Showing posts with label diplomasia. Show all posts
Showing posts with label diplomasia. Show all posts
February 15, 2018
KATUNI INASEMA
Madhumuni
diplomasia,
siasa
November 15, 2017
G40 HOI. GRACE MUGABE AKIMBIA NCHI
Madhumuni
diplomasia,
habari
MFAHAMU NDEGE ANAYEJENGA NYUMBA NA KUPANGISHA
NA
MWANDISHI WETU
KAMA
ulidhani ni binadamu pekee anajenga nyumba na kupangisha utakuwa unajidanganya
kwa kuwa mwambao mwa ziwa Nyasa katika Kijiji cha Mtupale kata ya Chiwanda,kuna
aina ya ndege anayeitwa Fundichuma (Hamerkop) ambaye anajenga nyumba na
kupangisha kwa ndege na viumbe wengine kama mijusi.
KAMA
ulidhani ni binadamu pekee anajenga nyumba na kupangisha utakuwa unajidanganya
kwa kuwa mwambao mwa ziwa Nyasa katika Kijiji cha Mtupale kata ya Chiwanda,kuna
aina ya ndege anayeitwa Fundichuma (Hamerkop) ambaye anajenga nyumba na
kupangisha kwa ndege na viumbe wengine kama mijusi.
Afisa
Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe ambaye pia ni mzaliwa wa
mwambao mwa ziwa Nyasa anasema ndege huyo anapenda kuishi jirani na ziwa au mto
kwa sababu chakula chake kikuu ni samaki.
November 08, 2017
MABALOZI WETU WASIWE WAZITO KUJENGA UCHUMI
NA GABRIEL MWANG’ONDA
RAIS John Magufuli ametimiza miaka miwili madarakani tangu alipoapishwa Novemba 5 mwaka 2015. Miaka hiyo serikali imefanya mambo mengi ambayo si lazima kueleza hapa leo. Lakini itoshe kusema lipo jambo ambalo ninajikita nalo ili kuangazia miaka hiyo. Ni dimplomasia ya uchumi.
RAIS John Magufuli ametimiza miaka miwili madarakani tangu alipoapishwa Novemba 5 mwaka 2015. Miaka hiyo serikali imefanya mambo mengi ambayo si lazima kueleza hapa leo. Lakini itoshe kusema lipo jambo ambalo ninajikita nalo ili kuangazia miaka hiyo. Ni dimplomasia ya uchumi.
Diplomasia
ya Uchumi (Economic diplomacy) limekuwa somo gumu sana kueleweka kwa mabalozi
wetu. Yaani sisi wengine tumeiimba mpaka tukaona tupumzika tu kwasababu somo
limekuwa gumu sana kwa balozi zetu. Binafsi
nimeliongelea sana kwenye ma redio nyingi hapa ndani ya nchi na nje pia, lakini
ndugu zetu wameamua kutoelewa tu hii dhana kitu ambacho kinaligharimu sana
Taifa letu.
| Ufukwe wa Ziwa Nyasa mkoani Ruvuma. Ni miongoni mwa vivutio vya utalii. |
Kila
balozi utakae onana nae ukimuongelesha kuhusu hii diplomasia ya uchumi
anasingizia udogo/ufinyu wa bajeti. Lakini hiki kamwe hakiwezi kuwa kikwazo kwa
mtu mzalendo mwenye ubunifu alienuia kwa dhati kabisa kuitumikia nchi.
Si
mambo yote yanahitaji fedha nyingi kuyafanya kuhusu hii dhana ya diplomasia ya
uchumi. Balozi zetu hata utume baraupepe kwa vitu ambavyo ni vya kawaida sana
bado hutojibiwa kabisa.
Madhumuni
diplomasia,
na Uchumi,
Nyasa,
uchambuzi
October 30, 2017
SEBASTIAN KURZ; Kiongozi mbichi anayeugusa ulimwengu
NA
MWANDISHI WETU
“ULIKUWA
unafanya nini ulipokuwa na umri wa miaka 31? Hiyo ni sentensi ya kwanza iliyoandikwa
na Mwanahabari wa Televisheni ya CNN, James Masters, kwenye tovuti ya CNN.
