Na. HONORIUS MPANGALA
MAISHA
kama yalivyo na tafsiri pana kwa binadamu tunaoishi katika hii dunia,inatufanya
tusiwe na maana halisi.Ujana kwa jinsi zote mbili yaani ya kike na ile ya kiume
una changamoto nyingi.
Waswahili
husema ujinga wa ujanani ndio umaskini wa uzeeni. Katika umri huo yatupasa
kujiandalia kila aina ya mazingira ili tuweze kuwa na uwepesi katika kutimiza
majukumu yetu uzeeni. Unamjua
msanii wa bongo fleva aliyesifika kwa kutoa wimbo ambao ulikuwa na ujumbe mzito
wa Starehe. Anaitwa Ferouz Mrisho kama watanzania wanavyomfahamu. Kabla ya hapo
alikuwa kundi la Daz Nundaz pamoja na Daz Baba.


