Showing posts with label diplomasia. Show all posts
Showing posts with label diplomasia. Show all posts

February 15, 2018

KATUNI INASEMA

November 15, 2017

G40 HOI. GRACE MUGABE AKIMBIA NCHI



Kwa mujibu wa taarifa ya Kituo cha Skynews kimesema kuwa Mke wa Rais Robert Mugabe,  Bi.Grace Mugabe ameondoka nchini Zimbabwe na kuelekea Namibia ikiwa ni saa chache baada ya Jeshi la Nchi hiyo chini ya Jenerali Costatino Chiwenga kuchukua madaraka kwa muda. 

MFAHAMU NDEGE ANAYEJENGA NYUMBA NA KUPANGISHA

NA MWANDISHI WETU

KAMA ulidhani ni binadamu pekee anajenga nyumba na kupangisha utakuwa unajidanganya kwa kuwa mwambao mwa ziwa Nyasa katika Kijiji cha Mtupale kata ya Chiwanda,kuna aina ya ndege anayeitwa Fundichuma (Hamerkop) ambaye anajenga nyumba na kupangisha kwa ndege na viumbe wengine kama mijusi.
Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe ambaye pia ni mzaliwa wa mwambao mwa ziwa Nyasa anasema ndege huyo anapenda kuishi jirani na ziwa au mto kwa sababu chakula chake kikuu ni samaki.

November 08, 2017

MABALOZI WETU WASIWE WAZITO KUJENGA UCHUMI

NA GABRIEL MWANG’ONDA 

RAIS John Magufuli ametimiza miaka miwili madarakani tangu alipoapishwa Novemba 5 mwaka 2015. Miaka hiyo serikali imefanya mambo mengi ambayo si lazima kueleza hapa leo. Lakini itoshe kusema lipo jambo ambalo ninajikita nalo ili kuangazia miaka hiyo. Ni dimplomasia ya uchumi.

Diplomasia ya Uchumi (Economic diplomacy) limekuwa somo gumu sana kueleweka kwa mabalozi wetu. Yaani sisi wengine tumeiimba mpaka tukaona tupumzika tu kwasababu somo limekuwa gumu sana kwa balozi zetu. Binafsi nimeliongelea sana kwenye ma redio nyingi hapa ndani ya nchi na nje pia, lakini ndugu zetu wameamua kutoelewa tu hii dhana kitu ambacho kinaligharimu sana Taifa letu.
Ufukwe wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma. Ni miongoni mwa vivutio vya utalii.
Kila balozi utakae onana nae ukimuongelesha kuhusu hii diplomasia ya uchumi anasingizia udogo/ufinyu wa bajeti. Lakini hiki kamwe hakiwezi kuwa kikwazo kwa mtu mzalendo mwenye ubunifu alienuia kwa dhati kabisa kuitumikia nchi.

Si mambo yote yanahitaji fedha nyingi kuyafanya kuhusu hii dhana ya diplomasia ya uchumi. Balozi zetu hata utume baraupepe kwa vitu ambavyo ni vya kawaida sana bado hutojibiwa kabisa. 

October 30, 2017

SEBASTIAN KURZ; Kiongozi mbichi anayeugusa ulimwengu



NA MWANDISHI WETU

“ULIKUWA unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Hiyo ni sentensi ya kwanza iliyoandikwa na Mwanahabari wa Televisheni ya CNN, James Masters, kwenye tovuti ya CNN. Sentensi hiyo ilinivutia zaidi, ingawa aliendelea na mengine, lakini staili pekee haikuwa kivutio, bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi. 

Mwandishi James Masters alikuwa anamzungumzia kijana mmoja aitwaye Sebastian Kurz kutoka Austria. Ni kijana ambaye anazidi kuvutia duniani kutokana na siasa zake ambazo kwa namna moja au nyingine ziliibua nchi hiyo kwenye ramani ya kidiplomasia. 

Baada ya hapo nililazimika kufuatilia habari zaidi za Sebastian Kurz. Niliyokutana nayo ni somo, ingawa kwa Tanzania lilianza muda mrefu.
Nimekuandalia makala haya msomaji ili kujifunza jambo katika malezi ya familia na taifa kwa ujumla. Austria ipo tayari kwa kiongozi kijana? Fuatilia.

Sebastian Kurz ni nani?

October 26, 2017

MWALIKO; WOTE MNAKARIBISHWA KWENYE MJADALA HUU


October 23, 2017

URUSI, CHINA KUTAWALA BIASHARA DUNIANI



 
MOSCOW, URUSI

MIKAKATI ya serikali ya Urusi kuifanya China kama mshirika thabiti na muhimu kiuchumi umechochea kukuza sekta ya biashara na kufikisha asilimia 22 katika mapato yake.

Gazeti la The Moscow Times limesema kuwa ushirikiana wa karibu baina ya Urusi na China umechangia kuimarisha mapato katika biashara na kufikia kiasi cha dola bilioni 80 mwaka huu huku matarajio yakiwa ni kufikiwa dola bilioni 200. 