Sentensi hiyo ilinivutia zaidi, ingawa aliendelea na mengine, lakini staili
pekee haikuwa kivutio, bali mtu aliyekuwa akizungumzwa alivutia zaidi.
Mwandishi
James Masters alikuwa anamzungumzia kijana mmoja aitwaye Sebastian Kurz kutoka
Austria. Ni kijana ambaye anazidi kuvutia duniani kutokana na siasa zake ambazo
kwa namna moja au nyingine ziliibua nchi hiyo kwenye ramani ya kidiplomasia.
Baada
ya hapo nililazimika kufuatilia habari zaidi za Sebastian Kurz. Niliyokutana
nayo ni somo, ingawa kwa Tanzania lilianza muda mrefu.
Nimekuandalia
makala haya msomaji ili kujifunza jambo katika malezi ya familia na taifa kwa
ujumla. Austria ipo tayari kwa kiongozi kijana? Fuatilia.
Sebastian Kurz ni nani?
October 26, 2017
MWALIKO; WOTE MNAKARIBISHWA KWENYE MJADALA HUU
October 23, 2017
URUSI, CHINA KUTAWALA BIASHARA DUNIANI

MOSCOW, URUSI
MIKAKATI
ya serikali ya Urusi kuifanya China kama mshirika thabiti na muhimu kiuchumi
umechochea kukuza sekta ya biashara na kufikisha asilimia 22 katika mapato
yake.
Gazeti
la The Moscow Times limesema kuwa ushirikiana wa karibu baina ya Urusi na China
umechangia kuimarisha mapato katika biashara na kufikia kiasi cha dola bilioni
80 mwaka huu huku matarajio yakiwa ni kufikiwa dola bilioni 200.
Madhumuni
Biashara,
diplomasia,
Uchumi
October 17, 2017
UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.
NA.
HONORIUS MPANGALA
ILIKUWA
miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila
mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile
Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika.
Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya
kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni
Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba
lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri
wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
![]() |
| KIKOSI CHA MISRI |
Fainali
ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho
kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa
moto wa kuotea mbali. Hapa
nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam
Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi
kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata
kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.
Madhumuni
afrika,
afya,
amani na upendo,
diplomasia,
jamii,
Michezo,
soka
October 16, 2017
“RAIS ANA MIAKA 31”
![]() |
| Sebastian Kurz |
James Masters alikuwa anamzungumzia Sebastian Kurz ambaye
amewahi kuwa waziri wa Ushirikiano wa
Kimataigfa tangu mwaka 2013 akiwa na miaka 27.
Sebastian Kurz ambaye amekuwa
Kansela wa Austria mwenye umri mdogo zaidi kwani sasa hivi ana miaka 31 tu.
Ni mwenyekiti wa chama cha OVP. Sebastian kuanzia jana jumapili
aanaongoza serikali ya Austria ( kama vile Rais hapa kwetu) baada ya chama
chake kushinda viti vingi vya bunge.
Madhumuni
Digitali,
diplomasia,
falsafa,
habari,
Historia,
Maendeleo,
Mafanikio,
Mazingira,
mila na desturi,
Politics,
Sheria,
siasa.,
uchambuzi,
Uchumi,
Usalama
September 30, 2017
UTUNZI WA VITABU NA KISWAHILI CHA PROFESA SHAOPING
NA KIZITO MPANGALA
KESI YA ALMASI
ni kitabu kilichoandikwa na Profesa Rao Shaoping wa China. Kitaaluma yeye ni
mhandisi. Alijifunza Kiswahili nchini Tanzania kwa muda wa mwaka mmoja na
ushee, mwalimu aliyemfundisha aliitwa Ali Omari Mzee.
