Showing posts with label utalii. Show all posts
Showing posts with label utalii. Show all posts
January 15, 2018
KARIBUNI RUVUMA. KARIBUNI KUTALII TUNDURU
December 28, 2017
UTAFITI: HISTORIA YA ENEO LA TINGITINGI ZIWA NYASA
...TULIPOFIKA hapa tukiwa
tunatafakari sehemu ya kupita Mdogo wetu Thobias (mwenye tisheti nyekundu) akaniambia
brother nimekumbuka movie moja inaitwa The Hard Way Is The Only Way. Akanielezea
kidogo maana jamaa anapenda movie sana.
Moja ya msitu ulioko eneo la jiwe maarufu Tingitingi.
Karibu na ukuta wa mawe wa wampoto.Hapa ilikuwa tunasikiliza sauti za kanga
pori tu na kuona kenge na mijusi wa rangi rangi.
UMENG’ATWA NA MANYIGU, LAKINI KIU BADO UNAYO.
NIKIWA njiani kurejea Dar es
salaam, mdogo wangu Honorius Mpangala alinitumia ujumbe mfupi katika simu
yangu, “Aisee tupo Tingitingi, lakini nimeng’atwa na manyigu. Vifaa tulibeba
kama kawaida,”.
Nikashangaa. Sikufikiria kama
eneo lile laweza kuwa na manyigu au hatari zozote za wanyama wakali. Leo pichani
anasema, “Nikiwa najikagua mkono na miguu baada ya kung'atwa na manyigu saba. Ilikuwa
tarehe 25/12 saa saba mchana pori moja kando ya ziwa Nyasa.Pori lenye msitu
unaogota katika maji ukiwa na mawe makubwa huko ndo maskani ya wanyama kama
ngedere, nyoka, nungunungu, mijusi wa rangi rangi,ndege kama kanga pori na Kwale.
Baada ya shambulizi nilijiziba uso na kuacha sehemu ya miguu kuwa wazi lakini
ajabu niling'atwa hadi kwenye makalio,”.
Madhumuni
kazi,
kumbukumbu,
Nyasa,
utalii
December 11, 2017
MAREKEBISHO: UTEUZI WA WAJUMBE WA KAMATI YA KITAIFA YA UTALII
December 01, 2017
WAZIRI MKUU ATAMBUE NYASA IMEJAA UTAJIRI
Na
MARKUS MPANGALA
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa
wakati akifunga mkutano wa tisa wa Bunge la 11 Novemba 17 mwaka huu alibainisha
jambo muhimu linalohusu ubora wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambayo inajumuisha
mikoa ya Ruvuma, Mbeya, Lindi na Mtwara.
![]() |
| Makala haya yalichapishwa katika safu yangu ya MAWAZONI ndani ya gazeti la RAI linalotoka kila alhamis |
Waziri mkuu katika hotuba yake
alimwagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangala kuanzisha
Mamlaka ya Fukwe za Bahari na Maziwa ili kutangaza utalii na kuendeleza fukwe
ambazo hazina shughuli.
Agizo la Majaliwa linaakisi
mpango wa serikali wa kuendeleza utalii Nyanda za Juu Kusini kwani kuna vivutio
vingi lakini pamekuwapo idadi ndogo ya watalii wanaotembelea ukanda huo,
ukilinganisha na Kaskazini.
November 24, 2017
JIWE LA POMONDA NA FORODHANI PANAWEZA KUTUPATIA WATU WA 'DIVING' KATIKA MASHINDANO YA OLIMPIKI.
NA HONORIUS MPANGALA
LICHA
ya kuwa mazingira mazuri na yenye kila aina ya vivutio lakini wafrika
tunashindwa kuwa wabunifu wa katika kuyafanya kama fursa.Mungu aliiumba Afrika
hivi ilivyo na kuweka jiografia ambayo nyakati zote watu Wa mataifa ya ulaya
wamekuwa wakivutiwa nayo.
![]() |
| Mmmoja wa Warukaji katika Jiwe la Pomonda, Ziwa Nyasa |
Iko
michezo mingi inayochezwa Ulaya na Amerika inatokana na jinsi wenzetu walivyo
makini katika kutumia mazingira yao katika kujipatia fursa ya maisha yao.
Nyakati zote mataifa ya wazungu yamekuwa na michezo mingi ambayo ina mashabiki
na wanafanya vyema,hakuna michezo ambao unakosa mashabiki Amerika na Ulaya.
