watoto wao (Nadhani wengine wamewahi kusikia masimulizi ya maisha ya Taji Liundi).

December 30, 2017

VITABU 50 NILIVYOSOMA MWAKA 2017

NAWASILISHA orodha ya vitabu nilivyosoma mwaka 2017. Ukitazama orodha zangu za usomaji vitabu utabaini kuwa ya mwaka imeongezeka. Nimesoma vitabu 50 na kuna mabaki kadhaa hayaguswa kabisa.
Mwaka 2017 nimejikuta nikiwa nimeongeza uwezo wa kusaka maarifa zaidi kutokana na ongezeko la vitabu ingawa sina desturi ya kupanga idadi yake.

Kwa mwaka 2018 ninatarajia kuongeza maarifa zaidi katika vitabu vya biashara na uchumi, lakini haina maana nitasoma vingi kuzidi ‘ala za roho” (riwaya). Pamoja na changamoto za majukumu na mengineyo, suala la vitabu limebaki kuwa nyeti maishani mwangu. 

December 04, 2017

MFADHILI WA DHIKI

Nikiwa katika ufukwe wa forodha ya Lundu, Nyasa.
Nilitamani nguo kupiga pasi,
Hakika hilo tena siwezi,
Kwetu umeme wa manati,
TANESCO hisani nifanyieni,

Umeme wahakika nipatieni.

Mimi ni muuza Juisi
Kama yule fundi Kinyozi,
Jenereta kwetu hatuwezi,
mitaji yetu kama mkwezi,
Umeme wahakika nipatieni.


November 25, 2017

UCHU WA MADARAKA DHIDI YA UZALENDO

KITABU: ZIMBABWE: STRUGGLES-WITHIN-THE-STRUGGLE (1957-1980)”
MWANDISHI: PROFESA MASIPULA SITHOLE
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA
JESHI la Zimbabwe limetangaza wiki iliyopita kuchukua madaraka nchini humo na kumwondoa Rais Robert Mugabe ambaye ametawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 38 hadi sasa. Kutokana na hali hiyo tunalaizmika kukumbuka namna mwanazuoni Profesa Masipula Sithole alivyobainisha matatizo ya Zimbabwe kupitia kitabu chake cha “Zimbabwe: Struggles-within-the-struggle (1957-1980)”

November 23, 2017

FREDDY MACHA ALIVYOLIZUNGUMZIA JUKWAA LA KISWAHILI SOCIETY

NA MARKUS MPANGALA 
SWALI: Naam, shikamoo Mzee Macha?
FREDDY MACHA; Marahaba. Habari zako bwana! uko wapi wewe siku hizi? Maana tangu tuliposalimiana pale Soma Café,Mikocheni na baadaye Nyumba ya Sanaa, Dar es Salaam wakati wa warsha nilizoendesha huko.
SWALI; Nipo hapa Bongo naendelea vema tu. Ni kweli, kitambo hatujawasiliana, pia nilifaidika sana na warsha zako hata hivyo si neno, tutaongea kidogo leo.
Freddy Macha
 FREDDY MACHA; Asante. Nadhani leo unalo la kuongea zaidi. Karibu.
SWALI; Ni kweli, nahitaji mengi kutoka kwako mzee wangu. Kiu yangu ni huu mradi wa Kiswahili Society, kwani umeeleza mahala fulani nikasoma nami nimevutiwa ili niwaarifu wasomaji. Je mradi huu ulianza lini na wapi?
FREDDY MACHA; Umeanzishwa na wanafunzi na Wahadhiri wa Kiswahili pale chuo cha lugha cha SOAS (School of Oriental and African Studies) hapa London,Uingereza.
SWALI: Nini dhumuni la kuanzishwa kwa Kiswahili Society?
FREDDY MACHA; Kuunganisha Wazungumzaji wa Kiswahili duniani lakini hasa hapa Uingereza.
SWALI: Nashukuru sana. Ndugu Macha, wewe ni Mwanamuziki,Mwanafasihi,na Mwandishi mkongwe. Katika fani hizi kuna mambo mengi umejifunza kutoka bara letu la Afrika,Latin Amerika,Marekani na sasa Ulaya. Unadhani jamii za watu wa Ulaya hususani Uingereza zinaweza kuhamasika kukiendeleza Kiswahili? 

November 15, 2017

ULINZI WA FAMILIA UPO MIKONONI MWETU

KATIKA kitabu hiki….. mhusika Ttiisa anafungua albamu. Ina picha nzuri kila anapofunua. Moja kwa moja anatupia jicho picha ya Suuna.Ni Suuna kipenzi chake. Aliyeingia nae penzini kwa miaka miwili (sasa), bila kujali namna Suuna alivyoleta ugonjwa wa Ukimwi ktk penzi lao (mechi za ugenini?).
 
