Showing posts with label Katiba. Show all posts
Showing posts with label Katiba. Show all posts

November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

September 29, 2017

KWA WAANDISHI WA VITABU NA MACHAPISHO MENGINE YA KISWAHILI.

NA MAUNDU MWINGIZI

Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), kwa mujibu wa sheria ndio chombo, kwa niaba ya serikali, kinachosimamia masuala yote yanayohusu lugha ya Kiswahili Tanzania. Kwa miezi kadhaa sasa limekuwa likiandaa kanuni mpya za Kiswahili Tanzania. Rasimu ya kanuni hizo imeshakamilika na baadhi ya wadau walipewa kuisoma na kutoa maoni yako, na baadaye wadau wachache walialikwa kwenye kikao kingine cha kupitia maoni yaliyotumwa na wadau juu ya rasimu hiyo. 

Wajumbe wa kikao wengi waliwakilisha wenzao kutoka sekta ndogondogo zinazogusa lugha ya Kiswahili. Mfano, Watunzi wa vitabu, waandishi wa habari za Kiswahili, Bodi ya filamu Tanzania, Wakalimani/Wafasiri wa kawaida na wale wakalimani wa lugha za alama, walimu wa Kiswahili kwa wageni, watu wa matangazo, wawakilishi kutoka vyuo vikuu, watu wa mashairi n,k. 