Madhumuni
afya,
amani na upendo,
Nyasa,
utalii,
uzuri
November 22, 2017
FUKWE ZA LUNDU, KARIBUNI ZIWA NYASA
Hapa ni Forodha ya Lundu. Eneo hili lina fukwe mzuri sana kama huu. Picha ya Juu ni upande wa Kusini mwa forodha. Picha ya chini ni upande wa kaskazini magharibi mwa forodha hiyo. Ufukwe huu umepokea wageni kutoka Ujerumani, Italia, na wengineo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Karibuni sana Lundu. Karibuni Wilaya ya Nyasa.
November 16, 2017
MBAMBA HILL KUWA HIFADHI YA PILI YA ASILI TANZANIA KUWA MJINI
NA MWANDISHI WETU
MKOA wa Ruvuma unatarajia
kupata hifadhi ya wanyamapori ya pili ya asili inayoitwa Kilima Mbamba (Mbamba
Hill) ambayo ipo mjini Mbamba Bay makao makuu ya wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.
Hifadhi pekee Tanzania ya
kwanza ya asili iliyopo mjini inaitwa Luhira iliyopo kilometa saba toka mjini
Songea mkoani Ruvuma iliyoanzishwa mwaka 1974. Mkoa wa Ruvuma unapata hifadhi
ya pili ya asili mjini.
Madhumuni
mbamba bay,
Nyasa,
utalii
November 15, 2017
KISIWA CHA MBAMBA BAY KIMEPENDEKEZWA KUWA HIFADHI
NYUMA
yangu ni kisiwa cha Mbambabay wengine wanakiita kisiwa cha Zambia kilichopo
Mbamba Bay wilayani Nyasa mkoani Ruvuma ambacho kimependekezwa kuwa Hifadhi ya
wanyamapori. Kisiwa hicho kina ukubwa wa hekta 27.kisiwa hicho kimejaliwa kuwa
na uoto unaovutia wa misitu ya miombo ambao ni maarufu duniani ambapo mawe
yanayozunguka katika kisiwa hicho ni mazalia ya samaki wa mapambano aina zaidi
ya 400 wanaopatikana katika ziwa Nyasa pekee.
Madhumuni
mbamba bay,
utalii
KIFAHAMU KISIWA CHA LUNDO KILICHOPO ZIWA NYASA
HISTORIA ya kivutio cha utalii,
kisiwa cha Lundo kilichopo Ziwa Nyasa, inaonesha kuwa kisiwa hicho kina ukubwa
za hekta 20 kimepewa jina la Lundo kwa sababu watu wa kwanza waliovuka kisiwa
hicho kwenda ng’ambo ya pili walifikia kijiji cha Lundo.
Kisiwa hicho tangu zamani
kilikuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa vijiji vya Lundo,Ngindo na Chinula
kwa sababu wakati wa vita ya Majimaji vilivyotokea kati ya mwaka 1905 hadi 1907
watu walikuwa wanakimbilia katika kisiwa hicho ambacho kina maeneo ya maficho.
Baada ya vita ya Majimaji
kuanzia mwaka 1908 kisiwa hiki kilitumika na wakoloni wa kijerumani kuwahifadhi
watu waliopata ulemavu kutokana na ugonjwa wa ukoma ambao baada ya uhuru
walihamishiwa katika makazi ya Ngehe wilayani Nyasa. Serikali imependekeza
visiwa vya Lundo na Mbamba Bay kuwa hifadhi za wanyamapori.
Visiwa hivyo vitakuwa ni
hifadhi ya pekee ya wanyamapori pamoja na samaki wa mapambo wanaozaliana katika
visiwa hivyo ndani ya ziwa Nyasa hivyo kuvutia watalii kufika kusini na
kutekeleza Sera ya nchi ya kufungua biashara ya utalii Kusini.
November 13, 2017
MILIMA NA MABONDE YA MATOGORO KIVUTO CHA UTALII
November 10, 2017
KINANDA: MAJI YA ZIWA NYASA YANAPUNGUA?
NA MARKUS MPANGALA
JIWE hili ni maarufu sana katika kijiji cha Lundu. Linaitwa Kinanda au kwa wenyeji tunaliita kienyeji “Chinanda”. Lipo katika forodha ya Chivanga. Picha hii ilipigwa mapema Mwezi Februari mwaka huu.
JIWE hili ni maarufu sana katika kijiji cha Lundu. Linaitwa Kinanda au kwa wenyeji tunaliita kienyeji “Chinanda”. Lipo katika forodha ya Chivanga. Picha hii ilipigwa mapema Mwezi Februari mwaka huu.
