Showing posts with label Taarifa. Show all posts
Showing posts with label Taarifa. Show all posts

May 05, 2018

TAARIFA MUHIMU: TUMESITISHA KUWEKA TAARIFA MPYA ZA NYASA

MARKUS MPANGALA
SALAAM nyi wasomaji wetu wapendwa! 
Ni matumaini yetu nyote mna afya njema na Mwenyezi Mungu amewajalia hilo bila hiyana. Tumshukuru zaidi.
Kwa muda mrefu  nimekuwa nikitoa huduma ya habari za mwambao wa Ziwa Nyasa na yatokanayo na wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma. Nimekuwa nikifanya hivi kama mapenzi yangu tu (bila kutafuta faida yoyote ya fedha). Sikulipwa chochote kwa kutoa huduma hiyo ya kutangaza vivutio vya utalii, utamaduni, changamoto na mambo mseto ya wakazi wa maeneo hayo. 

January 17, 2018

WASHINDI WA TUZO ZA USHAIRI NA FASIHI

January 04, 2018

NYASA YAKAMILISHA UJENZI WA BWENI YA WANAFUNZI

NA MWANDISHI WETU, NYASA
HALMASHAURI ya Wilaya Nyasa inamilisha ujenzi wa Mabweni ya Wasichana katika Shule ya Sekondari ya Mbamba bay (Mbamba Bay High School) iliyopo mjini Mbamba ikiwa ni njia ya kukamilisha mpango wa elimu bora kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Bweni hilo ambalo linaonekana picha linatarajiwa kuchukua idadi ya wanafunzi Wanafunzi 312 hivyo kuondokana na tatizo la makazi ya wanafunzi katika wilaya hiyo. Ujenzi wa Bweni hilo umetokana na juhudi za ushirikiano na Mbunge wa Jimbo la Nyasa ambaye pia ni Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Stella Manyanya pamoja na wadau mbalimbali. 

BENKI KUU YAFUTA LESENI ZA MABENKI MATANO

Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imezifutia leseni, na kuzifungia kufanya shughuli zozote, benki 5 za kibiashara ambazo ni Covenant Bank, Efatha Bank, Njombe Community Bank, Meru Community Bank na Kagera Farmers Cooperative Bank. Sasa wateja wa benki hizo watalazimika kuwasiliana na BOT ili kujua hatma yao.

November 24, 2017

TANZIA: MBUNGE WA SONGEA MJINI AFARIKI DUNIA



NA MWANDISHI WETU, SONGEA
MBUNGE wa Jimbo la Songea Mjini kupitia chama cha CCM ndugu Leonidas Tutubert Gama amefariki dunia usiku wa kuamkia leo hii katika Hospitali ya Peramiho ambapo alilazwa kwa saa chache kabla ya kifo chake.

November 15, 2017

TAARIFA RASMI KUTOKA JESHI LA ZIMBABWE

GOOD MORNING/AFTERNOON
Fellow Zimbabweans, following the address we made on 13 November 2017 which we believe our main broadcaster, ZBC and The Herald were directed not to publicise, the situation in our country has moved to another level.
Firstly, we wish to assure the nation that His Excellency, The President, of the Republic of Zimbabwe, Head of State and Government and Commander in Chief of the Zimbabwe Defence Forces, Cde R.G Mugabe and his family are safe and sound and their security is guaranteed. We are only targeting criminals around him who are committing crimes that are causing social and economic suffering in the country in order to bring them to justice.

October 11, 2017

TAARIFA KWA WANAHABARI

CHAMA cha ACT Wazalendo leo Oktoba 11/2017, kimewasilisha Mahakamani kesi ya kupinga uteuzi wa Katibu wa bunge uliokiuka Katiba na sheria za nchi. Taarifa zaidi juu ya suala hilo zitatolewa kesho baada ya taratibu za kimahakama kukamilika.

Abdallah Khamis
Afisa Habari ACT-Wazalendo

October 07, 2017

MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI.


NA MWANDISHI WETU

WIZARA  zimeongezeka kutoka 19 hadi 21, Mawaziri kutoka 19 hadi 21, Manaibu Waziri kutoka 16 hadi 21. Wataapishwa ni Jumatatu tarehe 9/10/2017 asubuhi kwenye saa tatu au saa tatu na nusu.

