Showing posts with label dondoo. Show all posts
Showing posts with label dondoo. Show all posts

November 01, 2012

JAMES ZOTTO ALIPOZUNGUMZIA MGOGORO WA ZIWA NYASA, KABLA YA KUWASILISHA UTAFITI WAKE KWENYE UMOJA WA AFRIKA NCHINI ETHIOPIA

Mgogoro wa mpaka Malawi na Tanzania: siasa na ukweli

Na James Zotto, University of Dar es Salaam
Ndugu zangu watanzania, naamini mnafuatilia vizuri tatizo la mpaka wetu wa ziwa Nyasa na Malawi! Na pia mmefanikiwa kusikia au kusoma hotuba ya Waziri wa Mambo ya nje, Benard Membe. Nilishtushwa kidogo na hotuba hiyo. Niharakishe kusema, mimi napenda utaifa wangu na uzalendo wangu. Lakini napenda sana kutetea mambo yangu kwa kukubali ukweli, kujua hali halisi, kukubali hata zile zinazonipinga, ili nami nijipange kujenga joja. Niongeze tu kuwa, eneo hili nafanyia study yangu ya PhD. Sidhani kama nipo sahihi zaidi na lengo langu si kusema nani anamiliki nini!  
James Zotto akiwa pembezoni mwa ziwa Nyasa.
Ukweli ninaofahamu, tatizo si kubwa sana kama tunavyolifikiri, na pengine tutachukua muda kupitia nyaraka zote muhimu. 
Kwanza, tunahitaji kwenda Idara ya Kumbukumbu ya Uingereza(Public Records Office). Pili tunapaswa kufuatilia Colonial Archives Potsdam, Ujerumani. 
Aidha, tufuatilie pia Malawi National Archives, Tanzania National Archives, Maktaba Chuo Kikuu cha Dar es salaam(UDSM) na Chancellor College Malawi. Ninaamini ubishi utaisha kwa kuwa nyaraka zote zipo.
Naomba nianze kujadili kwa kuweka angalizo katika suala hili ili ikilazimika, Malawi wasalimu amri kwa njia yoyote tutakayoamua, nitasema hapo baadaye. 
Angalizo lenyewe: ziwa Nyasa liligawanywa na mabeberu wa Kiingereza, Kijerumani na Kireno. mkataba wa mwaka 1890 uitwao Anglo-German Agreement, unasema mpaka wa uliokuwa miliki ya Ujerumani au kwa kiingereza German East Africa (Tanzania Bara ya leo) na Nyasaland (Malawi ya leo) unapita kando kando ya ziwa Nyasa kutoka mto Ruvuma(mkoani Ruvuma) mpaka mto Songwe(mkoani Mbeya).
Mkataba huo upo katika nyaraka nyingi sana. Mathalani katika Sheria za Kimataifa (International Law) wanafahamu jambo hilo na sina shaka ndugu zetu wanasheria wa kimataifa (International Lawyers) wanaelewa nini nazungumza! 
Sehemu nyingine ilikuwa ya mkataba ilikuwa mwaka 1891 kati ya Ujerumani na Ureno. Kulingana na mkataba huo, walikubaliana kuwa mipaka ilianzia mto Ruvuma kuelekea Portuguese East Africa (Msumbiji ya leo).
Mkataba mwingine ulikuwa ni kati ya Ureno ambayo ikawekeana mipaka na British Nyasaland (Malawi), kwahiyo, kipindi cha Ujerumani, mipaka inasomeka 'it passes along the shore of the lake (Nyasa).”
Hata hivyo kuliwahi kutokea mabadiliko ya mipaka hiyo. Mabadiliko ya mipaka yalianza kipindi cha ukoloni, kabla ya Ujerumani kuondoka.
                    
                             Kikwete na Banda
Marekebisho ya mipaka yalifanyika kati ya Ujerumani na Ureno kwa kusogeza mipaka mbele na kutamka, “0.5 KM from the original tripartite point” na vijisiwa vya mto Ruvuma vikagawanywa. Mipaka hiyo ipo hivyo hadi leo. 
Na eneo lingine ni kati ya Uingereza na Ureno, ambapo, kisiwa kilichopo eneo la Malawi kinamilikiwa na Msumbiji mpaka leo na eneo la ardhi lililopo Msumbiji linakaliwa na Malawi. 
Huo ulikuwa mkataba wa marekebisho na ipo hivyo mpaka leo. Kwahiyo, tulivyorithi mipaka, tumerithi na mabadiliko haya na hivyo hatuwezi kugombana na Msumbiji wala Msumbiji hawawezi kugombana na Malawi. 
Mpaka wetu na Malawi haukurekebishwa popote pale mpaka Ujerumani ilipoondoka nchini. Nafikiri viongozi wajiandae pia kwa hili ili tuweze kuwashinda ndugu zetu wa Malawi.
Marekebisho ya mipaka kipindi cha Uingereza:- sote tunajua German East Africa, ni sisi(Tanzania) pamoja na Rwanda na Burundi tuligawanywa katika sehemu kuu mbili.
Mosi, tulipokuwa chini ya League of Nations tukiangaliwa na Uingereza. Kuna mambo nahitaji tuweke sawa ili kuongeza hoja kwa mheshimiwa waziri wa mambo ya nje, Bernad Membe. 
Tulipokuwa chini ya League of Nations, tukaitwa ‘Mandated Territory’, na Uingereza ikawa ni ‘Mandatory Power’. Turudi katika Kamusi tutofautishe “a an annexed colony and a mandate.” 
Mpaka ukawekwa kati ya Ubelgiji na Uingereza, uliitwa The Milner-Orts Agreement of 1922! Naam, katika mkataba huu, mto Kagera ulikatwa katikati , hivyo  hadi naandika makala hii mipaka hiyo tumerithi hivyo. 
Hapakuna mahali popote pale ambapo eneo la ziwa Nyasa kama palirekebishwa kwa njia ya mkataba baina ya Nyasaland State na Tanganyika State.
Isipokuwa tofauti na Mandates zote, Tanganyika pekee, ilikuwa na tofauti ndogo, ambapo mpaka wake wa ziwa Nyasa ukapewa wanachoita 'Wording'. Na hivyo, ramani ya Tanganyika na Official Records zikaonyesha kuwa mpaka umepita katikati ya ziwa Nyasa! 
Hapa ndipo tatizo linapoanza na sisi tumeshindwa kusogea mbele kidogo. Ninachokisema hapa kipo pale National Archives Secretariat Files, Accession Numbere AB 8 na AB 30!

                 
James Zotto akiwasilisha utafiti wake kuhusu mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa.
Nafikiri hotuba yote ya mhehimiwa Waziri Membe imetokana na Files hizo, ndizo walizopelekewa. Ndugu zangu watanzania, ni muhimu kujadili zaidi ya hapo.
Twende mbele kidogo, ni kweli kama mheshimiwa alivyosema katika hotuba yake, ramani nyingi kuanzia mwaka 1922 hadi mwaka 1939 zinaonyesha mpaka upo katikati ya ziwa Nyasa! 
Je, ukweli huu utatutosha pekee mbeleni tukifikishana mbali? Hapana, tuendelee kusaidiana kwa hili, nafikiri ujumbe utawafikia tu.
Waziri Membe hakusema kuwa ramani zingine, japo chache muda huu na Official Reports hazionyeshi mpaka au zinaonyesha mpaka upo chini. Lakini ni chache! Kwanini hili?
Bado natafuta majibu, lakini kwa haraka, tunaweza kusema kuwa Uingereza ilitamani Tanganyika iwe koloni lake na si Mandate! Na pia ilishinikizwa na wawekezaji na hata jeshi ilisema afadhari waiteke ili liwe koloni na waachane na Mandate
Nahitaji tuelewe maana ya mandate. Hii yote ilitokea baada ya gavana Donald Cameroon, wa Tanganyika kusema kuwa “Tanganyika is a part of the British empire and it will remain so”.
Hii ni siasa na si ukweli kama unaelewa maana ya kuwa wao hawakuwa wamepewa koloni kama mali yao, bali kuliangalia hadi wananchi wapate 'akili' ili wapewe uhuru! 
Kwa hiyo na kimsingi, kwa maana ya sheria ya kimataifa, Tanganyika haikuwa Part ya British Empire kama yalivyo makoloni yaliyotekwa moja kwa moja na Uingereza yenyewe! 
Hapa pakatokea mvutano mkubwa sana katika House of Lords na House of Commons! Na hivyo basi, mtafaruku huu wa mipaka ulianzia hapo, hivyo hata waingereza wenyewe walivutana kuhusu mipaka. 
Kwa mfano, mwaka 1926, wajumbe wa mabaraza waliibana serikali iseme mipaka ya Tanganyika na ule wa ziwa Nyasa! Mabishano, kama haya yetu leo yalikuwa makubwa, ila si kwa kutishiana kwa kuwa walikuwa wenyewe na walitaka kuwekana sawa!     
                              