October 17, 2017

UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
ILIKUWA miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika. Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
KIKOSI CHA MISRI

Fainali ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa moto wa kuotea mbali. Hapa nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.

October 16, 2017

“RAIS ANA MIAKA 31”


Sebastian Kurz
JUMAMOSI nilikuwa nasoma makala ya James Masters kwenye tovuti ya CNN. Sentesi yake ya kwanza ilinivutia sana, “Ulikuwa unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Ingawa aliendelea na mengine lakini staili pekee haikuwa kivutio bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi.
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye amewahi kuwa waziri wa  Ushirikiano wa Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.  Sebastian  Kurz ambaye amekuwa Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu. 

Ni mwenyekiti wa chama cha  OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama chake kushinda viti vingi vya bunge. 

September 30, 2017

UTUNZI WA VITABU NA KISWAHILI CHA PROFESA SHAOPING

NA KIZITO MPANGALA

KESI YA ALMASI ni kitabu kilichoandikwa na Profesa Rao Shaoping wa China. Kitaaluma yeye ni mhandisi. Alijifunza Kiswahili nchini Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja na ushee, mwalimu aliyemfundisha aliitwa Ali Omari Mzee.
Profesa Shaoping ndiye msimamizi wa kazi za TAZARA wakati inajengwa. Alikuwa akimtafsiria Mwalimu Nyerere mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na wenzake. Pia alikuwa mkaliamani kwa Mh. Salim Ahmed Salim, Mh. Rashid Kawawa, Spika Adam Sapi kwa mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na Wachina wenzake. Na mwaka 2013 Profesa Shaoping alikuja tena nchini Tanzania kumtembela Mzee Ali Hassan Mwinyi.

Profesa Shaoping anasema hivi "ninaipenda Tanzania. Ninawapenda watu wa Tanzania". Profesa Shaoping anayafahamu maeneo mengi nchini Tanzania ambayo amewahi kutembelea, maeneo hayo ni kama vile Kisuwa cha Saa Nane, Arusha, Ifakara, Iringa, Kimbwe, Kidatu, Mikumi, Makambako, Mbarali, Tunduma, Zanzibar, Moshi, Dodoma na kadhalika.

Profesa Shaoping ameandika kitabu hiki kwa bidii mno. Anasema tangu tuwe Koloni la Mjerumani na baadae Mwingereza, wageni hao hawakuwa na morali ya kutunga riwaya za Kiswahili lakini yeye kama mgeni alipenda sana kuacha kitabu kwa Kiswahili, naam, ndicho hiki hapa pichani.

September 23, 2017

HONGERA DKT ASHA-ROSE MTENGETI MIGIRO.


UN-High Level Advisory Board on Mediation ni nini?
Siku ya tarehe 13/09/2017 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ndugu Antonio Guterrez alitangaza kuanzisha bodi mpya ambayo inaitwa Bodi ya Ushauri ya Masuala ya Upatanishi ya Umoja wa Mataifa-UN.

BODI HII NI NINI HASA?
High Level Advisory Board on Mediation ni bodi iliyoanzishwa kwa lengo la kumshauri Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya juhudi za upatanishi sambamba na kumpa mrejesho juu ya upatanishi duniani.
Bodi hii inaundwa na wajumbe 18 wakiwemo viongozi wa sasa na wastaafu, maafisa wa ngazi za juu na wataalamu mbalimbali kwa lengo la kuunganisha uzoefu, mbinu, maarifa na mawasiliano.

Wajumbe wake ni hawa wafuatao;
(1) Rais Michelle Bachelet wa Chile.
(2) Radhika Coomaraswamy-Mwanasheria wa Kimataifa wa Sri Lanka.
(3) Leymah Gbowe-Mshindi wa Nobel toka Liberia
(4) Jean-Marie Guehenno-Mwanadiplomasia wa Ufaransa
(5) Tarja Halonen-Rais wa kwanza mwanamke wa Finland 2000-2012
(6) David Harland-Mkurugenzi Mtendaji Centre for Humanitarian Dialogue.
(7) Noeleen Heyzer-Mjumbe Bodi ya wadhamini Chuo Kikuu cha Singapore 2013-to date.
(8) Nasser Judeh-Seneta Bunge la Jordan.
(9) Ramtane Lamamra-Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria 2013-2017.
(10) Graça Machel-Mpigania Uhuru wa Msumbiji...
(11) Asha-Rose Migiro-Balozi wa Tanzania UK
(12) Roden Muhammad Marty Muliana Natalalegawa-Indonesia
(13) Olusegun Obasanjo-Rais Nigeria 1999-2007.
(14) Roza Otunbayeva-Rais Mstaafu Kyrgyzstan.
(15) Michel Pierre-Louis- Haiti
(16) Jose Manuel Ramos-Horta- Timor ya Mashariki
(17) Gert Rosenthal-Ujerumani
(18) Justin Welby-UK
Ni imani yetu kuwa migogoro mingi itapata upatanishi wa haraka na wa kudumu.

©Uwanja wa Diplomasia.