Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

March 12, 2018

SASA MWATUGAWA KWA ITIKADI ZA KISIASA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
WAKATI aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa taifa hili la Tanzania alikuwa kiongozi aliyewaunganisha watanganyika, sasa mambo yamekuwa tofauti kiasi. Katika hili wako ambao wanashindwa kukemea kutokana na mitazamo ya namna gani wataweza kuonekana mbele ya wenzao kiitikadi.

Hatuko kama majirani zetu kwasababuya  misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ni mizuri na inayowafanya wananchi wake kuwa na hofu ya mungu.
Ni jambo la kawaida sana kumkuta mtanzania wa kabila la kisukuma akiwa na mifugo yake katika bondel la mto Lwika huko wilayani Nyasa akiipa malisho mifugo hiyo. Ni kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa letu kwa kuondoa suala la ukabila miongoni mwa watanzania.
 Tangu taifa hili liasisiwe hakuja wahi tokea ugomvi wowote uliohusisha makabila moja na jingine. Hii ni kutokana na kujaliana kwetu na kufuata ile misingi ya ugugu baina yetu kama taifa moja. Katika upande wa masuala ya kiimani iliwahi kutokea mara moja katika utawala wa awamu ya tano,mgomo wa wakristo na waisalamu ambao ulihusisha suala la kuchinja.

February 15, 2018

KATUNI INASEMA

January 05, 2018

AMBULANCE YA HOSPITAL YA WILAYA NYASA ILIVYONUSURIKA KUANGUKA.

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
AWALI niombe radhi kwa kukosa picha kwasababu nilipofika eneo la tukio simu yangu ilizima moto. Nakumbuka nilitumia simu yangu ndogo kumweleza kakangu Markus Mpangala kuwa narejea nyumbani lakini tumesimama mahali kuna gari inasaidiwa kunasuliwa toka ilikoegema. Ni mlima wa kwanza ukitoka kijiji cha Kihagara eneo la Camp, tulikuta hiyo Ambulance ikiwa imeshindwa kupanda mlima kwa uterezi na kuburuzika hadi pembezoni mwa barabara. Jambo la kuahukuru ni kwamba ilikuja kugota kwenye jiwe vinginevyo ingelala kwa ubavu katika kuta za barabara.
Barabara ya Lituhi kwenda Mbamba Bay  eneo la mtaa wa Likwambe katika Kijiji cha Lundu wilayani Nyasa.

December 07, 2017

KILICHOTOKEA KATIKA UCHAGUZI WA KATA 43 HAKINA TASWIRA NZURI 2020

NA HONORIUS MPANGALA 

TANZANIA ni nchi ambayo wananchi wake wamejengwa kwenye ushrikiano na mshikamano mkubwa sana katika aisha yao ya kila siku. Yawezekana misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ilikuwa haswa ambayo inatufanya hata wale wenye mitazamo tofauti kwenda sawa na wengine. 

Tumekuwa tukipata viongozi wetu kwa njia za uchaguzi kwa kuwapa nafasi wananchi kuchagua kiongozi wanayemtaka. Uhuru wa kuchagua ni moja ya vipengele vilivyoko katika Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inayotumika hadi sasa. Katiba imeeleza kila mtu anauhuru wa kuchagua na kuchaguliwa.

Wananchi wa Kijiji cha Katumba Kata ya Ibighi
Katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika katika kata 43 hapa nchini umenifanya nitafakari hatma ya Tanzania kwa yale ambayo nimepata kuyaona na kusikia toka maeneo tofauti. Hakika kuna mahali tumeteleza na tunapaswa kujisahihisha. Kuteleza ninakosema ni kwa yale matendo ambayo yamekuwa yakiibuka wakati wa uchaguzi mdogo katika maeneo tofauti.

November 15, 2017

HALI YA ZIMBABWE MCHANA HUU



1.Waziri wa Fedha wa Zimbabwe Ignatius Chombo amekamatwa na Jeshi la Zimbabwe. Pia wanajeshi wameua walinzi watatu wa waziri huyo. (Chanzo: PaZimbabwe).
2. Jeshi hilo pia lilitembelea nyumbani kwa Profesa Jonathan Moyo ambaye ni waziri wa elimu ya juu, amekamatwa (Chanzo: NewsDay)
3.Baadhi ya mawaziri wameripotiwa kutoroka, wakiwemo Saviour Kasukuwere  na Makamu wa rais Phelekezela Mphoko anayedaiwa kukimbilia Afrika kusini.