Rais Kikwete na Joyce Banda walipokutana katika kikao cha SADC mjini Maputo, Msumbiji.
Naam, ndipo Secretary of state for colonies alibanwa na mjadala ulikuwa wa kisheria zaidi ukihoji Status of the Mandate, British Empire n.k, na kama waingereza wana mamlaka ya kujipangia kuhusu koloni walilokabidhiwa kuliangalia(nieleweke na sio kulimiliki koloni).
Mwishowe wenye dhamana(Waingereza) walisema kwamba, hata wao wanashindwa kuelewa, 'What exactly is the sovereignty of  Tanganyika lying', jamani mnamwelewa huyu mtu wa kiingereza? 
Kwamaana hiyo, haelewi vizuri mipaka yetu, ambayo wenyewe ndo wameirekebisha au kuipa 'Wording'! hivyo, tatizo linaanzia hapa na si muda mwingine wowote!
Jambo kubwa ambalo Waziri Membe hakusema ni hili: kuanzia mwaka 1939, mambo yalibadilika na hawa hawa watu(Wakoloni) tunaochukua ushahidi kutoka kwao, wakafanya madudu! 
Na ilipoisha vita ya pili ya dunia, jamani oneni haya, hawa waingereza katika ramani zao, tena nyingi mno, tuangalie East Africana Section ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, katika sehemu ya Thesis, kuna Cabins 3 zimejaa ramani na bado ni mpya sana kutokana na kutunzwa na pia kutotumika sana.
Zinaonyesha, bila shaka yoyote, kuwa mpaka wa Tanganyika na Nyasaland unapita pembeni mwa ziwa na sio katikati! Nieleweke naonyesha tu mambo yalivyo ili tuweze kuchukua hatua zaidi. 
Hotuba ya Waziri Membe, iliishia nyaraka za mwaka 1939! Kumbe hawa jamaa walichora tena ramani zote zikionyesha mpaka upo pembeni mwa ziwa! Kwanini hili? Natafuta majibu.
Lakini kwa haraka naweza nikakisia mambo mawili. Mosi, karibu na vita vya pili vya dunia, ilisikika tetesi kule duniani(ughaibuni) kuwa, Ujerumani inarudi na inakuja kuchukua makoloni yake. 
Tukitaka kuhakikisha jambo hili, tusome National Archives of Tanzania, Secretariat Files zote zenye kichwa cha habari, 'The future of Tanganyika in British Empire'
Kwa hiyo, waingereza walihofia kutimuliwa na kurudi kwa wajerumani, na hivyo, wakarudisha ule mpaka wa awali wa mwaka 1890 unaotumiwa tena na Malawi kwa sasa! 
Na pia, katika kipindi hicho, baada ya kumalizika vita hivyo, Tanganyika ikawa chini ya Umoja wa Mataifa(United Nation Organisation), ambapo ilipewa Trusteeship Status!
                            
                                      RAMANI YA ZIWA NYASA.
Maana ya hii ni rahisi kuliko Mandate! Kwanini? Hii ilimaanisha ‘to be granted immediate independence’! maana ya neno ‘immediate’ hapa ni kwamba, kwa tafsiri yangu, waingereza walifahamu wanatimka mapema mno kwani mkataba unasema hivyo.
Nafikiri, wakarudisha ramani zikionyesha mpaka upo pembeni mwa ziwa na kitabu cha ‘Nyasaland’ cha mwaka 1958, kinaonyesha mipaka ya Nyasaland na ziwa lote likiwa kwao! 
SASA TUFANYE NINI WATANZANIA?
Tukitaka kuwashinda watu wa serikali ya Malawi, lazima tukisome vizuri kipindi hiki na tuelewe ukweli, hoja zipi zinawapa kiburi. Na hoja zipi sisi tuzitumie kupambana nao, tunaweza! 
Kwahiyo hatima ya nchi yetu haikujulikani itakuwaje. Kipindi hiki, pamoja na mipaka yake pia, tujiulize, kwa maana ya Mandate, waingereza walikuwa na ‘Legal Authority  'kurekebisha' mpaka wa ziwa nyasa? 
Na je makosa waliyofanya waingereza, ndio Legal backing yetu sisi Watanzania?  Hebu tuzame tena tutafute ukweli zaidi ili tuwashinde hawa jamaa wa Malawi!
Tulishindwana na Uingereza kurekebisha mipaka. Mwalimu Nyerere, alisubiri hadi Malawi ipate uhuru, ndipo akatoa miaka mitatu tu na asingetambua mipaka ya kikoloni(Soma Hansard, 1962). 
Malawi walipopata uhuru, kukawa na matatizo ambayo Waziri Membe aliweza kuyaeleza. Nampongeza kwa hilo, ni dhahiri mwaka 1964 wakati wa mgogoro wa baraza la mawaziri la Malawi, na baadhi ya mawaziri kutorokea nchini kwetu kupitia ziwa Nyasa, Rais Kamuzu Banda akaona ziwa ni infiltration route
                                
                             WAZIRI MEMBE akinawa maji ya ziwa Nyasa mjini Mbamba Bay.
Sera zetu za mambo ya nje za Tanzania zilikuwa tofauti na Malawi. Tanzania ilikuwa nchi iliyoongoza ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika, wakati wenzetu Malawi wakaunga mkono Makaburu na Wareno na wakawa na balozi sehemu hizo
Rais Banda akagombana na Mwalimu Nyerere, na matukio ya kutishiana kijeshi yalijitokeza kati ya miaka ya 1967-8; matusi na kejeli zikatawala kati yetu na wao.
Tunakumbuka tuliimba, .....kipara cha Kamuzu Banda kina magamba”, tuliimba tukiwa jeshini hayo. Mwalimu Nyerere  akasema suala mipaka ni hadi Malawi itakapota Sensible Leader akitokea Malawi ndipo tutajadili tena, sio utawala ule wa Kamuzu Banda! 
Kipindi chote hicho tulikuwa kimya, na kuanzia mwaka 1975, hatukuwa na tatizo, lakini sio kusema kuwa tulitatua tatizo la mipaka yetu na Malawi! 
Tulikaa kimya! Mipaka haina tatizo isipokuwa ni time bomb ambapo ikitokea rais mwendawazi akamwaga petroli tu, basi ni vurugu kubwa! 
Tuliirithi kupitia Article III ya Azimio la Umoja wa Afrika la mwaka 1964(OAU Charter, 1964), baadaya ya majadiliano makubwa na wengi wakaridhia “uti possidetis, ita possidetis principle” (so as you exist, so may you exist).
Kama kawaida yetu tulinakili kanuni za mipaka za kibeberu za Westphalia(Westphalia border inviolability)! Hatukupata muda mwingi wa kutafakari na kuangalia kila mpaka na matatizo yake....tulirithi na matatizo na yanatutatiza leo!!!
UTATUZI WA MGOGORO: Tusonge mbele! Nakiri tuna namna tatu ya kulimaliza;- moja ni kwa majadiliano ya kawaida(Diplomacy) kama Waziri Membe alivyosema katika hotuba yake. 
Pili ni kupigana vita (war is another means of diplomacy). Ndugu zangu watanzania nadhani mnataka kuniona kichaa kutamka hilo! Huo ndo ukweli, atakayeshindwa atasalimu kama ilivyokuwa kwa Uganda na sisi watanzania. 
                        
                     WAZIRI WA MAMBO YA NJE, BERNARD MEMBE.
Tatu; ni Mahakama ya Kimataifa(International Court of Justice) hapa nina wasiwasi. Kama nyaraka zenyewe ni zile za Waziri Membe tu, sijui kama tutafanikiwa kushinda kesi.
Tutulie, tuite wataalamu wetu wajikite ndani sana. Ni kweli kama alivyosema Waziri Membe kwenye hotuba yake kwa kunukuu kesi nyingi na zilizoshinda, na kwa kusema kuwa, tukienda mahakama ile sisi ndo tutashinda. 
Nina shaka, tumejipa favour  ya verdict, kabla ya kesi. Sijui, ila nina shaka kubwa, kuna kushinda, kushindwa au suluhu! Ninashaka tena na tena!
Mimi ni mzalendo, nataka ukweli kwa njia ya mahojiano na kuumiza kichwa, tutetee mali zetu tukijua tunawashinda kwa hoja.
WASIWASI: Inasemekana kuna mafuta ziwani,  kwahiyo tujue Marekani na washirika wake hawako mbali! Kampuni ya Surestream ya Uingereza ndio ilipewa leseni ya kutafiti mafuta na utawalawa Bingu wa Mutharika.
Lakini, tujue operesheni ya majeshi ya kibeberu na huyu mama Joyce Banda, ambaye ni mpwa wa Kamuzu Banda, anapata wapi hiki kiburi? Nyuma yake kuna nini na nani? Tuangalie haya pia. 
HITIMISHO: Tusiwe na hoja moja tu mkononi kama ndio water-tight evidence yetu kwa serikali na wananchi kwa ujumla. Tujaribu kuzibishanisha hoja zetu. Na hoja nzuri ni zile zinazopingana nasi na tusizozipenda, tukizielewa na kuzikubali ndipo tutajipanga namna ya kuzigalagaza. Tumwelewe vizuri adui yetu. Mungu ibaraki Tanzania, ziwa Nyasa, wanyasa, na watanzania! Tusing'ang'anie tu Reparian Law.
James Zotto ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam(UDSM). 

