Showing posts with label Sheria. Show all posts
Showing posts with label Sheria. Show all posts

December 28, 2017

AKAMATWA NA VITAMBULISHO 65 VYA KUPIGIA KURA

NA MWANDISHI WETU, SONGEA
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limemkamata Rajab Seleman (27) mkazi wa mkazi wa Nakawale Halmashauri ya wilaya ya Songea akiwa na vitambulisho 65 vya kupigia kura vya wakazi wa kijiji cha Nakawale.
Kamanda wa Polisi wa Ruvuma, SAPC Mushy
Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma SACP Gemini Mushy amesema mtuhumiwa Seleman ambaye pia ni mpigapicha na amefuzu mafunzo ya ualimu alikamatwa Desemba 26 mwaka huu majira ya saa saba mchana katika stendi ndogo ya mabasi ya abiria.

October 16, 2017

“RAIS ANA MIAKA 31”


Sebastian Kurz
JUMAMOSI nilikuwa nasoma makala ya James Masters kwenye tovuti ya CNN. Sentesi yake ya kwanza ilinivutia sana, “Ulikuwa unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Ingawa aliendelea na mengine lakini staili pekee haikuwa kivutio bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi.
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye amewahi kuwa waziri wa  Ushirikiano wa Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.  Sebastian  Kurz ambaye amekuwa Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu. 

Ni mwenyekiti wa chama cha  OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama chake kushinda viti vingi vya bunge. 

October 06, 2017

SOMO LA LEO; SHERIA

Kifungu cha 6(1)(h) cha Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Nam 7/2001 kinaipa mamlaka na uwezo Tume kukagua Magereza (pamoja na Vyuo vya Mafunzo) na sehemu ambazo watu wanazuiliwa kwa mujibu wa sheria ili kufanya tathmini na kukagua hali ya haki za watu wanaozuiliwa humo na hatimae kutoa mapendekezo yatakayotatua au kuondoa matatizo yatakayoonekana.