November 08, 2017

SASA NAMWELEWA HILARY CLINTON

NA  MARKUS MPANGALA
 
WAKATI wa kampeni za Uchaguzi nchini Marekani mwaka 2016, aliyekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha Democrat, Hilary Clinton alisema: “Kama mgombea (wanasiasa) anakasirishwa na sentensi moja iliyoandikwa kwenye mtandao wa kijamii basi huyo hafai kupewa mkoba wa nyuklia, maana vidole vyake vitabonyeza wakati wowote,”. 
 
Tafsiri ya Kiswahili ni yangu kwa sababu ninahitaji kurahisisha kueleweka hoja yenyewe. Maneno ya Hilary Clinton yalimlenga mgombea wa chama cha Republican, Donald Trump ambaye alishinda uchaguzi huo baadaye.

Clinton aliamini kuwa kitendo cha Trump kukasirishwa na sentensi zinazoandikwa kwenye mitandao ya kijamii ikiwamo yeye mwenyewe kujibu mapigo au kuwatisha watu, ilikuwa ni ishara ya mtu ambaye hawezi kustahimili ukosoaji au kukosolewa pale anapokuwa kiongozi.

Kwamba ili uwe kiongozi unatakiwa kustahimili au kama wasemavyo wahenga lazima uwe na ngozi ngumu hata kama utapigwa mishale ya kila namna. Hii ndiyo changamoto inayotukabili vijana, viongozi wa kila ngazi na watendaji mbalimbali kwenye vyombo vya uamuzi kwa maslahi ya Watanzania. 

Mara nyingi tumesikia wanasiasa au wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi wakijiapiza kufanya jambo hili au lile. Wengine wanatajwa kuudhika kutokana na maneno kadhaa yanayozungumzwa kwenye mitandao ya kijamii.

Tunafahamu kuwa ipo sheria ya mtandao na maudhui, ambapo inalenga kudhibiti nidhamu pamoja na kukabiliana na “hatari” yoyote inayoitwa kama udhalilishaji (Cyber Bullying), matusi na hulka mbaya dhidi ya viongozi au watu wa kada mbalimbali. 

Lakini katika kipindi hiki kuna jambo limenishangaza. Nashangaa kuona wanasiasa wetu nchini wanakasirishwa na ‘status’ zinazondikwa huko Facebook, Twitter, Instagram na kwingineko. 

November 02, 2017

UCHAGUZI KATA 43 KUFANYIKA NOVEMBA 26 MWAKA HUU


Kwa mujibu wa Tume ya uchaguzi. Uchaguzi wa udiwani Novemba 26.
1.      CCM-wagombea 43 katika kaata 43
2.    Chadema-wagombea 42 katika kata 43
3.    ACT-Wazalendo-wagombea 18 katika kata 43
4.    ADA-Tadea-mgombea mmoja katika kata 43
5.     ADC-wagombea wanne katika kaata 43
6.    NCCR-Mageuzi-wagombea 6 katika kata 43
7.     NRA-wagombea wawili katika kata 43
8.    SAU-wagombea wawili katika kata43
9.    TLP-mgombea mmoja katika kata 43
10.                        UDP-wagombea wawili katika kata 43
11.  CHAUMA-mgombea mmoja katika kata 43
12.CUF-wagombea 30 katika kata 43
13.DP-wagombea watatu katika kata 43

October 30, 2017

TAARIFA YA KUNG’ATUKA LAZARO NYALANDU, MBUNGE WA SINGIDA KASKAZINI



NIMEAMUA kujiuzulu NAFASI yangu ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, pamoja na nafasi zote za Uongozi ndani ya Chama kuanzia leo, Oktoba 30, 2017.

October 09, 2017

PROFESA KITILA MKUMBO ANG'ATUKA UANACHAMA ACT-WAZALENDO

NA MWANDISHI WETU
Katibu mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof. Kitila Mkumbo, amejiuzulu uanachama wa ACT-Wazalendo.
Kwa taarifa zaidi soma barua yake(pichani).


September 21, 2017

UCHAGUZI WA KENYA SASA KUFANYIKA OKTOBA 26



NAIROBI, KENYA
 Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya imetangaza tarehe 26 Oktoba kuwa siku ya uchaguzi mpya wa urais nchini humo. Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika  Oktoba 17 mwaka huu ikiwa ni siku chache baada ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya urais kutokana na kukubaliana na pingamizi la Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya, NASA. 

September 16, 2017

UBUNGE SASA MIAKA 7?


Mbunge wa Jimbo la Chemba, Juma Nkamia anatarajiwa kuwasilisha hoja binafsi Bunge ya kubadili kanuni na sheria zilizoweka ukomo wa nafasi ya ubunge kwa miaka mitano, ambapo sasa anapendekeza kufanyike mabadiliko ya kisheria ya ukomo wa ubunge uwe miaka 7 (Kama inavyoonekana pichani).
 
Je atafanikiwa?