April 17, 2010

SIRI

HIVI KUNA SIRI YA WATU WAWILI? KWANINI?

March 26, 2010

NAMJADILI KOERO JAPHET MKUNDI...


NILIAMUA KUIPITIA BLOGU YA RAFIKI YANGU KOERO MKUNDI KWA UMAKINI KABISA. NIMEFANYA HIVYO MAKUSUDI NA NATAKA YEYE MWENYEWE AYASOME MAONI HAYA YALIYOPO KATIKA BLOGU YAKE AKIJADILI SUALA LA UKANDAMIZWAJI WA WANAWAKE.

ZIPO SABABBU ZILIZONIFANYA NIKAMUA KUFANYA HIVI, NA NAAMINI ENDAPO ATASOMA KWA UMAKINI HALAFU AKARUDI KATIKA HOJA ZA MAKALA ZAKE, KUNA JAMBO ANAWEZA KULIONA KWA JICHO LA TATU.

SIWEZI KUSEMA NI NINI, LAKINI INAHITAJI AKILI NDOGO TU KUBAINI. SASA NIMEAMUA KUYAVULIA NGUO MAJI NA KUYAOGA,

 ANGALIA KWA UMAKINI MAONI HAYA AMBAYO NIMETAOA KATIKA BLOGU YAKE WALA SIJAONGEZA AU KUPUNGUZA, NINA HAKIKA UTAFAHAMU KWANINI NASEMA ......NAMJADILI KOERO JAPHET MKUNDI......

PENGINE BAADA YA MAONI YA WASOAMJI NAMI NITAWEKA HOJA YANGU KATIKA UKURASA.........someni wenyewe, na yeye mwenyewe apitie maana katoweka kijiweni kwangu na sababu anazijua mwenyewe...........

wavuti-nukta77 said...


Dada Mdogo Koero,
- uhuru wa kuandika haujaondoshwa.

- hujakiuka sheria wala kanuni.

- hujamzuia yeyote kusema ama kuandika kwa uhuru wake na kwa mujibu wa sheria.

- ukiandika kuhusu wanawake kwa kuwa ndiyo imekugusa na mwingine akataka kuandika kuhusu wanaume kwa kuwa ndiyo imemgusa, ni uchaguzi na uamuzi huru.
Sasa basi,

Makala uliyoandika kipindi kilichopita niliisoma na niliuelewa mtizamo wako na nilisoma baadhi ya maoni ya wachangiaji kwa wakati ule, nao walichukulia kwa mtizamo wako japo ni kweli kuwa wapo waliotoka katika mada kuu na kushambulia mwandishi, nani asiyejua kuwa binadamu ndivyo tulivyo? hasa pale unapokuwa unataka kutoa dukuduku kwa kisa kingine na kufananisha kisa cha sasa na kile kilichopita, ni rahisi sana kubwatuka yote yaliyoujaza moyo wako. Ila hiyo uichukulie kama changamoto kwani hakuna vita rahisi, hasa vita ya kudai haki yako. Unapozungumzia kuhusu wanawake si lazima matatizo yao yawe yamesababishwa na wanaume ingawaje ni vigumu kwa wengine kuliona hilo, vile vile unapozungumzia matatizo ya wanawake hutaacha kugusa wanaume kwa upande mwingine kutokana na jamii ilivyowalea na kuwakuza. Ndiyo maana jamii na jamii hutofautiana, hasa zile jamii ambazo kufanya kazi na kulea familia ni jukumu la wote kwa kuwa si rahisi kumpata 'yaya' wa kuwatunza watoto.

Usichoke kuandika, na mara zote uwe tayari kupokea mitizamo tafauti, inayolenga mada, na inayokulenga wewe binafsi kisha kama ulivyosema, 'ujumbe umefika' nami naongezea, 'that which will not kill you, will make you strong'.

Iko kazi pevu katika kuwaelimisha wanawake juu ya 'misingi na haki ya binadamu' humo ndani kumejaa kila aina ya mazagazaga ya imani, mila, desturi, taratibu, nk nk, tukivuka kigingi hicho tutakuwa tumepiga hatua moja nzuri sana.

PS: Si wewe peke yako unayedhaniwa kuwa kwa kuzungumzia habari za 'wanawake' basi ni 'feminist' ni wengi, mimi pia ni mmojawapo wa kuambiwa hivyo, inagwaje sijawahi kuisoma wala kutaka kuifahamu dhamira ya feminism. Ikiwa kinachoniudhi kimefanyika dhidi ya mwanamke, mwanaume, mnyama nk na inaonekana ni feminism, basi na iwe hivyo, ila kuandika ikiwa kipo cha kuandika ama kusema ikiwa kipo cha kusemea tutaendelea (hata tusipoandika ama kusema sisi, wapo watakaofanya hivyo).

Over and Out!

March 24, 2010 8:24 AM

Fadhy Mtanga said...

Da Koero, mimi sioni tatizo lako. Labda kama mtu ataniambia ukweli ni tatizo. Kama ukweli ni tatizo, basi wewe na da Subi mna matatizo na mnapaswa kuogopwa kama nini sijui!

Tutaishi hivi hadi lini? Kama tunayakubali mabadiliko mengine katika maisha, kama maendeleo ya teknolojia na sayansi, kwa nini hatuyakubali mabadiliko kijamii? Wanawake wataendelea kuwekwa second class hadi lini? Lazima usemwe ukweli. Na ukweli mzuri ni ule unaosemwa na mwathirika wa moja kwa moja wa kadhia fulani. Mambo ya wanawake lazima yasemwe na wanawake wenyewe. Kwani wao ndio waathirika wa moja kwa moja na manyanyaso na kutengwa.

Pana tatizo la wanaoitafsiri dhana ya feminism. Feminism maana yake ni tapo la kupigania ukombozi, haki na usawa wa wanawake. Kiufupi tunasema ni nadharia ya usawa wa wanawake. Ni mtu wa ajabu atakayeona hilo ni tatizo. Kama kuna hitilafu ya mbinu labda zinazotumika katika feminism, hilo ndilo linapaswa kusemwa.

Kuna watu na akili zetu timamu, tunapokusudia kumnyanyasa mwanamke, tunafungua hata Biblia, tunasimamia Mwanzo 3:16 "Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala."

Nimesoma kifungu hicho kwa sababu nikiwa mdogo nilipata kusikia mahubiri mahali kuhusiana na kifungu hicho.

Nimesema mengi. Nifupishe kwa kusema, ni wajibu wenu na haki yenu wanawake kupigania haki zenu.

Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

March 24, 2010 8:49 AM

Yasinta Ngonyani said...

Koero kwanza ahsante sana kwa mada hii nzuri na ambayo imerudiwa mara kwa mara na ambayo mada inarukia upande mwingine.

Saw:- Nimekuwa mara nyingi nikijiuliza hivi kwa nini mwanaume unajifanya kuweza kila kitu lakini lijapo suala la jamii linamshinda tuanze na shughuli za nytumbani utakuta mume anamwambia mke nimekuoa na kukulipia mahari kwa hiyo utazaa watoto, utawalea, utapika, utaleta maji, kuni na shughuli zote za nyumbani. Yaani anamfanya ni mtumwa kabisha Je huu kweli ni upendo wa mke na mume? Na hii inaendelea kizazi hadi kizazi Hivi hayupo au haiwezekana kuwe na MWENYEKITI WA DUNIA WA WANAWAKE. Maana hili swali sio nyumbani Afrika tu wanawake kupata mateso.

Hakika nawaambieni tukijaribu kuwaacha wanaume nyumbani yaani kubadili kazi itakuwa kasheshe. Kwa sababu mwanaume bila mwanamke bado hajakamilika lakini hata hivi anamfanya mwanamke ni mtumwa.Kweli hii ni haki je ule usawa upo wapi?