Katika albamu hiyo hiyo Ttiisa anatazama pia picha ya Ggenza, mtoto wake aliyekuwa na umri wa miezi minne tu lakini alifariki dunia. Kulikoni? Riwaya inakupa jawabu
**************
Ttiisa ana ukimwi. Amekutana na Dona ambaye hana kazi (hana ajira wala hajajiajiri). Makutano yao yanaleta matatizo makubwa ambayo ni somo kwa maisha ya Kampala ya leo (Uganda). Maisha yao hayaeleweki. Sasa walifanyaje hadi kueleweka? ...
Ndo utamu wa nakala ngumu(hard copy) unafunua ukurasa mmoja hadi mwingine kisha unapambia mate kwa mbaaaaali....
#ThanksMolio.B.#

November 12, 2017

NANA YAA ASANTEWAA: MALKIA WA MILKI YA ASHANTI ALIYEWAKINGIA KIFUA WAKOLONI WAINGEREZA.

Na Kizito Mpangala

Alizaliwa mwaka 1863 katika mji wa Besease katika jamii ya Ashanti yenye dhahabu nyingi, Ghana ya sasa, magharibi mwa Afrika. Kaka yake Nana Akwasi Afrane alikuwa ndiye Edweso (kiongozi, au chifu) wa milki ya Ashanti wakati huo. Nana Yaa Asantewaa akiwa bado binti alijishughulisha sana na kilimo. 

Kaka yake (chifu Akwasi) alipokuwa Edweso (kiongozi) alituma askari wake kwenda mapiganoni dhidi ya wakoloni. Baadae aliwekwa kizuizini na wakoloni katika visiwa vya Ushelisheli pamoja na mfalme Prempeh I. Akiwa kizuizini, Nana Akwasi Afrane alimteua dada yake NANA YAA ASANTEWAA kuwa malkia wa milki ya Asante. 

Mwaka 1899 gavana wa wakoloni Waingereza Frederick Hodgson aliitisha mkutano mjini Kumasi ili kulazimisha apewe kiti kilichotengenezwa kwa dhahabu tupu ambacho ni alama takatifu ya Ashanti ambapo askari wa kikoloni walishindwa kukipata kiti hicho, hii ni baada ya kufikiri kwamba ugumu wa kuwatawala Waashanti ungeisha baada ya kupata kiti hicho cha dhahabu. Nana Yaa Asantewaa alimteua mjukuu wake mkubwa kuwa mkuu wa miliki ya Ashanti mara baada ya kufariki kaka yake. 

November 08, 2017

UCHAMBUZI WA TAMTHILIYA YA BLACK MAMBA

KITABU: BLACK MAMBA
MWANDISHI: JOHN RUGANDA
MCHAMBUZI: KIZITO MPANGALA.

Black Mamba ni tamthiliya iliyoandikwa na John Ruganda kutoka nchini Uganda. Namba za usajili ni 978-9966-46-378-X na kuchapiswa na East African Educational Publishers. Kina jumla ya kurasa 70 tu. Wahusika wa tamthilya hii ni Profesa Coarx (kitivo cha sosholojia), Berewa mfanyakazi wa Profesa Coarx, Namudd mke wa Berewa, Odiambo mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya Sosholojia, Catherine Smith mkufunzi mpya kitivo cha Sosholojia, Ofisa wa Polisi na msaidizi wake. Na mhisika msaidizi ni Namatta ambaye ni kahaba. 

November 04, 2017

KITABU CHENYE UTATA KUHUSU RAIS ZUMA CHAPIGWA MARUFUKU



PRETORIA, AFRIKA KUSINI

MAJASUSI wa Afrikia Kusini wanataka kufutiliwa mbali kwa kitabu kipya chenye utata kuhusu madaia yua rais Zuma kujilimbikizia fedha kimakosa ,wakisema kuwa kitabu hicho kimajaa makjosa na kinakiuka sheria ya ujasusi.

Shirika hilo la Ujasusi limetishia kwenda mahakamani iwapo wachapishaji wa kitabu hicho NP watakataa kukifutilia mbali kitabu hicho kwa Jina “The Presidency Keepers: Those Keeping Zuma in Power and Out of Prison''-Wale wanaomueka Zuma mamlakani na kutokwenda jela, kilichotungwa na mwandishi aliyeshinda tuzo la uandishi wa uchunguzi Jacques Pauw.