Rais Magufuli: Pia tumeongeza Mawaziri 2 na Manaibu Waziri 5
Rais Magufuli: Waziri wa Mazingira amebaki kuwa January Makamba, Naibu atakuwa Mh. Kangi Lugola.


Rais Magufuli: Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi tumeigawa na kuwa Wizara 2 za Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Selemani Jaffo amepandishwa na kuwa Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, kabla alikuwa Naibu kwenye Wizara hiyo. Mbunge George Mkuchika ameteuliwa kuwa Waziri Ofisi ya Rais Utawala Bora.

Rais Magufuli: Mbunge Luhaga Mpina ameteuliwa kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Abdallah Ulega ameteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Wizara hiyo. Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kuwa chini ya Waiziri Dr Philip Mpango na Naibu Waziri Dr Ashatu Kijaji

Wizara ya Kilimo Waziri ni Charles John Tzeba, na Naibu Waziri ni Marry Mwanjelwa. Wizara ya Habari utamaduni wasanii na Michezo, Waziri ni Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri ni Juliana Shonza

Wizara ya Madini, Waziri ni Angela Kairuki na Naibu Waziri Harun S Nyongo. Wizara ya Nishati, Waziri atakuwa Medadi Kalemani, Naibu Waziri atakuwa Subira Hamisi.

Katibu wa bunge atakuwa Steven Kagaigai na Dkt. Thomas Kashilila atapangiwa kazi nyingine.







September 29, 2017

SHULE YA MSINGI CHIMATE INA HALI MBAYA

Kwa yeyote aliyezaliwa au kusoma kijiji cha Chimate, wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma, au hata kuweka makazi huko, unaombwa kuungana na wananchi kusukuma maendeleo ya Kijiji hicho.

Kwa hatua za awali ni jitihada za kuhakikisha ujenzi wa jengo la vyumba vya madarasa 3, ambapo uongozi wa Kijiji unakusudia kulibomoa jengo hilo na kulijenga upya kutokana na ufa unaohatarisha maisha ya wanafunzi na walimu.

Njooni tuungane na wana Chimate wenzetu waliopo katika kundi la Whatsapp tayari kwa kuendeleza kijiji hicho, waweza kufanya mawasiliano kupitia namba hizi 0762 996 271 au 0768 841 819 au 0753 771 328 au 0713 599 462.
ASANTENI

September 21, 2017

UJENZI WA UKUTA MKOANI MANYARA

PICHANI:  Meja Jenerali Michael Isamuyo atua Mererani, Mkoani Manyara kukagua maeneo ambayo ukuta utajengwa kwa ajili ya ulinzi wa madini.


Wananchi wakiangalia Helikopta ya JWTZ iliyomleta meja jenerali Michael Isamuhyo kusimamia ujenzi ukuta wa eneo la vitalu A hadi D katika machimbo ya Tanzanite ,Mirerani.

PICHA KWA HISANI YA; Innocent Vitalis Inno

KWANINI MAJAJI WANAVAA MAWIGI?



Kwa wenye taaluma mjadala huu unafaa. Kuna mengine pia yamesema, mfano majina ya Victoria Falls, Ziwa Victoria na kadhalika. Makala hayo yalichapwa kwenye gazeti la THE CITIZEN toleo la Jumatano, Septemba 20, 2017. 

Swali linabaki kwanini Majaji huvaa mawigi hadi sasa wakati ni ishara ya ukoloni? Kwa mujibu wa gazeti hilo Wigi moja hugharimu kiasi cha Dola za Kimarekani 6,500.

June 27, 2014

NANI RAIA HALALI?



Na James Zotto, UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM

Labda mimi pia niwape habari kama hii ya Mh. Msando Alberto: Kule kwetu Nyasa, kijiji na kata ya Liuli, kulitokea mzee mmoja anaitwa John John Mpembo Nyirenda. Hili jina linafana na koo za Malawi, Zambia, Msumbiji na Tanzania.

In short, koo nyingi za mwambao wa ziwa zinamchanganyiko wa nchi hizi na hata Swaziland, Lesotho na Afrika Kusini pia.Ni sawasawa tu na sehemu zingine zote za mipakani si Tanzania tu. 