Tukija kwenye swala la elimu nimeshuhudia mwenyewe na pia kusoma katika vitabu mbalimbali kuwa kuna jamii nyingi wanaamini kuwa hakuna faida kumshomesha mmtoto wa kike, ni kupoteza pesa bure tu. Ndio lakini wanasahau kuwa ni watoto wakiume ndio wawapao mimba watoto wa kike na mwisho kuacha masomo. Kama alivyosema D Subi hii yote inatokana na bado tupo kwenye zile imani za zamani, pia mila na desturi.Kwa hiyo hii ndio inatufanya tuamini kuwa wanawake hawawezi kitu hakuna haja ya kumsomesha kwani akishaolewa basi anakuwa ukoo mwingine. Basi kama wendawazimu na tutakuwa tu kwani ni lazima hili swala la haki za wanawake lipiganiwe na muda wenyewe ndio sasa.Upendo Daima!!

March 24, 2010 2:38 PM

Anonymous said...

Ningependa sana kusikia wanawake mnaongelea nini cha kufanya sasa kuweza kujenga uhusiano na hisia mpya ambayo itampa mwanamke haki sawa na mwanaume bila kuathiri jinsia ya mtu.

Pia, kama wanawake wataacha kupoteza muda mwingi kuzungumzia historia, badala ya kupanga mikakati ya kuondokana na tatizo hili, basi itakuwa ni kupoteza muda bure.

Ukitanguliza chuki kwa kutafuta haki, hata yule ambaye anashutumiwa kwa kukalia haki hataweza kukaa na wewe kusikiliza mlolongo wa pointi za maana ulizo nazo.

Koero, mada zako unazileta vizuri sana, lakini unaingia kwa gia ya hasira na chuki kwa wanaume kiasi kwamba unaonekana kama ....... kwa wanaume, matokeo yake unaishia kusemewa hovyo tu.

Mimi nafikiri mabadiliko yamesha anza kujitokeza, usitegemee kwa usiku mmoja utageuza dhana hii iliyopo.Mambo ni polepole

Bado mimi binafsi sijakuona kama kweli wewe ni mtetezi au mtu wa kukashifu jinsia fulani ndani ya ukweli unaoutoa.

March 24, 2010 4:29 PM

Mzee wa Changamoto said...

"The Way You See The Problem Is The Problem"

Ameeeen

March 24, 2010 11:38 PM

Masangu Matondo Nzuzullima said...

I second the motion..."The Way you see the problem is the problem"

Safari bado ni ndefu!

March 25, 2010 2:55 AM

Markus Mpangala said...

KOEROOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! andika kwa uhuru, andika kwa



mtazamo wako sidhani kama kuna haja ya kuangalia nani anasema nini. Hujui watu tunatofautiana? nakumbuka ulinishtua shutuma hizo, lakini niliandika inawezekana kila mtu anaona aonavyo, hivyo wewe andika unachoamini.

Ingawaje mimi huwa napingana na mambo kadhaa ikiwemo la kulazimisha vita dhidi ya wanaume au kumtazama mwanaume kama tatizom lakini naheshimu sana mchango wako na wengine, nawasikiliza sana kama nilivyosema kwa

Dk Benadetha Kilian kwamba siyo haki kudai usawa wa uwiano wa maamuzi kati ya wanaume na wanawake kwamba lazima tuunde mfumo wa kulenga jinsia, nsema katiba inasema wazi wote ni sawa na hakuna mwanaume aliyepewa haki zaidi.


si kweli kwamba wanawake wananyima haki, usawa hauombwi jamani, utafuteni, sidhani kama wanaume walipewa haki au usawa, na nani aliwapa?

kwa ypte haya lakini nakubali tunahitajika kuzingatia katibu na siyo kusema tuwape upendeleo wanawake na swali linakuja nai alimpa mwanaume?


KWAHIYO, KWA MAONI YANGU KOERO unastahili kuandika kwa haki na kwa ujnzi wa hoja, mwangalie Rais Arroyo hakufika pale kwa kupendelewa bali ana sifa.

kama wanawake kupata fursa au kukandamizwa mimi nalia na hawa wanaharakati wanaotumila 'mihela' kufanya makongamano huku wahitaji wanaumia.

inakera, lakini nani alipewa dhamana zaidi wakati katiba inatamka wote sawa/

ANDIKA, NDIYO UANDISHI WA RAIA HUU, WATU TUNATUKANWA SANA KATIKA MAKALA ZETU, MIMI NI MPINZANI WA MASUALA KADHAA YA MAREKANI

nimeshaitwa gaidi mara kadhaa na nimeongea sana na wakurugenzi wa ubalozi wa marekani mwaka 2008 nikiandikia Rai, nilisema nitaacha kuipinga endapo itaacha ufidhuli.

ninatukanwa hadi kesho na hata na rafiki zangu, lakini nasema mimi siyo RUNNING DOGS vile vijibwa vinavyobweka lakini having'ati na havina msimamo wa masuala wnayotetea.

kwahivyo SIMAMA andika bila WEWE WANAWAKE

WATASAIDIWAJE?????????????????????????????? ANDIKA ANDIKA ANDIKA tena uwe unaandika ukiwa na HASIRA KALI ndiyo hoja inapanda vema kichwani.

March 25, 2010 8:12 AM

John Mwaipopo said...

Leo sichangii.

March 25, 2010 12:31 PM

Anonymous said...

Mwaipopo una busara. Kama mambo menyewe ndio haya. Haina haja bro! Even me, sitacomment again on this childish blog. Koero is an emotional wreck and I swear she will never have a stable marriage huyu. Frustrated and emotionally unstable women like these are dangerous even if they have kids.

Blogs zingine ni miyeyusho tu. Kwa nini ufungue blogu if you can handle the heat? Unataka kila mtu akubali tu mawazo yako finyu? Jesus was criticized sembuse weye uliyekimbia shule? Please? Kama ligwaride limekuwa too much, funga blogu ukauze....bullshit!

March 26, 2010 3:19 AM

Anonymous said...

Mdau wa March 26,2010 3:19, Taratibu ndugu yangu wewe ni mtu mzima na watu tunakueshimu. Kuna haja gani ya wewe kutumia lugha chavu za mitaaani kwenye blog hii?

"Kaero is an emotional wreck" sasa umeishageuka psychologist, wakati unashindwa kujitibu mwenyewe.

Blog za watanzania zimejaa, haukulazimishwa kuingia humu au kucomment chochote, Please grew up!!!

Bloggers, msiwanyamanzie watu kama hawa pindi wanapoingia kwenye viwanja vyenu, kwani njemba kama hizi lengo lao ni kulimit the freedom of speech.

HAHAHAAAAAAAA! HE CAN'T STAND WOMEN IN PANTS.

March 26, 2010 2:50 PM

Anonymous said...

Mdau wa March 26,2010 3:19, Taratibu ndugu yangu wewe ni mtu mzima na watu tunakueshimu. Kuna haja gani ya wewe kutumia lugha chavu za mitaaani kwenye blog hii?

"Kaero is an emotional wreck" sasa umeishageuka psychologist, wakati unashindwa kujitibu mwenyewe.

**************

YOU DON'T HAVE TO BE A PYSCHOLOGIST TO IDENTIFY SOMEONE WHO IS SICK AND NEEDS EMOTIONAL HELP

*************************

Blog za watanzania zimejaa, haukulazimishwa kuingia humu au kucomment chochote, Please grew up!!!

************************

I AM FREE TO VISIT ANY BLOG AND LEAVE MY COMMENTS. PLEASE GREW UP - NO COMMENT HERE. HUNIJUI!!!

*************************

Bloggers, msiwanyamanzie watu kama hawa pindi wanapoingia kwenye viwanja vyenu, kwani njemba kama hizi lengo lao ni kulimit the freedom of speech.

***********************

IT IS PEOPLE LIKE YOU WHO WANT TO LIMIT THE FREEDOM OF SPEECH. SIMPLE, KAMA HAMTAKI KUWA CRITICIZED, THEN DISABLE YOUR COMMENTS PAGE. YOU ARE STILL KIDS WHO CANNOT BE CHALLENGED. MKIGUSWA KIDOGO TU MNAPIGA MAKELELE. THIS BLOG HAS A LOT OF PROBLEMS AND YOU KNOW IT!!!

**************************

HAHAHAAAAAAAA! HE CAN'T STAND WOMEN IN PANTS.

*************************

NAKANYAGA WANAWAKE KWA UZURI NA I AM NOT SCARED OF NO ONE, EVEN YOUR MOM. UKIMLETA MI NABWENGA TU...

