Showing posts with label jamii. Show all posts
Showing posts with label jamii. Show all posts

March 21, 2018

JE, JAMII IMECHOKA KUISHI KWA MAFUNDISHO YANAYOTOLEWA KWA MIFANO?

Na KIZITO MPANGALA

Mafundisho ni moja kati ya elimu ambayo haina mpinzani katika maisha yetu ya kila siku. Mafundisho hayo yapo kwa namna mbalimbali, kuna mafundisho ya jumla, kuna mfundisho ya kipekee ambayo hugusia katika uga husika kama vile mafundisho ya dini, mafundisho ya stadi za kazi, mafundisho ya maadili, mafundisho ya rika na kadhalika. Hayo yote husaidia kujenga jamii na kuiweka katika mwenendo unaokunalika na wengi na ambao una manufaa mazuri kawa jamii hiyo na pengine hata kuakisi kwa jamii nyingine mahali popote duniani.
Mafundisho ya kijinsia yana umuhimu mkubwa sana katika maisha yetu. Jinsia fulani ifundwe yale yanayopaswa kufanyika nayo ili kuendeleza maadili au jeme lipatikanalo kutoka katika mafundisho hayo. Ikiwa mtu wa jinsia tofauti ataifunda jinsia nyingine fundisho fulani, kinachotakiwa ni kufikiri kilichosemwa ili kubaini kama kina manufaa ya kurekebisha kitu fulani kwa jinsia iliyofundwa au kama kina maudhui mabaya dhidi ya jinsia iliyofundwa kishapo hukumu itolewe, iwe hukumu chanya au hukumu hasi.
Kitendo cha kutoa mafundisho kinaweza kuwa cha namna mbili. Huenda mafundisho yakatolewa kinagaubaga au kwa kutumia mifano ambayo inalenga kurekebisha jambo fulani katika jamii. Ikiwa hilo linafanyika, si vema kulalamika ghafla bila kufikiri lengo au dhamira ya mafundisho hayo. Na kwa sasa jinsi ilivyo rahisi kusambaza taarifa katika mitandao basi ndani ya dakika kadhaa dunia yote huenda ikajua kinachojiri na kisha kila aliyepata taarifa anatoa maelezo yake kadiri ya taarifa ilivyomfikia. Watasifu, watalaani, watahamasisha watu kuwa watulivu, watamshutumu mnenaji, watamtetea mnenaji na kadhalika.
Katika suala hili la kuishi katika mafundisho yanayotolewa kwa mifano, inawezekana mfundaji anakuwa na nia ya kuonya au kurekebisha jambo fulani lakini huenda akaeleweka tofauti na lengo la fundisho lake. Hii inatokea mara nyingi na pengine husababisha maandamano ambayo yanaweza kuzua madhara kwa waandamanaji wakiwa wanakemea fundisho wasilolikubali au kama limefikirirwa kuwa ni la kejeli kawa kundi fulani katika jamii.

February 12, 2018

ANA KWA ANA NA MBUNGE WA VITI MAALUMU CHADEMA, NDUGU UPENDO PENEZA


Sisi katika blogu yetu tunakutana na wanasiasa mbalimbali bila kujali itikadi zao. Au pia viongozi wa kila kada tunazungumza nao bila kujali fani zao. 
Madhali wengi wao ni marafiki zetu maana ni watanzania wenzetu basi huwa tunazungumza nao mambo yahusuyo  ustawi wa jamii yetu kwa ujumla wake. Tunazungumzia maendeleo ya elimu, uchumi, siasa, utamaduni, afya na kadhalika.
Madhumuni yetu ni kuendelea kuzungumzia maendeleo ya wananchi pamoja na furaha ya jamii. Tunajikita katika maslahi ya taifa letu. Tanzania ni nchi yetu na hatuna kwingine. Tutailinda na kuikosoa ikibidi.
Pichani; kutoka kushoto ni Gabriel Mushi (mwandishi wa gazeti la RAI), mhariri wa Blogu hii Markus Mpangala (katikati) na Mbunge wa Viti maalumu ndugu Upendo Peneza.