August 24, 2013

OLE WENU WAJUMBE WA MABARAZA YA KATIBA


Niseme mapema naungana na Jaji Warioba ambaye ameonya vyama vya siasa pamoja na wajumbe wa Mabaraza ya katiba kutumia ajenda za vyama hivyo badala ya kutoa mapendekezo kwa Tume.
Kuna mambo yanasikitisha juu ya tafsiri ya wajumbe wa Mabaraza ya Katiba, badala ya kufanya upembuzi yakinifu juu ya Katiba Mpya, baadhi ya wajumbe wamegueza vikao hivyo kuwa sehemu ya kulalamika, kutuhumu na kuhukumu.
Hivi karibuni tumemsikia Profesa Mwesiga Baregu akimuonya mjumbe mmoja aliyeshutumu kuwa eti wasomi wanaipeleka pabaya nchi hii bila kuchambua mapendekezo yaliyoko kwenye Rasimu ya katiba mpya.
Nitangulie kusema, ujumbe wangu wa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba, wanapaswa kupendekeza mambo muhimu kwa niaba ya wananchi kwenda Tume ya Rasimu ya Katiba.
Acheni kubeba magunia ya malalamiko na kugeuzwa madaraja ya vyama bali ongezeni mapendekezo nyeti na kushauri marekebisho pale inapotakiwa. Lawama kwa Tume ya Jaji Warioba hazitasaidia.
Kwa mfano, baadhi ya Wajumbe, wanachangia maoni  kwa kutumia waraka ambao unaelezwa kusambazwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenda kwa wanachama.
Tunafahamu kuwa CCM haitaki muundo wa serikali tatu bali inaunga mkono serikali mbili. Mpaka wakati huu, waraka wa CCM umezusha rabsha kidogo miongoni mwa wananchi ambao wanadhani chama hicho ndicho kinastahili zaidi kusikilizwa ama kinabeba uamuzi wa kufikiri wa watanzania.
Nadhani muundo wa serikali mbili unatakiwa kutetewa kwa hoja, na sio hisia sababu hakuna sehemu nzuri ya kuwasilisha mapendekezo kama muda uliopangwa mpaka Tume ikakamilisha shughuli zake.
Kuna hatari moja inayoweza kutokea kwenye mchezo huu ambao umeasisiwa na CCM, kwamba katika kipindi hiki tunachotakiwa sio kwuaelekeza wajumbe wa Mabaraza ya katiba waseme nini, bali kuwapangia maeneo ya kuzungumzia bila kuathiriwa na ajenda ya chama chochote.
Kama CCM inadhani serikali tatu ni tatizo basi inayo haki ya kupinga kwa hoja sio vinginevyo. Onyo langu kwa wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ni hili, leo hii mnaweza kujisikia fahari sana kutumika kwa matakwa ya CCM ambacho ni chama cha siasa.
Lakini kuna kipindi tutafika mahali tutalazimika kufumua mambo mengi kutokana na mzaha unaofanywa sasa. Tume ya Katiba inaongozwa kwa taratibu ambazo zinaelekezwa kwenye kanuni ya Mabadiliko ya Katiba ambayo watu (wajumbe) wanatakiwa kutoa maoni yao sio kutumwa na chama chochote.
Kuna kelele nyingi nchini Misri, Rais Mohamed Mosri aligombana na raia wa nchi hiyo kwenye utungaji wa Katiba mpya kama tunavyofanya sisi hapa nchini.
Wakati chama chake kikipendekeza kuundwa kwa Jamhuri ya Kiislamu kama Katiba ya mwaka 1980 ilivyosema, wao wakataka kuwalazimisha wananchi wakubali hata kwa shuruti. Mpaka leo hakuna utulivu Misri.
Sasa, kwa wajumbe wa Mabaraza ya Katiba wanaodhani kuwa kuteuliwa wkao ni kama sehemu ya kucheza ndombolo ama kwasakwasa waache mara moja. Suala la katiba mpya sio kitu cha kuchezea hata kidogo.
Ni lazima wajumbe wa Mabaraza ya Katiba wafahamu kuwa wamekabidhiwa jukumu zito sana la kuimarisha na kusimika ujenzi wa taifa letu.
Leo hii tunaweza kuchekelea sana waraka wa CCM, ama hata ungekuwa wa chama chochote, lakini huko tuendako tutaanza kutafuta mchawi, na baadaye tutanyoosheana vidole na kumgeukia Jaji Joseph Warioba na timu yake iliyoketi na kutumia nguvu pamoja na akili zao kukusanya maoni ya watanzania wote kuunda Katiba.
Tukishatafuta mchawi kitakachofuata ni kukosa maelewano na kuanza kutwangana wenyewe. Tumeunda Mabaraza ya Katiba ili kufanikisha mchakato wa kupatikana Katiba Mpya sio sehemu ya kupiga porojo ama kuimba nyimbo za vyama vya siasa.
Kwenye mabaraza ya Katiba hatuzungumzii maslahi ya chama chochote bali tunaizungumzia Tanzania ambayo inahitaji uponyaji wetu.
Mabaraza ya Katiba sio sehemu ya kupenyeza sumu za kulalamika na kubebeshana tuhuma ambazo haizna msaada wowote kwa taifa. Hakuna nchi yoyote itakayotusaidia kukamilisha mchakato huu, na tusipokuwa makini leo basi tutalia na kusaga meno.
Onyo langu moja, Wajumbe msigeuze mikutano ya Mabaraza ya Katiba kama sehemu ya mikutano ya kisiasa. Nimemaliza.

July 16, 2013

IJUE RASIMU YA KATIBA 2013; MAPITIO NA MAPENDEKEZO


Na Edgar Mwandemani.


Ibara ya 78 na 79

Weredi na wasomi wengi wamekwisha kutoa maoni yao, wengi wakijielekeza katika suala la muundo wa muungano. Mimi kwa leo nitaanza na ibara tajwa ambazo haiyumkiniki zinaweza kusahaulika.

Ibara hizi kwa pamoja ni juu ya malalamiko kuhusu uhalali wa matokeo na Kiapo cha Rais!

Zinasema:

Ibara ya 78 (2) na ( 3)- Mlalamiko ya matokeo
(2.) Malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais yatawasilishwa Mahakama ya Juu ndani ya muda wa siku saba baada ya siku ya kutangazwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais.

(3.) Mahakama ya juu itasikiliza na kutoa uamuzi wa shuari la kupinga matokeo ya Uchaguzi wa Rais katika kipindi cha siku kumi na nne tangu kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwa mujibu wa ibara ndogo ya (2) na uamuzi huo utakuwa wa mwisho.