KOERO, CLOSE THE BLOGU IF YOU CAN'T HANDLE THE HEAT..........

chib said...

Mengine yanarekebishika, suala la kuzaa ni la mama pekee, lakini pale wanapolazwa zaidi ya mmoja kitandani, ni uelekeo mbovu wa uongozi. Lakini hata ukienda wodi za watoto hospitali za watu wote, utakuta hadithi ni ile ile, sasa sijui hapo tena kuna akina mama basi ndio inakuwa hivyo.....

Kuna mtu alisema... suala la ukombozi kwa wanawake, litaanzia kwa wanawake wenyewe.....

Mambo ya kusutana kwa tarumbeta yaishe nk

Je wanawake mko tayari? Au kimebaki ni kilio cha walio wanyonge tu!! Na wale wenye uwezo wamekaa kimya tuuuu

March 4, 2010 2:14 AM

Albert Paul said...

Kuna kina mama waendao umbali mrefu kuteka maji lakini kwa kutumia magani, wapo pia wanawake waendao umbali mrefu kuchukua kuni na mkaa kwa magari,kwa kuwa tu anaendesha gari au huduma hizi zipo karibu(lkn swala ni lile lile la utekaji wa maji au uletaji wa mkaa) hapa haionekani kama ni unyanyasaji,na hakuna aulizaye waume zao wako wapi.

Wapo wanawake wafuao lundo la nguo za waume zao. Kwa sababu tu umechukuliwa kama utaratibu,basi hata wanawake wenyewe hawaoni kwamba ni unyanyasaji bali ni wajibu wao. Kijana amekuwa akifua nguo zake hadi alipooa lakini baada ya kuoa,swala la kufua linakuwa si wajibu wake tena,kwani tayari yupo mtu mahsusi.Kuna makabila fulani ambayo mwanamke ili amsalimie mwanaume ni lazima apige magoti,au akimkaribisha mwanaume chakula lazima apige magoti,makabila mengine chakula kikitengwa,wanaume wanakula kwanza,wakishiba,kinachobaki ndio wanawake huanza kula. Ajabu kabisa,wanawake wa jamii hizi wanaridhika kabisa na yote haya. Nataka tu kusisitiza pointi ya Ndugu Chacha Wambura kuwa kuna some social and cultural factors lazima zibadilishwe. Kingine ni kuwa tunajaribu kulinganisha mazingira tuliyokulia sisi na mazingira waliokulia watu wengine na kisha tuna conclude kuwa upande ambao unaishi chini ya standard yangu basi unanyanyasika na bila kujua kuwa pamoja na mgawanyo wa majukumu,wanawake wanalazika kukabiliana na hali halisi ya mazingira yao. Kama nilivyotangulia kusema,wakati mwamke wa kijijini anatembea umbali mrefu kuteka maji na kuchanja kuni,mwanamke wa mjini anaendesha gari umbali mrefu kuchukua maji au mkaa au kuni au kwa sababu huduma ya maji ipo karibu basi haoni tabu wala kuhisi ananyanyaswa bali anaona ni wajibu wake.

Ninachoshauri hapa ni kuwa,mbali na kuelezea madhila yawakutayo wanawake ktk mazingira waliyopo,pia fursa nyingi zitumike kutoa elimu juu ya namna rahisi ya kukabiliana na hali halisi za mazingira yao,kutoa elimu kwa jamii juu ya usawa wa kijinsia,uhamasishaji kwa jamii mbalimbali juu ya kuachana na tamaduni na kanuni ambazo zinamlazimisha mwanamke kukubali na kuona mambo fulani (ambayo kimsingi hayakuwa haki yake) kuwa sehemu ya maisha yake na mwisho kuihamasisha jamii na serikali juu ya uboreshaji wa mazingira waishio ili kurahisisha upatikanaji wa huduma muhimu za jamii na zilizo ktk ubora unaotakiwa.

March 4, 2010 11:50 AM

John Mwaipopo said...

Koero asante kwa hii makala. nadhani mimi ni mmoja wa walengwa wa makala hii.

tofauti na chapisho lililopita, hili linaongelea zaidi sera na sio kuonewa ama mfumo dume kama ambavyo matatizo ya wanawake yamekuwa yakitafutiwa mchawi.
tunaposema matatizo ya wanawake tusisahau kuna matatizo ya wanaume hata kama hawayasemi. post iliyopita ilikuwa inamfanya mwanaume aonekane chanzo cha matatizo ya wanawake, kitu ambacho nilitoa angalizo kuwa umetuonyesha wanawake wakitaabika lakini hukuonyesha wanaume zao wako wapi na wanafanya nini. kujifungua ni wajibu wao na nilisema tutamuuliza mungu kwa nini wajifungue wanawake tu. nikauliza hao waume zao wako wapi ili tubaini unyanyasaji huu. sijapata jibu bado.

matatizo ya wanawake mara nyingi yanahusishwa na wanaume. ni kama vile matatizo ya afrika yanapohusishwa na ukoloni kila uchao pasi na kujiangalia kwanza sisi wenyewe. matatizo aliyokuwa nayo mama yangu katu hayakusababishwa na baba yangu.

kwa mfano unaongelea wakinamama kurundikana mawaodini wakati na baada ya kujifungua. sidhani kama hili linasababishwa na wanaume wao. wanaume wao wanakuwa wamehusika na kuwapa mimba tu. hili ni la kisera na kiuongozi kama alivyosema chib. katika hili wote wanawake na wanaume wanahusika. sio wanaume peke yao. tanzania tuna uchaguzi wa kuiweka serikari madarakani kila baada ya miaka mitano. wanaojitokeza kupiga kura wengi ni wanawake. sasa kwa nini wasichague serikari ambayo itajenga mahospitali ambayo hawatalala wawili-waili. watawachagua walewale ambao hawanunui vitanda na hawajengi hospotali.

suala la maji nalo ni kama hilo hapo juu. ni la uongozi ambao sote, wanawake na wanaume, tunauweka madarakani.

Umeongelea kulea kwa shida kuwa wanawake wanahangaika mfano feri kuchuuza samaki kwa ajili ya malezi ya watoto wao. kwanza sidhani kuwa suala la kuzaa ni bahati mbaya. ni makubaliano ya mwanamke na mwanaume kuzaa isipokuwa kama mama alibakwa. Pili kibaolojia tu mtoto akiwa mdogo atakuwa karibu na mama yake ili ahudumiwe ipasavyo. hii haimaanishi baba zao hawajishughulishi na malezi ya watoto. unapotoa mfano wa wakinamama pekee kurundikana feri kuchuuza samaki, pia usisahau ni akina baba wangapi wanasukuma mikokoteni (ukilinganisha na wanawake),wanapiga debe na kadhalika ili kupata kipato cha kusaidia kulea watoto wao. kati ya wafungwa wa wakina mama na akinababa wapi ni wengi ambao walidiriki kujihusisha na uhalifu ili kusaidia familia zao. jibu unalo.

bado hujabainisha unaongelea jamii ipi. kwenye post iliyopita nilikuuliza vipi jamii za kipemba na baadhi kule tanga na hata dar es salaam ambako mwanamke ni marufuku hata kwenda sokoni kununua dagaa kwa pesa alizotafuta mumewe. kaziye ni kupaka hina mwili mzima. haruhusiwi kujishughulisha kwa lolote.

ili tuimbe wimbo mmoja naomba mnisaidie haya mambo.sidhani kuwa matatizo ya wanawake yanaletwa na wanaume. huwa najiuliza hivi kwa nini wanawake wengi ma-activists huwa ama wameachika kwa wame zao ama ndoa zao ziko alijojo. hili sijapata jibu kokote kule.

March 4, 2010 12:02 PM

Anonymous said...

Naona unataka watu wote wakubaliane na wewe kwa kila unachosema. This is not your first time to complain. Ukipingwa au kuhojiwa kiduch tu "Oh, you people hamnielewi"....

You are missing the big picture. One goal ya kuanzisha blogu ni pamoja na kuwa ready to be criticized, querried etc. Not everytime watu wakikuquestion unaanza kulalamika. Anakuwa questioned professor Mbele sembuse wewe!

Your argument here is flawed because you are trying to look at women problems in ISOLATION. May be you need to look at comparative data across Africa; then you will be able to make informed claims. Women problems are deep rooted and will not be dealt with properly by superficial attraction of sympathy.

Next time you see women going to fetch water, ask yourself and then ask them why?

Bear this in mind!

March 4, 2010 10:51 PM

Msomaji Wako said...