October 12, 2014

KWANINI AFRIKA HATUNA AFRICOPHONE AU BANTUPHONE?



Na Markus Mpangala, Dar es salaam

KUNA wakati unaweza kujiuliza utamaduni wa viongozi wetu kuzithamini jumuiya za nje ya Afrika unetokana na nini. Tunaweza kujitetea kwa namna nyingi ikiwemo uchumi duni unaosababisha tukose nguvu ya kitaifa.

Unaweza pia kuorodhesha sababu nyingi mno ambazo zinaweza kutunyima uwezo wa kuwa na jumuiya zinazotambulisha uwezo wa kiafrika kwenye siasa, uchumi, utamaduni na jamii.


Yapo maeneo tumeweza kuyalinda na kuonesha sisi ni waafrika halisi na tunalinda uafrika wetu. Bahati mbaya pia yapo maeneo yanayojenga nguvu na ubora wa Afrika hayajapewa kipaumbele.



Moja ya kazi za Cheik Anta Diop,

Mwanazuoni Cheikh Anta Diop alihubiri sayansi, siasa na utamaduni wa Afrika. Diop alihubiri uafrika kama Marcus Garvey, Malcolm X, na wengineo. Diop alihubiri ubora na nyakati zilizovurugwa katika historia ya mwafrika.

Kwamba Afrika kuna utamaduni, lugha, mazingira, staha na mambo yanayoweza kulibatumbulisha bara hilo kwa Uafrika wao.


Katika bara la Afrika ambalo linatajwa kugunduliwa kwa binadamu wa kwanza kuishi, lina sifa nyingine mbaya zaidi kwamba baadhi ya wakazi wake hawazipendi nchi zao.
Kwamba hawapendi utambulisho wao.

Hawapendi utamaduni wao na ndio maana hujishughulisha kubadilisha wajihi (kujichubua) na mengine yasiyowatambulisha kama waafrika.

Madai haya yamekuwa yakitolewa na wataalamu pamoja na wanahistoria wengi wa Ulaya pamoja na Amerika.
Sababu kubwa inajulikana kuwa waafrika wamejikuta kwenye utegemezi mkubwa wa kiuchumi, kisiasa na kijamii.


Jambo zuri zipo jamii ambazo zinalinda tamaduni zao na zinajali zaidi. Hata hivyo katika Bara la Afrika kuna vituko vingi na kuonesha dhahiiri kutegemea mawazo na fikra za kigeni.
Katika Afrika kuna nchi zipo kwenye Jumuiya ya Madola. Kwamba ni nchi zinazofurahia kutawaliwa na ukoloni wa Uingereza.


Katika Jumuiya ya Madola kuna wanachama wanaokutanishwa kila mara kwenye mikutano yao. Nchi hizo ambazo ni makoloni ya zamani ya Uingereza kwa upande wa siasa.


Upande wa pili kuna Michezo ya Jumuiya ya Madola ambao huwakutanisha mataifa yote yaliyotaliwa na Uingereza. Kwamba mataifa hayo licha ya kupata uhuru wa bendera bado yamekubali kuwa chini ya himaya ya wakoloni.


Safari hii wakoloni wakiwa wanatawala kutoka nchini mwao. Katika maeneo hayo mawili kutoka sehemu moja; waziri mkuu wa Uingereza huendesha vikao na mikutano pamoja na marais wa Afrika hususani nchi zilizotaliwa na Uingereza.


Rais Julius Nyerere na Fidel Castro wa Cuba.

Kwenye michuano ya Jumuiya ya Madola Malkia Elizabeth II wa Uingereza kuwahutubia wanamichezo na wanaoshiriki michezo hiyo wakiwakilisha kutoka mataifa yaliyokuwa chini ya himaya ya ukoloni.


Michuano ya mwaka huu ilifanyika mjini Glasgow nchini Scotland. Malkia anatawala nchi hizo kwa namna nyingine katika michezo ya madola na katika uchumi na siasa kwenye jumuiya hiyo.


Hayo ni mataifa yaliyotawaliwa na Uingereza, kwamba tunajinasibu kupinga ukoloni na kufundisha wanetu kuwa akina Kibanga waliwachapa makonde wakoloni hata wakatokomea.
Kwenye chaguzi mbalimbali ndani ya Umoja wa Afrika, mataifa yaliyotawaliwa na Uingereza yanaweza kujipanga na kutamba kuteteana ikiwemo kupeana nafasi za vyeo na kupigiana upatu kwa wagombea wao.


Mataifa haya ndiyo yanajigamba ni wazungumzaji wa lugha ya kiingereza na yanaitwa kwa kifupi Anglophone.
Tukigeukia upande wa pili tunakutana na mataifa yaliyotaliwa na Ufaransa. Mataifa haya yanajigamba kuwa ni wazungumzaji wa lugha ya Kifaransa, na huitwa Francophone.


