NA. HONORIUS
MPANGALA
WAKATI aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa taifa
hili la Tanzania alikuwa kiongozi aliyewaunganisha watanganyika, sasa mambo
yamekuwa tofauti kiasi. Katika hili wako ambao wanashindwa kukemea kutokana na
mitazamo ya namna gani wataweza kuonekana mbele ya wenzao kiitikadi.
Hatuko kama majirani zetu kwasababuya
misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ni mizuri na inayowafanya
wananchi wake kuwa na hofu ya mungu.
Ni jambo la kawaida sana kumkuta mtanzania wa
kabila la kisukuma akiwa na mifugo yake katika bondel la mto Lwika huko wilayani
Nyasa akiipa malisho mifugo hiyo. Ni kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na
waasisi wa taifa letu kwa kuondoa suala la ukabila miongoni mwa watanzania.
Tangu taifa hili liasisiwe hakuja wahi tokea
ugomvi wowote uliohusisha makabila moja na jingine. Hii ni kutokana na
kujaliana kwetu na kufuata ile misingi ya ugugu baina yetu kama taifa moja. Katika upande wa masuala ya kiimani iliwahi
kutokea mara moja katika utawala wa awamu ya tano,mgomo wa wakristo na
waisalamu ambao ulihusisha suala la kuchinja.











