NA MWANDISHI WETU, SONGEA
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma
limemkamata Rajab Seleman (27) mkazi wa mkazi wa Nakawale Halmashauri ya wilaya
ya Songea akiwa na vitambulisho 65 vya kupigia kura vya wakazi wa kijiji cha
Nakawale.
![]() |
| Kamanda wa Polisi wa Ruvuma, SAPC Mushy |
Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma
SACP Gemini Mushy amesema mtuhumiwa Seleman ambaye pia ni mpigapicha na amefuzu
mafunzo ya ualimu alikamatwa Desemba 26 mwaka huu majira ya saa saba mchana
katika stendi ndogo ya mabasi ya abiria.