Kitabu hicho kinadai kwamba Rais Zuma kwa muda wa miezi minne alipokea mshahara kutoka kwa mfanyibiashara mmoja mbali na mshahara anaolipwa na serikali na kwamba hakuutangaza mshahara huo kwa watoza ushuru wa taifa hilo.

Baada ya nakala za kitabu hicho kuchapishwa siku ya Jumapili katika gazeti moja, msemaji wa bwana Zuma alitoa taarifa ,akikana makosa yoyote dhidi ya rais Zuma akidai kwamba alikuwa mwathiriwa wa kampeni mbaya ya kumchafulia jina.

"Maswala ya ulipaji wa kodi ya rais hayana makosa '',ilisema taarifa hiyo.
Nakala za kitabu hicho zinauzwa kwa kasi huku raia wakijaribu kukinunua kabla ya kuisha katika soko.

©BBCSWAHILI

November 02, 2017

FURSA: SEMINA YA WANAZUONI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM


KAMPUNI YA MKUKI NA NYOTA WAINGIA SOKO LA VITABU CHINA


NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

KAMPUNI ya Mkuki na Nyota ambayo hujishughulisha na uchapaji wa vitabu imetanua wigo wa soko lake la uchapishaji na utangazaji wa vitabu baada ya kusaini makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) la nchini China.
 
Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi wa MNN, Mkuki Bgoya amesema kuwa wamesaini Makubaliano na Shirika la World Affairs Press (WAP) ya China kufanya kazi pamoja katika miradi mbalimbali ya kuchapisha na kuvitangaza vitabu ikiwa ni njia mojawapo ya kutanua soko la kampuni hiyo barani Asia.

Mkuki na Nyota ni kampuni mashuhuri kwa uchapaji wa vitabu ambayo ilianzishwa mwaka 1992 jijini Dar es salaam. Mwanzilishi wa kampuni hiyo ni Walter Bgoya ambaye alitumia uzoefu wake wa miaka 18 ya kuwa Meneja Mkuu wa Tanzania Publishing House. 

October 27, 2017

KWANINI WILAYA YA NYASA IMESHIKA MKIA KATIKA MATOKEO YA DARASA LA SABA?



RAYMOND NDOMBA, SONGEA
WILAYA ya Nyasa iliyopo mkoa wa Ruvuma imekuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu 2017 kimkoa. Swali la kujiuliza ni kwanini hali hiyo imetokea. 


Mawazo yangu ni haya; Pamoja na sababu nyingi zilizosababisha matokeo hayo ya aibu kubwa. Wazazi wanapaswa kubeba lawama kubwa. Wengi wao hawafuatilii maendeleo ya watoto wao, pia makuzi na malezi mabaya.

Miaka ya hivi karibuni (kuanzia mwaka 2000), Wazazi wengi katika wilaya ya Nyasa hawajali elimu, hawajigusi katika ufuatiliaji wa watoto wao kielimu na hata kitabia (Angalia matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule za msingi na sekondari kunzia miaka hiyo ya 2000 kwa shule kongwe ndani ya wilaya). 

October 26, 2017

MWALIKO; WOTE MNAKARIBISHWA KWENYE MJADALA HUU


October 21, 2017

UCHAMBUZI WA KITABU CHA UHAMASISHAJI

KITABU: ISHINDE TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO
MWANDISHI: JOEL NANAUKA
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA


JOEL NANAUKA ni miongoni mwa waandishi wazuri katika vitabu vya uhamasishaji na utambuzi. Kitabu chake cha “Ishinde Tabia ya Kughairisha Mambo” kimechapishwa na kampuni ya Benison Communication &Printing iliyopo Dar es salaam na kupewa nambari za usajili ISBN 978-9987-761-99-9.

October 18, 2017

RIWAYA YA WANG LIPING

KITABU: DOUDOU NA MAMA WAKWE ZAKE
MWANDISHI: WANG LIPING
MCHAMBUZI: KIZITO MPANGALA
Doudou Na Mama Wakwe Zake ni hadithi iliyoandikwa kwa lugha ya Kichina na mwandishi Wang Liping na kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili na wakalimani Chen Lianying na Han Mei. Kitabu hiki kina jumla ya kurasa 261 na kimegawanyika katika sehemu 24 za masimulizi yenye mtiririko mzuri ambapo sehemu inayofuata inategemea mhimili kutoka sehemu iliyopita. Kimechachapishwa na Zhenjiang Literature and Art Publishing House kikiwa katika lugha ya kichina na baada ya kutafsiriwa kwa Kiswahili kimechapishwa na Mkuki Na Nyota jijini Dar es Salaam Tanzania na kupewa namba za usajili (ISBN) 978 – 9987 – 08 – 284 – 1. Shukrani kubwa ziende kwa wakalimani  Chen Lianying na Han Mei kwa kutangaza lugha ya Kiswahili.