Nimeandika chapter two ya thesis yangu kuhusu Social formation na peopling ya watu wa ziwa nyasa. Pia someni Seligman, Ehret, etc mtaona watu wa bara hii wamezungukaje/asili yao. 

Huyu Mzaee niliyemtaja alikuwa Mwanajeshi wa Jeshi Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Watu wa Tanganyika/Tanzania Bara. Alipostaafu, akarudi kijijini kwetu Liuli.

Kulikuwa na imani mzee mmoja alikuwa anafuga mamba. Ni kweli ziwa letu lilikuwa na mamba wengi, ila sijui ni wa Mungu au binadamu.Watu walikuwa wanauliwa sana na mamba. 

Huyu mwanajeshi mstaafu alisaidia kutega mitego, mamba wengi waliuawa. Tukawa tunaogelea kwa raha zetu. Huyu mzee alikuwa hataki kusikia uchawi, tena hasa kijana kalogwa, maana aliamini ndo nguzo ya Taifa na Liuli ya Nyasa. Kwa ukali wake, akabatizwa jina la MREMA.

Akifananishwa na Lyatonga Mrema wa Vunjo wa kipindi kile. Akagombea udiwani huyu mzee. Kampeni za nini? Alishinda kwa kura zote. Aligombea na binamu yake ambaye hawaelewani....wote asili yao Malawi.

Ukoo wa Kondowe! Huyu binanamu, inaaminika, akamchongea Uhamiajji kuwa Mh. Diwani wetu wa Nyasa si MTANZANIA. Nafikiri anamihela binamu huyu na nafikiri walidhani angegombea hata Ubunge.

Na angeshinda kweli. Eh...Uhamiaji wakafanya mambo. Wakamvua Uraia. Tukampoteza Diwani wetu kipenzi. Akaomba Uraia. Akapewa 'fasta'!
Msando, naomba usome hii habari, itakufariji na kuelewa nchi hii.

Sasahivi baba huyu kafa. Ulikuwa msiba wa aina yake. Si watu ni kama wingu hakuna pa kukanyaga, shujaa. Jiulize! Tulikuwa na mwanajeshi, tena mwenye kacheo, lakini si Mzawa....Hamuoni ni hatari?

Tulikuwa na Councillor lakini si mzawa, hamuoni hatari? ila kwa yote, yupi bora, huyu ambaye kaitwa si raia aliyepigania haki ya vijana, kaleta amani ama hawa wajiitao wazawa wachawi na waonevu na hawana la maana?

Lakini wote koo zao ni asili ya Malawi haimaanishi zimeanzia malawi. Alizaliwa Liuli, baba yake pia, mababu zao ndo walihamia.......La sivyo, chukua robo tatu ya Nyasa na uiondoe siujui uipeleke wapi sasa na ndivyo hata maeneo mengi ya mpakani na hata kati.

NANI RAIA WA NCHI HII? Naombeni jibu. Kama ndo hivyo, lile darasa letu la HGL-1998-2000 lililoongoza nchi nzima kwa matokeo na ambalo limetoa watu wataalamu wanaosaidia nchi hii, basi karibu lote linatokea mpakani, na hivyo si RAIA? I wanted to share this with you.

June 16, 2013

MADE IN TANZANIA: HATIMAYE, HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUWA



Mwanafunzi wa Chuo kikuuu cha Dodoma, ndugu Justice Donatus amefanikiwa kutengeneza mtandao wake wa kijamii JUST LIKE FACEBOOK IS,uitwao MAYOCOO ambao utasaidia kuiunganisha jamii ya kitanzania na kimataifa....Mtandao huu umezinduliwa Jumamosi iliyopita tu....Watanzania tunaweza jamani,haya mambo sio tu Mark Zuckerberg aliweza,hata sisi tumeweza...Nampongeza sana dogo,ndo yuko mwaka wa 3 pale UDOM...Namuombea asiache chuo kama alivyofanya Mark,Warren Buffet na Bill Gates...WATANZANIA WENZANGU TUSAPOTI KILICHO CHETU....Mimi Nimeshajiunga na MAYOCOO, Follow me kwa jina la GIOVANNI

Habari hii kwa hisani ya SETH DE JESUS GIOVANNI