Vipengele hivi vinafanana kimaudhui na Ibara ya 140 (1) na (2) ya Katiba ya Kenya kama ilivyopitishwa 2010. Tofauti zake ni lugha (kiingereza kwa kiswahili) na mpangilio wa namba- kimsingi tumechukua kama vilivyo!

Ibara ya 79- Kiapo cha Rais
(1) Rais Mteule ataapishwa na Jaji Mkuu na atashika nafasi ya madaraka ya Rais Mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote, hatashika madaraka kabla ya kupita siku thelathini kutoka siku ya matokeo ya uchaguzi wa Rais yalipotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi au siku ya kuthibitishwa na Mahakama ya Juu.

Moani: Ibara hizi mbili zinatoa Haki kwa kunyang'anya haki- ni vipengere kinzani. Itakumbukwa kuwa vipengele hivi ni ingizo jipya mara baada ya malalamiko ya muda mrefu juu ya uwazi wa matokeo ya rais ikiwemo haki ya kuyapinga.

Nirejee tena Katiba ya Kenya; katika Ibara 141 (2) (a) na (b) juu ya kuchukua ofisi- Kiapo!

2) The president elect shall be sworn in in the first Tuesday following:-
(a) the fourteenth day after the date of the declaration of the result of the presidential election, if no petition has been filed under Article 140; or
(b) the seventh day following the date on which the court renders a decision declaring the election to be valid, if any petition has been filed under Article 140.

Maoni: Kimsingi vipengele hivyo katika Katiba ya Kenya vinatoa masharti kuwa hakutakuwa na kuapishwa kwa rais wala kukamata madaraka mpaka ile haki iliyotolewa katika ibara ya 140 itekelezwe pasipo shaka- uchaguzi wa uliomalizika mwezi Machi, 2013 umethibitisha hilo. Sisemi tuige kila kitu kutoka katika kipengele hiki lakini kwa kuwa lengo ni kuweka uwazi katika mchakato wa matokeo ya rais hatuna budi kuiga jambo hili.

Kwa upande wa Ibara tajwa katika rasimu yetu zimetoa na kunyang’anya haki hii. Ibara ya 79 (1) ndio imenyang’anya haki iliyotolewa na Ibara ya 178 (1) na (2) kwa kuruhusu kuapishwa kwa Rais mara baada ya matokeo kutangazwa. Kipengele hiki kimeyapa uhalali matokeo yatakayotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi mara baada ya kutangazwa hata bila ya kusikiliza pingamizi lolote na kwamba rais aliyeapishwa atasubiri siku 30 kabla ya kushika madaraka. Hapa tumedanganywa! Mtu haapishwi na kusubiri kushika madaraka; anaweza kusubiri kuapishwa ili ashike madaraka lakini si vinginevyo. Siku 30 zinazotajwa hapa ni kiini macho, kwani ni kwa namna gani mamlaka yoyote itaweza kutengua kiapo cha mtu eti kwa kuwa tu mahakama imesema sio halali. Hizi ni fujo!

Inawezekana tulitaka kuiga mfumo wa Marekani ambapo Rais Mteule husubiri siku 100 kabla ya kushika madaraka. Lakini kwa kuwa kiapo huenda na madaraka, Rais Mteule wa marekani huwa na siku 100 za mpito kabla ya kuapishwa na kushika madaraka- Hapishwe halafu akasubiri siku 100 kabla ya kushika madaraka. Kiapo ni kazi kiapo ni mamlaka hakiwezi kwenda kinyumenyume.

Aidha, tukirejea tena kwa wenzetu Kenya kwa mara nyingine, mara baada ya matokeo kutangazwa na Uhuru Kenyatta kutangazwa mshindi huku mpinzani wake Raila Odinga akiwasilisha malalamiko Mahakama ya Juu dhidi ya matokeo: ililazimu mamlaka husika kuwasihi Rais Mteule na Mwenza wake pamoja waache mara moja misafara na ziara kana kwamba wameshashika madaraka kwani kiapo bado na lolote linaweza kutokea. Shukrani kwamba mambo yalibaki kama yalivyotolewa na Tume.

Tuendelee na mjadala mimi nimeanza kwa Ibara hizo.