Profesa
Shaoping ndiye msimamizi wa kazi za TAZARA wakati inajengwa. Alikuwa
akimtafsiria Mwalimu Nyerere mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na wenzake. Pia
alikuwa mkaliamani kwa Mh. Salim Ahmed Salim, Mh. Rashid Kawawa, Spika Adam
Sapi kwa mazungumzo aliyokuwa akijadiliana na Wachina wenzake. Na mwaka 2013
Profesa Shaoping alikuja tena nchini Tanzania kumtembela Mzee Ali Hassan
Mwinyi.
Profesa
Shaoping anasema hivi "ninaipenda Tanzania. Ninawapenda watu wa
Tanzania". Profesa
Shaoping anayafahamu maeneo mengi nchini Tanzania ambayo amewahi kutembelea,
maeneo hayo ni kama vile Kisuwa cha Saa Nane, Arusha, Ifakara, Iringa, Kimbwe,
Kidatu, Mikumi, Makambako, Mbarali, Tunduma, Zanzibar, Moshi, Dodoma na
kadhalika.
Profesa
Shaoping ameandika kitabu hiki kwa bidii mno. Anasema tangu tuwe Koloni la
Mjerumani na baadae Mwingereza, wageni hao hawakuwa na morali ya kutunga riwaya
za Kiswahili lakini yeye kama mgeni alipenda sana kuacha kitabu kwa Kiswahili,
naam, ndicho hiki hapa pichani.
Madhumuni
diplomasia,
elimu,
falsafa,
Teknolojia,
utulivu
September 23, 2017
HONGERA DKT ASHA-ROSE MTENGETI MIGIRO.
UN-High Level Advisory Board on Mediation ni nini?
Siku ya tarehe 13/09/2017 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ndugu Antonio Guterrez alitangaza kuanzisha bodi mpya ambayo inaitwa Bodi ya Ushauri ya Masuala ya Upatanishi ya Umoja wa Mataifa-UN.
BODI HII NI NINI HASA?
High Level Advisory Board on Mediation ni bodi iliyoanzishwa kwa lengo la kumshauri Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya juhudi za upatanishi sambamba na kumpa mrejesho juu ya upatanishi duniani.
Bodi hii inaundwa na wajumbe 18 wakiwemo viongozi wa sasa na wastaafu, maafisa wa ngazi za juu na wataalamu mbalimbali kwa lengo la kuunganisha uzoefu, mbinu, maarifa na mawasiliano.
Wajumbe wake ni hawa wafuatao;
(1) Rais Michelle Bachelet wa Chile.
(2) Radhika Coomaraswamy-Mwanasheria wa Kimataifa wa Sri Lanka.
(3) Leymah Gbowe-Mshindi wa Nobel toka Liberia
(4) Jean-Marie Guehenno-Mwanadiplomasia wa Ufaransa
(5) Tarja Halonen-Rais wa kwanza mwanamke wa Finland 2000-2012
(6) David Harland-Mkurugenzi Mtendaji Centre for Humanitarian Dialogue.
(7) Noeleen Heyzer-Mjumbe Bodi ya wadhamini Chuo Kikuu cha Singapore 2013-to date.
(8) Nasser Judeh-Seneta Bunge la Jordan.
(9) Ramtane Lamamra-Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria 2013-2017.
(10) Graça Machel-Mpigania Uhuru wa Msumbiji...
(11) Asha-Rose Migiro-Balozi wa Tanzania UK
(12) Roden Muhammad Marty Muliana Natalalegawa-Indonesia
(13) Olusegun Obasanjo-Rais Nigeria 1999-2007.
(14) Roza Otunbayeva-Rais Mstaafu Kyrgyzstan.
(15) Michel Pierre-Louis- Haiti
(16) Jose Manuel Ramos-Horta- Timor ya Mashariki
(17) Gert Rosenthal-Ujerumani
(18) Justin Welby-UK
Ni imani yetu kuwa migogoro mingi itapata upatanishi wa haraka na wa kudumu.
©Uwanja wa Diplomasia.
Madhumuni
diplomasia
Subscribe to:
Posts (Atom)