Aghalabu kwenye kinyang’anyiro cha uongozi ndani ya Umoja wa Afrika (AU) tunashuhudia mnyukano mkubwa baina ya pande mbili; Anglophone dhidi ya Francophone.


Kwamba wale wenye kundi la Francophone walipiga kampeni kubwa kwa ajili ya Jean Ping ambaye ni mgombea kutoka kambi yao wakati wa kinyang’anyiro cha Ukuu wa Tume ya Umoja wa Afrika.


Mgombea wa Anglophone, Dk. Dlamini Nkosozana-Zuma alimshinda Jean Ping wa kambi ya Francophone, hivyo kuwa mkuu mpya wa Tume ya Umoja wa Afrika.


Kwenye nchi za Francophone, ulimwengu ulishuhudia wakiundiwa jukwaa jingine la Francafrique ambalo lilikuwa mahususi kuziweka pamoja na kujenga uhusiano baina ya nchi za Kiafrika zilizotaliwa na Ufaransa.


Francafrique ni sawa na ilivyokuwa ajenda ya Francophone. Ufaransa haikuishi hapo, iliwahi kumpa mwaliko aliyekuwa Rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa kuhudhuria mkutano mkubwa wa kundi la Paris Club.


Kundi hilo linahusisha wachumi wenye nguvu zaidi na wanaotoa misaada ushauri wa kiuchumi na madeni kwa mataifa mbalimbali.


Ureno nao hawajabaki nyuma. Mwaka 1996 nchi zote zilizotawaliwa na Ureno zilijumuishwa kwenye jukwaa lao, Lusophone Africa.


Nchi zinazounda Lusophone Africa ni Angola, Cape Verde, Guinea-Bissau, Msumbiji, na Sao Tome and Principe. Awali nchi hizo ziliunda umoja wao wa ushirikiano unaojulikana kama PALOP (African Countries of Portuguese Official Language).


Hilo lilikuwa kujibinafsisha kwenye himaya ya Ureno sambamba na mkondo wa Anglophone na Francophone.
Katika dhana hii kulikoni bara la Afrika hatuna Bantuphone wala Africophone? Kwamba imekuwaje rais kwa viongozi na wananchi wa Afrika kujitambulisha kwenye Jumuiya za wakoloni wao Anglophone (Uingereza), Francophone (Ufaransa), Lusophone Africa (Ureno)?


Kwa mantiki hiyo lazima tujiulize maswali, inawezekanaje waafrika wakakubali kuwa jumuiya za Bantuphone na Africophone hazifai kwao, badala yake kuzing’ang’ania zile za wakoloni?


Ni kitu gani kinakwamisha kuundwa jumuiya za kiafrika kama Bantuphone na Africophone kuliko kuwekeza akili zetu kwa jumuiya za kikoloni?


Swali hilo linaweza kujibiwa kirahisi mno, kwamba huenda waafrika wanajisikia fahari zaidi kuongozwa na wakoloni licha ya kudai walipambana ili kuwafukuza kwenye ardhi zao.
Wakoloni wanatumia mbinu za jumuiya hizo kama nyenzo ya kuendeleza ukoloni wao kwa mataifa. Sielewi ndugu zangu.


Baruapepe; mawazoni15@gmail.com

© Andunje wa Fikra, 2014

August 24, 2013

CHADEMA NDANI YA WILAYA YA NYASA

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa akizungumza wakati wa mkutano wa katiba mpya, Mbamba Bay.

 Na Vitus Matembo, Mbamba Bay

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. SLAA, Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee walizungumza na wananchi wa Wilaya ya Nyasa wakati wakiahimiza suala la katiba mpya na mamlaka ya Zanzibar.

Leo kutakuwa na mkutano wa KISIASA hapa Mbamba bay. Viongozi wa Chadema walifaka kwa Helikopta wakitokea SONGEA. Karibu watu wote walichangamka sana kwenye mkutano huo na kupata ari mpya ya uimarifu wa Sera katika KUIJENGA NYASA YETU.

Helikopta waliyosafiria
Hoja kubwa ya Chadema jana katika mkutano uliofanyika kwa muda wa dk.45 ni kuhusu Mabadiliko ya katiba mpya. Wanapinga kuhusishwa Zanzibar kwenye katiba wakati tayari wanakatiba yao.
Pia ile ni nchi inayojitegemea kwa kuwa ina RAIS, BENDERA, AMIRI JESHI, KATIBA,NYIMBO YA TAIFA n.k..  KIUFUPI wamejitahidi kuelewesha umma juu ya mapungufu yaliyomo kwenye RASIMU YA KATIBA MPYA.