January 26, 2018

TUNAPOKOSEA NI PALE TUNAPOCHANGANYA ELIMU,SIASA

NA HONORIUS MPANGALA
HISIA zangu zimenifanya niwe mtu tofauti kabisa kuhusiana na matumizi ya baadhi ya maneno hapa nchini. Mengi hutumiwa na viongozi wa ngazi za juu kuwaona wale waliopo chini au wasio na vyeo kama wao kuwa  wenye kiwango fulani cha dhiki kinachostahili kuitwa cha chini. Ni hapo ndipo nakuwa na hisia tofauti sana juu ya kutumia maneno fulani dhidi ya kundi jingine hasa lile ninaloongoza au viongozi wanaloliongoza. 
Makala hii imechapishwa katika gazeti la MTANZANIA toleo la leo
Japokuwa nimekuwa mtu nisiyependezwa na na hili neno “Wananchi wa hali ya chini”' lakini najiuliza hao wa hali ya juu ni akina nani, wanafanya nini kutokuwa na hali ya chini na njia zao zikoje ili tuwaambie wa hali ya chini wajifunze kwenda huko juu? 
Suala elimu katika nchi yoyote ni muhimu na linatakiwa kupewa kipaumbele sana. Kiuhalisia mazingira ya wanafunzi kwa shule nyingi zinazomilikiwa na serikali zimekuwa na changamoto kubwa na kupelekea hata matokeo mabaya kwa shule hizo.

Lakini unakuta baada ya kutazama wapi walipojikwaa wao wanakawaida ya kulaumu mwendo Wa aliyedondoka kuwa hatazami vyema au hatembei vyema.

Tangu iliposemwa elimu bure maisha ya wanafunzi yamekuwa na changamoto zake na wazazi waliipokea katika mitazamo yao hii hoja. Kutokana na kuzoea kupewa pewa tangu zama za wakaloni, waafrika wengi wamekuwa wavivu wa kujitafutia wao na kutatua changamoto wao huku wakitegemea tusaidiwa kama ilivyokuwa katika maisha ya ukoloni au kwa wale waliokuwa wanaishi karibu na Taasisi za kidini zilivyokuwa zikitoa misaada.

December 27, 2017

SAMAKI ZIWA NYASA

Inakadiriwa kuna aina 700-1000 ya Samaki wa aina ya Cichlids katika Ziwa Nyasa. Samaki hao hawapatikani sehemu zingine duniani isipokuwa Ziwa Nyasa (Endemic). Samaki hao hutafutwa sana na wageni ambao hutengeneza MatankiMaji ya vioo kwaajili ya maonyesho (Aquarium).

MUHIMU; Pichani ni ufukwe wa Lundu upande wa kaskazini-magharibi unaitwa "Bandarini". Ni sehemu iliyokuwa inatumiwa na meli za MV. Iringa na MV.Songea kutia nanga. Katika ratiba iliyopo Meli mpya za mizigo ya MV.Ruvuma na MV Njombe hazitatia nanga hapa kwetu.

Lundu, Nyasa
Disemba 22/2017.

November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

October 17, 2017

UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
ILIKUWA miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika. Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
KIKOSI CHA MISRI

Fainali ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa moto wa kuotea mbali. Hapa nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.

June 27, 2014

RADIO CONSULT LIMITED



RADIO CONSULT LTD

Ni kampuni inayotoa huduma za ushauri wa kitalaamu kwa masuala ya radio. Moja ya huduma tunazotoa ni kama ifuatvyo:-
Tunatoa huduma zifuatazo:-
1. Wanaotaka kuanzisha kituo cha radio, tunatoa huduma zote ikiwemo kuandika maandiko ya uombaji wa leseni TCRA.
2. Tunauza vifaa vya radio kwa order (Transmitter, mixer, microphones, Hybrid Telephones, antenna, STL n.k)
3. Tunadesign studio za mazoezi kwenye vyuo vya unadishi wa habari kwa bei nafuu. 4. Kuandaa ratiba za vipindi vya radio (scheduling&Planning)
5. Media Research
6. Kuandika maandiko (Business Plan, Strategic Plan, Editorial Policy, Feasibility Study n.k)
7. Tunatoa mafunzo mbalimbali (Uandaaji wa vipindi, Management, Marketing, ICT for radio, Internet Radio, Journalism n.k)
8. Tunachuo cha media pia www.dmctanzania.org. Kwa huduma zaidi fika ofisini kwetu Nanenane Mbeya, jengo la Chai (RSTGA) au tupigie simu namba 0768188429 au 0759307280 au tuandikie email: consultancy@radiotz.com zaidi tembelea www.radiotz.com Facebook: www.facebook.com/radiotz

August 24, 2013

ZIARA YA MCHEZAJI WA ZAMANI WA MACHESTER UNITED, QUINTONE FORTUNE HAPA NCHINI KATIKA JUHUDI ZAKE ZA KUSAIDIA JAMII KAMA MWAKILISHI WA TIMU HIYO

FORTUNE na Mimi alipotembelea ofisini.