Ni hadithi inayofahamisha maisha ya kawaida ya Wachina lakini mafundisho yake yanafaa kwa kila mmoja wetu duniani. Hadithi hii kwa mara ya kwanza iliingia nchini Tanzania ikiwa kama mlolongo wa tamthiliya ambapo ilikuwa imefanyiwa marekebisho ambayo yalifanya mazungumzo ya wahusika yasikike kwa Kiswahili. Ilikuwa ikionyeshwa na shirika la habari la taifa (TBC) mwaka 2011.

September 29, 2017

UTAFITI: UHANDISI NI FANI INAYOLIPA ZAIDI

WANAFUNZI wa elimu ya juu ambao husomea taaluma ya uhandishi au biashara katika wana nafasi kubwa kuwa mabilionea kuliko wanafunzi wanaosomea taaluma nyingine.

Aidha, wanafunzi wale ambao tayari wameingia katika soko la ajira katika kazi ya mauzo au biashara ya hisa ni miongoni mwa wenye fursa kubwa  kuwa katika sehemu watu matajiri duniani.

Kwa mujibu wa utafiti uliyofanywa hivi karibuni na shirika la ajira la Aaron Wallis, ambalo utafiti wake umeangalia watu matajiri duniani zaidi 100 ili kuona kama kuna uwiano au uhusiano wowote kati ya taaluma yao ya kwanza na jinsi walivyokuwa matajiri au kutengeneza utajiri.

Ripoti hiyo ilibaini  kwamba kazi yao ya kwanza, kati ya mabilionea wakubwa wa juu waliajiriwa kwa mara ya kwanza katika mashirika ambalo sio yao. Pia  kuna wajasiriamali ambao walianza kampuni zao wenyewe na wengine wale walioajiriwa katika biashara za kifamilia  katika nafasi masoko na mauzo.
Mabilionea 10 wa mwanzo kati ya 53 ambao waliajiriwa  katika shirika ambalo sio yao wakati mabilionea tisa tu walianza kazi yao kama mfanyabiashara wa hisa au mauzo.

Utafiti huo pia uligundua kuwa matajiri wakubwa duniani 75 kati ya watu 100 akiwemo Bill Gates, Warren Buffet, George Soros na Jeff Bezos wana elimu ya ngazi ya shahada tu.

Kati ya hao 75,  matajiri 22 walisomea shahada katika taaluma ya uhandisi (ikiwa ni pamoja na mwanzilishi wa mtandao wa Amazon, Jeff Bezos na  mwanzilishi wa Google Larry Page, aidha matajiri 16 walisomea masuala ya biashara ambapo 11 wamesoma taaluma ya fedha na uchumi.

Mabilionea 30 kati ya 100 wanautajiri wa kurithi au wanafanya kazi katika biashara ya kifamilia, wakati 17 walianza kampuni zao wenyewe. Mwezi Julai mwaka huu, muda mfupi tajiri Jeff Bezos alichukua nafasi ya Bill Gates kuwa mtu tajiri zaidi duniani baada ya kuongezeka kwa hisa katika mauzo ya mtandao kabla ya ripoti yake ya mapato, lakini hisa zilishuka tena na Gates alirejea katika nafasi ya kwanza.

Bill Gates ambaye ana utajiri wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 87, na amekuwa mtu tajiri  zaidi duniani tangu mwaka 2013. Billionea huyu mwenye moyo wa kusiadia ametoa dola bilioni 31.1 ya utajiri wake katika kusaidia jamii kupitia taasisi mbalimbali, wakati Jeff Bezos ametoa dola milioni 100 kwa mujibu wa jarida la Forbes  la nchini Marekani.

Hata hivyo, ripoti imebaini kuwa matajiri wengi katika 100 wamesomea shahada ya kwanza ya uhandisi kama orodha ilivyoeleza. Matajiri wakubwa 22 duniani wanataaluma ya uhandisi, ambapo matajiri 16 wamesomea masuala ya biashara, katika fedha na uchumi (11) sheria (6) sayansi ya kompyuta (4) historia (3) Falsafa (2), Siasa (2), lugha ya Kiingereza (2), Historia (2), Hisabati (2) na masuala ya madawa (1).

©MTANZANIA