Nimependa sana waliochangia wote hasa waliokusahihisha, hasa Albert na John. Hakika hao ni wachambuzi makini, na nimefurahia ya kwamba hata hawachoki kukukosoa kila mara.

Una nia nzuri ya kuwatetea wanawake wenzako lakini kwa njia mbovu, maana wewe unaenendeshwa na hisia na hasira kali badala ya kutumia busara na hekima. Hujiulizi chanzo na hulka za watu, unaiga malezi ambayo si ya kiafrika na wakati huo unawatetea waafrika. Ni sawa na wale wanaotetea ushoga uwepo Afrika bila kuzingatia maadili ya kiafrika.

Hoja zako ni za chuki kwa wanaume, unawaona kama mashetani, kama ukiondoa dhana hiyo utagundua wewe una hisia tu, na kulazimisha wasomaji wako waamini kwamba wanawake wanafanyiwa ukatili na wanaume na ndio maana umezungumzia kuzaa kwa shida, sasa ulitaka wanaume na wao wazae!!! Huu usawa ukitumiwa vibaya ndio utaona watu wanalazimisha kuoana wakiwa wa jinsia moja. Hoja yako ni kupandikiza chuki na wala sio kutetea wanawake.

Kuna baadhi ya wanawake ni makatili kuliko hata wanaume, zingatia yule mama wa Mbagala aliyekuwa anamtesa mtoto wa kike wa kambo mpaka kumsokomeza vitu kwenye njia ya kizazi, je huyo mama ni mwanaume!Mbona hujamzungumzia!!

Wanaharakati wa kike ambao wanakuja kwa hasira sana kama zako huishia kuachana na wanaume wao. Utawakuta wote wenye midomo fyongo hawana wanaume, maana wako kwenye kilele cha chuki na hawaambiliki.

Nakuhakikishia wanawake wengi wakimwona mwenzao anamwachia mume wake kufagia nyumba, kumtawaza mtoto, kupika, kupepeta mahindi, kudeki, kubeba kuni,nk watashamshangaa mwanamke mwenzao huyo hata kama huyo mwanamke atakuwa anapasua mawe, kupiga debe, kubeba watu kuvuka mto wakati wa mafuriko, kuzibua au kuchimba choo na makaburi nk

Unapaswa kuelewa kuna tofauti ya mwanamke na mwanaume, usilazimishe usawa wakati hata kimaumbile kuna tofauti.

Rudi kwenye biblia usome, maana hata Mungu alisema mwanadamu atazaa kwa uchungu, kama unapingana na Mungu, nakutakia kila la heri, na nitashauri uende pale Muhimbili kitengo cha magonjwa ya akili. Kama una sikio la kufa, basi hapa tunampigia mbuzi zumari.

Mwisho ukiona kila mtu hakuelewi, basi ujiulize kwa nini, maana wewe ndio unaweza kuwa tatizo, nyani haoni..........

March 5, 2010 12:15 AM

Anonymous said...

Naona watu wanazungumza kwa hisia kali sana, karibu wamevuka mipaka karibu ya kumkashifu hata na Koero!

Ni kweli Koero unaandika makala na kuhitimisha bila hisia ya kisayansi. Unatakiwa ufanye utafiti uwaulize hao wakina mama kama kweli wanaona wanafanya kazi wasizostahili. Usikurupuke na kumwaga hasira kwenye blogu yako.

Mie nina mke mfanyakazi na kipato chake ni zaidi ya cha kwangu, na kila mtu nyumbani anafurahia majukumu yake hata kama mimi nimechelewa kurudi nyumbani, natekeleza yale yanayonihusu.

Huo usawa unaoupigania ni wanaume kuchukua majukumu ya kina mama, lakini mbona haupiganii wakina mama kwenda kugonga kokoto, kuchimba madini kama akina wana apolo, kwenda kuvua samaki usiku wa manane na wanaume wawahi feri asubuhi kuja kununua samaki. Mbona pale kunapotokea vita ni wanaume wengi ndio wanaenda huko kuuwawa na wanawake wanabaki kutunza familia. Huoni ni mgawanyo wa kazi, au hujui?!.

Kwa ujumla kazi za wanaume ni hatarishi kuliko za wanawake, lakini wanaume wameumbwa na mioyo migumu na kijasiri, badala ya kulalamika tu.

Mija alisema wanawake mnapenda sana upendeleo, ni kweli kabisa, na hiyo inawadhalilisha, inabidi mjitutumue lakini sio kwa kuchukulia mambo kijuujuu na hasira ya mfumo dume.

Mara ngapi kwenye misururu akiwepo mwanamke pekee wanaume wanampa fursa ahudumiwe kwanza, ni sawa na bomba la maji hapo Kigogo.

Mnasahau ya kwamba wanawake ndio wana maamuzi yote nyumbani ya kitu gani kitapikwa nyumbani, nini anunue nk. Ukiwapa wanaume utalia

Wanaume tupo tayari kwa usawa lakini iwe pote, piganieni na nyie kuwa matopazi, ingieni vitani, bebeni mizigo hapo kariakoo, geuzeni wanaume wazae na kunyonyesha. Ukipata mtoto wa kiume anayetaka kuolewa na kidume mwingine mpe haki yake nk.

Pole Koero, acha jazba, andika kama mwanaharakati na wala sio kama mbeijing!

Wanaume watakuwa tayari kubadilika wakiletewa hoja zenye maana na sio za kufikirika

March 5, 2010 10:42 AM

Upepo Mwanana said...

Hii mada imenichanganya kidogo hasa baada ya kusoma hisia za watu!

Mimi namshukuru Mungu kwa kunipa baba aliyenipa muongozo wa kuishi na watu wote, nawashukuru na kaka zangu kwa kunipa heshima kubwa kama mtoto wa kike. Imenipa fursa ya kufanya kazi na wanaume huku nikiwa naheshimika kama ninavyowaheshimu na wao, na nimekuwa planner wakati wao wamekuwa watekelezaji bila kupunguza heshima.

Kwa mtazamo wangu siulaumu kwa hisia kali mfumo dume, nahisi tatizo lipo kwetu wanawake pale tunaposhindwa kujitambua ya kuwa tunatakiwa kuwa ngangari kwenye kila kitu tukija na nguvu ya hoja na sio hoja ya nguvu.

Matatizo mengi ya akina mama yanahusiana na mfumo mbaya wa kiungozi au kisiasa, kukosekana kwa hospitali za kujifungua sio sababu ya mfumo dume, kwani wanaokufa ni wengi wakiwemo watoto na wanaume pia.

Sababu za akina mama kuzaa majumbani ni tatizo la akina mama wenyewe, kwani kuna ushahidi kuna sehemu wakunga wa jadi huwalazimisha mabinti wawapo hospitali kuondoka wakati wa kujifungua ukikaribia, pia wauguzi wakunga wengine (tena wanawake), wana matusi mabaya sana wakati wa uchungu, pia kukosekana wa zana za kujifungua watu hunyang'anywa walizokuja nazo kuwasaidia wasio nazo, hivyo akina mama wajawazito huchelewa makusudi ili zana zao zisichukuliwe, na pia kuepuka kulala wengi kitanda kimoja. Mfumo dume hauna chochote hapa.

Hulka ya waafrika pia ni chanzo cha baadhi ya MATATIZO YA AKINA MAMA.

Kwa mtazamo wangu nafikiri hatuwezi kuubadili kwa ghafla mfumo huu, tunahitaji kuwaelimisha akina mama wenzetu kwanza na ndipo hapo shughuli ya kuweka huo usawa wa kweli utakuja, lakini siamini ya kuwa total reversal is fair, yaani leo baba aanze kulea mtoto nyumbani, afue nk, je akina mama usawa utakuwa wapi, kwenda kufanya kazi ngumu? La hasha, tunapaswa kuheshimiana na kupendana, we need badly each other. Hakuna mambo ya visasi au kukomoana. Mimi naona wanawake tuache kufikiria kupendelewa au kuonewa huruma kwanza, tuingie kwenye ushindani wa kikweli na wanaume kama tunataka usawa. Angalau huo ndio mtazamo wangu binafsi

Yasinta Ngonyani said...

Kwa kweli inaumiza sana jinsi wanaweke tunavyoteseka. Sijui hii ni laana. Nashindwa hata la kusema maana ni kweli watu tunalia na tunalia lakini......basi ngoja niache kwani chozi lanidondoka hapa sioni kitu..

March 1, 2010 11:18 AM

Mija Shija Sayi said...

Yasinta si laana wala nini, ni kwa sababu wanawake tumezidi kulialia sana na kupenda upendeleo. Kwa ufupi sisi wenyewe tunayataka, hebu angalia uwezo tulio nao wa kuyakabili maisha, kuanzia zoezi zima la mimba hadi kuzaa, kuitunza familia peke yetu huku waume zetu wakiwa vilabuni, kudunduliza vijihela vidogo tulivyo navyo hadi kusomesha wanetu na mengi mengine.