![]() |
| Honorius Mpangala akiwa katika Jiwe la Kinanda, Februari mwaka huu. |
Lipo
jambo moja la kusikitisha ni kwamba kiasi cha Maji katika Ziwa Nyasa si kama
kile kilichokuwa zamani. Katika miaka ya 1980 hadi miaka 90 jiwe hilo
lilizungukwa na Maji. Lakini miaka mwanzoni mwa 200o kumekuwa na mabadiliko
mengi katikam ziwa.
MAJINA YA MITAA HUFANANA
![]() |
| Mtaa wa Muhoro |
Pichani
ni mtaa mmojawapo ulipo jijini Dar es salaam. Ni mtaa wa Muhoro. Katika
kumbukumbu zangu mtaa kama huu wenye jina hili upo katika Kijiji cha Lundu, kilichopo
Kata ya Mbaya, Tarafa ya Ruhuhu, wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma. Lundu ni
miongoni mwa vijiji vyenye historia kubwa na kipo mwambao wa ziwa Nyasa.
Kumbukumbu
hizo za kihistoria zinaonyesha uhusiano wa watu na namna wanavyoingilia au
kuathiriwa na maisha ya eneo moja kwenda jingine.
Hakuna
taarifa rasmi inayosema mtaa wa Muhoro wa Dar es salaam ulianzishwa kwasababu
gani, sambamba na ule wa kijiji cha Lundu.
MUHIMU:
Kuanzia mwaka huu tutakuwa na habari kemukemu za kihistoria kuhusiana na
ukoloni,wamisionari,wangoni na mengineyo katika mwambao wa Ziwa Nyasa (husuani
Tarafa ya Ruhusu).
Endelea
kubaki nasi…
![]() |
| Honorius Mpangala akiwa na Alfred Mpangala katika kibao chenye jina la Mtaa wa Muhoro jijini Dar es salaam |
MAJIMAJI FC KUFANYA ZIARA NYASA
November 09, 2017
WILAYA YA NYASA INAO UTAJIRI WA VIVUTIO VYA UTALII
Madhumuni
mbamba bay,
Nyasa,
utalii,
utulivu
November 04, 2017
UTALII: UFUKWE WA KIJIJI CHA LUNDU
Wilaya ya Nyasa imebarikiwa kuwa na fukwa zuri zinazotokana na ziwa Nyasa. Huu mojawapo ya ufukwe wenye historia kubwa sana, kupokea wageni kutoka Ujerumani, Uingereza, Italia na nchi mbalimbali ambao wengi wao walikuja kupitia Shirika la Benedictine Fathers la Peramiho na wengine kwa njia zao binafsi. Ni ufukwe wenye kumbukumbu nzuri sana kwa wakazi na wageni.
KARIBUNI NYASA.
KARIBUNI NYASA.
Madhumuni
amani na upendo,
habari,
lundu,
Nyasa,
utalii
November 01, 2017
WAZIRI KAZINI
![]() |
| Waziri wa Maliasili na Utalii nchini, Hamis Kigwangallah, akiwa kwenye ziara ya mojawapo ya Mbuga za wanyama |
October 21, 2017
TABASAMU NA KITABU
Madhumuni
afya,
amani na upendo,
malezi,
mawazoni,
Nyasa,
Teknolojia,
urafiki,
utalii,
utamaduni,
uzuri,
vicheko,
Vitabu,
wageni,
wazo
October 13, 2017
WATALII TOKA ULAYA WATEMBELEA HIFADHI YA LUHIRA
SONGEA, RUVUMA
Watalii toka nje ya nchi wameanza kutembelea hifadhi ya
Asili ya Luhira iliyopo katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma. Takwimu za mwaka 2016/ 2017 zinaonesha kuwa hifadhi hiyo
imepokea watalii toka nchi za Ujerumani,Afrika ya Kusini,India,Ufaransa,Italia,
Uholanzi na wageni toka mikoa mbalimbali nchini ambao pia wanafanya utalii wa
kuchunguza aina ya mimea na ndege katika hifadhi hiyo.
Msimamizi wa Hifadhi hiyo Msonda Simwanza anasema
wanajiandaa kuweka mazingira ambayo yatawezesha wanyama kama tembo,simba na wanyama
wengine adimu kuishi katika hifadhi hiyo bila kuleta athari kwa wanyama na
binadamu.
Subscribe to:
Posts (Atom)




















