Showing posts with label Linda. Show all posts
Showing posts with label Linda. Show all posts

November 16, 2017

MV NJOMBE INAVYOFUNGUA FURSA KWA WAKAZI ZIWA NYASA.


Honorius Mpangala, 0628994409

NA. HONORIUS MPANGALA
AKIWA katika kampeni za urais mwaka 2005 Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete katika ardhi ya Kyela Mkoani Mbeya alihaidi meli. Alirudia tena kauli hiyo alipokuwa katika ardhi ya Mbamba Bay Mkoani Ruvuma. Baada ya kipindi cha utawala wake hatimaye meli alizoahidi tayari zimeonwa na Wanyasa. 

MV Njombe imekamilika na kufanikiwa safari moja ya majaribio kutoka Bandari ya Itungi hadi Mbamba Bay.  Yapo mambo ambayo ni fursa kwa wakazi wa Nyasa kutokana Meli hii. Kama inavyoitwa ni meli ya mizigo ni chombo kitakachoweza kuwainua kiuchumi wakaza wa Nyasa kama watakitumika ipasavyo. Kuinuka kiuchumi kutatokana na kujikita katika shughuli ambazo wakazi wake watajishughulisha na shughuli kama ilivyo kilimo biashara na hata ufugaji wa kisasa na wenye tija katika maisha ya leo.
Kilimo cha biashara ni moja ya ujasiriamali ambao watu wengi wamekuwa wakijishughulisha nao. Katika mwambao wa Ziwa Nyasa hususani wilaya Nyasa yapo mabonde ambayo yanaweza kufanyika kilimo cha mazao ya muda mfupi na kwa mfumo wa kilimo cha umwagiliaji, na kile cha kutegema mvua na kuleta tija.


October 27, 2017

KWANINI WILAYA YA NYASA IMESHIKA MKIA KATIKA MATOKEO YA DARASA LA SABA?



RAYMOND NDOMBA, SONGEA
WILAYA ya Nyasa iliyopo mkoa wa Ruvuma imekuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba mwaka huu 2017 kimkoa. Swali la kujiuliza ni kwanini hali hiyo imetokea. 


Mawazo yangu ni haya; Pamoja na sababu nyingi zilizosababisha matokeo hayo ya aibu kubwa. Wazazi wanapaswa kubeba lawama kubwa. Wengi wao hawafuatilii maendeleo ya watoto wao, pia makuzi na malezi mabaya.

Miaka ya hivi karibuni (kuanzia mwaka 2000), Wazazi wengi katika wilaya ya Nyasa hawajali elimu, hawajigusi katika ufuatiliaji wa watoto wao kielimu na hata kitabia (Angalia matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule za msingi na sekondari kunzia miaka hiyo ya 2000 kwa shule kongwe ndani ya wilaya). 

October 17, 2017

TAKWIMU MUHIMU ZA WILAYA YA NYASA HADI OKTOBA 2017


1. Total Number of Hamlets in the District = 425

2. Total Number of Households for Nyasa dc = 31,146

3. Total Female Population for Nyasa dc = 74,768.


4.Total Male Population for Nyasa dc = 71,392.

5. Total Population for Nyasa dc = 146,160.

6. Total Number of Secondary school = 14

7. Total Number of Primary School = 106
Total Number of Villages = 84


8. Total Number of Ward = 20

9. Total Number of Division = 3

CHANZO: Nyasa dc statistics

December 17, 2013

DARAJA LA KULIPIA LINDA - CHIULU



Na Vitus Matembo, Mbamba Bay

Wilaya ya Nyasa inazo changamoto nyingi  kiuchumi na kijamii. Suala la Miundombinu ni muhimu na moja ya kazi kubwa inayopaswa kufanywa na wabunge kwa wetu pamoja na viongozi mbalimbali. 
Bila sh.500 huwezi vuka toka kijiji kimoja na kingine. Hao ni vijana walioamua kujenga madaraja haya ili kupata kipato kidogo. Hilo boti hutumika wakati wa kifuku (Masika). NDIO HALI HALISI, SASA TUTAFANYAJE!!!!.