Kama yote haya tunayaweza tujue hata machozi tunaweza tukajifuta wenyewe tusisubiri kufutwa, ni suala la kuamua na KUJIAMINI tu.

Tusikubali na tusikubali kwa vile:-Nia tunayo na Nguvu tunazo za kuweza kumuangamiza huyu adui UWOGA.

Subirini niingie madarakani.

March 1, 2010 3:40 PM
Kissima said...

Dada Koero, yawezekana kabisa wanawake hao walikuwa wanakabiliana na hali halisi ya mazingira yao,ninamaanisha kwamba hali hiyo wasingeweza kuikwepa kulingana na mazingira yao. Je, unafahamu waume zao walikuwa wapi kwa wakati huo? Yawezekana kabisa kuwa kuna mgawanyo wa majukumu kiasi kwamba waume wao nao walikuwa ktk mazingira fulani wakipigika vilevile na pengine kwa kazi wazifanyazo ungeweza tena kuwahurumia mara mia zaidi. Kwa hiyo kabla ya kusema wanawake hao wananyanyasika ni vema pia tukajua upande mwingine nao unafanya nini na kama hakuna mgawanyo sahihi wa majukumu pia ijulikane.

March 1, 2010 4:49 PM

John Mwaipopo said...
au inawezekana koero uliwaona wanawake wajane tu. huko ulikopita hakukuwa na wanaume? na kama wakikuwako wakikuwa wanacheza karata ama wanakunywa pombe? kama walikuwa wakistarehe, basi tuna haja ya kuwalilia wanawake watesekao. nasema watesekao maana wengine wanatesa kutegemea jamaii na jamii. kule tanga na pemba mwanamke haruhusiwi kufanya kazi ama hata kwenda sokoni kufanya manunuzi. kazi yake ni kupaka hina kila mtindo na kujifukiza udi na kula kungumanga. mchangiaji mmoja ameongelea pengine ni mazingira yao ndio yanawalazimu kufanya hivyo. hebu tujuze waume zao walikuwa wapi na wakifanya nini.

hilo la kubeba mimba na kuzaa tutamuuliza mungu siku ikifika.

March 1, 2010 6:11 PM

Mzee wa Changamoto said...

Ouch!!!!

Heaven Help Us All

March 2, 2010 6:04 AM

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Mnalitazama hili suala kwa mtazamo na mantiki gani? Mmejaribu kuongea na akina mama hawa wakawaambia kwamba wana shida? Kuweni makini na jambo hili ili msije mkaingia katika mkumbo ule ule wa 'wataalamu" wa Anthropolojia na Historia kutoka Ulaya waliofikia majumuisho (generalizations0 ya kushangaza walipotia guu lao Afrika kwa mara ya kwanza!
Nendeni mkaongee na wanawake hawa kwanza. Mtakayojifunza huko yatawashangaza na pengine yatabadili maoni yenu kabisa. Nina mifano mingi ya ninachokisema hapa!

March 2, 2010 11:20 PM

Mija Shija Sayi said...

Hii ndiyo raha ya kublogu jamani, tunajifunza mengi. Mwl Masangu umeongea jambo la msingi sana.

March 3, 2010 3:03 PM

Anonymous said...

You ran away from UDSM claiming that the education there is NO good. It is beginning to show now; and you will live to regret that decision of yours regardless of whether you are rich or not.

Probably people don't understand you because your articles are superficial, emotional and half cooked. If you had stayed at Mlimani ant took classes on Philosophy, Psychology and Fundamental Statistics/Logic, it would have helped you a lot - not to become rich but kupanua akili yako and your thinking capacity.

Punguza kupiga makelele. There is a reason people don't understand you. Your mother was right; and she will always be right. You need to go back to school girl!!!

MWISHO WA KUNUKUU. LEO SITASEMA, KWANI HAPO NDIPO PENYE AKILI NA HEKIMA.
NAWASILISHA!

Markus H. Mpangala

March 24, 2010

CHEMSHA BONGO, SHINDANO, ZAWADI NONO

KAMA KWELI UNA 'MIAKILI', nataka uanze kusumbua kichwa kwa neno hili.
Hivi karibuni kumezuka neno fulani hivi lenye kumaanisha jambo fulani. Neno lenyewe linaitwa 'MKUU WA POSTA'.

Limeene neno hili, linazidi kukua, lakini usifikirie lina maanisha kazi ya ofisi za Posta, bali ni jina la mtu mwenye tabia fulani hivi.

Mwenye tabia hiyo ndiyo huitwa 'MKUU WA POSTA' ili kumtaja hadharani kutokana na tabia yake hiyo.

JE UNAWEZA KUNG'AMUA NENO HILI LINA MAANISHA NINI KATIKA TABIA?

October 31, 2008

Je mungu alituumba majuha?

hivi kweli mungu alituumba waafrika kuwa majuha? soma hapa www.raiamwema.co.tz katika safu ya fikra mbadala ya Mwanafalsafa Ayoub Rioba. Namwita Mwanafalsafa kwa vigezo vyangu kwani ni muumini wa fikra zake kama ilivyo kwa Jenerali Ulimwengu na wengine

September 13, 2008

wanyasa hamniamini......simwogopi Yasinta

Hebu nicheki, vazi nilipendalo la Taifa(jezi ya taifa), yaani kila kona mnanicheki mimi sijui nimewavutia kwa hilo pozi kwani hapo ni mapumziko ya mchana wa leo. mazoezi ni katika jua kali pumzi mithiri ya mamba/ling'wina

June 04, 2008

Wanacheza,wanaselebuka na kuvinjari

sina maneno hapo,umenuna?kazi kwako ukiwa unakasirika mara nyingi utazeeka lakini ukicheka sana picha itapotea...polepole basi karibu nyasa hata kimyakimya

Wamo,Siyo Samaki pekee

kama unafikiri wanyasa wanachokiweza ni kuvua samaki na kujua majiraya kutega nyavy zao basi hujakosea ila hujui nini kinachoendelea hapo.Tazama wanaume wakiwa mzigoni wamekaza viuno,meno,miguu mpaka ngozi hakuna masihara hapo utaumia.kwanza inabidi uwe umeshiba sahani kama tano za ugali wa muhogo ikiwa wewe ni mgeni,lakini wenyewe ni nguvu za asili wale hawajui kwendaklabu za mazoezi kama huko mijini kwenu wanaogopa kansa shauri ya kutu za vyuma.

April 20, 2008

Ziwa Limechafuka,Wanyasa na Ngalawa Tu

Nilikaa juu ya jiwe nikiangaza huku na huko kuwatazama wanyasa wanavyohaha katika shughuli zao za maisha ya hapa na pale.Nikaona ngalawa zinaumiza vifua vya wanyasa kwani hali siyo nzuri katika ziwa kwa sasa.Hakika ziwa nyasa limechafuka namaanisha dhoruba kali sana wiki hili,kila myasa/mvuvi unayemuona kanuna,kafura kama chatu ghadhabu imejaza vibaba wala haimithiriki zaidi ya hapo,hawacheki.Ziwa linanguruma mawimbi makali makali,nyavu zinapotea nyakati hizi shauri maboya yanazama kwa kushindwa kuhimili nguvu ya mawimbi.Lakini pamoja na kuchafuka kwa ziwa hilo hakuna hata mvuvi anayethubutu kusema atabaki nyumbani kujipumzisha au kurejesha zana za uvuvi nyumbani ili kupisha dhoruba hiyo,wapi bwana sahau kabisa habari ya wanyasa kuogopa dhoruba nyakati hizi au kuacha ngalawa ili kukosa kitoweo,hakuna mnyasa anayefikiri kula nyama za kuku wasiokomaa,wanaotafunika hata mifupi,wanaokuzwa kwa kudungwa sindano,wanatia kinyaa kuwala,au chipsi za huko mijini.Wanyasa wanaelewa uzuri wa kuwa wajuzi wa ziwa hili ambalo wenyewe wanasadiki kuwa hakuna ziwa lenye dhoruba kali ulimwenguni zaidi ya hili.Hakuna aliyeka chini kuacha ngalawa au kuacha kupanda mitumbwi.Yaani uvuvi unaendelea kana kwamba ziwa lipo shwari wakati "limekasirika" utafikiri limedungwa sindano ya kukasirika.Yote hao ni kitoweo cha asili hiki utamu adimu huu.

March 29, 2008

Wanyasa wangali wakiselebuka na Nyakati maalumu

Amini usiamini,utake usitake wanyasa ni wanadamu wanaofahamu namna ya kuzitumia hizi nyakati maalumu.Hawasiti kuselebuka kwa raha zao huku wakipiga ngoma za Lindeko,Madogoli n.k lakini kuna jambo nilisahau wakati naandika hapa kuhusu shamrashamra hizo,kuna aina fulani ya ngoma nilizisahau lakini kwa bahati mbaya,lakini nimekumbushwa na dadangu wa blogu ya Ruhuwiko{ngoja nitaandika ili uisome blogu yake},kanikumbusha Lizombe,Muhambo wa wamatengo,nami dakika hii nakumbuka Chomanga,mganda,makanya,sindo n.k
Kwa sasa huku Nyasa ni kama nyakati maalumu zipo kila siku kwani watu tunaselebuka kwa raha na kusahau uchungu fulani wa maisha{bila shaka unajua namaanisha nini}.Huku watu wajipa likizo isiyo na malipo,wanakunywa pombe zao za asili komoni,lihutapahi,mbege,chimpumu ya wamatengo na hizi zinazozalishwa huko mjini kifupi hazina soko hapa nyasa hazitakiwi.Basi jumapili ya pasaka yenyewe watu wamependeza,wafurahia siku hiyo,wanatabasamu hapa na pale wanakumbushana pasaka ya miaka iliyopita n.kWatu wanakumbuka mambo mengi ya kitamaduni ambayo yanawafanya waone fahali kuzaliwa na kuishi nyasa.Yaani mambo bado yanaendelea hapa watu hatujapumzika na wala nilipoibukia pale Mbinga sikapenda kukaa sana nikarudi nyasa ili nijionee furaha hizi.Siyo siri dadangu pale Sweden amekumbuka mengi anakosa nyakati hizi kwa wanyasa.Hii ndiyo nyasa watu wanajimwaga mitaani.Lakini kikubwa unywaji wa pombe hizi mjini hutumia mishkaki lakini hapa watu kama kawaida yao samaki maarufu kwa jina la "Kapili" yaani ni kama 'kachumbari' ya pombe kwa walevi na wanywaji .Samaki hawa wanakuwa wamekwisha kuchomwa na kukaushwa vyema basi inakuwa utamu juu ya utamu na pilipili pembeni yake.Wasiolewa kazi yao kukumbushana na kujadili maisha n.k kina dada wanajumuika kupiga gumzo na kina kaka maana ni nyakati maalumu hizi huja mara chache.Watu wanafurahia maisha acha wajifurahie

February 23, 2008

Haa!!Kumbe Watawala wetu "VAYIVA?"

Jamani tusishangaane hapa,mbona hii hatari kwa wanyasa sisi?Yaani hawa viuongozi wetu "VAYIVA"? haya maajabu wala hawaoni noma!.Neno "VAYIVA" lina maana "WANAIBA",nimelitumia hili kustaajabishwa na hali ya majambazi wa wa nchi yetu ambao tumewapa mamlaka ya kutuongoza.Wezi wakubwa hawa na kikundi chao na wizi yaani "VAYIVA" hawana hata aibu halafu wanalilia kusikilizwa mbona makubwa.Huku nyasa wala hatuna habari lakini eti nimefika hapa Mbinga ndiyo napewa kale haotuba ka mnyakyusa aliyesoma kale karipoti kanakowataja wale wezi wetu.Yaani "VAYIVA"?..

December 26, 2007

NYASA;krisimasi,furaha,burudani na uhai wa wanyasa

Naam nilikuwa katika kijiji lundu kujionea burudani na furaha ya kusherehekea krisimasi ambayo bila shaka ni ni wakati wa wazazi,watoto,ndugu,jamaa na marafiki kujumuika katika simu hii ambayo hupatika mara moja kwa mwaka pale wakristo wanapokumbuka siku ya kuzaliwa Yesu krsito.Ni kawaida yangu kutulia katika siku za aina hii lakini nilishindwa kutulia ilibidi nijiulize nitaandika nini nikifika Mbinga asubuhi hii maana wenzenu mambo ya mtandao haya mapaka tusafiri kidogo ndipo tuandika katika blogu namna hii.Naam nimekuwa katika mzunguko mkali wa siku hiyo ya krisimasi ili kujionea burudani,furaha na uhai wa wanyasa katika maisha yao lakini nikaona sisi bina damu tuna kawaida ya kusahau matatizo siku kama hizi maana nikaona hata wale maadui wanakumbatiana kwa wema kuikumbuka siku ya mwokozi wao.Asubuhi hii ikawa balaa maana kuna jamaa alikwenda kuvua samaki hivyo nimemwahidi kwenda kupata japo kitoweo kumbe mwenzie naondoka zangu kusafisha macho mjini Mbinga angalu nione wamjini wanaburudika vipi hata siku kama ya leo.Nimekuta watu wamelewa,wanatapika hovyo,mara mafumanizi na uchafu kibao na nikaambiwa na mwenyeji wangu kuwa kuna mwanamke mmoja kafumaniwa na kijana wa kinyasa mtaa wa Flastoo.Hapo nikaguna huyu mnyasa yuko hai kweli? nikambiwa wanyasa wana mbio katika hatari maana jamaa kachia mbio kuokoa uhai wake....si unajua fumanizi za wenyemali.Sasa badala ya furaha,burudani na uhai wa wanyasa jamaa kasafiri hadi hapa mjini halafu anajiona wa leoleo na vihela mbuzi vyake akakoswakoswa na wenye uchu wa kutanya uhai wa wenzie na bahati yake kwa wanyasa kuwa mbio kali ni sifa moja ya uhai wako nyakati za hatari.Ndiyo wanyasa wa mbio za ajabu mithiri ya swali mbugani.Lakini baada ya kuandika hapa mjini katika blogu hii natarajia niende zangu kijiji maana jamaa akija nadhani ataghadhibika kwani nimeahidi kununua samaki wake ili apate pesa za kuburudika na furaha ya familia maana jana kalewa mipombe halafu kasahau familia lakini kaahidi leo ni burudani ya familia yote sasa watoto wako juu kwelikweli maana wanataka kuonyesha uwezo wao wa kuburudika. mapumziko mema,watu wote wa ughaibuni maana najiuliza hivi Ndesanjo anasoma habari za wanyasa kweli?vipi kaka Jeff,DaMija,Michuzi na kitoto pale London?sijui lakini polepole,KARIBUNI NYASA!

October 21, 2007

Nyasa,habari,mseto na karibu njema

Naam leo nizungumzie jambo lamseto tu au kama habaro fulani tu ili tuendele na mambo ya ukanda huu.Ni maeneo ya ajabu sana kwani kuna baadhio ya maeneo yana kumbukumbu za vita baina ya wanyasa,wamatengo dhidi ya wangoni wavamizi hawa waliotoka nchi za kusini mwa afrika.kuna mapango yenye kusimuliwa na wazee wetu namna vita hivyo ilivyokuwa huku wanyasa wakipoana tokana na uwezo wao wa kuogelea hivyo walipozidiwa walikimbilia ndani ya maji.Tukumbuke wakati huo sialaha kubwa ilikuwa mishale,majambia,mapanga n.k lakini maadui waliweza kuopeshwa na silaha hizo.Maeneo haya yana mambo ambayo wakati mwingine hayajionyeshi kwa uwazi bali mpaka unapofanya uchunguzi na kuwahoji waliokula chumvi nyingi ndipo unaweza kupata habari motomoto za nyasa.Mfanao wenye asili ya wanyasa ni kundi kubwa ambalo limesambaa Malawi kwa kiasi kikubwa na lugha zao hushabiahiana hata asili ya majina yao.Nilibahatika kukutana na "mkoloni" mmoja hivi{mzungu} yeye ameweka maisha yake katika mji wa Mbamba Bay ambao ni kama kitovu kikuu ca maeneo haya achilia mbali Liuli na Lituhi au Lundu.Yeye anauwezo wa kuongea kiswahili fasaha kuzidi mzaliwa wa nchi yetu.anavutiwa na historia inayofungamana ya wanyasa,wangoni,wamatengo na wenyeji wengi wa malawi.Nyasa ina mambo mengi ya kumbukumbu ya taifa ambayo hayaandikwa.Mfano uwepo wa kituo cha Jando na unyago katika kijiji cha KILOSA ambapo majengo au eneo lake limehifadhiwa kwa ajili ya kumbukumbu za vizazi vijavyo.Tutaendelea polepole na mengine mengi,huu ni mwanzo tu na mengi ya mkoa wa Ruvuma hususani wilaya ya Mbinga tutajadili na kuyaweka pazuri.KARIBUNI NYASA.